Ukweli mchungu: Kama unaishi Tanzania halafu wewe ni maskini huna akili timamu

Ukweli mchungu: Kama unaishi Tanzania halafu wewe ni maskini huna akili timamu

Please uzi huu naomba ukae jukwaani angalau kwa mwaka mmoja . Vijana wanalia njaa huku wamezungukwa na vyakula, waamke wale.

Hili ndilo hitimisho langu na ndio ukweli wenyewe.

Najua maskini watanijia juu wakitamani kuniua kwa kuwaambia ukweli.

Lengo sio kuwaumiza mioyo , lengo ni kuwaamsha. Tokeni usingizini mkapate mali.

Sizungumzii kuwa matajiri, nazungumzia ustawi wa maisha ya kawaida. Kumiliki Nyumba, biashara, gari au hata shamba.

Nchi hii yenye hifadhi za wanyama nyingi, mapori tengefu mengi, bahari imelala kutoka Kaskazini Mashariki mpaka kusini Mashariki mwa nchi, misitu mingi, ardhi yenye rutuba haina hesabu.

Ina maana shetani amefunga akili zako usiione fursa angalau moja kati ya mamilioni ya fursa?
Unasubiri serikali ikupeleke kwa nguvu Makete ukalime Viazi?

Unasubiri serikali ikupeleke kwa nguvu kwenye migodi na mialo ya dhahabu ukachimbe?

Kama huna ustawi katika maisha yako jua tu kuwa shetani ameharibu akili zako kwa ufupi amekufanya usiwe na akili timamu.

Amka.
Wengine watasema tatizo mtaji. Serious?

Nimeona watu wengi sasa wana pesa, mtaji wao wa kwanza ulikuwa nguvu na uthubutu.
Nenda kwenye migodi, mtaji wako ni nguvu tu, acha ulevi na uzinzi utafanikiwa.
Unaweza ukawa na mada nzuri yenye motivation ila uwasilishaji wako ukaspoil mada yote....

Umezungumzia Nchi kuwa na hifadhi za wanyama na hifadhi tengefu...
Unataka wazifanyie nini wakati Hifadhini Raia Hawaruhusiwi? We unaishi wapi? Hata kuwinda panya tu Serengeti ni kosa linaloweza kukufunga Miaka 100 jela...

Unazungumzia kuhusu Mashamba yenye Rutuba? Asilimia 100 ya mashamba hayo ni mali ya Serikali, ulitaka vijana wakayachukue ili waingie Mgogoro na Serikali (Bado hatujasahau yule mtu aliouziwa pori tengefu)..

Unazungumzia kilimo cha Viazi Makete....
Unajua Kijana alioko Dar mpaka Makete nauli ni Bei gani?
Unajua Mbegu za viazi ni kiasi gani?
Unajua kukodi shamba ni kiasi gani?
Unajua mbolea na pembejeo nyingine ni kiasi gani?
Unajua kutafuta Labour wa kupalillia na kutunza hayo mashamba ni kiasi gani?

Unasema watu waende Migodini umewahi kufanikiwa kwenda Migodini?
Au ni story ulizosimuliwa mtaani?..

WAKATI MWINGINE SHIRIKISHA AKILI KABLA YA KUANDIKA MADA AMBAYO WEWE MWENYEW U AIONA NI 🚮🚮🚮
 
Unachosema ni sahihi, na upande mwngine si sahihi, watu wamekuwa wakulima miaka mingi January Hadi Decemba Kila siku shambani kwa miaka zaidi ya 30 Hadi leo hana kitu. Mfumo wa masoko na bei za mazao vinadidimiza mkulima, watu walio wengi hushangilia vyakula vinaposhuka bei, bila kuangalia gharama za uzalishaji.

