Unajua Mungu aliumbwa na nani?

Unajua Mungu aliumbwa na nani?

Huna lolote unalojua wewe pamoja na kufatilia hili jukwaa kwa miaka miwili bado hujapata kitu cha kutushawishi zaidi ya kutaka watu wakujazie comments Tu "NI KIJANA KIMWILI ILA KIFIKRA WE NI MZEE TENA KIKONGWE" Huna tofauti na mtoto aliyetoka kuachishwa kunyonya na mama yake
Personal attack

Huwezi kujadili hoja unamjadili mtu.
 
Hii mijadala ya kumchokono chokonoa Mwenyezi Mungu iishe sasa. Dhana ya Uwepo wa Mungu ipo kiimani zaidi. Mambo ya kusema eti nani alimuumba Mungu ni ujinga na ukosefu wa kuelewa mambo mengine.

Yai na kuku kipi kilitangulia. Tuanzie hapo kwanza. Maana hii hapiop kiimani.
 
Kujua kama kuna Mungu wala sio complex issue.
Ipo hivi.. Mungu=Muumba(aliyekuumba wewe, huyo ndiyo Mungu wako)
Labda kama useme wewe haujaumbwa umejileta mwenyewe hapa duniani na wazazi wako uliwaleta wewe hapa duniani, na wazazi wa wazazi wako uliwaleta wewe hapa duniani. Labda ikiwa hivyo unaweza ukasema hakuna Mungu. AHSANTE
Mimi kama sijui chanzo changu ni kipi kunafanya jibu liwe Mungu?
 
Hii mijadala ya kumchokono chokonoa Mwenyezi Mungu iishe sasa. Dhana ya Uwepo wa Mungu ipo kiimani zaidi. Mambo ya kusema eti nani alimuumba Mungu ni ujinga na ukosefu wa kuelewa mambo mengine.

Yai na kuku kipi kilitangulia. Tuanzie hapo kwanza. Maana hii hapiop kiimani.
Kwanini kuhoji dhana yenye utata kuhusu mungu iwe ujinga,?

Ujinga ni nini?
 
Kwasababu hojayako ilijielekeza kwa Mungu na mwanadamu so siwezi kuuliza kwa kutumia "nini" ila ukitaka naweza kukuuliza pia
Nini kilitengeneza au kiliweka hizo mechanisms?
Mimi sijaleta hoja yoyote mezani, wala sijasema Mungu hayupo....simply mimi nimesema tu hivyo vitu ulivyokuwa unasema kama jinsi jicho linaweza kuona rangi,sijui utumbo kula ugali, mechanisms zake zinajulikana na ni vitu biological kabisa.

Sasa ukauliza tena nani kaiweka hiyo mechanism
Hata kama nikisema Sijui ni nani kaweka hiyo mechanism haitamaanisha ni Mungu ndiyo kaweka...

Wewe unayesema ni Mungu kaweka, unatakiwa uthibitishe. na ukithibitisha beyond doubt, Mimi nitaamini na kumuabudu.

Lakini kama ukishindwa kuthibitisha, Tusiseme ni Mungu bali tuseme ni hizo mechanisms.
 
Unadhani uwepo wa nyota utapingana vipi na madai yangu hapo juu?
Dogo usitafute sifa kupitia MUUMBA wako, kama nilivyokushauri hapo juu uvitazame na utafakari ni namna gani vingeweza kuwepo bila nguvu ya uumbaji na haujatilia maanani.

Kama tu ambavyo huwezi kuyageuza macho yako na kukitazama kisogo chako tambua pia fikra na akili zako zina ukomo, hivyo utakuwa sahihi sana kuamini uwepo wa MUNGU.
 
Dogo usitafute sifa kupitia MUUMBA wako, kama nilivyokushauri hapo juu uvitazame na utafakari ni namna gani vingeweza kuwepo bila nguvu ya uumbaji na haujatilia maanani.

Kama tu ambavyo huwezi kuyageuza macho yako na kukitazama kisogo chako tambua pia fikra na akili zako zina ukomo, hivyo utakuwa sahihi sana kuamini uwepo wa MUNGU.
Kama sijui hizo nyota zilitokea vipi hakufanyi jibu liwe ni mungu...kitendo cha kukimbilia kusema ni mungu ni uvivu wa kufikiri hivyo unaamua kutafuta jibu jepesi " mungu kaumba"
 
Unajikanyaga si umesema Mungu kaandika kitabu? Ebu rudia kusoma Uzi wako.
Nimekuuliza swali hujajibu.

