UKWELI MCHUNGU: Wazazi wengi hawana upendo wa kweli

UKWELI MCHUNGU: Wazazi wengi hawana upendo wa kweli

Kama Mume.

Nimeshasema wengi wanasomesha watoto sio Kwa sababu ya upendo Bali Kwa sababu ya uwekezaji wa baadaye ili wasaidiwe. Tofautisha uwekezaji na Upendo.

Hilo utaliona kwenye matamshi Yao. Utajua huyo Mzazi alikusomesha Kwa upendo au Kwa kutaka faida ya baadaye.

Tuache tabia hizi
Lakini kumbuka kwamba mwanaume ni mzazi kwa maelezo yako anakuwa na side mbili hapo zinazokinzana
Nashindwa kuelewa hapo
 

I Disapprove of What You Say, But I Will Defend to the Death Your Right to Say It​


Umepuyanga hadi umepuyanga tena. Unasema mme anaempenda mke ndo mwenye upendo wa kweli? Mume huyu huyu ambae anakuletea mchepuko na ana uwezo wa kukufukuza akipata mali?

Wewe endelea kuamini unachoamini ila kwa sisi wazazi tunaelewa. Personally mzazi wangu pamoja na kwamba leo hii niko kwangu na ndoa yangu ananiona nastahili msaada wake. Hata akiona umetoa kitu kusaidia ndugu ambao ni wanae wa damu anakutumia hela unamuuliza ya nini anasema aah najua tu maisha magumu unatamani umwambie hii sio sawa hawa ni jukumu langu.

Na mimi kama mzazi, niko napambana usiku na mchana wanangu nawaanadalia mazingira hata siku nikidondoka leo niwaachie knowledge na mali. Ile
Dhana ya kwamba acha mtoto aje ajitaftie ni kama kukomoa. Basi usizae. Kama una uwezo ya nini kutupa mali wakati kuna viumbe umetengeneza? Mtoto muelekeze
Njia njema na hata akiwa anakua asijue kwamba kuna mali zake zinamsubiri anaweza kubweteka. Ila ajue yeye ni kijana wako unaetegemea aje kuwa mfano katika jamii.

Sasa we usisemee wazazi wako kwenye general rule mkuu. Usijenge chuki ndani ya mioyo ya watu waanze kuwaona wazazi wao kama takataka. Maana kuna watu wana akili za kushikiwa wanabeba bandiko lako wanalihamishia kichwani kama mataaira.

Mzazi atabaki kuwa mzazi hata maandiko yamesema.
Mungu wabariki wazazi wetu waliotulea kwa shida..

Ila kwa kuwa umesema ni baadhi ya wazazi basi nyie wenye wazazi wa hivyo Mungu awape tumaini la milele huku mkijikumbushia na waefeso 6:2-3. Na ile amri ya Kuheshimu Baba na mama ndo amri yenye ahadi. Hata mzazi akutese vipi. Baraka na laana vipo katika kurudisha kwako. Kama mzazi anakutesa bora ukae mbali kuliko kumvunjia heshima. Tunawaona wazazi wanaonyang’ana vitu vya watoto wao kwa nguvu kwasababu ni mzazi inatesa haswa lakini kwakuwa ni mzazi unabaki unaugulia moyoni.

Wewe kama mzazi. Unategemea nini kwa mtoto wako? Unataka mtoto wako akikua aje kuwa mtu wa namna gani?
 
Yaani umeandika kinyume kabisa.Watu wanazaa watoto ili wapate warithi wa mali walizonazo siyo ili waje kuwasaidia kwa kipato NO.Chukulia kuwa umemlea mtu mpaka anafikia umri wa kujitegemea akiondoka kwenda kuanza maisha yake utashindwa nini kuendesha maisha yako bila msaada wake,kwani ulipokuwa unamlea alikuwa anakusaidia ? sasa utashindwa nini.
 
Kiongozi ni km umeyachukua kichwani mwangu kongore Sana Kwa hayo madini.
 
