Umoja wa Israel na Marekani uko sawa na ule wa Ujerumani na Austria 1914

Umoja wa Israel na Marekani uko sawa na ule wa Ujerumani na Austria 1914

  1. Coincidence za matukio ya WWI ndizo zinahitimisha kwamba Sasa Kuna WWIII.
  2. Kwamba kudharau UN resolutions ndipo kunapelekea WW. UN resolutions hazijaanza kudharauliwa Leo Wala Jana. Mfano, Mwaka 2001 UN iliizuia US isivamie Iraq lakini Marekani alikiuka.
Japokuwa naamini (ndivyo inavyoaminika) WWIII itaanzia mashariki ya kati, lakini siamini kama vita itatokea Kwa mtiririko ule ule wa matukio ya 1900s (kama sijakuelewa vibaya).

US na Israel Wana mkataba wa kudumu wa kusaidiana katika shida na Raha. Israel ni mnufaika Namba Moja wa misaada ya kijeshi kutoka US (kiufundi, latest tech ya zana za kivita, nguvukazi za wanajeshi, budget ktk masuala ya ulinzi na usalama, n.k). Mwaka jana, baada ya shambulio la 2023 October 7, Marekani iliongeza budget (mpaka kufikia Us $ 12 billion) kuisaidia Israel kujiimarisha zaidi ktk medani za kivita.
Kwa hiyo, nionavyo Mimi, ili vita ya WWIII ili ije kuwa rasmi ni pale Israel atakapozidiwa na hatimaye US kuingilia kati yeye kama yeye ili kumlinda Mtoto wake ; hapo Sasa wale mahasimu wa US nao hawatakuwa mbali na mchezo wa piga nikupige.
Unataka USA afanyeje ili uamini kwamba ndie anayewapiga Iran, Hezzibollah, Hamas na Houthi

Hizi vita zote ukijumuisha na Ukraine Marekani ndio Injinia
 
  1. Coincidence za matukio ya WWI ndizo zinahitimisha kwamba Sasa Kuna WWIII.
  2. Kwamba kudharau UN resolutions ndipo kunapelekea WW. UN resolutions hazijaanza kudharauliwa Leo Wala Jana. Mfano, Mwaka 2001 UN iliizuia US isivamie Iraq lakini Marekani alikiuka.
Japokuwa naamini (ndivyo inavyoaminika) WWIII itaanzia mashariki ya kati, lakini siamini kama vita itatokea Kwa mtiririko ule ule wa matukio ya 1900s (kama sijakuelewa vibaya).
Kuna utafiti ulifanywa na Prof Graham T Allison wa Harvard University na kuunda nadharia iitwayo The Thucydides Trap akifanyia tafiti chanzo cha vita baina ya madola ya kale ya Sparta na Athene (The Peloponessian War), iliyotokea miaka zaidi ya 2000 iliyopita.

Katika tafiti hii, alipitia vita kubwa zilizotokea miaka 500 iliyopita tokea mwaka 1500 hadi 2000 na kufahamu kwamba taifa dogo linapoanza kukua kiuchumi na kuanza kutishia mustakabali wa dola lenye nguvu duniani kwa wakati huo ni lazima vita itokee.

Tafiti yake inaonesha Case Study ya mataifa 16 makubwa, na kuangalia chanzo cha mvutano wao. Mara zote chanzo zimekuwa taifa dogo linalokuwa (Rising Power) kuanza kutishia taifa ambalo linatawala kwa wakati huo (Rulling Power). Ni mara nne tu katika hizo Case Study 16 ambapo mataifa yalikubali kukaa chini na kuelewana na kuzuia vita kubwa.

The Franco Prussian War 1871
-France (Rulling Power) vs Imperial Germany (Rising Power)

First World War 1914
- Great Britain (Rulling Power) vs Imperial Germany (Rising Power)

Second World War 1939
- Great Britain (Rulling Power) vs Nazi Germany (Rising Power)

Kiufupi sababu za vita kubwa huwa ni zilezile The Balance of Power.
Thucydides Trap.png
 
"History doesn't repeat itself but it often ryhmes" Mark Twain

Kabla ya mwaka 1914, Ujerumani na Austro-Hungary walikuwa ni mataifa ambayo hayawezi kutenganishwa kwa lolote lile. Mkubwa alikuwa Ujerumani na mdogo alikuwa ni Austria.

