Ukweli wasioupenda Watanganyika au Watanzania Bara

Ukweli wasioupenda Watanganyika au Watanzania Bara

Waarabu na Wazanzibari ni ndugu wa damu na wa asili kabisa maana Waarabu ndio walioleta ukombizi kwa Taifa la Zanzibar.

Waarabu ndio watu walioweza kuishi kijamii pamoja na Wazanzibari kwa miaka mingi hadi kuchanganya damu na Wazanzibar walio wengi na kuishi km jamii moja tena kwa upendo kabisa.

Waarabu ndio walioipa Nchi ya Zanzibar hadhi na heshima kimataifa na kujulikana kama ni nchi, bila ya Waarabu hata hao Vibaraka CCM-ZANZIBAR wasingeweza kupata nyadhifa mbali mbali za utawala hapo Zanzibar badala yake wangekua tu ni watu dhalili kwenye mkoa wa Tanganyika.

Kwahiyo ni wazi kuwa Waarabu walikuja Zanzibar kwa ajili ya ukombizi na kuwasaidia Wazanzibari waweze kuwa watu wenye hadhi na kuheshimika dunianiani kote.

Mwarabu hivi sasa ndio anaeijenga Zanzibar sijamuona Mtanganyika akija kuekeza Zanzibar sekta muhimu kama bandari kujenga majumba viwanja vya ndege naona mikataba imetiwa na waarabu sijamuona hata mtanganyika mmoja au.

Tusisahau fadhila kwa Uchu wa Madaraka na Njaa. WENYE AKILI WAMESHANIELEWA!!

Na anaebisha Abishe kwa Hoja na sio Porojo
Sasa wewe unaeashindanisha waarabu wa Oman na watanganyika hujasema mzanzibar mweusi kaifanyia nini zanziba mfanya yeye ni wa kupokea tuMsimamo wangu kwenye hili ni kuwa system ya utawala wa ccm umekaa kimagumashi hawataki watoto wetu wajue baadhi ya historia our history has to make us strong lazima ifundishwe kama ilivyo bila kuchakachulia,kama wazaibar wanaudugu wa damu na Oman waachwe lakini pia wana udugu na tanganyika hata sultan akitaka kurudi awe mfalme kama uingereza shughuli za utawa awepo waziri
 
Sasa watanganyika wawekeze Zanzibari nyie wenyewe Zanzibari mkae kula urojo kweli. Yaani umeandika kabisa unamaliza MB unamsifia mwarabu anavyoendeleza ZnZ na Mtanganyika anavyoshindwa kuwekeza ZnZ bila kusema huyo mzanzibari mwenyewe anakaa upande upi
Ina maana yeye kaona wazanzibar ni watu wa kuekezwa tu, wao hawawezi kuwekeza
Anasifia waarabu kuwekeza Zanzibar na kusema watanganyika hawajawekeza Zanzibar, ila hasemi wazanzibar wamewekeza wapi?
Akili zimejaa urojo naacha kula huu mdebwedo.
 
Kaka usisahau, ukinyosha kidole cha shahada kwa mtu mwingine, vidole 3 vinaelekea kwako mwenyewe!
Waarabu waliofanya biashara ya watumwa (kitu kibaya!) kwa jumla hawakuwinda watumwa (najua kuna mifano ya kinyume, lakini haihusu idadi kubwa), walinunua.
Nani aliuza? Siyo machifu wa bara, "mashujaa" kama Mirambo (aliyekamata watumwa kati ya hao ambao hakuchinja na kuwaweka katika jeshi lake), hata watu binafsi walioenda kushika mabinti waliotembea kukusanya kuni au kuchukua maji mtoni, hadi watu binafi walioamua kumwuza jirani aliyekuwa na madeni? Nenda Bagamoyo , tembelea makumbusho, soma habari za watumwa zilizosimulia maisha yao na jinsi walivyokamatwa na kutendewa.

Tena ni dhahiri si Waarabu wote. Kushtaki kabila au taifa au kundi la watu kwa jumla kwa makosa ya wengine kati yake ni ujinga.
nimezungumza ukweli ambao either utake au usitake, lini mirambo alitoka Tabora akaenda bagamoyo kuuza watumwa?? unaongelea kuhusu kunyoosha kidole kwani mleta mada kasema nini nami nimejibu nini?? Kaongelea kuhusu waarabu nami nimejibu kuhusu waarabu period!!!

sasa ukisoma kwa kukurupuka halafu ukajibu kwa kukurupuka utabaki hivyo hivyo, sina cha kuongeza.


hizo ngozi zote nyeupe hakuna ambae alikuwa na upendo kwa sisi watu weusi, japo kuna wengine ufedhuli wao ulikuwa wa kutisha, lakini yaliyopita si ndwele tusamehe lakini tusisahau na watoto na wajukuu zetu waambiwe ukweli.
 
