Ulishawahi kupatanisha changamoto ya ziada katika ndoa ambayo haina mtoto/watoto? Hii inahitaji hekima na busara nyingi sana

Ulishawahi kupatanisha changamoto ya ziada katika ndoa ambayo haina mtoto/watoto? Hii inahitaji hekima na busara nyingi sana

Hii misimamo ya hivi huwa imekaa kibinafsi sana ingawa n mizuri kwa muhusika
Binafsi kwangu furaha ya viumbe nilowaleta duniani naipa kipaombele sana .kuna namna watoto walolelewa na wazazi wote wawili hujengeka,labda itokee mzazi mmoja ametangulia mbele za haki...familia ni nguzo aise hasa kwa walio na hofu ya Mungu

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app

Yah ni ya kibinfsi sababu usipokuwa mbinafsi na furaha yako kitakachotokea ni kwenda kuwaamishia stress zako watoto..

Umesalitiwa na mwenzako ila hasira zako unaendea kumalizia kwa mtoto aliyefanana na mumeo.

Kitu kidogo unapiga mtoto mpk unategua mguu ukiulizwa nina stress..


Sijui km unajua kulea ni kazi?na hapa sizungumzii kulisha mtoto ambaye kwa mwezi ht kilo 10 hawezi maliza.Nazungumzia ukomavu wa kihisia wakulea mtoto na mtoto akajifunza kitu kutoka kwa baba au mama yake,mtoto akakua akiwa na haiba nzuri...

Huwezi kuniambia nipo busy kulea mtoto wakati mama yao ameshanipa kidonda ambacho siwezi kupona nikiwa nae.Kila mtu ana kiwango chake cha kuvumilia changamoto,changu kikifika watoto hawatasaidia kitu.

Tupo tunakula baba nimenuna au tunaangalia tv siongei kitu na mke wangu sasa unawafundisha nini watoto yaani kipi hasa wanachojifunza kwa kuwa na wazazi wawili????Watoto wanahitaji kuona baba na mama wanafuraha,wanacheza mziki pamoja mbele yao,wanapiga story huku wanacheka kwa furaha.Hiko ndo watoto wanataka kuona na sio sura ya baba yenye hasira mda wote au mama mwenye majonzi mda wote.Mnawatisha tu na kuona maisha ni mabaya.

Tatizo langu sio ubinafsi tatizo langu ni i am very genuine nitakuvumilia nachoweza kukuvumilia ukivuka mstari sitawaza mara mbili.Naacha familia hata ya watoto 50 naenda ku enjoy maisha yangu tutakutana kwenye matunzo.
 
Ndoa inakuwa ngumu sana km haina mtoto, kuna rafiki yangu alimuuliza mumewe mbona unachelewa sana kurudi home mumewe alimwambia niwahi kurudi ntacheza na nani hapa nyumbani.Daah alinipigia simu analia na walikaa bila ya mtoto miaka 6. Lakini sasa hv wana watoto wawilli.
 
Habari za muda huu waungwana wa jamiiforums

Kupatanisha changamoto ya ziada katika ndoa ambayo haina mtoto hata mmoja, kunahitaji hekima na busara nyingi sana.

Hakuna ndoa yoyote hapa duniani ambayo ni rahisi kuipatanisha kwa maana kila ndoa ina changamoto zake, lakini ukweli wa mambo ni kwamba ndoa zisizo na watoto ni ngumu sana kuzipatanisha (kukitokea changamoto ya ziada) kuliko zile zenye watoto wengi au walau mtoto mmoja.

Kupatanisha ndoa iliyodumu kwa muda wa miaka 7 bila mtoto alafu iibuke changamoto nyingine mpya (ambayo inaweza kuwa ya kawaida katika ndoa zote hata zile zenye watoto) kama vile baba kuchelewa kurudi kazini, inahitaji hekima na busara ya hali ya juu sana.

Kwanini ninasema hekima kubwa inahitajika katika kupatanisha changamoto za ziada katika ndoa isiyo na watoto? Kwa utafiti mdogo nilioufanya kwa miaka kadhaa nyumba mpaka sasa nimegundua ya kwamba, ndugu na marafiki wengi wanaoitwa kwenda kusikiliza changamoto za ndoa yoyote ile, hukimbilia kwa watoto kama ngao ya kutaka baba na mama (wanandoa) wasitengane bali waendelee kuishi.

Hahahahaaaa unacheka? Unafikiri ninatania mkuu. This is very true my friend. Watu wengi wanaokwenda katika vikao hivi vya upatanishi hukimbilia kuwaambia wanandoa ya kwamba "Sasa Infantry Soldier na Bushmamy mkiachana leo hii, hawa watoto wenu watano wataishi vipi?"

"Sawa nyie watu wazima mnaweza mkawa na chuki zenu, lakini vp kuhusu future ya watoto jamani Soldier? Ina maana unataka kutengana na Bushmammy kisa tu chai ameiunga kwa nazi? Labda ndio mapishi yao huko Tanga mvumilie tu atabadilika taratibu" Hahahahaaaa, I'm joking, lakini bila shaka umepata mantiki yangu?

Watoto/Mtoto hutumiwa kama ngao ya kuzifanya ndoa nyingi ziendelee kuwa hai lakini licha ya ukweli kwamba baba na mama kila mmoja anakuwa analala chumba chake huko ndani au wanalala chumba kimoja lakini mwingine anatandika godoro chini.

