Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Panafanana na Same haponimetoka kuua hili dude masaa machache yaliyopitaView attachment 2892845
Oya hamieni PM mnaharibu uziOooh ni mda sana aiseee duuuh
Basi sasa hivi huku ni lami mpaka pwani kule.....
Pia watu wamejua kujenga an kiufupi hutojutia kuja kivinjeni...
Mji umeendelea sana sana
Siku Uje Huku Nachingwea kijiji cha Kilimarondo uone Tembo wanacheza na wanakijiji bila ShidaMimi kuna siku niko na Pikipiki nimetoka site huko nyengedi napanda Milima ya rondo mida ya saa 2 usiku aisee Mara simba huyu hapa nilianguka na Pikipiki nikainyanyua sikugeuka nyuma nilipofika kijijini palepale nilizimia.
Kuna siku tena natoka makangaka naelekea kiranjeranje kupanda basi saa 12 Asbh niko na miguu aisee ghafla naona simba dume na jike huwez amini simba Walikuwa hawana njaa walinisindikiza ila Mimi begi nilitupa na Viatu nilikimbia baadae akaja jamaa wa baiskeli aliokota viatu na begi kauliza nani mwenye begi nikamtajia vitu vilivyopo ndani kitambulisho na nguo akanipa begi.
Kuna siku tena niko speed natoka kinyope nakuja Rutamba pale katikati chui huyu hapa kainua miguu aisee nilinyosha wanguwangu akaruka pembeni.
Siku nyingine tuko na gari Tukaona tembo wanne ruangwa wanapita.
Kiboko ashanikosa kwenye mtumbwi mto ruvuma daraja la mkenda.hakuwa na mtoto alikuwa anaibuka nasikia akiwa na mtoto ndo anakuwa mkali.
Nyoka ndo sana barabarani nishkutana nao zaidi ya Mara tatu ila wadogo wadogo sijawahi kukutana na joka kubwa na kuna siku tumekaa kwenye mti ghafla nyoka kadondoka.
Aisee tunaoishi huku lindi tumepakana karibu sana na pori kubwa la selous yaani tunapocheza Cheza huku njiani tunakutana na viumbe machachari hapa ninahamu tu kuja kukutana na mamba live ndo sijawahi kumuona.
Aiseeee, umetumia nini kuliua?nimetoka kuua hili dude masaa machache yaliyopitaView attachment 2892845
Vifutu hao, wana tabia ya kuwa wawili wawili.. Shamba nishaua mara kadhaaNilikoswa koswa na nyoka nimeenda Kwa jirani kama saa moja hiv wakat naingia nasikia kitu kinafoka sikuwa na toch na umeme ulikuwa hakuna nikasimama bahat nzuri walikuwa na tochi wakamulika aisee bonge la joka wakamuua hatujakaa vizuri mwingine anakuja wakamuua nae nafikir ni wale wanatembeaga wawili wawil
Umemuonea ru huyonimetoka kuua hili dude masaa machache yaliyopitaView attachment 2892845
Hii sio Ruaha Mitaa ya Tungamalenga huko?nimetoka kuua hili dude masaa machache yaliyopitaView attachment 2892845
Siku niko selous ndani huko mahenge balaa kwanza jamaaa.Mimi kuna siku niko na Pikipiki nimetoka site huko nyengedi napanda Milima ya rondo mida ya saa 2 usiku aisee Mara simba huyu hapa nilianguka na Pikipiki nikainyanyua sikugeuka nyuma nilipofika kijijini palepale nilizimia.
Kuna siku tena natoka makangaka naelekea kiranjeranje kupanda basi saa 12 Asbh niko na miguu aisee ghafla naona simba dume na jike huwez amini simba Walikuwa hawana njaa walinisindikiza ila Mimi begi nilitupa na Viatu nilikimbia baadae akaja jamaa wa baiskeli aliokota viatu na begi kauliza nani mwenye begi nikamtajia vitu vilivyopo ndani kitambulisho na nguo akanipa begi.
Kuna siku tena niko speed natoka kinyope nakuja Rutamba pale katikati chui huyu hapa kainua miguu aisee nilinyosha wanguwangu akaruka pembeni.
Siku nyingine tuko na gari Tukaona tembo wanne ruangwa wanapita.
Kiboko ashanikosa kwenye mtumbwi mto ruvuma daraja la mkenda.hakuwa na mtoto alikuwa anaibuka nasikia akiwa na mtoto ndo anakuwa mkali.
Nyoka ndo sana barabarani nishkutana nao zaidi ya Mara tatu ila wadogo wadogo sijawahi kukutana na joka kubwa na kuna siku tumekaa kwenye mti ghafla nyoka kadondoka.
Aisee tunaoishi huku lindi tumepakana karibu sana na pori kubwa la selous yaani tunapocheza Cheza huku njiani tunakutana na viumbe machachari hapa ninahamu tu kuja kukutana na mamba live ndo sijawahi kumuona.
Meatu au bariadi?Nikiwa A level Simiyu huko natoka Dormitory niende class kusoma ilikuwa saa nane nilikutana na Fisi kama watatu uzuri wanazengo walishatuambia Fisi wa kawaida huwezi kukutanan nae ila wa kufugwa unakutana nae na kama hajatumwa kwako hakudhuru kwa hiyo nilisimama tu wakapita nikaenda Class kupiga shule
Ni wanene alafuVifutu hao, wana tabia ya kuwa wawili wawili.. Shamba nishaua mara kadhaa
MaswaMeatu au bariadi?
Hivi ukiganda tu hakufanyi chochote?Mwaka 1959 niko machungani kijijini Ng'waukoli nikasikia mbuzi wanapiga makelele sana na mikikimikiki mingi wakizunguka jiwe fulani hivi. Kwenda kuangalia nikakutana uso kwa uso na chui. Niliganda pale pale maana ningepiga hatua tatu nne hivi ningemfikia. Basi tulibaki tumetazamana pale tu mara huyo akanyanyuka na kwenda zake pole pole bila shari yo yote. Inavyoonekana alikuwa ni jike na alikuwa na mimba karibu kabisa ya kujifungua.
Ni miaka zaidi ya 60 imepita lakini sijasahau tukio lile maana huyu mwamba akikuamria kukutoboa koo ni sekunde tu. Mungu ni mwema!
View attachment 2892997
Yes, wanene, sio warefu saana, rangi kama chatu au majani yaliyokauka.Ni wanene alafu