Ukweli kuhusu Wakatoliki kutokuabudu sanamu zilizopo makanisani

Ukweli kuhusu Wakatoliki kutokuabudu sanamu zilizopo makanisani

Niko Parokia ya Mwenye heri Isidori Bakanja, Boko. Hebu njoo nione uwezo wako wa kunizuia.

Maana hata askofu wangu anaujua msimamo wangu na hajawahi kunisema vibaya kama wewe "mtakatifu mbarikiwa"
Bora wewe unajitambua ni haya haya yaliyonitoa huko nilipoanza kusoma biblia mwenyewe badala ya misale ya waumini nikaacha kwenda huko maana niliamini kufuata imani binafsi au msimamo wako tu haitoshi ni sawa na kusafiria boti mbovu ukiamini utafika salama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
acheni Ibada ya Sanamu wakati Yesu aliyekuwa amekufa yuko hai.
Kwa nini ni rahisi kudanganywa kwa mambo yaliyonje ya bibilia wakati bibilia mtu anayo mkonono?
Sanamu Nyingi za Italy mwanzoni kabla ya ukatiliki kuwa dini ya Roman empire zilikuwa ni sanamu za miungu ya kirumi na ziliabudiwa. Kilichofanyika ni kuzibadili majina na edititng kidogo. Madona akawa Mary, Apollo akawa Yesu etc.
 
nachukia dhehebu...sijataja mtu..
uwege unasoma vizur basi kabla hujajibu..
ila hapa kila mtu ana uhuru wa kueleza yake ya moyoni
KAMA NIMEKUKERA AM SOREEE[emoji4] [emoji4] [emoji4]
Hilo dhehebu lako unalolipenda unalipenda kwa vitendo?Kiimani haikusadii chochote kuchukia dhehebu la roma huku hilo la kwako unalolipenda hulitendei haki?
Je unampenda jirani yako?je unasali kwa dhati kwa imani yako?je unasaidia wahitaji?
Haya ni baadhi ya mambo ya msingi kwako hayo ya kuchefuliwa na uroma haukusaidii chochote.
 
Kujipa moyo tu. Haina maana kbs kusema ipo lakini haimaanishi kuabudiwa. Sasa ya nin mle ndani?!! Kubusu,kupiga ishara ya msalaba huku unaiangalia sanamu au picha nini maana yeke km sio kuabudu?! Heshima,mazoea,taratibu?!!
Mambo ya imani yana mengi ya kuhoji ila majibu yapo kwenye biblia
Pilipili usiyoila inakuwashia nini?
 
Ningependa kushauri wote wenye tatizo juu ya kuabudu sanamu wapitie hii post yako.
Neema, baraka na Upendo wa MUNGU, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Ushirika wa Roho Mtakatifu viwe nanyi nyote......!!!!. Ndugu zangu kumekuwa na kelele za hapa na pale kuwa eti Wakristo Wakatoliki wanaabudu Sanamu, hoja hii SIYO YA KWELI Kabisa. Nasisitiza siyo ya Kweli,Jamani mbona mnatuwekea maneno mdomoni ???.,nasema hivi Wakatoliki hatuabudu Sanamu.Weeee !!! hebu tuliza Munkali, fuatana nami.

A:UTANGULIZI.
Katika Biblia MUNGU alikataza Ibada ya Sanamu, lkn jinsi alivyokataza, katazo hilo limewaacha Wakristo Wengi njia panda, hivyo kujikuta wakichanganyikiwa.
Kutoka 20:4-"Usijifanyie Sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu chochote kilicho juu Mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia ".

Kumbukumbu la torati 5:8-"Usijifanyie Sanamu ya kuchonga, mfano wa kitu chochote kile kilicho juu Mbinguni, au kilicho chini duniani, au kilicho majini chini chini ya nchi ".