Austro-Hungary lilikuwa ni taifa linalotawaliwa na familia ya Habsburg (The Habsburg Family) ambayo pia ndiyo familia iliyokuwa inatawala dola la rumi takatifu almaarufu kama The Holy Roman Empire kwa miaka zaidi ya 500.

The Habsburg Family ilikuja kudidimia na dola lao la rumi kuanguka na kubakiwa na nchi ndogo yenye mipaka midogo ya Austro-Hungary. Ujerumani kama taifa ilizaliwa mwaka 1871, na baada ya hapo ilishikamana na Austria wakiwa na imani kwamba Austria ni ndugu zao wa damu.

Austro-Hungary ilikuwa na mikakati ya kutawala makoloni yake ya Ulaya Mashariki ambako watu wengi ni Slavic, tena wenye dini tofauti. Jambo baya ni kwamba Austro-Hungary aliamini kabisa kwamba wao walikuwa na haki kutoka kwa MUNGU ya kutawala eneo lote la Ulaya hasahasa maeneo yaliyowahi kuwa sehemu ya The Holy Roman Empire.

Austro-Hungary aliyakalia maeneo kama Serbia, Slovenia, Croation, Bosnia na Herzegovina ambayo baadaye yalikuja kuunda taifa liitwalo Yugoslavia. Slavic People walianza harakati za kudai uhuru kwa njia ya vurugu dhidi ya Austro-Hungary na kupelekea machafuko na umwagikaji mkubwa wa damu.

Slavic People waliungwa mkono na taifa kubwa la kislav la Urusi, ambalo lilikuwa ni adui mkubwa wa Ujerumani na Austro-Hungary. Hivyo Urusi akawa anawatumia Slavs walioko ndani ya dola la Austro-Hungary na Ottoman Empire kuleta taharuki.

Ikumbukwe, mwaka 1914, wanaharakati wa kundi la kigaidi na wadai uhuru wa Kislavic liitwalo The Black Hand lilifanya mauaji ya mwana mfalme wa Austro-Hungary, Archduke Ferdinand alipoenda kufanya matembezi kwenye makoloni hayo. Kijana mdogo aitwayo Gavrilo Princip alimuua Ferdinand na mke wake Sophia na kusababisha vita ya kwanza ya dunia.

=============================================
Uhusiano wa hiyo nadharia yangu ya hapo juu, unafanan na kile kinachoendelea leo duniani, hasahasa kule Mashariki ya kati, ambapo Marekani ndiyo Ujerumani ya leo na Israeli ndiyo Austro-Hungary.

Ujerumani lilikuwa ni taifa lenye nguvu zaidi za kijeshi barani Ulaya kwa wakati ule na lilikuwa ndilo linamkingia kifua Austro-Hungary alipotishiwa na Urusi na mataifa mengine ya Ulaya.

Austro-Hungary kama Israel, walikuwa wanaamini kwamba maeneo yaliyowahi kuwa ya The Holy Roman Empire na The Habsburg Empire ni lazima yarudishwe na kuendelewa kushawishiwa kwa namna yoyote hata kama jambo hilo lingezua taharuki. Habsburg waliamini kabisa walikuwa na haki kutoka kwa MUNGU maana miaka ya nyuma watawala wake walipakwa mafuta na Papa wa Vatican ili watawale Ulaya nzima. Haya mawazo yaliendelea kuwakaa hata baada ya falme zao kuanguka.

The Black Hand, walikuwa ni wapigania uhuru wa Bosnia waliotumia mbinu za kigaidi dhidi ya Austro-Hungary ambayo ilikuwa inatawala nchi yao na kusema kwamba ni haki yao ya KIMUNGU kufanya hivyo. Unaweza kudhani walikuwa wanatania lakini kwa kipindi hicho, watu wengi waliamini kabisa The Habsburg walichaguliwa na MUNGU kutawala Ulaya yote hasahasa kupambana na dola la kiislamu la Uturuki almaarufu kama The Ottoman Empire.

