Ukweli Mchungu: Rais Samia hupendwi na Wananchi wengi

Mbona povu mkuu, mi nimesema wanawake wanauita MCHELE SAMIA. .Kosa langu ni lipi?
2025 chama kikimpitisha hao hao wanawake mnaoketi pamoja na kupeana majina ya mchele wataupika na utaula mpaka 2030.
 
Uko sahihi kabisa. Wamama wengi hawamkubali kabisa huyu Rais. Na hata hoja ya kutopendwa nayo ina ukweli ndani yake.
CCM itaendelea kukuongoza na ikimpitisha samia 2025 wamama watampitisha kwa kishindo. Hili utalishuhudia TBC au mitandaoni kama jibu la nadharia ulizonazo.
Maeneo mengi ya vijijini ambako ccm imekuwa ikikusanya kura za bure, kwa sasa hali ni tofauti kabisa. Kuna watu hawataki hata kumsikia, au kumuona kwenye picha. Hii siyo dalili nzuri hata kidogo.
Hakuna kura za bure kuna kura za Watanzania na zitaendelea kuwepo kwa 2025-2030.
Natamani 2025, angejitoa kwenye mchakato. Ila ndiyo tena. Madaraka yamesha mnogea. Ngoja tuone kitakachotokea.
Tanzania inaongozwa na CCM, akijitoa, bado CCM ni ile ile, wembe ni ule ule, kilio kwa wasioitaka ni kile kile.
 
Hata mimi kwa kweli simpendi kama akiendelea hivi, naomba nisiwe mnafiki.

Siwezi kumpenda mtu anayedharau wanyonge,

siwezi kumpenda mtu anayewapuuza akina mama wenye shida anasema,"waondosheni wanatupigia kelele",

siwezi kumpenda mtu anaeziba masikio asisikie raia wanataka nini,

siwezi kumpenda mtu anayejinasibu eti hupaswi kuwafurahisha watu,

siwezi kumpenda mtu ambaye anaingia mikataba ya kuliumiza Taifa n.k
 
Umeandika ujinga!

Huyo unae msema watu walikuwa wanajazana kwenye Vibanda kusikilizà hotuba zake. Hadi anakufa watu wamejazana kulia kila Kona. Hadi Leo wanamililia.
Hiyo kwenda uwanja wa taifa watu walipewa hadi usafiri wa bure na kuhamasishwa kwenda, na wengine haya maagizo yalitoka wahudhurie, lengo ni kuficha picha hasi ya kuchukukiwa kwake. Watu walikuwa wanalia kwakuwa ni msiba wa kwanza wa rais kufia madarakani hapa nchini, na covarage ya msiba ikiyokuwepo. Watu walikuwa wanajazana kwenye vibanda kusikiliza hotuba zake kwani zilikuwa na mvuto, sana sana watu waliokuwa wanasikiliza ili waone maamuzi ya sifa za kijinga na udhalilishaji wa watu. Ifahamike ilikuwa ni style mpya ya kutawala kwa rais kuonekana kwenye media kila siku. Wangeachwa wale waliokuwa wanashangilia msiba wake ndio ungejua hujui.

Kipimo halisi cha kukubalika kwake ilikuwa ni kuheshimu uchaguzi ili ukweli ufahamike. Kwanza alianza kwa kupika idadi ya wapiga kura, kisha akapanga idadi ya kura alizotaka atangazwe nazo. Uhalisia hata wapiga kura hawakufika 10m siku ya uchaguzi mkuu. Wajinga wa aina yako ndio waliamini propaganda zake. Sasa kama uliamini ule uongo wake kuwa chini ya utawala wake alijenga viwanda 4,000+ ambavyo havionekani, utaacha kuamini propaganda zake kuwa alikuwa anakubalika sana?
 
2025 chama kikimpitisha hao hao wanawake mnaoketi pamoja na kupeana majina ya mchele wataupika na utaula mpaka 2030.
we mduanzi nikome peleka zaga zaga zako pemba huko
 
Wanaomzunguka wanamharibia alafu akiondoka hao hao watananga kimafumbo majukwaani.
 
Huyu mama tangu aharibu kwenye bandari sina hamu naye.Akimaliza muda wake aende tu.Wazanzibar hamnaga uchungu na cha wenzenu nyinyi kila kitu mnachukulia poa na Waarabu ndio miungu watu yenu.Yaani wakati Magu anaongelea mikataba ya hovyo alikuwa amekaa mbele kabisa leo hii anafanya kile kile kilichokuwa kinapigiwa kelele hivi mtu wa hivi unaweza kusema ana akili gani?Aende bwana goooo!
 