Sehemu hizi ktk Biblia zikichukuliwa jinsi zilivyo maana yake zinakuwa zimetoa katazo la kutengeneza Sanamu kitu chochote kile wala picha hata Video .Sasa Ndugu Zangu, Walioweka picha za wapendwa wao majumbani, maofisini, vyombo vya Usafiri na kwenye mabango ya Matangazo ni Wakatoliki tu ???. Hivi pesa tunazotumia si zina picha za Viongozi,Wanyama na mimea, je kwa mujibu wa Vifungu tulivyosoma si mnakosea Jamani ??, Mnaonaje km mngetuachia hayo Manoti na masarafu ya hela sisi Wakatoliki ??, Najua wako wenye Vichwa vya Panzi hao watashupaza shingo kuwa picha sio sawa na Sanamu, Nawaambia tulizeni boli, twende taratibu tuwakokote "SLOW LEARNERS ".Nakwambia hivi Kibiblia "SANAMU ni SAWA NA PICHA ni SAWA na SANAMU ".Upo hapo ???!!!. Kama unabisha soma hapa Marko 12:15-16.

15 Tumpe, tusimpe ?,naye akijua unafiki wao, Akawaambia, mbona mmenijaribu ? Nileteeni dinari niione.
16 Wakaileta. Akawaambia ,ni ya nani Sanamu hii na anwani hii ?? wakamwambia ni ya Kaisari.

-Unaona ???!!!. Picha ya Kaisari, kiongozi wa nchi ambayo ipo kwenye Fedha, hapa ktk Biblia inatajwa km Sanamu ya Kaisari na hata Yesu Mwenyewe aliitumia sarafu hiyo. Kumbe mtaona kuwa kwa kuishia ktk mstari wa "4" sura ya 20 ya Kitabu cha Kutoka na mstari wa "8" sura ya 5 ya Kitabu cha Kumbukumbu la torati, Mwenyezi MUNGU amekataza kila kitu kihusucho Sanamu na picha ,lkn ili kujua ni kwanini MUNGU aliagiza hivyo au dhamira yake nini, na kwamba lengo lake si kuzuia Sanamu km Sanamu bali Ibada kwa Sanamu, hebu sasa tusome taratibu na kwa tafakari ya kina mistari inayofuata.Kutoka 20:4-6 na Kumb. 5:8-10.

Kutoka 20:4-6.
4 Usijifanyie Sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu chochote kilicho juu Mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia. Kwa kuwa mimi Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu :nawapatiliza wana maovu ya Baba zao,hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri Zangu.

Kumbukumbu la torati 5:8-10.
8 Usijifanyie Sanamu ya kuchonga, mfano wa kitu chochote kilicho juu Mbinguni, au kilicho chini duniani, au kilicho majini chini ya nchi.
9 Usivisujudie wala kuvitumikia.Kwa kuwa mimi Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, nawapatiliza wana uovu wa baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
10 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri Zangu.

Kumbe hoja ya msingi hapa ni "USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA".na Mwenyezi MUNGU ametoa sababu ya Kwanini "TUSIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA ".Nayo ni kwamba -yeye ni MUNGU mwenye wivu. Kumbe anachokataza MUNGU ni kuchonga Sanamu na kisha Sanamu hizo kuanza kuabudiwa kanakwamba ni MUNGU Mwenyewe, na MUNGU anatoa katazo hilo kwasababu Waisraeli waliyafanya hayo,walichonga Sanamu na wakaziabudu. Kujua kwamba MUNGU alizuia tu Kuabudu Sanamu na si kuzitengeneza hebu tuone jinsi MUNGU Mwenyewe alivyoamuru mara kadhaa Sanamu kutengenezwa na kuwekwa Hekaluni .

B:BIBLIA TAKATIFU, INAFUNDISHA
KUWA MUNGU ALIRUHUSU SAN
AMU KUTENGENEZWA.
1.Mungu alimwamuru Musa kutengeneza Sanamu za Makerubi na kisha kuwekwa Hekaluni -Kut. 25:18-19.