Hivyo, binafsi nalifananisha kundi la The Black Hand, kama makundi ya Hamas, Hezbollah na PLO, ambayo yanaamini kabisa yanapigania uhuru wao na kutumia mbinu za kigaidi kupata huo uhuru. Lakini upande wa pili, haya makundi yaliitwa makundi ya kigaidi na mataifa ya Ujerumani na Austro-Hungary, ambayo yalitumia mbinu zote kupambana nayo.

Urusi ya kipindi kile, ndiyo Iran ya leo hii. Urusi ilikuwa na imani kwamba inalinda dini ya Kiorthodoksi na kulinda jamii ya Kislaviki dhidi ya uvamizi wa Ujerumani, Austro-Hungary na Ottoman Empire. Hivyo warusi waliyaunga mkono makundi kama The Black Hand katika kusababisha taharuki.

Tatizo ni kwamba, alipouwawa Archduke Ferdinand, Austro-Hungary alisema The Black Hand wamefanya ugaidi hivyo Bosnia kama nchi itabidi iwajibike na isipofanya hivyo itavamiwa kijeshi. Ujerumani bila kufikiria aliiunga mkono Austro-Hungary kwa kusema wana haki na kuihakikisha msaada kijeshi endapo itatishiwa na Urusi wakati inavamia Bosnia.

Matukio ya mwaka 1914 yalikuwa hivi:
1. Archduke anauwawa na mke wake Sophia.
2. Austro-Hungary inatoa masharti na kusema Bosnia iwajibike.
3. Bosnia inagoma kuwajibika, Austro-Hungary anatangaza vita na kuvamia kijeshi.
4. Urusi kuona Austro-Hungary imevamia Bosnia, yeye anaitangazia vita Austro-Hungary.
5. Ujerumani kuona Austro-Hungary atabagazwa na Urusi, yeye anaitangazia vita Urusi.
6. Bahati mbaya sana, Urusi alisaini mkataba wa ulinzi na Ufaransa ambaye naye anaitangaza vita dhidi ya Ujerumani.


Mambo yameenda, mwishowe Uturuki na Uingereza wakaingia kwenye vita na jambo ambalo lilitegemewa kuwa la wiki tu, likaenda miaka minne na kuua mamilioni ya binadamu wasio na hatia. Ikumbukwe wakati vita inarindima, taifa la Marekani lilikuwa limekaa pembeni na kutofungamana na upande wowote (A Neutral State) hadi pale maslahi yake yalipoguswa.

Ikumbukwe kipindi hiki, Marekani ndiyo lilikuwa moja kati ya mataifa yanayokuwa kwa kasi kiwango cha kushindana na Ujerumani na Uingereza hata kuwapita kwenye uzalishaji na uchumi (GDP in PPP). Hivyo dunia nzima ilitegemea kukopa na kununua kwa Marekani ili kuendesha vita tokea mwaka 1914-1917.

Leo hii, Marekani ya mwaka 1914 haina tofauti na Uchina ya mwaka 2024. Mbali na kuwa na mvutano na Marekani, lakini ukweli ni kwamba dunia nzima kuanzia Marekani, Ulaya, Asia na Afrika tunategemea Uchina kwa uzalishaji wa kiviwanda. Uchina anatumia mabavu, lakini mpaka sasa hajawahi kutumia jeshi lake kuvamia nchi yoyote ile duniani, mbali na kuvamia Vietnam mwaka 1979.


===================================================
Binafsi naamini kwamba tayari WW3 imeshaanza, sema itachukua muda mrefu mpaka tuje kukubali kwamba imeshaanza. Ukisoma historia utafahamu kwamba vita ya kwanza ilianza mwaka 1871 baada ya Franco-Prussia War, ambapo Ufaransa alitandikwa na Ujerumani na kunyang'anywa vipande vya ardhi. Matukio ya vita ndogo-ndogo na uaduia yaliendelea duniani kote kwenye makoloni hadi kufikia tamati mwaka 1914.

