Umoja wa vyama 10 vya upinzani nchini Tanzania vimefungua kesi Mahakamani Kuu kupinga muswada wa sheria ya vyama vya siasa

Umoja wa vyama 10 vya upinzani nchini Tanzania vimefungua kesi Mahakamani Kuu kupinga muswada wa sheria ya vyama vya siasa

Mkuu mbona unanichanganya?Hoja ya hao wasanii ni kulizuia bunge kufanya kazi yake ya kutunga sheria au kuomba mahakama itamke kua muswada wa sheria ya vyama ni batili?
Naona unahamisha magoli kisayansi
Kwa upeo wangu mdogo wanatakiwa waiache sheria ipite,wakaipinge mahakamani,lakini hawana uwezo wa kulizuia bunge lisitunge sheria
Hii ilishindikana pia wakati wa kutunga sheria ya bunge la katiba,wapinzani walijaribu kuitumia mahakama wakakwama
Isome vizuri hiyo ibara usikopi nusu nusu, inazungumzia vyote unaweza kupinga sheria au (hatua) process.
 
Wewe utakua ni kiongozi huko upinzani Maana tafsiri ya upinzani waliyo nayo ndio kama yako.

Yanapokuja katika maswala ya msingi ya kitaifa watu huweka itikadi zao pembeni na kulisupport Hilo jambo lakini hapa kwakua tafsiri iliyopo kwenye akili za viongozi wa upinzani pamoja na wafuasi wao kuwa upinzani ni kupinga kila kitu basi wao hata katika Yale maswala ya muhimu yenye faida kwa Taifa wao wanapinga ili mradi eti wabakie na heshima Yao kuwa wao ni wapinzani. Huko ni kupotoka na kujenga tafsiri potofu ya upinzani kwenye akili za watu.
Hata hiyo kupinga kila jambo huwa kuna hoja za msingi sana kwa wapingaji, mnapaswa muwe huru kifkra ili muwasikilize hao wanaopinga siyo mnashupaza shingo hamtaki mkosolewe kana kwamba kila mnalofanya liko sahihi kwa %100 kitu ambacho ni kujidanganya

2020 John Walker out
 
Wapinzani mnafanya mambo ya kutia aibu kabisa;

Mtu anaamua kwa makusudi kabisa kukiuka masharti ya dhamana; wenzake wanaamua kukutana huko hotelini na kumtangaza kuwa ni mfungwa wa kisiasa. What a shame.
Wewe unaona ni mfungwa wa ubakaji?

2020 John Walker out
 
Someni hiyo Ibara ya Katiba ya JMT muone kuwa hawajakurupuka kufungua kesi.

30.-(1) Haki na uhuru wa binadamu ambavyo misingi yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja kwa maana ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa kwa haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma.

2)......

3) Mtu yeyote anayedai kuwa sharti lolote katika Sehemu hii ya Sura hii au katika sheria yoyote inayohusu haki yake au wajibu kwake, limevunjwa, linavunjwa au inaelekea litavunjwa na mtu yeyote popote katika Jamhuri ya Muungano, anaweza kufungua shauri katika Mahakama Kuu.

4).......

5) Endapo katika shauri lolote inadaiwa kwamba sheria yoyote iliyotungwa au hatua yoyote iliyochukuliwa na Serikali au mamlaka nyingine inafuta au inakatiza haki, uhuru na wajibu muhimu zitokanazo na ibara ya 12 hadi 29 za Katiba hii, na Mahakama Kuu inaridhika kwamba sheria au hatua inayohusika, kwa kiwango inachopingana na Katiba ni batili au kinyume cha Katiba basi Mahakama Kuu ikiona kuwa yafaa au hali au masilahi ya jamii yahitaji hivyo, badala ya kutamka kuwa sheria au hatua hiyo ni batili, itakuwa na uwezo wa kuamua kutoa fursa kwa ajili ya Serikali au mamlaka nyingine yoyote inayohusika kurekebisha hitilafu iliyopo katika sheria inayotuhumiwa au hatua inayohusika katika muda na kwa jinsi itakavyotajwa na Mahakama Kuu, na sheria hiyo au hatua inayohusika itaendelea kuhesabiwa kuwa ni halali hadi ama marekebisho yatakapofanywa au muda uliowekwa na Mahakama Kuu utakapokwisha, mradi muda mfupi zaidi ndio uzingatiwe.
Shukrani mkuu kwa kuweka kumbukumbu hii ili hawa vichwa maji waweze kuelewa msingi wa shauri la kupinga mswada huo kupitishwa kuwa sheria

2020 John Walker out
 
Mtanyooka tu!
Hivi kwa akili yako nani kanyooka kama sio lijiwe?
We kila anachogusa anaumbuka unadhani anasikia raha? Ni aibu tu mtu mzima kuonekana ovyo!
 
Nimemsikia ndugu yangu Zitto Zuberi Kabwe leo akiipongeza mahakama kwa kuacha likizo na kuja kusiliza shauri walilolifungua kama vile ambavyo wengine wamekuwa wakiipongeza pale inapotoa hukumu vile wanavyokuwa wakihitaji mfano. Abdul Nondo, Tundu Lissu, Halima Mdee na Wengineo wengi.
Je mahakama ikifanya maamuzi kinyume na matarajio yake ataipongeza au atasema mahakama imemezwa na serikali?
Doublestandards in the game.
Kwenye kundi la mamba hata kenge wamo. Kwenye mahakama wamo kenge pia, kama yule Mashauri wa Kisutu au yule wa kesi ya Lema Arusha ambaye hata kwenye appeal ,Jaji alimtukana kiutu uzima yeye na ofisi ya DPP
 