Niliwahi kwenda stone town nikaona pale watumwa walipokuwa wakihifadhiwa.

Ama kweli waarabu ni watu wema sana.

Waje tu kuwachukua ndugu zao waende nao Oman.
Mleta mada ni Mwarabu wala usijisumbue
 
nimezungumza ukweli ambao either utake au usitake, lini mirambo alitoka Tabora akaenda bagamoyo kuuza watumwa?? unaongelea kuhusu kunyoosha kidole kwani mleta mada kasema nini nami nimejibu nini?? Kaongelea kuhusu waarabu nami nimejibu kuhusu waarabu period!!!

sasa ukisoma kwa kukurupuka halafu ukajibu kwa kukurupuka utabaki hivyo hivyo, sina cha kuongeza.


hizo ngozi zote nyeupe hakuna ambae alikuwa na upendo kwa sisi watu weusi, japo kuna wengine ufedhuli wao ulikuwa wa kutisha, lakini yaliyopita si ndwele tusamehe lakini tusisahau na watoto na wajukuu zetu waambiwe ukweli.
Mirambo alikwenda pwani kabla ya mwaka 1860 (kama Bagamoyo, sijui). Alipokuwa kijana alishiriki mwenyewe katika biashara ya misafara ya ndovu na watumwa. Baadaye akiwa mtema na kupanusha himaya yake alituma misafara.
Alikuwa na nguvu kwa sababu alikuwa na gobori nyingi kwa rugaruga zake. Hakutengeneza, alinunua. Hapa aliuza meno za ndovu na watumwa ili aweze kupata silaha za kushambulia majirani. Pia alilazimisha misafara kutoka pwani kumlipa ushuru mkali. Hakuweka watumwa huru waliopitishwa katika maeneo yake, aliwatumia kupata ushuru.
Je hii ya "rangi" unamaanisha kweli? Mirambo unamruhusu kuvinda na kuuza watumwa (kwa sababu ya rangi yake), lakini Mwarabu ni mbaya kupita kiasi? Vipi kama tutazame wote kama watendaji wa maovu walioendesha biashara hiyo, kama wauzaji na wanunuzi?
 
Waarabu na Wazanzibari ni ndugu wa damu na wa asili kabisa maana Waarabu ndio walioleta ukombizi kwa Taifa la Zanzibar.

Waarabu ndio watu walioweza kuishi kijamii pamoja na Wazanzibari kwa miaka mingi hadi kuchanganya damu na Wazanzibar walio wengi na kuishi km jamii moja tena kwa upendo kabisa.

Waarabu ndio walioipa Nchi ya Zanzibar hadhi na heshima kimataifa na kujulikana kama ni nchi, bila ya Waarabu hata hao Vibaraka CCM-ZANZIBAR wasingeweza kupata nyadhifa mbali mbali za utawala hapo Zanzibar badala yake wangekua tu ni watu dhalili kwenye mkoa wa Tanganyika.

Kwahiyo ni wazi kuwa Waarabu walikuja Zanzibar kwa ajili ya ukombizi na kuwasaidia Wazanzibari waweze kuwa watu wenye hadhi na kuheshimika dunianiani kote.

Mwarabu hivi sasa ndio anaeijenga Zanzibar sijamuona Mtanganyika akija kuekeza Zanzibar sekta muhimu kama bandari kujenga majumba viwanja vya ndege naona mikataba imetiwa na waarabu sijamuona hata mtanganyika mmoja au.

Tusisahau fadhila kwa Uchu wa Madaraka na Njaa. WENYE AKILI WAMESHANIELEWA!!