Mambo muhimu kuzingatia kwasasa ni haya
-Anguko la USSR 1991,
-Uvamizi wa Yugoslavia na NATO 1999,
-Uvamizi wa Afghanistan 2001 na Iraq 2003,
-Kujitanua kwa makundi kama NATO, QUAD, ANZUS n.k
-Uvamizi wa Ukraine 2014
-Arab Spring 2011
-Kukua kwa Uchina (The Ascendancy of China)
-Kukua kwa sayansi na teknolojia ambako kumeleta mataifa kujiamini mno.
-Gaza Genocide, Invasion of Lebanon, Hamas Invasion of Israel.



NB: Hapa litakuja kutokea tukio moja baya mno na wote watabwaga manyanga.

ENIWEI, ni mtizamo tu na kuna sababu nyingi nimeziacha zilizosababisha WW2 ambazo pia ni muhimu kuzipitia, mfano kufeli kwa UMOJA WA MATAIFA (The League of Nations) ambapo Adolf Hitler kama afanyavyo Benjamini Netanyahu leo na watawala kama Trump, Bush, Putin, Blair, Clinton wamefanya waziwazi kupuuza maamuzi ya UNITED NATIONS na kutumia mabavu kulinda maslahi yao.

Mussolini na Hitler waliyatoa mataifa yao LEAGUE OF NATIONS na kuapa kwamba watapambana na umoja huo kwa namna yoyote ile. Hili halina utofauti na kile ambacho Israel na Marekani wamekionesha juzi baada ya kutishia waziwazi kusema watavishambulia vikosi vya walinda amani wa UNITED NATIONS endapo hawataondoka.

=================================================
Indeed these are interesting times, and I say "What a good time to be alive"

Point of correction The Holy Roman Empire was neither Holy nor an Empire. Ila ilikuwa loose confederation of Germanic states.

Haikuwa German ilikuwa Prusia
 
Point of correction The Holy Roman Empire was neither Holy nor an Empire. Ila ilikuwa loose confederation of Germanic states.

Haikuwa German ilikuwa Prusia
That's really debatable, some scholars like Prof Roy Casagrande believe that The Holy Roman Empire was not Roman, not Holy and not an Empire. But what are the facts: It dominated a huge chunk of a land mass which was once a Western Roman Empire. And it was ruled by a single emperor who owed his pedigree to Emperor Charlemagne, king of Franks and Lombards.

This kind of debate is similar to that of saying The Byzantine Empire was not Roman Empire because it was neither Catholic nor Latin.

And by the way, Prussians and Austrians are ethnically German.
 

Katika tafiti hii, alipitia vita kubwa zilizotokea miaka 500 iliyopita tokea mwaka 1500 hadi 2000 na kufahamu kwamba taifa dogo linapoanza kukua kiuchumi na kuanza kutishia mustakabali wa dola lenye nguvu duniani kwa wakati huo ni lazima vita itokee.
Naomba unifahamishe, Kwa Sasa, ni taifa gani Dogo linatishia mustakabali wa Dola kubwa ya US? Huo udogo unapimwa Kwa mambo gani?

Kiufupi sababu za vita kubwa huwa ni zilezile The Balance of Power.
Kama lengo ni "The balance of power", mara baada ya WWII, Kwa nini Dunia ilikubali US kuwa superpower? Dunia haikujua kwamba wanaokuwa vilanja wa Dunia mara nyingi ndiyo wanaokuwa chanzo Cha machafuko? Kwa nini Sasa hivi ndipo Kuna umuhimu wa kuwepo hiyo inayoitwa "The balance of power"?.

Kama balance of power itapatikana (au ipo) Kwa muktadha wa kutooneana; je, inamaana kwamba hakutakuja kupatikana superpower mwingine? Au machafuko mengine?



Superpower "the controller of world" .
 