Anayepanga bei ni mnunuzi si mkulima ndo maana sector wengi hawapigi hatua, kwa upande wa mifugo tatizo ni ardhi, migogoro mingi kati ya wakulima na wafugaji inaanzia kwenye ardhi, maeneo unayoona yako wazi yanamilikiwa, kwa vijana ni changamoto, hivyo unavyolaumu kuwa wamelala siyo kweli.
 
Matajiri huwa hawaandiki mipasho kama uliyoandika mkuu...

Huwa wanawaeleza watu mbinu za kufanikiwa au wanawawezesha watu namna ya kufanikiwa...

Kuna watu wanapambana kila jua linapokuchwa, wapo kwenye mapambano ya kujikwamua kichumi iwe ni migodini, mashambani, viwandani n.k lakini maisha yangali yamewapiga konde la TKO...

Mathalani kuna wakulima wanaopambana usiku na mchana kwa kilimo, wanapata mavuno mengi tu lakini kwao masoko inakuwa mtihani wanaishia kuuza mazao kwa walanguzi...

Kuna factors nyingi sana zinazomfanya mtu atoboe kwenye nchi zetu hizi za kiafrika, juhudi ni kitu kimojawapo lakini sio kwamba kila mwenye juhudi atatoboa...
 
You were born with a silver spoon in your mouth
Ni ngumu kujua watu wanapitia nini ukiskia mtu kalala njaa utamuita mzembe kwasababu nyumbani umezoea kuona magunia ya Michele,sukari, friji imejaa vyakula

Ni ngumu sana kuelewa.
 
Unachosema ni sahihi, na upande mwngine si sahihi, watu wamekua wakulima miaka mingi January Hadi decemba Kila siku shambani kwa miaka zaidi ya 30 Hadi leo Hana kitu mfumo wa masoko na bei za mazao vinadidimiza mkulima, watu walio wengi ushangilia vyakula vinaposhuka bei, bila kuangalia gharama za uzalishaji, anayepanga bei ni mnunuzi si mkulima ndo maana sector wengi hawapigi hatua, kwa upande wa mifugo tatizo ni ardhi, migogoro mingi kati ya wakulima na wafugaji inaanzia kwenye ardhi, maeneo unayoona yako wazi yanamilikiwa, kwa vijana ni changamoto, hivyo unavyolaumu kuwa wamelala siyo kweli
unatetea ujinga. watu wengi tu wametoboa kwenye kilimo. wewe unalimia wapi huko
unataka ulime mwaka mmoja tu utoboe
 
Nchi hii yenye hifadhi za wanyama nyingi, mapori tengefu mengi, bahari imelala kutoka Kaskazini Mashariki mpaka kusini Mashariki mwa nchi, misitu mingi, ardhi yenye rutuba haina hesabu.
Jamaa yangu nilitaka nikupe bonge la tusi ila nimekustahi tu, ila kiufupi nawaonea huruma wanaokutegemea au km ni Baba wa familia nawaonea huruma sana familia yako na km una watoto nawasikitikia watoto wako kwa kua na Baba mwenye akili fupi akili kiazi
 
Tunapigwa majungu ya wazi wazi😆
Hivi shule zimefungwa...??
Asubuhi na Mapema tumeshaanza kutoana Akili.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
Jamaa yangu nilitaka nikupe bonge la tusi ila nimekustahi tu, ila kiufupi nawaonea huruma wanaokutegemea au km ni Baba wa familia nawaonea huruma sana familia yako na km una watoto nawasikitikia watoto wako kwa kua na Baba mwenye akili fupi akili kiazi
Humu JF wengi ni wajinga sana aisee
 
Kutoboa unatakiwa uwe umefikia hatua gani kwenye maisha ya kibongo au uwe unamiliki mali na kiasi gani cha fedha? Samahani mkuu nijibu ili nijue nimetoboa au bado
uwe at least na uhakika wa kula na kulisha watu wako, uhakika wa kuwa na sehemu ya kuishi na sasa ikupe mwanya wa kutafuta mambo mazuri
kinyume chake hata kula ni changamoto
 
Back
Top Bottom