Uongozi wa UDSM watoa angalizo uwepo wa CHATU maeneo ya Shule ya Msingi Mlimani

Uongozi wa UDSM watoa angalizo uwepo wa CHATU maeneo ya Shule ya Msingi Mlimani

Hebu sikilizeni hawa wazee wetu walipotukanya kuwa makini na Chatu.
 
Ni kweli watu wa Dasilamu wanashangaza kama sio wanasikitisha kwa vituko vyao.
Laiti wangelifika huku Umasain ndani ndani huku wajionee jinsi chatu anavyodharaulika na hakuna mtu anahangaika naye ila tunakwepesha kuchunga mbuzi na kondoo eneo hilo au kwenda na mbwa mahali hapo kwani mbwa lazima atajipeleka mwenyewe kwa chatu na aliwe kiulaiiiini. Ukisikia mara moja tuu kwii-kwiiiii. Ujue huyo mbwa imeenda.
UJITANI KWETU chatu anachapwa viboko kwa kutumia fimbo nyembamba,anachapwa vya kutosha baadae anahamishwa kutoka karibu na makazi ya watu au machungio ya mifugo na kupelekwa porini.

Kipigo anachopewa siyo cha kumuua,bali ni kumlegeza misuli tu akose nguvu za kuleta ubishi wakati akihamishwa.
Sasa eti kule kwa Chalamila watu wanataka TAMWA sijui games waje wawape usaidizi.
Mbona waliweza kuwadhibiti wale WAHUNI PALE TEGETA KWA NDEVU?
 
inanikumbusha dodom wkat fulan tuolikuwa mapori ya swaswa kwa shughul flan watu walitaharuk kusikia tembo wapo .taan
 
Huyo Chatu kaja na mwanafunzi wa first year.
Ila watu wa Dar waoga sana, huku Tukuyu tunaishi hao hao chatu hawana madhara
kabisa, usijekuta kuna first year kaja nae, usiku anabadilika anakuwa mamake mchana chatu
 
Uongozi wa udsm utakuwa umeona dalili za uharibifu wa mazingira katika maeneo hayo,sasa wameona labda watumie mbinu hii ya kuwepo kwa huyo kiumbe maeneo hayo ili kuwatia jamba jamba waharibifu wa mazingira .Otherwise mbinu kama hizi ndio zilisaidia miaka ya nyuma watu kuto kuharibu mazingira,kama misitu na vyazo vya maji . Maana haingii akilini yaani watu ambao ni wasomi ,wanaotegemewa kama kisima cha maarifa nchini waaze kulilia kulilia kwamba kuna huyo kiumbe maeneo hayo, kama wanajua ni hatari maeneo hayo si watoe taarifa mamlaka husika waje wamtafute na wamtoe hapo , au wale ambao wanasomea mambo ya kemia watengeneze kemikali kumnasa au ndio mnaiomba serikali kiana iwaletee wazungu kutoka south Africa au Marekani ili ije imnase , kwa maoni yangu hii ndio furusa ya kudhihirisha quality of education how to deal with any challenge.
 
Najaribu kupata picha ya Itakavyokuwa hao vijana wa W/Pori (Game officers) kizazi cha Dotcom watakavyojipanga kumsogelea huyo chatu ilhali wao wenyewe hata kumshika kinyonga ni mtihani- ni waoga mno kupita maelezo.
Ngoja nimwite Mtani wangu awasaidie ila wasisahau "kitu kidogo" kama shukrani.
😃😃😃 wengi wasomea kufaulu mitihani .
 
Hawa wanyama wanaozurura kwenye makazi ya watu ukiwagusa tu utaona mbio za mamlaka ya wanyama pori watakavyokuja haraka, ila hao wanyama wakijeruhi watu watakuja kwa kuchelewa. Wanadai mishahara yao inatokana na uwepo wa wanyama hao na wana thamani kubwa kuliko mtu!

Utakamatwa kwa kuleta taharuki mtaani. Interesting times 😂 😂 😂 😂
 
Uongozi wa udsm utakuwa umeona dalili za uharibifu wa mazingira katika maeneo hayo,sasa wameona labda watumie mbinu hii ya kuwepo kwa huyo kiumbe maeneo hayo ili kuwatia jamba jamba waharibifu wa mazingira .Otherwise mbinu kama hizi ndio zilisaidia miaka ya nyuma watu kuto kuharibu mazingira,kama misitu na vyazo vya maji . Maana haingii akilini yaani watu ambao ni wasomi ,wanaotegemewa kama kisima cha maarifa nchini waaze kulilia kulilia kwamba kuna huyo kiumbe maeneo hayo, kama wanajua ni hatari maeneo hayo si watoe taarifa mamlaka husika waje wamtafute na wamtoe hapo , au wale ambao wanasomea mambo ya kemia watengeneze kemikali kumnasa au ndio mnaiomba serikali kiana iwaletee wazungu kutoka south Africa au Marekani ili ije imnase , kwa maoni yangu hii ndio furusa ya kudhihirisha quality of education how to deal with any challenge.
Umenikumbusha mbali sana. Kule Arusha tulikuwa tunaambiwaga kwenye chanzo cha maji kuna chatu. Tulikuwa hatusogelei kabisa.
 
Back
Top Bottom