Unataka USA afanyeje ili uamini kwamba ndie anayewapiga Iran, Hezzibollah, Hamas na Houthi

Hizi vita zote ukijumuisha na Ukraine Marekani ndio Injinia
Sijakataa kwamba US hausiki, ila siamini kama ushirika wake ni wa 100% kwenye kila angle ya vita, kwamba Marekani anafanya kila kitu yeye mwenyewe.

Nahitaji ushahidi ktk hilo, Kwa kuwa Mwaka 2007 kulikuwa na mjadala mkali sana kule US kwamba Israel hastahili kuendelea kusaidiwa ktkt sector yoyote ile, eti Kwa kuwa Sasa inajiweza kiuchumi na technology za vita.
Poll iliyopigwa iliamua kwamba Israel aendelee kusaidiwa kijeshi tu. Mwezi wa nne 2024 Marekani ilitishia kuzuia misaada Kwa Israel Kwa kuwa ilikuwa ikikiuka sheria za vita pale Gaza, Kwa kuwauwa watoto.
 
Naomba unifahamishe, Kwa Sasa, ni taifa gani Dogo linatishia mustakabali wa Dola kubwa ya US? Huo udogo unapimwa Kwa mambo gani?

Kama lengo ni "The balance of power", mara baada ya WWII, Kwa nini Dunia ilikubali US kuwa superpower? Dunia haikujua kwamba wanaokuwa vilanja wa Dunia mara nyingi ndiyo wanaokuwa chanzo Cha mafuko? Kwa nini Sasa hivi ndipo Kuna umuhimu wa kuwepo hiyo inayoitwa "The balance of power"?.

Kama balance of power itapatikana (au ipo) Kwa muktadha wa kutooneana; je, inamaana kwamba hakutakuja kupatikana superpower mwingine? Au machafuko mengine?

Superpower "the controller of world" .
Taifa kubwa ni USA, na taifa linalokuwa ni PRC. USA kama taifa kubwa ana sehemu tano ambazo ni muhimu kwa usalama na maslahi yake (Strategic Areas):

1. Sehemu ya kwanza- The Western Hemisphere
2. Sehemu ya pili- Continental Europe
3. Sehemu ya tatu- The Persian Gulf
4. Sehemu ya nne- Asia Pacific
5. Sehemu ya tano- Central Asia/Middle East

Europe matatizo yametokea kwasababu NATO ilianza kujitanua baada ya kuona Urusi iliyotegemewa kwamba haitafika mwaka 2005 salama imeanza kukua na kuanza kujenga ushawishi wake maeneo ya Ulaya, hasahasa kwenye jamhuri za zamani za kisovieti. Marekani akaanza kutanua NATO huku akiizunguka Urusi pande zote. Urusi kang'aka na kuanza kuvamia Georgia na Ukraine mataifa ambayo ni sehemu zake kubwa za ushawishi. Ulaya Marekani anatumia NATO na EU kupambana na Urusi.

Asia Pacific, kuna taifa jingine ambalo linakuwa kwa kasi na kutishia mustakabali wa Marekani. PRC, mpaka sasa ni taifa la pili kiuchumi duniani (In terms of GDP) na la kwanza (In terms of PPP). Kiufupi, hata USSR wakati inapambana na USA, ilikuwa ina uchumi asilimia 20% tu ya ule wa Marekani. PRC, imekuwa ni tofauti kabisa kwasababu ameshampiku Marekani kama The World's Factory, The World's Leading Exporter of Merchandise and World's Largest Producer of Scientific Research.

Asia Pacific, USA anatumia makundi kama QUAD, ASEAN na AUKUS kama nyenzo za kumdhibiti (Containment) PRC asikue. USA kaenda mbali na kuanzisha alliances na nchi binafsi kama Japan na South-Korea ambazo zinamsaidia kumweka PRC kwenye kapu kwa kutumia Taiwan.

Persian Gulf, ni sehemu ambayo Marekani hakuwahi kupata mpinzani kwa miaka mingi. Lakini kuanzia 1979 mambo yake yalianza kuharibika baada ya kibaraka wake Shah kupinduliwa na serikali ya kiislamu kuingia. Iran ni taifa ambalo linakuwa mno kijeshi na haliko chini ya ushawishi wa Marekani kama ambavyo mataifa mengine kama Qatar, UAE, Israel na Saud yapo. Iran yuko na PRC na Russia.

