Unampigia simu kwa namba ngeni halafu hapokei baadaye anakwambia hapokeagi namba ngeni

Unampigia simu kwa namba ngeni halafu hapokei baadaye anakwambia hapokeagi namba ngeni

Ukipiga once na kuona mtu hapokei si utume sms?

Hivi hata matumizi ya sms watu hatuyajui kweli?? Unakuta 10 missed calls, huyo mpigaji anajitambua kweli?
Mwanao, mwenza wako au yeyote wa karibu nawe amepata dharula au tatizo kama ajali, kuibiwa simu, kuugua nk kisha ameomba simu kwa mtu Ili akufahamishe wakati wewe unadhani kupokea simu ngeni ni tatizo.
Wakati mwingine jamaa yako amelazwa hospitali au kapigwa dawa za kulevya au amepelekwa kituo cha polisi au shida nyingine.
Huyu amejitokeza kukupigia akiwa ""Msamaria mwema" kisha wewe unabakia na msimamo huo wa kutopokea simu.
Huenda mwisho wa yote hasata itakuwa kwa aliyehoma kupokea simu.
Hata hivyo mwisho wa yote uamuzi wa mhusika [hata kama una utata] uheshimiwe.
 
Kwa tunaotumia simu moja kwa mambo binafsi na biashara hatuna budi kupokea kila simu, iwe ya mganga au wale jamaa wa freemason muda mwingine mambo magumu unapokea hadi zile namba za tigo/voda kwa kuhisi ni wateja[emoji23]
Uko sawa mkuu
 
Y

Yes, mtazamo wako unaweza kuwa sahihi. Lakini mtu kama tapeli si unamsikiliza unampuuza au unamkatia simu baada ya kumsikiliza. Sasa hii ya kupuuzia namba ngeni, what if ni shida ya dharura au ni mchongo wa maana ambao watu wanakusogezea?
Weee ukute ni baba mwenye nyumba anakumbusha kodi sijalipa mwezi wa pili, au deni la vikoba. Aaah jitambulishe kwanza
 
Unaombwa ombwa hela na watu ambao hutaki kuwapa. Na hutaki kumwambia kuwa hutaki jumps bali unataka ajiongeze na hajiongezi
 
Mimi mwenywe nawashangaa Sana wenyemsimamo huu Sasa vipi mtu kama kapata dharula ,

Mimi binafsi nikikuta mamba ngeni napokea naongea nae kama kakosea namba namwambia sio Mimi unaye mtafuta,nikikuta missed call napiga kujua nani kanitafuta.
Hiyo dharura kapata nani? Mpigaji au mpigiwaji? Dharura yako ndo nihangaike mimi? Na kama wewe ni mtu wangu wa karibu ntakuwa nimekwambia utaratibu wa kupiga kwa namba ngeni. Tuma sms kwanza ujitambulishe
 
Muwe mnatuma sms za kujitambulisha kwanza ili hata asipopokea ujue kafanya makusudi.

Wengi wanaogopa matapeli wa ile pesa tuma namba hii
Mtu asiyepokea namba ngeni, au anayebadili laini kila siku, huwa anakuwa na amma madeni ya aibu na hana mpango wa kulipa, hivyo hudhani wanaompigia ni wadeni wake. Au anakuwa afeshafanya ubaya mwingi kwa watu, hivyo anahisi anatafutwa, au ni mtu mwenye majivuno au ujinga au vyote kwa pamoja. Ila mtu muungwana wa wastani tu, hawezi kuacha kupokea siku kwa hoja eti namba ngeni.
 
Pole sana, jiongeze, tuma sms kabla ya kupiga alafu ndiyo piga...
 
Mwingine akipiga anaanza kubwabwaja kabla ya kujitambulisha,Kuepusha zile vurugu za eti Umefuta namba yangu unaona bora usubirie kwanza ikiwezekana umtafute kwenye muamala umjue kwanza wengine wanapiga kwa Nongwa na si Vinginevyo.
 
Asilimia kubwa kuna namba za watu wanakuwa hawataki kuzipokea kwa sababu zao binafsi, kwa hiyo inapoingia namba ngeni wanahisi ndio huyo huyo ameamua kubadilisha namba. So njia rahisi ni kutuma msj ww ni nani ili mhusika apokee
 
Hao watu ni waoga au matapeli

Ni hawajiamini kupokea namba ngeni kwa sababu kuna mtu ambaye hawapokei simu yake wanahofia ametumia namba ngeni kuwapigia

Watu hawa mara nyingi ni watu wanaodaiwa hawalipi au malaya
Uliyoongea ni ukweli tupu, ila hili neno "malaya" ungeliwekea shadow maana ni neno la aibu lakini linapendwa sana kufanywa na jamii.
 
Namba kama ni landline [emoji338] sawa nitapokea ila kama namba ngeni wengi ni matapeli na kama ikitokea mtu ananitafuta ni lazima ajiongeze kama sijapokea anajua sijapokea kwa kuwa namba ni unknown

Hapo huwa wanatuma msg ya kujitambulisha
Namba nyingi huku huwa za insurance au utapeli wa Inland revenue au matapeli wa aina hiyo

Ushauri tuma msg jitambulishe nae atapiga tu
 
Mie nimemwiga rais wetu mstaafu marehemu mkapa ninamajina 6 kwenye simu yangu mmoja nikimwambia nisaidie haraka milion 20 mudahuohuo napata na haulizi lini itarudi Wala hutasikia sehemu
 
Back
Top Bottom