Una uthibitisho gani kuwa hayo maneno kwenye Quran ni ya mungu na si mtu tu aliyeyatunga?
 
Mimi ni kijana ambaye Kwa muda wa miaka 2 nimekuwa nikifatilia mijadala mbalimbali hapa Jf katika jukwaa hili la intelligence. Moja ya mijadala ambayo imekuwa ikinivutia sana ni hii ya dhana ya uwepo wa Mungu.

Swali kubwa ambalo nimeku wa nikijiuliza ni " Mungu alitoka wapi"

Baada ya kuisoma sana biblia na Quran pamoja na kuwahoji viongozi mbalimbali wa dini, hatimaye nikapata jibu la swali lililonitatiza muda mrefu, Mungu alitoka wapi?

Nimegundua kuwa muumba wa Mungu ni mwanadamu. Yes mwanadamu kama Mimi na wewe ndiye aliyemuumba Mungu.

Kwanini nimefikia hitimisho hilo?

Vitabu tunavyoaminishwa kuwa ni vya Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu ( biblia & Quran) ni vitabu vyenye makosa mengi sana ya kimantiki na habari nyingi zenye utata, jambo ambalo tusingetegemea liwepo katika kitabu kilichoandikwa kwa muongozo kutoka kwa Mungu mkuu mwenye uwezo asiyeshindwa na kitu.

Uwepo wa habari hizo zenye utata zinadhihirisha moja kati ya mambo yafuatayo.

1. Mungu hana ukuu tunaoambiwa ndio sababu ameshindwa kutoa mwongonzo mzuri katika kuandika kitabu kisicho na makosa ya kimatinki.

2. Habari hizi ni zao la fikra za mwanadamu aliyeishi katika zama za giza na ujinga. Mwanadamu ambae alitaka kutafuta majibu mepesi katika maswali magumu yaliyomzunguka ndio sababu zina utata.

Kama jibu ni 1 basi Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu hayupo Bali aliyepo ni dhaifu na mbabaishaji aliyeshindwa kuandika vizuri kitabu kinachomuelezea yeye mwenyewe.

Kama jibu ni 2 ,basi Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu hayupo ndiyo sababu akatokea mtu akatunga habari kutokana na fikra zake mwenyewe. Angekuepo asingeruhusu magepu katika fikra za mwanadamu ambayo yamepelekea mwanadamu huyo kujitungia majibu mepesi na habari zenye utata ili kuziba hayo magepu katika fikra zake.

Pointi zote mbili utaona zinaonyesha kuwa Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu mjuzi wa yote hayupo Bali " ama aliyepo ni dhaifu,mbabaishaji na asiye na uelewa wowote kuhusu ulimwengu, ama dhana nzima ni hadithi ya kutungwa katika fikra za mwanadamu aliyeishi katika zama za ujinga na kukosa access ya taarifa mbalimbali.

Nawasilisha.
Bora umwamini tu, hata kama kweli hayupo haudhuriki, kuliko kutomwamini na ukamkuta kwenye kiti cha hukumu!
 
Hakuna vitisho hapo mkuu...utatishika vipi na kitu cha kufikirika?
Sawa mkuu mimi pia nafatilia comment za watu.

Bahati mbaya mpaka thread ya 4 hii sijaona comment iliyonishawishi kutoka kwa waumini wa dini. Ni jazba, vitisho na kuuliza maswali yasiyokua na uhusiano kimantiki kuhusu dhana ya uwepo wa Mungu. Hii dhana ya uwepo wa Mungu hata mimi pia ilianza kugoma kuingia kichwani tangu nikiwa o-level nilijiuliza maswali mengi sana, kwanini vitabu vya Mungu vina mkanganyiko, kwa maelfu ya miaka Mungu alishindwa kujidhiirsha yeye mwenyewe afrika mpaka akasubiri atambulishwe na wakoloni?, mababu zetu waliokufa kabla ya ujio wa hizi dini je saiv wapo motoni?

Tangu kuletwa kwa hizi dini takribani miaka 500 sasa hivi je sala na maombi vimesaidia kumaliza tatizo gani hapa afrika? Yaani maswali ni mengi sana bahati mbaya sijawahi kupewa majibu ya kuniridhisha kwaiyo naishi kwa kuongozwa na ubinadamu.

Dini naichukulia kama namna fulani tu ya kujumuika na jamii ila sio muongozo wa maisha
 
Unao ufahamu kuhusu ulimwengu wa ROHO yaani usioonekana
 
Kama kuna makosa ya uandishi umeyalinganisha na yepi sahihi
 
Back
Top Bottom