Huku USA anaitumia Israel kuratibu mambo yake hasahasa kupiga Lebanon, Syria na Gaza. Kiufupi mataifa yaliyokuwa yanataka kukua na kutishia maslahi yake kama Iraq yalishavamiwa, amebakia Iran ndiye anayesumbua na anatafutiwa sababu ashughulikiwe.

NB 1: Baada ya WW2 dunia haikukubali USA awe Super-Power, ila ni kwasababu yeye na USSR ndiyo mataifa yaliyoibuka na nguvu zaidi baada ya mataifa mengine kuanguka.

NB 2: The Concept of Balance of Power, ndiyo ilisaidia kudumisha amani Ulaya kwa miaka zaidi ya 100 tokea mwaka 1814 baada ya Napoleonic Wars kuisha. Mataifa yote ya Ulaya yalikubaliana kwamba ili kuzuia vita ni lazima yahakikishe kwamba hakuna taifa ambalo litajitanua kuwa kubwa kuliko jingine na kuleta matatizo. Lakini mwaka 1871, Prussia walianza kujitanua na kutengeneza taifa la Ujerumani ambalo liliharibu mzani wa nguvu barani Ulaya. Mfaransa na Mjerumani wakaanza kutandikana na kuviziana kuanzia Asia, Afrika na Amerika.

NB 3: USA ni mnufaika mkubwa wa vuruge za Ulaya na Asia.
 
That's really debatable, some scholars like Prof Roy Casagrande believe that The Holy Roman Empire was not Roman, not Holy and not an Empire. But what are the facts: It dominated a huge chunk of a land mass which was once a Western Roman Empire. And it was ruled by a single emperor who owed his pedigree to Emperor Charlemagne, king of Franks and Lombards.

This kind of debate is similar to that of saying The Byzantine Empire was not Roman Empire because it was neither Catholic nor Latin.

And by the way, Prussians and Austrians are ethnically German.
So if we compare Austria-Hungary and Israel we are missing a point what the main purpose of Islamic revolution in Iran.

reasons German Reich started WWII ni Treaty of Versailles pamoja na Idea kuwa Watu wa Jamii Moja lazima waishi chini ya Dola Moja, i.e Germanic people should be under single rule.

Tuangalie hili swala kwa wakati huu.
Moja ya Sababu Putin ameivamia Ukraine ni "Russia speaking people are being oppressed by Ukraine regime" so we will invade Ukraine to protect them.

Second thing why Iran ni Adui wa nchi zote za middle East baada ya Mapinduzi ya Kiislam ya 1979.
Iran wanaamini hivi kuwa all so called slamic lands should be ruled by Muslims under Imam of Iran (Iran Supreme leader) their goal can never be achieved if America and Israel are in middle east, why? Because the Americans and Israelis are most powerful forces in the region.
To achieve their goals first they have to make sure all monarchies are overthrown, this is very big serious concern to Hashimities of Jordans, Saudis, Omanis, UAE, and almost every one in middle east.
To address hii hatari mataifa yenye wasiwasi na Iran yameziharika Israel na Marekani zifanya mashirikiano ya Kijeshi.

Kwa maoni yangu Austria-Hungary is very comparable to Iran than Israel
 
Taifa kubwa ni USA, na taifa linalokuwa ni PRC. USA kama taifa kubwa ana sehemu tano ambazo ni muhimu kwa usalama na maslahi yake (Strategic Areas):

1. Sehemu ya kwanza- The Western Hemisphere
2. Sehemu ya pili- Continental Europe
3. Sehemu ya tatu- The Persian Gulf
4. Sehemu ya nne- Asia Pacific
5. Sehemu ya tano- Central Asia/Middle East

Europe matatizo yametokea kwasababu NATO ilianza kujitanua baada ya kuona Urusi iliyotegemewa kwamba haitafika mwaka 2005 salama imeanza kukua na kuanza kujenga ushawishi wake maeneo ya Ulaya, hasahasa kwenye jamhuri za zamani za kisovieti. Marekani akaanza kutanua NATO huku akiizunguka Urusi pande zote. Urusi kang'aka na kuanza kuvamia Georgia na Ukraine mataifa ambayo ni sehemu zake kubwa za ushawishi. Ulaya Marekani anatumia NATO na EU kupambana na Urusi.