Na anaebisha Abishe kwa Hoja na sio Porojo
Ngoja na mimi nije niwekeze!
IMG-20220211-WA0037.jpg
 
Ukiachana na historia ya kwenye vitabu, nimepata bahati ya kufika Zanzibar na kutembelea Soko la zamani la watumwa. . .niliyojifunza pale hakika nilisikitika, ndipo nilipoamini Waarabu (wa zama hizo) hawakuwa na utu kabisa, kuanzia kuwachukua watumwa bara na kisha kuwaleta Zanzibar,(enzi hizo bandari ipo Mangapwani) kuwafunga kwenye mti na kuwachapa mijeledi na mtumwa ambae halii ndio anaonekana mkakamavu...

kisha wanapelekwa mpaka sehemu ya kutunzia watumwa (ipo mpaka leo) ambako wanafungiwa kwa siku 3 bila chakula wala maji!!!,(kumbuka minyororo mizito bado mmefungiwa nayo mikononi, miguuni na shingoni) kisha ndio mnatolewa ambao atakutwa amekufa anatupwa na waliobaki wanaenda kuuzwa.

Ikitokea katika kundi la watumwa wa kike wanaouzwa tajiri akitaka “kuonja" alikuwa anachagua mmoja na kumfanyia hiko kitendo hapo hapo hadharani. (kama ambavyo mnafahamu wanaume tulivyo , mwenzako akifanya kitu nawe unataka kufanya, mfano katika kundi mmojà akisogea pembeni na kufungua zipu ili achimbe dawa utakuta wawili watatu wanaungana naye kufanya hivyo, hata walipokuwa wanatwaa mtumwa mmoja wa kike na kumfanyia ushenzi, basi wengine nao waliungana kufanya ufedhuli huo kwa wengine kwenye kundi hilo)

Watumwa waliteswa sana, sana , sana!!! na hao waarabu ambao leo hii watoto wao tunaishi nao kwa amani.

Cha kusikitisha zaidi ni kitendo cha kuwahasi watumwa kiume waliosafirishwa kwenda Arabuni( walienda maelfu lakini mpaka leo hii jiulize kwanini hakuna masalia ya weusi kama sio ukatili wa waarabu ambao waliwahasi bila taratibu za kitabibu, yaani wanakata hizo gololi kisha unapakwa chumvi nyingi, na kutokana na kuvuja damu nyingi wengi walikufa, wachache waliobahatika kupona waliuzwa arabuni kwa hela nyingi, walivyoona wakubwa wanakufa sana basi wakawa wanawahasi watoto).

Bado ambao walikataa utumwa na kuleta uasi njiani waligeuzwa na kuf**lwa mbele ya watoto na wanawake, ili kuwafanya wajisikie majuto, na hata walivyokuwa wanasafiri na majahazi ilikuwa ni desturi ya waarabu kuwachukua watumwa wa kiume na kuwageuza ili kukidhi haja zao.

hivi vyote vilifanyika na historia ipo fika Zanzibar au hata Bagamoyo soko la watumwa uone historia, picha na vithibitisho vingine kuhusu ufedhuli huo waliofanyiwa mababu zetu (leo hii tunacheka nao hakika mababu zetu wakifufuka watasikitika sana).

Dini hizi hizi tulizoletewa tunafundishwa kusamehe waliotukosea, ilhali waliotuletea hizo dini walitufanyia ukatili huku tukishuhudia nasi tunachekelea kama mazombi. Tuishi kwa amani, tupendane na tusonge mbele tukitaka kuleta habari za historia na tuzibebe chuki za mababu zetu basi tutachukiana daima na tutauana.

Japo Muingereza alikomesha utumwa wa waarabu lakini naye alitesa manamba mashambani, Mbelgiji aliua watu wengi kongo, na mkaburu aliangamiza vizazi Afrika kusini, Huu ushenzi tuliofanyiwa waafrika ni mkubwa lakini tumesamehe na tuishi kwa amani bila kubaguana ila!!, nasisitiza tena ila tusisahau na tuwaeleze vizazi vilivyopo na vijavyo namna ambavyo mababu zao walipitia mateso makubwa ya wadhalimu waliokuja ili kutimiza haja za nafsi zao.
Utumwa ulikuwa ni mfumo kama ilivyokuwa Ukoloni nk. Watumwa waliuzwa kwanza na jamii au Tawala zao.

Historia ya watu weupe Zanzibar imeanza na Waajemi baadae Wareno na ndipo walipokuja Waarabu. Uwepo wa Waarabu wa Oman ulitokana na kitendo cha Seyyid Said bin Sultan kuhamishia Makao makuu ya Utawala wake Zanzibar.