Tena aki na mama ndo hawampendi kabisa. Kuna mama mmoja anasikiliza radio one sasa kuna muda wanaweka ujumbe wa Samia Suluhu Hassan utasikia wamama wanakwambia mwenzao "zima kwanza/toatoatoa.../we punguza sauti kwanza/
Ukweli hata mimi nikisikia wanataka kuweka ujumbe wa Samia nikiwahi nazima redio upite kwanza.
 
Umenena vema Uchaguzi umekuwa tu kama ni takwa la kidemokrasia lakini hauna maana halisi ya uchaguzi
 
Kwa uzoefu wangu utawala wa mkapa ndio ulioanza kusomba watu kuwatoa sehemu tofaoti hata mzee nyundo kwenye mikutano yake walikuwa wabasombwa watu bodaboda bajaji watiliwa mafuta
 
Kelele za chura azizuii ng,ombe kunywa maji,bora kupata akili ikakosa mali leo unamchukia samia unaipenda ccm na huyo mbunge wako samia uongozi wake utakoma na utabaki na salakasi za ccm tu watu kama nyiyi ndio msio faa msio jua chanzo cha haya yote
 
Mkuu tulishamsikia Borntown akijidai mbele ya wavaa kijani wenzake kuwa 2025 atakuwa ni mama tu,eti hakuna mtu maarufu nchi hii kama first lady. Sasa kama mwenye nchi na mwenye chama kasema sisi ni nani hadi tukatae sisi ni mazombie tu mkuu huwezi fananisha na majirani zetu wa Malawi,Zambia na hata Kenya.jamaa wamesha jimilikisha nchii hii yao kama kaya yao binafsi.
 
Mafisadi papa sio watu wakuridhika, yeye alidhani anaweza ingia ubia nao wakudumu. Hawa watu wapo kila sehemu ukionda maslahi yao awataacha kukutungia uongo kila uchao.

Mafisadi wadogo wadogo wanaumiza wananchi kwenye haki zao; hawa wanaongeza hasira kwa raia dhidi ya serikali.

Wapinzani sio watu watakao kusifia milele, hasa Lissu agenda yake ni moja tu kuona siku moja wanaitoa CCM madarakani kwa imani yake aina credibility tena na fitna anaijua.

Dr Slaa nae fitna ya siasa anaijua na uwezo wa kutunga uongo anao wakiungana na Lissu hao watu wawili upinzani kuchere mshike-mshike lazima CCM iipate, hasa kipindi hiki mama aeleweki.

Katibu wa uenezi CCM ni mtu mwenye kuweza porojo; yeye kamweka anaemjua mwenyewe toka sakata la bandari limeanza ata porojo zake atujazisikia.

Raisi mwenyewe awezi tetea maamuzi yake ata yaliyo sahihi anataka hiyo kazi afanyiwe na wengine.

Bora Magufuli alichagua kundi la wananchi walio wengi wampende, na kupambana majizi ata yakichukia poa tu.

Bi Tozo yeye kachagua mafisadi sasa yamemgeuka na wananchi wengi washasumbuliwa vya kutosha awamuelewi, haki waliyoionja kwa miaka mitano aipo tena.

Ndio aelewe ni kweli Magufuli alikuwa anauwa watu na kuwatupa kwenye viroba beach au hadithi tu.

Ni kweli alizuia uhuru wa habari au alikuwa anapambana na wapotoshaji tu.

Raisi Kenyatta Dodoma kwenye kumuaga Magufuli “dada yangu Samia, ushauri ninaokupa katika uraisi wako umechongewa njia na mtangulizi wako baki hapo hapo usitoke”.
 
anayumba, taifa lishamshinda, kama anataka walau asikilizwe na kupewa heshima yake ana mambo 2 tu kabla ya 2025.
1. Achomote battery suala la DP World.
2. Atupatie Katiba Mpya.
 
Kushapaza shingo kunawaponza wengi
Tunaitaka Tanganyika Yetu tufanye yetu
 
we mbwa una kitu kinakuwasha, umejaa uongo na uzushi wa kipumbavu, nani alikutuma huko kote na umetumia gharama za nani. Subiri uchaguzi mkuu 2025 omba uzima.
 
Huku kanda ya ziwa angelijuwa mwanamke hatakiwi kuwa kiongozi.
Acha uwongo wako huo, kanda ya ziwa wanawake ndio wenye nguvu, waganga wa kienyeji karibu wote ni wanawake na wana nguvu ajabu ktk koo zao. Hiyo kanda yako sijui ni ipi. Hangaya ni jina la kiume? Mbona alikuwaga chifu wa wasukuma, acheni uzandiki wenu. Mama tunampenda tena sana labda nyie mashoga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…