Asia Pacific, kuna taifa jingine ambalo linakuwa kwa kasi na kutishia mustakabali wa Marekani. PRC, mpaka sasa ni taifa la pili kiuchumi duniani (In terms of GDP) na la kwanza (In terms of PPP). Kiufupi, hata USSR wakati inapambana na USA, ilikuwa ina uchumi asilimia 20% tu ya ule wa Marekani. PRC, imekuwa ni tofauti kabisa kwasababu ameshampiku Marekani kama The World's Factory, The World's Leading Exporter of Merchandise and World's Largest Producer of Scientific Research.

Asia Pacific, USA anatumia makundi kama QUAD, ASEAN na AUKUS kama nyenzo za kumdhibiti (Containment) PRC asikue. USA kaenda mbali na kuanzisha alliances na nchi binafsi kama Japan na South-Korea ambazo zinamsaidia kumweka PRC kwenye kapu kwa kutumia Taiwan.

Persian Gulf, ni sehemu ambayo Marekani hakuwahi kupata mpinzani kwa miaka mingi. Lakini kuanzia 1979 mambo yake yalianza kuharibika baada ya kibaraka wake Shah kupinduliwa na serikali ya kiislamu kuingia. Iran ni taifa ambalo linakuwa mno kijeshi na haliko chini ya ushawishi wa Marekani kama ambavyo mataifa mengine kama Qatar, UAE, Israel na Saud yapo. Iran yuko na PRC na Russia.

Huku USA anaitumia Israel kuratibu mambo yake hasahasa kupiga Lebanon, Syria na Gaza. Kiufupi mataifa yaliyokuwa yanataka kukua na kutishia maslahi yake kama Iraq yalishavamiwa, amebakia Iran ndiye anayesumbua na anatafutiwa sababu ashughulikiwe.

NB 1: Baada ya WW2 dunia haikukubali USA awe Super-Power, ila ni kwasababu yeye na USSR ndiyo mataifa yaliyoibuka na nguvu zaidi baada ya mataifa mengine kuanguka.

NB 2: The Concept of Balance of Power, ndiyo ilisaidia kudumisha amani Ulaya kwa miaka zaidi ya 100 tokea mwaka 1814 baada ya Napoleonic Wars kuisha. Mataifa yote ya Ulaya yalikubaliana kwamba ili kuzuia vita ni lazima yahakikishe kwamba hakuna taifa ambalo litajitanua kuwa kubwa kuliko jingine na kuleta matatizo. Lakini mwaka 1871, Prussia walianza kujitanua na kutengeneza taifa la Ujerumani ambalo liliharibu mzani wa nguvu barani Ulaya. Mfaransa na Mjerumani wakaanza kutandikana na kuviziana kuanzia Asia, Afrika na Amerika.

NB 3: USA ni mnufaika mkubwa wa vuruge za Ulaya na Asia.
Sawa boss, nimekusoma vizuri tu. Juzi tu hapa (wiki iliyopita) Putin alisema Marekani wamechelewa kuikwamisha China kusonga mbele. Putin alisema China ya Sasa haikamatiki kiteknolojia, manufacturing industries, na sector zinginezo. Putin huyo huyo katabiri kwamba, miaka michache ijayo, makampuni ya US hayatakuwa na nguvu Tena ktk ushindani wa kibiashara dhidi ya Yale ya China.
Je, Marekani atakubali Hali hiyo iendelee Kwa makampuni ya China yaendelee kustawi? au ndiyo itakuwa WWIII uliyoizungumza Kwa lengo la "balance of power" ? Ngoja tusubiri.
 