18 Nawe fanya makerubi mawili ya dhahabu :uyafanye ya kazi ya kufua, katika hiyo miisho ya kiti cha rehema, huku na huku.
19 Weka kerubi Moja mwisho Mmoja, na kerubi la pili mwisho wa pili. Fanya hayo makerubi ya kitu kimoja na kiti cha rehema, mwisho huku na mwisho huku.

Mambo hayo !!!, MUNGU anamwamuru Musa kutengeneza Sanamu za makerubi, makerubi wawili hao hukaa juu ya sanduku atokeapo Bwana. Kwa hiyo Bwana amesema ktk Biblia yeye hukaa juu ya Makerubi, rejea 1Sam.4:4, 2Sam.6:2 , 2Fal.19:15 ,Zab.80:1.
Katika Kitabu hicho cha Kutoka 26:1:Mwenyezi MUNGU anaendelea kutilia msisitizo juu ya kuwekwa kwa Sanamu za makerubi ktk Hekalu .

2.MUNGU alimwamuru Musa kutengeza Sanamu ya nyoka wa Shaba -Hesabu 21:8.

8 Bwana akamwambia Musa, jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi ".

Ona sasa !, MUNGU anamimina uponyaji wake ndani ya Sanamu ya nyoka wa Shaba, kwamba mtu akiumwa na nyoka, aitazamapo Sanamu hiyo ataishi ,Hebu fikiri hapo, Kwanini asingesema kuwa labda watu wataje tu jina lake nao wataishi ? Au Musa awaguse tu nao wataishi ?. Mwinjili Yohane hueleza kuwa Sanamu hiyo ya nyoka wa Shaba ni mfano wa Kristo aliyeinuliwa msalabani. Kama vile Waisraeli walivyomtazama nyoka wa Shaba walipona, vivyo hivyo kila Mmoja anayemtazama Kristo msalabani kwa kusadiki (Jicho la IMANI) ana Uzima wa milele. rejea Yohane 3:14-15.

14 Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa,
15 Ili kila aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye.

3.Katika Kitabu cha Wafalme, Mfalme Sulemani alijenga Hekalu na Kisha kulipamba Hekalu hilo kwa Vito vya Dhahabu na SANAMU.rejea 1Wafalme 6:23-28.

23 Akafanya ndani ya chumba cha ndani makerubi mawili ya mzeituni, kwenda juu mikono Kumi.
24 Na bawa Moja la kerubi lilikuwa mikono mitano urefu wake, na bawa la pili la kerubi mikono mitano ,mikono Kumi toka mwisho wa bawa Moja hata mwisho wa bawa la pili.
25 Na kerubi la pili lilikuwa mikono Kumi :makerubi yote mawili yalikuwa ya cheo kimoja na namna Moja.
26 Kwenda juu Kwake kerubi Moja kulikuwa mikono Kumi, na kerubi la pili vivyo.
27 Akayaweka hayo makerubi katika nyumba ya ndani, na mabawa ya makerubi yakanyoshwa, bawa la moja likafika ukutani huko, na bawa la kerubi la pili likafika ukutani huko :mabawa yao yakagusana katikati ya Nyumba.
Akayafunika makerubi kwa dhahabu.

Mfalme Sulemani, hakuishia kuweka Sanamu za makerubi tu, kama tulivyoona hapo, bali aliweka hata SANAMU za Wanyama km vile Ng'ombe na Simba, rejea 1Wafalme 7:23-26,27-29.Aidha Mfalme Sulemani alilipamba Hekalu hili kwa Michoro rejea 1Wafalme 7:36.
Baada ya Ujenzi wa Hekalu kukamilika, Mwenyezi MUNGU alimtokea Mfalme Sulemani na kumwambia kuwa Nyumba hiyo, yaani Hekalu, ameitakasa na tena Macho yake MUNGU na Moyo wake utakuwapo hapo siku zote. rejea 1Wafalme 9:1-3.