Tangu hapo biashara kubwa waliofanya ilikuwa ni Kilimo na mauzo ya karafuu. Biashara ya Utumwa ilikuwepo ndiyo lakini haikuwa msingi Mkuu wa uchumi na ilisimamiwa na mawakala na wanufaika Wakuu walikuwa Wazungu waliokuwa na Mashamba makubwa. Oman kipindi hicho ilikuwa nchi maskini kiasi kwamba wakati Utawala wa Seyyid Majid bin Said ulipojitenga na Oman ilibidi Zanzibar iwe inaipa Ruzuku Oman.

Kwa hiyo kuwaona Waarabu wote kama wafanye biashara ya Utumwa si sahihi na ni mwendelezo wa siasa za chuki zisizo na maana.
 
Utumwa ulikuwa ni mfumo kama ilivyokuwa Ukoloni nk. Watumwa waliuzwa kwanza na jamii au Tawala zao.

Historia ya watu weupe Zanzibar imeanza na Waajemi baadae Wareno na ndipo walipokuja Waarabu. Uwepo wa Waarabu wa Oman ulitokana na kitendo cha Seyyid Said bin Sultan kuhamishia Makao makuu ya Utawala wake Zanzibar.

Tangu hapo biashara kubwa waliofanya ilikuwa ni Kilimo na mauzo ya karafuu. Biashara ya Utumwa ilikuwepo ndiyo lakini haikuwa msingi Mkuu wa uchumi na ilisimamiwa na mawakala na wanufaika Wakuu walikuwa Wazungu waliokuwa na Mashamba makubwa. Oman kipindi hicho ilikuwa nchi maskini kiasi kwamba wakati Utawala wa Seyyid Majid bin Said ulipojitenga na Oman ilibidi Zanzibar iwe inaipa Ruzuku Oman.

Kwa hiyo kuwaona Waarabu wote kama wafanye biashara ya Utumwa si sahihi na ni mwendelezo wa siasa za chuki zisizo na maana.

Thanks
 
Tataizo la Zanzibar ni viongozi wao wa CCM, ulaji na maisha yao yanategemea kuwakwao ndani ya chama hicho. Na chama hichi nguvu yake ni bora.
Viongozi hao wamekuwa wakikitumia chama hiki kupata maisha huko Zanzibar, kikitoka tu madarakani nao maisha watakuwa hawana, hivyo kwao muungano ni maisha bila muungano watakufa.
Wapinzani wa kubwa wa kujitegemea kwa Zanzibar ni waba CCM waliopo Zanzibar.
Wazanzibar mtawazuru watanganyika buree, ilhali tatizo lenu ni CCM Zanzibar. Wao ndo uwaita wanajeshi toka bara ili wawasaidie kuwa madarakani huko.
Lijueni tatizo lilipo ili mpate suluhisho sahihi.
Adui yenu ni wana CCM Zanzibar hukohuko
 
Yaani unawatukuza Waarab makatili, na walio wageuza kuwa Watwana wao miaka nenda! Mpaka pale mlipokuja kukombolewa tarehe 12 January 1964 na yule Mgalatia John Okello, mwenye asili ya Uganda!

Waarabu na Wazanzibari ni ndugu wa damu na wa asili kabisa maana Waarabu ndio walioleta ukombizi kwa Taifa la Zanzibar.

Waarabu ndio watu walioweza kuishi kijamii pamoja na Wazanzibari kwa miaka mingi hadi kuchanganya damu na Wazanzibar walio wengi na kuishi km jamii moja tena kwa upendo kabisa.

Waarabu ndio walioipa Nchi ya Zanzibar hadhi na heshima kimataifa na kujulikana kama ni nchi, bila ya Waarabu hata hao Vibaraka CCM-ZANZIBAR wasingeweza kupata nyadhifa mbali mbali za utawala hapo Zanzibar badala yake wangekua tu ni watu dhalili kwenye mkoa wa Tanganyika.

Kwahiyo ni wazi kuwa Waarabu walikuja Zanzibar kwa ajili ya ukombizi na kuwasaidia Wazanzibari waweze kuwa watu wenye hadhi na kuheshimika dunianiani kote.

Mwarabu hivi sasa ndio anaeijenga Zanzibar sijamuona Mtanganyika akija kuekeza Zanzibar sekta muhimu kama bandari kujenga majumba viwanja vya ndege naona mikataba imetiwa na waarabu sijamuona hata mtanganyika mmoja au.

Tusisahau fadhila kwa Uchu wa Madaraka na Njaa. WENYE AKILI WAMESHANIELEWA!!