Huo ni uoni wako hafifu unaotokana na udini na upifu uliokujaa. Hakuna mwenye akili timamu asiyeona genocide inayofanywa na Wazayuni waliyojificha kwenye koti la Uisraeli.
Unajua neno Genocide kwenye huo mgogoro lilianzia wapi?
Anyway, kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake, kama maoni yangu ni uoni hafifu ni vizuri pia.
Bora mimi mwenye uoni hafifu kuliko wewe unaebeba vitu kama dodoki na kuvitapika hivyo kisa fulani kasema.
 
Binafsi naamini WW3 imeshaanza tayari, sema itachukua muda mrefu wengi kufahamu kwamba tayari dunia imeshavuka mstari na mambo hayawezi kurudi kama ilivyokuwa zamani.

Siasa za dunia huendeshwa na RealPolitik a.k.a The Balance of Power. Mzani wa nguvu wa dunia usipowiana tu ni lazima mataifa makubwa yapigane kimabavu. Ukraine na Gaza vimekuwa vichocheo vikubwa.

Njia pekee ya kuzia vita baina ya Israel na Iran ni kuhakikisha The Balance of Power in the region is restored. Hapa itawalazimu Iran na Israeli waheshimiane kimaslahi (Spheres of Influence & Interests). Ambapo ni lazima Iran akubali kuitambua (Formal Recognition) Israeli kama taifa huru na sehemu ya Mashariki ya kati, huku Israeli akikubali The Two States Solution kama ambavyo United Nation Resolution 242 inataka.

Huku upande mwingine, itabidi Iran iwe A Nuclear Power ili kuhakikisha Absolute Deterrence dhidi ya NATO+ISRAEL. Yanayoikuta Iran leo hii hayana utofauti na yalichokikuta Pakistani kuanzia mwaka 1971-1998, ambapo India alikuwa ana nguvu kubwa kijeshi kuliko Pakistani, na mara zote alivamia na kumtandika vibaya mno. Mwaka 1998 India akamua kabisa kuandaa vikosi na kufanya majaribio ya silaha za nyuklia jambo ambalo lilimtishia kabisa Pakistani.

India alikuwa anajianda kumtafutia Pakistani sababu kule Kashmiri ili amtandike na kumvamia. Mataifa kama Uchina ikabidi waisaidie Pakistani kupata silaha za nyuklia kwa haraka ili kuweza kurudisha The Balance of Power in Central Asia. Baada ya Pakistani kufanya majaribio ya nyuklia, ikamlazimu India kurudisha makabrasha ya vita kwenye kabati na mpaka leo hajathubutu kuivamia Pakistani.

Hili linawezekana japo lina hatari kubwa mno: Litapelekea Nuclear Weapons Race duniani kote, ambapo Saudi Arabia, UAE na Qatar watazitaka hizo silaha kwasababu hasimu wao anazo. Pia NATO na QUAD wanaweza kuruhusu taifa kama Japan, Taiwan kuwa na silaha za nyuklia ili kumkomesha Uchina.

Dangerous times indeed.
kuna uwezekano Iran tayari analo bomu la nyuklia,
 
Unajua neno Genocide kwenye huo mgogoro lilianzia wapi?
Anyway, kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake, kama maoni yangu ni uoni hafifu ni vizuri pia.
Bora mimi mwenye uoni hafifu kuliko wewe unaebeba vitu kama dodoki na kuvitapika hivyo kisa fulani kasema.
Kinachoendelea Gaza ni vita kati ya Israel na hamas kama ambavyo Israel inapambana na Hezbollah.

Je, huko Ukraine Russia inafanya Genocide?
Genocide is an international crime which can be committed against a group of people (ethnicity, religious or nationality), during both peace times and an armed conflict.

Unaposema kwamba Afrika Kusini ndiyo ametunga neno GENOCIDE ilhali kuna mkataba wa kimataifa ambao unakataza GENOCIDE, THE GENOCIDE CONVENTION 1948 unataka sisi tukueleweje labda ???
 
Back
Top Bottom