1 Ikawa Sulemani alipokwisha kuijenga nyumba ya Bwana, na nyumba ya Mfalme, na mambo yote yaliyoingia moyoni mwake Sulemani, naye akataka kuyafanya,
2 basi, Bwana akamtokea Sulemani mara ya pili kama alivyomtokea huko Gibeoni.
3 Bwana akamwambia, Nimeyasikia maombi yako na dua zako, ulizotoa mbele Zangu. Nimeitakasa nyumba hii uliyoijenga ili niweke jina langu humo milele, tena macho yangu na Moyo Wangu utakuwapo hapo siku zote.

Ona sasa !!!, MUNGU anavyolitakasa na kulikubali Hekalu lililokuwa limejengwa na Mfalme Sulemani, Kama Kweli SANAMU zingekuwa ni Chukizo kwa Mungu hapo MUNGU si angelimkaripia Sulemani ??. Lkn MUNGU hakufanya hivyo kwasababu Mfalme Sulemani hakuweka Sanamu hizo kwa nia ya Kuziabudu km ambavyo Kanisa Katoliki linafanya kwa kuweka Sanamu si kwa lengo la Kuziabudu.

4.Wafilisti walipo lichukua Sanduku la Agano la Kale kwa nguvu Kutoka kwa Waisraeli na kisha kuadhibiwa na MUNGU ,Walipotaka kulirudisha waliwauliza Makuhani na Waaguzi, wafanye nini watakapokuwa wanalirudisha Sanduku hilo ili kujipatanisha na MUNGU, waliambiwa kuwa -Watoe sadaka ya kuteketezwa ya ng'ombe wawili na SANAMU TANO ZA DHAHABU ZA MAJIPU na TANO Za PANYA -Rejea 1Samweli 6:1-15.(Kutokana na urefu wa somo Naomba ujisomee Mwenyewe, maana sio vizuri kukutafunia kila kitu).

5.Katika Agano jipya, Sanamu za Viongozi wa Serikali ziliwekwa katika Fedha na kisha kutumika katika Mzunguko wa Kiuchumi. rejea Marko 12:13-17.

13 Wakatumwa Kwake baadhi ya Mafarisayo na Maherodi, ili wamnase kwa maneno.
14 Hata walipofika walimwambia, Mwalimu twajua ya kuwa wewe u mtu mkweli, wala hujali cheo cha mtu ,kwa maana hutazami sura za watu, lakini katika Kweli waifundisha njia ya Mungu. Je, ni halali kumpa kaisari kodi au siyo ?
15 Tumpe, tusimpe ? Naye, kujua unafiki wao, Akawaambia, mbona mmenijaribu ? Nileteeni dinari niione.
16 Wakaileta Akawaambia, ni ya nani Sanamu hii na anwani hii ? Wakamwambia ni ya Kaisari.
17 Yesu akajibu, Akawaambia, mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu. Wakamstaajabia sana.

Mafarisayo na Maherodia wanapomjaribu Yesu juu ya kulipa kodi kwa Kaisari swali lao linajibiwa kwa kutumia sarafu yenye SANAMU ya mtawala Yaani Kaisari, Jibu la Yesu linakuwa "Mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari, na Mpeni MUNGU yaliyo ya MUNGU ".Fikiri hapo !, Mbona Yesu hasemi msitumie hii Dinari kwasababu ina Sanamu ya Kaisari maana kadiri ya Kumb.5:8 na Kut. 20:4,ni kosa. Lkn Yesu hawakatazi kwasababu anajua kuwa Mungu hachukii Sanamu km Sanamu, bali anachukia Ibada ya Sanamu.