Lakini kumbuka kwamba mwanaume ni mzazi kwa maelezo yako anakuwa na side mbili hapo zinazokinzana
Nashindwa kuelewa hapo

Mwanaume Kwa mkewe. Sio Kwa mtoto.
Hata hivyo wapo wazazi wenye upendo WA kweli Kwa watoto wao. Ila hao ni wachache Sana.

Angalia familia zenye upendo Kwa watoto wao. Hata watoto wenyewe utakuta wanapendana wao kwa wao.

Ukuona ndugu hawapendani wewe usipate shida kuchunguza, angalia Wazazi wao utaelewa nikisemacho.

Hao wanaosema wazazi wao waliwapenda waangalie je wanapendana wao Kwa wao yaani watoto?
Ukiona mtu anakuambia wazazi walitupenda alafu muda huohuo hakuna upendo baina ya Kaka na wadogo watu jua hapo anaongopa
 
Yaani umeandika kinyume kabisa.Watu wanazaa watoto ili wapate warithi wa mali walizonazo siyo ili waje kuwasaidia kwa kipato NO.Chukulia kuwa umemlea mtu mpaka anafikia umri wa kujitegemea akiondoka kwenda kuanza maisha yake utashindwa nini kuendesha maisha yako bila msaada wake,kwani ulipokuwa unamlea alikuwa anakusaidia ? sasa utashindwa nini.

Unataka kusema Watu wote wanamali za kuwaridhisha watoto wao?
Upendo ni zaidi ya Urithi
 
Ninachompendea ROBERT HERIEL anaongea kitu na kama ni muhanga wa hiyo kitu basi unagundua anagusa mulemule.... Imagine mimi Baba yangu mzazi alishawahi kuniropokea kwamba "Kuanzia leo wewe sio mwanangu, nahesabia sina mtoto tu, maana huna msaada wowote kwangu sasa wewe wa nini kwangu" ilikuwa tunaongea kwenye cm kisa aliniomba hela nikamuambia hali haipo sawa ile kitu iliniuma kinoma ukizingatia nipo kwenye situation ngumu sana kimaisha maana hata nilipokuwa naishi palikuwa kwa mwana tu alinihifadhi so, akili ilikuwa inawaza nikusanye vijiehela ninavyopata kwenye vibarua na mimi nihamie gheto kwangu kumbuka mimi nipo Dar mzee yupo Moshi nilichomjibu ni kwamba "haina tatizo mzee me pia naanza kuhesabu sina baba na wala usiwe na wasiwasi sitokutafuta tena" kweli zikapita weeks hatujawasiliana siku moja akapiga anajichekesha... Me nikawa nishaelewa hapa hamna upendo wa kweli wala nini watu wanajali pesa tu so, acha tuishi kinafiki na mzee nikipata vielfu kumi namtumia till now tunaishi tu.


Baada ya hapo nikawa nikihisi pengine wamama ndo wana upendo kweli kuliko wababa maana wao ndo walituzaa.... Mwaka jana mama pia akani-disappoint mno kwa maneno yake.... Dah yeye ndo aliniongelea vibaya mpaka nikajikuta nimekata cm.... Kumbuka hata hawajanisomesha nikafika levels za juu no, Wala hawajui huku Dar najishughulisha na nini wao hujua kujifanya wana upendo na mimi pale wanapoona messages za Transactions ndo utaona mara "Oooh lini utakuja kutusalimia, Oooh ni muda sasa mimi baba, mama sinakuona sio vizuri"

Dah! oya wanangu Rafiki wa kweli kwa sisi wanaume ni Mungu na Hela tu wakuu... Usiamini upendo wowote mbali na hapo labda kama umezaliwa kwenye familia yenye misingi mizuri ya kipato.


Umasikini ni laana.
 

I Disapprove of What You Say, But I Will Defend to the Death Your Right to Say It​


Umepuyanga hadi umepuyanga tena. Unasema mme anaempenda mke ndo mwenye upendo wa kweli? Mume huyu huyu ambae anakuletea mchepuko na ana uwezo wa kukufukuza akipata mali?