Kama mtoto anatumika kama ngao kwenye ndoa zilizobahatika kupata walau mmoja, sasa zile ambazo zimekaa miaka 7 hazina kabisa unafanyaje kusuluhisha changamoto ya zaida inapojitokeza?

Ni ngumu sana ndugu zangu. Yaaani ni ngumu kweli kweli. Inahitaji watu wenye hekima na busara level ya ndugu zangu Kiranga na Mshana Jr ndio wanaoweza kunusuru ndoa za namna hii. vinginevyo labda Mungu pekee ndiye aingilie kati.

OMBI LANGU: Mungu tunakuomba uendelee kuwapa moyo wa uvumilivu na subira wanandoa wote ambao mpaka sasa hawajapata watoto/mtoto katika maisha yao na waamini ipo siku wewe kama muweza wa yote utawafungulia milango ya baraka na kuwapa hitaji hilo la mioyo yao kama ulivyomfanyia Sarah, mke wa Ibrahim. Amen.

Maoni ya wadau;
==========


USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
OMBI LANGU: Mungu tunakuomba uendelee kuwapa moyo wa uvumilivu na subira wanandoa wote ambao mpaka sasa hawajapata watoto/mtoto katika maisha yao na waamini ipo siku wewe kama muweza wa yote utawafungulia milango ya baraka na kuwapa hitaji hilo la mioyo yao kama ulivyomfanyia Sarah, mke wa Ibrahim. Amen.[emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545]
 
Kuna watoto wengi hawana baba wala mama huko mitaani watu wa adopt waache kukariri maisha
Kibongo bongo bado sana..kwanza hizo process, pili utapigiwa makelele na familia hadi uone maisha mabaya utaambiwa kuna ndugu wengi tu saidia hao. Jamii yetu bado sana kukubali mtoto 'asiyejulikana'. Tuna safari ndefu.
 
Nimeshahudhuria kesi za ndoa kadhaa na mwalimu wangu,huku mimi nikiwa mbeba vitabu vya marejeo. Kwetu sisi hakuna changamoto ya ndoa ambayo haijaandikiwa kitabu.

Wanandoa wengi hawajui ni watu gani sahihi wa kuwapelekea matatizo yao. Hili hupelekea au limepelekea ndoa nyingi sana kuvunjika kwa mambo ambayo ukiyaweka katika mizani ya haki hayakidhi vigezo vya kuachana.

Suala la kutopata mtoto kwalo huwa ni nje ya uwezo wa husika, ni jambo la kawaida na linataka subira sana na wanandoa wenyewe kuwa na msimamo madhubuti,hasa wahusika wakijua ya kuwa maisha si kupata mtoto au kukosa mtoto,bali kuna lengo la ndoa yaani utulivu na watoto ni natija ya ndoa. Wapo walio kaa bila mtoto zaidi ya miaka 14 na mwisho wa siku wakaja kuruzukiwa mtoto. Walipitia changamoto nyingi sana ila miongoni mwa sababu zilizo wasaidia pakubwa walikuwa ni watu wa dini sana. Yaani wanajua nini maana ya makadirio na nini maana ya uvumilivu.

Naendelea ....
 
OMBI LANGU: Mungu tunakuomba uendelee kuwapa moyo wa uvumilivu na subira wanandoa wote ambao mpaka sasa hawajapata watoto/mtoto katika maisha yao na waamini ipo siku wewe kama muweza wa yote utawafungulia milango ya baraka na kuwapa hitaji hilo la mioyo yao kama ulivyomfanyia Sarah, mke wa Ibrahim. Amen.[emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545]
Thanks bro.
 
Kibongo bongo bado sana..kwanza hizo process, pili utapigiwa makelele na familia hadi uone maisha mabaya utaambiwa kuna ndugu wengi tu saidia hao. Jamii yetu bado sana kukubali mtoto 'asiyejulikana'. Tuna safari ndefu.
Wabongo wengi bado ni washamba sana linapokuja suala zima la kusaidia watoto yatima pamoja na kuwafanya adoption.
 
Nimeshahudhuria kesi za ndoa kadhaa na mwalimu wangu,huku mimi nikiwa mbeba vitabu vya marejeo. Kwetu sisi hakuna changamoto ya ndoa ambayo haijaandikiwa kitabu.

Wanandoa wengi hawajui ni watu gani sahihi wa kuwapelekea matatizo yao. Hili hupelekea au limepelekea ndoa nyingi sana kuvunjika kwa mambo ambayo ukiyaweka katika mizani ya haki hayakidhi vigezo vya kuachana.

Suala la kutopata mtoto kwalo huwa ni nje ya uwezo wa husika, ni jambo la kawaida na linataka subira sana na wanandoa wenyewe kuwa na msimamo madhubuti,hasa wahusika wakijua ya kuwa maisha si kupata mtoto au kukosa mtoto,bali kuna lengo la ndoa yaani utulivu na watoto ni natija ya ndoa. Wapo walio kaa bila mtoto zaidi ya miaka 14 na mwisho wa siku wakaja kuruzukiwa mtoto. Walipitia changamoto nyingi sana ila miongoni mwa sababu zilizo wasaidia pakubwa walikuwa ni watu wa dini sana. Yaani wanajua nini maana ya makadirio na nini maana ya uvumilivu.

Naendelea ....
Umeandika msaafu mrefu duuuh
 
Back
Top Bottom