C:HITIMISHO .
Wapendwa sana wanajukwaa,Bado nina mengi ya kuwaeleza Kuhusu Sanamu, lkn nahisi nitawachosha sana lkn naamini nimetoa mwanga angalau kidogo tu. Tukumbuke kuwa hata sisi Wanadamu tuliumbwa kwa Sura na mfano wa MUNGU -rejea Mwanzo 1:26 ,hivyo hata sisi ni Sanamu, maana kitu chochote kilichoumbwa au kutengezwa kwa mfano wa kitu kingine ni Sanamu. Naendelea kukazia kuwa Wakatoliki HATUABUDU SANAMU, Sanamu hutumika tu Kanisani kwaajili ya kumrahisishia muumini kuelewa IMANI yake, sawa na wewe Unapotaka Kumuelezea Mwanao juu ya Namna Babu yake aliyefariki miaka mingi kabla ya yeye kuzaliwa kwa kutumia Picha. Hata katika Elimu Walimu huwa wanatumia mbinu mbalimbali kuhakikisha kwamba Wanafunzi wanaelewa somo lake, wapo wanatumia Picha, Michoro, Sanamu na kufanya ziara za Kimasomo. Tulipokuwa Sekondari ktk Maabara ya Biolojia kulikuwa na Sanamu kubwa ya SKELETON ya binadamu iliyotumika kujifunzia na Wanafunzi wa Dini zote tuliitumia kujifunzia lkn sikuwahi kusikia mtu yeyote akikataa au kulalamika kuwa mbona Sanamu zimekatazwa.Hivyo Kanisa Katoliki haliabudu Sanamu, Tunayemwabudu ni MUNGU Mmoja, ktk Nafsi tatu Yaani MUNGU Baba, MUNGU Mwana na MUNGU Roho Mtakatifu.
Karibuni sana, kwa maswali, dukuduku, n. K. Matusi mwiko.

C. C. Edwayne
Ningependa kushauri wote wenye tatizo juu ya kuabudu sanamu wapitie hii post yako.
 
Huu ndio ukweli ambao Roman imeamua kuuachia katika kipindi hichi cha mfungo wa kwalezima

And the LORD said to Moses, "Make a fiery serpent, and set it on a pole; and every one who is bitten, when he sees it, shall live." So Moses made a bronze serpent...

Numbers 21:8-9
Recently we received an 80-page booklet entitled "What's Behind The New World Order?" It can be traced back to the writings of Ellen G. White, foundress of the Seventh Day Adventist Church. According to this booklet, the Catholic Church is behind the New World Order. The booklet claims that this is true, since the Church is the beast of Revelation (Rev. 17). It attempts to prove this claim by exposing the "marks of the beast." Due to limited space, only one charge will be considered. This is a common charge used against the Catholic Church.

According to this booklet, one "mark of the beast" is the alteration of God's Commandments. The booklet claims that the Catholic Church dropped the "Second Commandment" which forbids "graven images", i.e. statues. Allegedly the Catholic Church condones statue worship.

Now one version of the Ten Commandments can be found in the fifth chapter of the Book of Deuteronomy (also Exodus 20). Comparing Deut. 5:6-21 in a Catholic Bible with that found in a Protestant Bible reveals no essential differences. A few words may differ but that is due to differing translations. The major difference is not content but how Catholics and Protestants traditionally divide up and number these Commandments. Unfortunately the Bible lumps the Ten Commandments all together without division or numbering. (The verse numbers are no help since they were added by Bible scholars many centuries after Christ.)

Traditionally Catholics consider Deut. 5:6-10 as the First Commandment, verse 11 as the Second Commandment, verses 12-15 as the Third Commandment and so on. Verse 21 is split up into the Ninth and Tenth Commandments - distinguishing the desire (lust) to commit adultery from the desire (greed) to steal. This division scheme was advocated by St. Augustine in his writings on Exodus. Traditionally Protestants consider Deut. 5:6-7 as the First Commandment, verses 8-10 as the Second Commandment, verse 11 as the Third Commandment and so on. Verse 21 is kept together as the Tenth Commandment.