Na anaebisha Abishe kwa Hoja na sio Porojo
Wewe aleesha ni Mzanzibari au Muarabu?, tuanzie hapo kwanza...
 
Watanganyika tutakujaje kuwekeza zbar wakati,wanzanzbr wanatubagua!!?, Mtanganyika zbar haruhusiwi kumiliki ardhi , mtanganyika zbar haruhusiwi kuajiriwa ,ondoeni huo ubaguzi uone Kama watanganyika hawajaja kuijenga zbar kuliko hao arabu!
 
Swali gani? Je sio wako Wazanzibari Waafrika, Waarabu, Wahindi - na tangu karne mchanganyiko wa kila aina? Siyo hii ni Zanzibar hasa na sifa yake?
Nimeona ameongelea Wazanzibari na Waarabu, mimi najua ni wote ni Wazanzibari tu labda asili ndio kama ulivyosema.
 
Watanganyika tutakujaje kuwekeza zbar wakati,wanzanzbr wanatubagua!!?, Mtanganyika zbar haruhusiwi kumiliki ardhi , mtanganyika zbar haruhusiwi kuajiriwa ,ondoeni huo ubaguzi uone Kama watanganyika hawajaja kuijenga zbar kuliko hao arabu!

Yaani pori lote lililoko Tanganyika huwezi pata ardhi mpaka uje Zanzibar , punguza kula ugali

IMG-20220216-WA0055.jpg
 
Waarabu na Wazanzibari ni ndugu wa damu na wa asili kabisa maana Waarabu ndio walioleta ukombizi kwa Taifa la Zanzibar.

Waarabu ndio watu walioweza kuishi kijamii pamoja na Wazanzibari kwa miaka mingi hadi kuchanganya damu na Wazanzibar walio wengi na kuishi km jamii moja tena kwa upendo kabisa.

Waarabu ndio walioipa Nchi ya Zanzibar hadhi na heshima kimataifa na kujulikana kama ni nchi, bila ya Waarabu hata hao Vibaraka CCM-ZANZIBAR wasingeweza kupata nyadhifa mbali mbali za utawala hapo Zanzibar badala yake wangekua tu ni watu dhalili kwenye mkoa wa Tanganyika.

Kwahiyo ni wazi kuwa Waarabu walikuja Zanzibar kwa ajili ya ukombizi na kuwasaidia Wazanzibari waweze kuwa watu wenye hadhi na kuheshimika dunianiani kote.

Mwarabu hivi sasa ndio anaeijenga Zanzibar sijamuona Mtanganyika akija kuekeza Zanzibar sekta muhimu kama bandari kujenga majumba viwanja vya ndege naona mikataba imetiwa na waarabu sijamuona hata mtanganyika mmoja au.

Tusisahau fadhila kwa Uchu wa Madaraka na Njaa. WENYE AKILI WAMESHANIELEWA!!

Na anaebisha Abishe kwa Hoja na sio Porojo
Waarabu ndio walioleta biashara ya utumwa Znz na Tanganyika hao wazanzibar weusi ndio waliokuepo ni watumwa kipindi cha utumwa.
 
Ni kweli maneno yako siwezi kubadili historia lakini la kusikitisha historia tunaiona inajirudia kila baada ya miaka mitano . Tunawaona akina Mahita , Kikwete, Mwinyi nk.wanavyotufanyia . Sio wote lakini wengi wako hivyo . Wako wachache sana akina Ponda vitendo vyao tunaviona vya kupigania haki , na hao walipigwa risasi na kuwekwa jela na hao viongozi wa Kiislamu. Hayo mapenzi ni povu la mdomo na hapa kwenye kioo. ACTIONS SPEAK LOUDER THAN WORDS
Mimi nakuelewa sana, na tatizo naloliona hutaki kuwataja waznz ambao ndio sehemu ya uharibifu wa znz, hutaki kuwashutumu walevi wa kiunguja na kipemba ambao ni sehemu ya uharibifu wa znz. Kwa mfano chanzo wa kikamatwa mashekhe wa uamsho ni waislam wa znz.

Lkn unawajeshimu kwa sababu ya uznzr wao pamoja ni walevi baadhi yao na kuwakashifu waisalam wa Tanganyika kuwa si lolote zaidi ya utanganyika wao.

Kubwa pemgine una upofu wa kutoelewa chanzo cha tatizo na kuwa na uoni huo finyu.