Imefunguliwa Mahakama Kuu ya Tanzania, case no. 31/2018 ipo mbele ya jopo la majaji 3, Sehel, J., Maghimbi, J., na Masoud, J.
Kuna mwandishi wa pili kauliza swali zuri sana kwamba wanapinga contents au process. Katika majibu naona Bashange anajichanganya sana; mara aseme ni suala la kikatiba mara siyo la kukatiba. Kama ni suala la kikatiba basi mahakama hiyo haina nguvu ya kulisikiliza hilo suala. Watapigwa PO keshokutwa na mambo yanaishia hapo hapo. Kama hawajajiandaa vizuri basi kesho PO inawahusu. Halafu Zitto anaulizwa swali zuri badala ya kujibu anasema kesho mahakama inaweka historia!
Wanajichanganya sana na wataweka historia ya kujichanganya
 
Kuna mwandishi wa pili kauliza swali zuri sana kwamba wanapinga contents au process. Katika majibu naona Bashange anajichanganya sana; mara aseme ni suala la kikatiba mara siyo la kukatiba. Kama ni suala la kikatiba basi mahakama hiyo haina nguvu ya kulisikiliza hilo suala. Watapigwa PO keshokutwa na mambo yanaishia hapo hapo. Kama hawajajiandaa vizuri basi kesho PO inawahusu. Halafu Zitto anaulizwa swali zuri badala ya kujibu anasema kesho mahakama inaweka historia!
Wanajichanganya sana na wataweka historia ya kujichanganya
Mbona walijibu vizuri tu kuwa wanapinga vyote content na process, akatolea mfano wa content ni ku criminalise shughuli za kisiasa, process ni kutoshirikishwa kwa wadau, hata hivyo tusi predict hukumu kama alivyofanya Zitto na wewe.
 
Wapinzania wamefungua kesi na majibu yao kabisa kwa mtazamo wangu hi kesi itatupiliwa mbali kwasababu kesi imefunguliwa kwa mtazamo tu Wala si kisheria.

Lets wait and see
 
Wapinzania wamefungua kesi na majibu yao kabisa kwa mtazamo wangu hi kesi itatupiliwa mbali kwasababu kesi imefunguliwa kwa mtazamo tu Wala si kisheria.

Lets wait and see
Inatupiliwa mbali saa kumi na moja asubuhi!
 
Wewe ndio kituko, kasome ibara ya 30 ya katiba ya JMT, mtu yeyote atakayeona haki zake zinavunjwa au ZINAELEKEA kuvunjwa ana haki ya kwenda mahakamani kuzuia,

Mahakama inajua shauri lililopo ndiyo maana imekubali kesi ifunguliwe, kusingekuwa na haki hiyo wala isingesumbuka kusitisha likizo.
Nijuavyo kupokelewa maombi ni hatua moja, kukubalika kusikilizwa shauri ni hatua nyingine.
 
Someni hiyo Ibara ya Katiba ya JMT muone kuwa hawajakurupuka kufungua kesi.

30.-(1) Haki na uhuru wa binadamu ambavyo misingi yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja kwa maana ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa kwa haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma.

2)......

3) Mtu yeyote anayedai kuwa sharti lolote katika Sehemu hii ya Sura hii au katika sheria yoyote inayohusu haki yake au wajibu kwake, limevunjwa, linavunjwa au inaelekea litavunjwa na mtu yeyote popote katika Jamhuri ya Muungano, anaweza kufungua shauri katika Mahakama Kuu.

4).......

5) Endapo katika shauri lolote inadaiwa kwamba sheria yoyote iliyotungwa au hatua yoyote iliyochukuliwa na Serikali au mamlaka nyingine inafuta au inakatiza haki, uhuru na wajibu muhimu zitokanazo na ibara ya 12 hadi 29 za Katiba hii, na Mahakama Kuu inaridhika kwamba sheria au hatua inayohusika, kwa kiwango inachopingana na Katiba ni batili au kinyume cha Katiba basi Mahakama Kuu ikiona kuwa yafaa au hali au masilahi ya jamii yahitaji hivyo, badala ya kutamka kuwa sheria au hatua hiyo ni batili, itakuwa na uwezo wa kuamua kutoa fursa kwa ajili ya Serikali au mamlaka nyingine yoyote inayohusika kurekebisha hitilafu iliyopo katika sheria inayotuhumiwa au hatua inayohusika katika muda na kwa jinsi itakavyotajwa na Mahakama Kuu, na sheria hiyo au hatua inayohusika itaendelea kuhesabiwa kuwa ni halali hadi ama marekebisho yatakapofanywa au muda uliowekwa na Mahakama Kuu utakapokwisha, mradi muda mfupi zaidi ndio uzingatiwe.
Umefanya vema kuweka vifungu hivyo katiba. Vyote vinaxungumzia sheria zinaxokiuka misingi ya katiba, sio Mswaada ulioko bungeni unaojadiliwa na muhimili mwingine wa kutunga sheria na haujawa SHERIA bado. Kwa sasa vyama vilitakiwa kujenga ushawishi kwa wabunge wengine, muswada usipitishwe bungeni na kama ukipita na kuwa sheria ndio nafasi ya kuomba Mahakama kutafsiri ukiukwaji wa haki. Mahakama kuingilia jambo linalojadiliwa na halijaamuliwa na bunge ni chanzo cha mgogoro wa kikatiba.
 
Kwani mlikatazwa na nani kuwa na wabunge wengi. Vyama 10 mmeshindwa kuwa na wabunge kwa umoja wenu kufikia idadi sawa na CCM. Hapo ni tatizo, mjitafakari.
 
Back
Top Bottom