Unaye mtu wa kukusikiliza? Kuna muda unapitia hali unapitia unatamani kumweleza mtu mmoja upate ahueni lakini hayupo

Pole sana..... Njoo pm
 
Kiukweli natamani sn niwe na mtu wa kumwambia na kuongea naye.Ninayo mengi sana na sielewi nifanyeje?
 
Pole sana.
Najua upo katika hali gani sasa, jipe moyo acha kuwaza sana watu ambao wamekutenga hasa familia. Kama unapata mahitaji muhimu. Jaribu kutafta jambo la kukufanya uwe bize, pia jaribu kwenda kwenye nyumba za ibada kama unaamini. Tafta mahubiri uwe unasikiliza YouTube au muziki au movie zenye mafundisho. Usijihisi mpweke hicho ndo kinachangia pia watu wasichangamane nawe.
 
Nishakuwa mvivu wa hayo mambo kwasababu ya uzito. Sipendi kabisa kuyasikia
Kwamba uzito umekuletea uvivu? Huwezi ku~ride tena wallah🀣
 
Sawa mtumishi
 
Sawa ahsante sana
 
Ishini maisha sasa,ule utoto wa kudhani ndugu pekee ndiye mtu muhimu ktk maisha muusahau.
Unaweza kuja mjini hapa au kwingine,ukakutana na mtu au watu kadhaa ukatokea kuwaamini nao kukuamini kuliko hata ndugu zako wa damu.

Fikiria sekunde kadhaa hapo,sasa hivi ni nani ktk circle yako ya marafiki atakuwa wa kwanza kujua endapo umekamatwa na polisi,unaumwa sana,una shida na ushauri nk.

Mungu aliweka siri kubwa sana ktk hilo,hata wanafiki na waovu wana rafiki zao ambao hujisikia aman kuwaambia jambo lolote.
 
Kuna siku nikaenda kupima ngoma. Nesi akaniuliza nikikupa majibu mtu wa kwanza kumshirikisha ni nani? Nikamwambia sina. Akashangaaa snaa
 
Pole sana, binafsi nimepitia mengi mno lakini yote nimeyamudu bila kumshirikisha yeyote yule, naisubiri Kwa hamu siku ambayo moyo wangu utakapojaa.
 
Mnaweza kuzaliwa baba na mama mmoja bado msielewane au hujawahi kusikia ndg wamoja wanafanyiana fitina ktk maisha? Tafuta rafiki km huna kuna viongozi wa kiroho sio mpk awe mchungaji au mtume na nabii, mtaani unapoishi wapo watu waume kwa wake wenye umri wa wazazi wako fuata hao watakusaidia sababu wameona mengi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…