Wewe endelea kuamini unachoamini ila kwa sisi wazazi tunaelewa. Personally mzazi wangu pamoja na kwamba leo hii niko kwangu na ndoa yangu anawaza ananiona nastahili msaada wake. Hata akiona umetoa kitu kusaidia ndugu ambao ni wanae wa damu anakutumia hela unamuuliza ya nini anasema aah najua ty maisha magumu unatamani umwambie hii sio sawa hawa ni jukumu langu.

Na mimi kama mzazi, niko napambana usiku na mchana wanangu nawaanadalia mazingira hata siku nikidondoka leo niwaachie knowledge na mali. Ile
Dhana ya kwamba acha mtoto aje ajitaftie ni kama kukomoa. Basi usizae. Kama una uwezo ya nini kutupa mali wakati kuna viumbe umetengeneza? Mtoto muelekeze
Njia njema na hata akiwa anakua asijue kwamba kuna mali umemuachia. Ila ajue yeye ni kijana wako unaetegemea aje kuwa mfano katika jamii.

Sasa we usisemee wazazi wako kwenye general rule mkuu. Usijenge chuki ndani ya mioyo ya watu waanze kuwaona wazazi wao kama takataka. Maana kuna watu wana akili za kushikiwa wanabeba bandiko lako wanalihamishia kichwani kama mataaira.

Mzazi atabaki kuwa mzazi hata maandiko yamesema.
Mungu wabariki wazazi wetu waliotulea kwa shida..

Ila kwa kuwa umesema ni baadhi ya wazazi basi nyie wenye wazazi wa hivyo Mungu awape tumaini la milele huku mkijikumbushia na waefeso 6:2-3. Na ile amri ya Kuheshimu Baba na mama ndo amri yenye ahadi. Hata mzazi akutese vipi. Baraka na laana vipo katika kurudisha kwako. Kama mzazi anakutesa bora ukae mbali kuliko kumvunjia heshima. Tunawaona wazazi wanaonyang’ana vitu vya watoto wao kwa nguvu kwasababu ni mzazi inatesa haswa lakini kwakuwa ni mzazi unabaki unaugulia moyoni.

Wewe kama mwanaume. Unategemea nini kwa mtoto wako?

Wazazi wenye mawazo Kama yako ni wachache Sana.

Mimi ninaushahidi wa wazazi wengi wanazaa watoto wengi ili wapate msaada uzeeni
 
Ninachompendea ROBERT HERIEL anaongea kitu na kama ni muhanga wa hiyo kitu basi unagundua anagusa mulemule.... Imagine mimi Baba yangu mzazi alishawahi kuniropokea kwamba "Kuanzia leo wewe sio mwanangu, nahesabia sina mtoto tu, maana huna msaada wowote kwangu sasa wewe wa nini kwangu" ilikuwa tunaongea kwenye cm kisa aliniomba hela nikamuambia hali haipo sawa ile kitu iliniuma kinoma ukizingatia nipo kwenye situation ngumu sana kimaisha maana hata nilipokuwa naishi palikuwa kwa mwana tu alinihifadhi so, akili ilikuwa inawaza nikusanye vijiehela ninavyopata kwenye vibarua na mimi nihamie gheto kwangu kumbuka mimi nipo Dar mzee yupo Moshi nilichomjibu ni kwamba "haina tatizo mzee me pia naanza kuhesabu sina baba na wala usiwe na wasiwasi sitokutafuta tena" kweli zikapita weeks hatujawasiliana siku moja akapiga anajichekesha... Me nikawa nishaelewa hapa hamna upendo wa kweli wala nini watu wanajali pesa tu so, acha tuishi kinafiki na mzee nikipata vielfu kumi namtumia till now tunaishi tu.


Baada ya hapo nikawa nikihisi pengine wamama ndo wana upendo kweli kuliko wababa maana wao ndo walituzaa.... Mwaka jana mama pia akani-disappoint mno kwa maneno yake.... Dah yeye ndo aliniongelea vibaya mpaka nikajikuta nimekata cm.... Kumbuka hata hawajanisomesha nikafika levels za juu no, Wala hawajui huku Dar najishughulisha na nini wao hujua kujifanya wana upendo na mimi pale wanapoona messages za Transactions ndo utaona mara "Oooh lini utakuja kutusalimia, Oooh ni muda sasa mimi baba, mama sinakuona sio vizuri"

Dah! oya wanangu Rafiki wa kweli kwa sisi wanaume ni Mungu na Hela tu wakuu... Usiamini upendo wowote mbali na hapo labda kama umezaliwa kwenye familia yenye misingi mizuri ya kipato.


