Umewahi kukutana ana kwa ana na mnyama gani mkali?

Umewahi kukutana ana kwa ana na mnyama gani mkali?

Mimi kuna siku niko na Pikipiki nimetoka site huko nyengedi napanda Milima ya rondo mida ya saa 2 usiku aisee Mara simba huyu hapa nilianguka na Pikipiki nikainyanyua sikugeuka nyuma nilipofika kijijini palepale nilizimia.

Kuna siku tena natoka makangaka naelekea kiranjeranje kupanda basi saa 12 Asbh niko na miguu aisee ghafla naona simba dume na jike huwez amini simba Walikuwa hawana njaa walinisindikiza ila Mimi begi nilitupa na Viatu nilikimbia baadae akaja jamaa wa baiskeli aliokota viatu na begi kauliza nani mwenye begi nikamtajia vitu vilivyopo ndani kitambulisho na nguo akanipa begi.

Kuna siku tena niko speed natoka kinyope nakuja Rutamba pale katikati chui huyu hapa kainua miguu aisee nilinyosha wanguwangu akaruka pembeni.

Siku nyingine tuko na gari Tukaona tembo wanne ruangwa wanapita.

Kiboko ashanikosa kwenye mtumbwi mto ruvuma daraja la mkenda.hakuwa na mtoto alikuwa anaibuka nasikia akiwa na mtoto ndo anakuwa mkali.

Nyoka ndo sana barabarani nishkutana nao zaidi ya Mara tatu ila wadogo wadogo sijawahi kukutana na joka kubwa na kuna siku tumekaa kwenye mti ghafla nyoka kadondoka.

Aisee tunaoishi huku lindi tumepakana karibu sana na pori kubwa la selous yaani tunapocheza Cheza huku njiani tunakutana na viumbe machachari hapa ninahamu tu kuja kukutana na mamba live ndo sijawahi kumuona.
Siku Uje Huku Nachingwea kijiji cha Kilimarondo uone Tembo wanacheza na wanakijiji bila Shida
 
Mwaka 1959 niko machungani kijijini Ng'waukoli nikasikia mbuzi wanapiga makelele sana na mikikimikiki mingi wakizunguka jiwe fulani hivi. Kwenda kuangalia nikakutana uso kwa uso na chui. Niliganda pale pale maana ningepiga hatua tatu nne hivi ningemfikia. Basi tulibaki tumetazamana pale tu mara huyo akanyanyuka na kwenda zake pole pole bila shari yo yote. Inavyoonekana alikuwa ni jike na alikuwa na mimba karibu kabisa ya kujifungua.

Ni miaka zaidi ya 60 imepita lakini sijasahau tukio lile maana huyu mwamba akikuamria kukutoboa koo ni sekunde tu. Mungu ni mwema!

Screenshot_20240203_162043_Samsung Internet.jpg
 
Nilikoswa koswa na nyoka nimeenda Kwa jirani kama saa moja hiv wakat naingia nasikia kitu kinafoka sikuwa na toch na umeme ulikuwa hakuna nikasimama bahat nzuri walikuwa na tochi wakamulika aisee bonge la joka wakamuua hatujakaa vizuri mwingine anakuja wakamuua nae nafikir ni wale wanatembeaga wawili wawil
Vifutu hao, wana tabia ya kuwa wawili wawili.. Shamba nishaua mara kadhaa
 
Mimi kuna siku niko na Pikipiki nimetoka site huko nyengedi napanda Milima ya rondo mida ya saa 2 usiku aisee Mara simba huyu hapa nilianguka na Pikipiki nikainyanyua sikugeuka nyuma nilipofika kijijini palepale nilizimia.

Kuna siku tena natoka makangaka naelekea kiranjeranje kupanda basi saa 12 Asbh niko na miguu aisee ghafla naona simba dume na jike huwez amini simba Walikuwa hawana njaa walinisindikiza ila Mimi begi nilitupa na Viatu nilikimbia baadae akaja jamaa wa baiskeli aliokota viatu na begi kauliza nani mwenye begi nikamtajia vitu vilivyopo ndani kitambulisho na nguo akanipa begi.

Kuna siku tena niko speed natoka kinyope nakuja Rutamba pale katikati chui huyu hapa kainua miguu aisee nilinyosha wanguwangu akaruka pembeni.

Siku nyingine tuko na gari Tukaona tembo wanne ruangwa wanapita.

Kiboko ashanikosa kwenye mtumbwi mto ruvuma daraja la mkenda.hakuwa na mtoto alikuwa anaibuka nasikia akiwa na mtoto ndo anakuwa mkali.

Nyoka ndo sana barabarani nishkutana nao zaidi ya Mara tatu ila wadogo wadogo sijawahi kukutana na joka kubwa na kuna siku tumekaa kwenye mti ghafla nyoka kadondoka.

Aisee tunaoishi huku lindi tumepakana karibu sana na pori kubwa la selous yaani tunapocheza Cheza huku njiani tunakutana na viumbe machachari hapa ninahamu tu kuja kukutana na mamba live ndo sijawahi kumuona.
Siku niko selous ndani huko mahenge balaa kwanza jamaaa.
 
Nikiwa A level Simiyu huko natoka Dormitory niende class kusoma ilikuwa saa nane nilikutana na Fisi kama watatu uzuri wanazengo walishatuambia Fisi wa kawaida huwezi kukutanan nae ila wa kufugwa unakutana nae na kama hajatumwa kwako hakudhuru kwa hiyo nilisimama tu wakapita nikaenda Class kupiga shule
Meatu au bariadi?
 
Mwaka 1959 niko machungani kijijini Ng'waukoli nikasikia mbuzi wanapiga makelele sana na mikikimikiki mingi wakizunguka jiwe fulani hivi. Kwenda kuangalia nikakutana uso kwa uso na chui. Niliganda pale pale maana ningepiga hatua tatu nne hivi ningemfikia. Basi tulibaki tumetazamana pale tu mara huyo akanyanyuka na kwenda zake pole pole bila shari yo yote. Inavyoonekana alikuwa ni jike na alikuwa na mimba karibu kabisa ya kujifungua.

Ni miaka zaidi ya 60 imepita lakini sijasahau tukio lile maana huyu mwamba akikuamria kukutoboa koo ni sekunde tu. Mungu ni mwema!

View attachment 2892997
Hivi ukiganda tu hakufanyi chochote?
 
Back
Top Bottom