According to the RSV Bible and Catholic Tradition, the First Commandment is:
(6)I am the LORD your God,...(7)You shall have no other gods before me. (8)You shall not make for yourself a graven image, or any likeness of anything that is in heaven above, or that is in the earth beneath, or that is in the water under the earth; (9)you shall not bow down to them or serve them; for I the Lord your God am a jealous God, visiting the iniquity of the fathers upon the children to the third and fourth generation of those who hate me, (10)but showing steadfast love to thousands of those who love me and keep my commandments. [Deut. 5:6-10; RSV]

Verse 7 forbids the worship of other gods, while verses 8-9 forbid the making of graven (carved) images that would be worshipped as gods, i.e. idols. Now worshipping statues with divine honor is one way of worshipping other gods. Verse 7 is a general statement of the First Commandment, while verses 8-9 give a specific case of this Commandment. Verses 9-10 present the punishments and rewards that are associated with these Commandments.
By combining together Deut. 5:6-10 into one Commandment, the Catholic Church is accused of altering the Commandments and covering up God's command forbidding graven images. Suspicions are further fueled when Catholic books only present the general form of the Commandment, Deut.

5:7, in order to expedite memorization. Now one must ask the question: "Does God forbid the making of statues, or does He condemn the worship of statues?" If God condemns the divine worship of statues, then the Catholic division scheme is justified since these images would be "other gods before" Him. A separate Commandment based on Deut. 5:8-10 would be redundant.
Now if God simply forbids the making of graven images, then there are problems elsewhere in the Bible. First, in Exodus 25:18-21, God commands Moses to make two statues of angels (cherubim) for the top of the Ark of the Covenant. Later in Numbers 21:8-9, God commands Moses to make a bronze serpent, so that the people who were bitten by snakes could look upon it and be healed.

Now it is true that centuries later King Hezekiah destroyed it; however, this action was done because the people worshipped it as a god (2 Kings 18:4). In the Gospel, Jesus compared Himself to the bronze serpent (John 3:14). Continuing in the Old Testament, the inner sanctuary of the Temple contained two large statues of angels according to 1 Kings 6:23-28. In the following verses, Solomon also had the walls of the Temple decorated with carved images of angels, palm trees and flowers (1 Kings 6:29ff). During the Babylonian Captivity, Ezekiel had a vision from God about the design of the new Temple. According to Ezekiel 41:17-25, this new Temple contained graven images of angels and palm trees. These passages in the Bible indicate that God does not forbid the making of statues. If God truly condemned the making of graven images in the "Second Commandment", then He must have changed His mind later in the Old Testament.

The Catholic Church during the Council of Trent (1545-1563) issued a clear statement concerning images and statues. According to the 25th Session of this General Council:
The images of Christ and of the Virgin Mother of God, and of the saints are to be had and retained particularly in churches, and due honor and veneration are to be given them; not that any divinity or virtue is believed to be in them on account of which they are to be worshipped, or that anything is to be asked of them, or that trust is to be reposed in images, as was of old by the Gentiles, who placed their hopes in idols; but because the honor which is shown them is referred to the prototypes which these images represent; so that we through the images which we kiss...or bend the knee, adore Christ and venerate the saints, whom they represent. [The Canons & Decrees of the Council of Trent (TAN Books, 1978) p. 215-6]

The Church does NOT compel her members to kneel or pray before images. No one is allowed by the Church to pray to images since they have no ears to hear or power to help us. The Church allows for the veneration of images as long as the honor is directed towards Christ and His saints.

On a related issue, some Christians may object to the veneration of images of the saints since they believe that honor should be directed towards God alone and not towards Mary or the saints (1 Tim. 1:17). This objection arises from a confusion between divine honor (adoration - supreme honor proper only for God) and respectful honor proper for men. According to the Bible, the people of God bowed down before King David to show him honor (2 Sam. 24:20; 1 Chron. 29:20; 21:21). Obadiah in 1 Kings 18:7 fell prostrate before Elijah showing him reverence for being a prophet of God. In the Ten Commandments, we are told to honor our mother and father (Deut. 5:16).