Umasikini ni laana.

Pole Sana Mkuu.
Endelea tuu kuwaheshimu Sana wazazi wako.
Ila kimsingi suala la upendo Kama huna lolote ni nadra Sana.
 
Mtoto ukifanikiwa kila mzazi anataka atambulike Kwa jina lako.
Mfano Baba Ommy Dimpo, ilhali anawatoto wengine zaidi ya kumi ambao ni apeche Akili.
Au Mama Kanumba, ilhali wapo watoto wengine.

Hata mtoto mwenye kipato akifariki mama au Baba husikia uchungu zaidi kuliko akifa apeche Alolo.
Rejea Mama Kanumba, kafiwa na watoto wawili lakini haachi kumtaja Kanumba kuwa huyo mtoto ndiye kamuuma zaidi.

Lakini Kwa upande wa Mume na Mke hiyo ni tofauti Kabisa. Hata kama Mkeo ni Masikini, kifo cha mke achana nacho
Mtoto mwenye kipato akifariki utasikia mama analia MUNGU UMENIWEZAAAA KWA NINI UMEMCHUKUA JIMMY,MBONA UMENIKOMOA MIMI.....,sasa wengine inabidi mstop kulia muangaliane sasa huyu mama alitaka achukuliwe nani?
 
Umeongea ukweli kabisa wazazi wa siku hizi wanapenda sana mtoto mwenye uwezo,hata wajukuu wakikutana likizo kale ka mwenye hela kanatreatiwa kama ka princess..tupambane tu kutafuta hela
 
Mtoto mwenye kipato akifariki utasikia mama analia MUNGU UMENIWEZAAAA KWA NINI UMEMCHUKUA JIMMY,MBONA UMENIKOMOA MIMI.....,sasa wengine inabidi mstop kulia muangaliane sasa huyu mama alitaka achukuliwe nani?

😂😂😂😂😂

Na watoto wakigundua tabia za namna hii Kwa wazazi upendo wao Kwa mzazi unapungua. Pia wao wanapunguza kupendana na kushirikiana.
Wanaishi kinafiki nafiki. Kisa walizaliwa tumbo moja.
 
Umeongea ukweli kabisa wazazi wa siku hizi wanapenda sana mtoto mwenye uwezo,hata wajukuu wakikutana likizo kale ka mwenye hela kanatreatiwa kama ka princess..tupambane tu kutafuta hela

Mzazi WA hivyo hawezi kumfundisha mtoto Upendo.
Watu wanasema siku hizi hakuna upendo kumbe ndivyo tulivyolelewa.
 
Sawa.
Huwezi elewa mpaka uelewe
Kuna watu wameumbwa kuishi kwa kufuata mkumbo tu ila sio kuelewa mambo yanakwenda vipi. Kama huyu kasoma ameona hajaelewa badala ya kuuliza maswali apewe ufafanuzi anatapika mashudu na buni inayotengeza kahawa.
 
Mtoto ukifanikiwa kila mzazi anataka atambulike Kwa jina lako.
Mfano Baba Ommy Dimpo, ilhali anawatoto wengine zaidi ya kumi ambao ni apeche Akili.
Au Mama Kanumba, ilhali wapo watoto wengine.

Hata mtoto mwenye kipato akifariki mama au Baba husikia uchungu zaidi kuliko akifa apeche Alolo.
Rejea Mama Kanumba, kafiwa na watoto wawili lakini haachi kumtaja Kanumba kuwa huyo mtoto ndiye kamuuma zaidi.

Lakini Kwa upande wa Mume na Mke hiyo ni tofauti Kabisa. Hata kama Mkeo ni Masikini, kifo cha mke achana nacho

Wapo hivyo kabisa mtoto ambae kafanikiwa ndio atapendwa huyo na kusikilizwa
 
Back
Top Bottom