Nirejee lengo la historia si kuisoma na kujitengenezea chuki. Laa, Bali lengo kubwa la historia ni kujua matatizo na mafanikio ya nyuma ili Mimi na wewe tuweze kuiandika historia mpya itakayosomwa na vizazi.

Sasa hiyo mifano ya majina ya kiislam uliyoitaja waliyoyafanya hatuwezi kuyabadili. Lkn wanayoyafanya sasa sisi tunaweza kuyabadili.

Na ili uweze kubadili kwanza tujue chanzo cha tatizo hadi kuwa wako tayari kushirikiana na waislam wenziwao ambao ni waznz kuwaletea mateso na ukatili kwa waznz wasio na hatia. Je tatizo ni utanganyika.?!?!

Binafsi kwa utafiti mdogo nilioufanya na naoendelea kuufanya naamini tatizo si utanganyika.

Bali Ujamaa. Mwalimu Nyerere ktk maono yake alipata kutamka kuwa ujamaa ni imani. Na kama tunavyojua dini ni imani na hivyo ujamaa ni dini.

Hivyo kauli ya mzee Nyereee hakukurupuka. Kwani asili ya ujamaa ni ukomunist. Na ukomonist ni imani isiyoamini uwepo wa Mungu. Na kwamba wanaamini dini zinatokana na ufinyu wa kufikiri wa mwanadamu. Hivyo kutokana na uanzishwaji na uwepo was imani hii ya ukomonist (ujamaa ). waislam pia waliathiriwa na wanaendelea kuathiriwa na imani hii.

Na ili kukata mzizi was fitna serikali ikapigilia msumari kuwa serikali ya ccm haiamini Mungu na hivyo haiamini dini.

Huu ndio msingi was imani ya Ujamaa.

Kwa hiyo ukiniuliza kwa nini waislam was Tanganyika na wa znz walishiriki uhalifu na bado wanaendelea kushiriki uhalifu kwa jimbo LA znz, nitasema tatizo ni imani ya ujamaa.

Iliyowalevya na kuutumikia ujamaa zaidi kuliko imani ya asili yao (uislam) na kuwaona wapinga ujamaa na wasioshiriki imani ya ujamaa ni maadui zaidi kuliko watu wengine.

Sasa kama nawe uko ktk chama. Na misingi ya chama hicho ni itikadi ya ujamaa. Wewe nawe utaendelea kuwaona waislam wa Tanganyika ni maadui kwenu.

Kinyume chake tunaweza kuandika historia mpya. Kwa kuikataa itikadi ya kijamaa.

Kama kuna maeneo ndani ya znz ambapo muislam mtanganyika hawezi kupewa mke kwasababu yeye ni mtamganyika wao pia wameathiriwa na itikadi ya ujamaa.

Kwa kifupi ujamaa umeshindwa na ni adui yetu namba 1 tunaepaswa tumuondoe.

Tunaweza kuishi bila ujamaa kama ndio msingi wa itikadi yetu, pia tunaweza kuishi bila ubepari kuwa ni msingi wa itikadi yetu pale watu wema watakapoamua kushiriki siasa. Na kuanchana na wahuni na wajamaa watuongoze.

Watu wema wapo tz bila kujali imani wetu. Kwani ktk ulimwengu huu ambapo kuna makundi ya watu wenye mchanganyiko wa utamaduni na imani huwezi kujifungia na kudhani utaweza kuishi na watu wenye imani yako pekee. Huku bara hata baadhi ya misikiti inaajiri walimzi wa viatu wa imani nyengine. Maadamu hatuwashinikizi waamini tunayoyaamini sisi, wala wao hawatulazimishi tuamini wanayoyaamini wao.

Nimalizie kwa maneno machache ya kimombo yanayitofautisha aina za watu hapa duniani.
1. Kundi la Whats happen
2. Lets happen
3. Makes happen.

Kundi no 1. Linakuhusu unapemda kufatilia nini kimetokea.

Kundi no 2 ndio watz wengi wengine na hasa waswahili wao ni hewawa wacha yatokee.

Kundi no 3 wako wachache, wao wanataka kutengeza historia mpya. Ndugu yangu napenda ubadili ubongo wako ufikiri kama wanavyofikir Kundi la 3.

Kinyume chake nitakuweka ktkt kundi lililotengenezwa hadi kuzuzuka.

Nini maoni yako.
 
Back
Top Bottom