Even Jesus defended and obeyed this Commandment (Mark 7:9-13; Luke 2:51). At least for Mary, our honor to her is in imitation of Jesus, her Son (1 Cor. 11:1). The Church allows for the veneration of the saints and their images as long as it remains honor proper for men. It is good to honor the saints for their love and trust in God (Matt. 22:31-32; Heb. 11:1-12:1).
The Catholic Church has not altered the Ten Commandments of God. The Church has not dropped the "Second Commandment" as the booklet alleges. The Catholic numbering scheme may differ with the Protestant numbering scheme, but this is due to a difference in tradition and not an alteration of God's Commandments. Unfortunately the Bible is not clear on how to divide or number the Ten Commandments. If this difference is scandalous, it would be interesting to know what the author of the booklet thought of Jesus Christ when He reduced God's Commandments to the Two Great Commandments in Matt. 22:36-40.

Finally the Church strictly condemns the adoration (divine worship) of statues, images or even the saints, since this is idolatry and in direct violation of the First Commandment. For Christians a crucifix should not be considered merely as a statue of Jesus hanging on a cross, but as a reminder of the high cost of our salvation as well as His words to us:
"If any man would come after me, let him deny himself and take up his cross and follow me." [Mark 8:34]

Printed with permission from A Catholic
NAFIKILI KUFIKIA LEO UBISHI UTAKUWA UMEFIKIA MWISHO.

hauwezi kuwa mwisho kwa sababu kuna watu nao hawajaleta ushahidi wao mahakamani
 
mbona povuu tenaaa...halafu hicho kiingereza chako ni cha wapi[emoji23] [emoji23] [emoji23]

Kwann uwachukie ??
Jiulize kwanza unayemuabudu ww, ndiye wanaye muabudu wao?
Kama Yesu aliacha amri mpya ya upendo, na hakusema umpende uliyenae dhehebu moja au la, kwann ww unachukia community ya Catholic? Au Haumuamini Yesu??
 
Nimekuwa namsikiliza mhubiri mmoja nadhani ni msabato. Kila mara anarejea juu ya makanisa, anayosema ni waabudu Sanamu na wanaosali jumapili (akiita siku ya jua) badala ya sabato. Nadhani ni wakati muafaka wa kumjibu. Uongo ukirudiwa mara kwa mara wasikilizaji wanaweza kudhani ndiyo ukweli. Wajuzi wa mafundisho ya RC ni wakati sasa wa kujibu
 
Nimekuwa namsikiliza mhubiri mmoja nadhani ni msabato. Kila mara anarejea juu ya makanisa, anayosema ni waabudu Sanamu na wanaosali jumapili (akiita siku ya jua) badala ya sabato. Nadhani ni wakati muafaka wa kumjibu. Uongo ukirudiwa mara kwa mara wasikilizaji wanaweza kudhani ndiyo ukweli. Wajuzi wa mafundisho ya RC ni wakati sasa wa kujibu
Wanakuja
 
Nimekuwa namsikiliza mhubiri mmoja nadhani ni msabato. Kila mara anarejea juu ya makanisa, anayosema ni waabudu Sanamu na wanaosali jumapili (akiita siku ya jua) badala ya sabato. Nadhani ni wakati muafaka wa kumjibu. Uongo ukirudiwa mara kwa mara wasikilizaji wanaweza kudhani ndiyo ukweli. Wajuzi wa mafundisho ya RC ni wakati sasa wa kujibu
Labda nami niweke neno kdg.. je siku ya sabato ya bwana ni lini? Kama ni jmos au jpili bas naomba aya toka kweny biblia. Pia kama unaweza muuliza huyo mchungaj ingekua heri atupe majibu hayo, lingine... Ni nani aliezipa majina cku tulizonazo? Maana kweny maandiko hazijaandikwa jmos au jpili!!
 
Back
Top Bottom