Upigaji Uyui: Waziri Mkuu ashangazwa kibanda cha Mlinzi VETA kujengwa kwa Tsh. milioni 11, aagiza waliyosimamia ujenzi kukamatwa

Upigaji Uyui: Waziri Mkuu ashangazwa kibanda cha Mlinzi VETA kujengwa kwa Tsh. milioni 11, aagiza waliyosimamia ujenzi kukamatwa

Watu ambao hawajawahi kujenga ndio watashangaa mimi nikikiangalia hicho kibanda mbona pesa hiyo ni halali!.

  1. Kuchimba msingi vibarua 500,00
  2. Kujenga Msingi mawe zege 1,000,000
  3. Kuinua kuta 1,000,000
  4. Madirisha 3 ya PVC za Uturuki 3,000,000
  5. Milango miwili ya Mninga 1,000,00
  6. Bati ya South 1,000,000
  7. Tails za mable 1,000,000
  8. Scatting ya black granite 500,000
  9. Rangi ile washable 500,000
  10. Msimamizi 1,000,000
  11. 10% ya aliyetoa kazi 1,000,000 hapo kuna wizi gani?.
JIfunze kuangalia quality kabla hatujakimbilia kupigia kelele wizi na ufisadi, ujenzi wa majengo yoyote ya umma unatanguliwa na BOQ.
Kwa msio jua quality ya ujenzi, nendeni makaburi ya Kinondoni kuna kaburi pale limegharimu TZS 36.M!.

Mfano mimi natamani tomb stone yangu iwe kama ile ya ku roll, find out how much it costs, tusishabikie tuu ufisadi!.
P
Waziri Kassim ameteleza
 
Sema awamu ya tano kulikuwa Kuna majambazi wakubwa nikikumbuka ile TL 1.5 ilivyoibwa kama mvua
 
Waziri mkuu Majaliwa ameiagiza Takukuru kuwakamata wote waliosimamia ujenzi wa Chuo cha Veta Uyui

Majaliwa ameshangaa kuona kibanda cha mlinzi kimegharimu tsh 11 milioni

Source ITV habari
 


Mupe.....Muruke.....

Imerudi Tena Kwa Kasi
 
JIfunze kuangalia quality kabla hatujakimbilia kupigia kelele wizi na ufisadi, ujenzi wa majengo yoyote ya umma unatanguliwa na BOQ.
Kwa msio jua quality ya ujenzi, nendeni makaburi ya Kinondoni kuna kaburi pale limegharimu TZS 36.M!.

Mfano mimi natamani tomb stone yangu iwe kama ile ya ku roll, find out how much it costs, tusishabikie tuu ufisadi!.
P
Wewe utajenga kwa kutumia Kodi / Jasho la wananchi ambao hata milo miwili kwa siku tatu ni tatizo ?
 
Kuna wakati ni vigumu sana kufananisha ujenzi kwa kutumia force account kuoka eneo moja na lingine.

Kuna baadhi ya maeneo wananchi wanajitolea nguvu kazi na kukusanya mchanga pamoja na mawe.Maeneo mengine kila kitu unanunua kuanzia mchanga.
Hata kama ni hivyo. Hicho kibanda ndiyo kigharimu Milioni 11?
Kila kitu ni tozo bila kujali uchumi wa wananchi. Sasa hivi kumtumia mtu 150,000 unakatwa kama 3,000 hivi bado huko hajatoa. Vifurushi kila siku vinabadilishwa wanavyotaka ndiyo matokeo yake haya. Wanapesa nyingi ambazo wamezipata siyo kihalali.
 
Iko aina ya 4 ya Demokrasia inaitwa homophrodite demokrasi. Hii wananchi wanakua na vyama vingi. Hivyo vyama vingi vinaunda mirengo. Mirengo inatoa mgombea Urais atayepigiwa kura na wananchi akishindanishwa na wamrengo mingine na wagombea binafsi wa Urais. Vyama pia vinatoa wawakilishi wagombea wa ngazi mbalimbali wachaguliwe na wananchi. Baada ya hapo mrengo utakatoa utakaotoa Rais na Makamu wake wanaunda serikali kutoka vyama vya mrengo huo. Wakati mwengine waziri mkuu asiwepo wakati mwengine awawepo inategemeana ilimradi wanasiasa wamethia jinsi ya kugawana vyeo. Wakati mwengine Rsis aamue kuendesha serikali na makamu wake au amuache na aendeshe na wapinzani wake. Wakati mwengine makamu wa Rais ampinge Rais na aendeshe shughuli zake za kisiasa kivyake.
 
Gharama ya ujenzi inachangiwa na factor nyingi sana...Kuna gharama ya kuendesha ofisi ambapo utakuta mkandarasi yupo Dar, Kuna gharama ya kusafirisha vifaa kutoka Dar hadi Tabora, unaweza kuta gharama ya kufanya plumbing (piping) ni kubwa sana kutokana na kibanda Cha mlinzi kuwa ghetini ambapo ni mbali kutoka sehemu ya mwisho wa maji taka.

Hapo bado utakuta waya wa Armoured kwa ajili ya kuepeleka umeme kwenye hicho kibanda kimetembea umbali zaidi ya mita 300m kutoka sehemu yenye main panel. Bado Kuna cut and fill kibao ili mandhari yawe mazuri.

Kuna factor nyingi sana, Kama angesema mradi wa Chuo kizima ni kibubwa ingeleta maana, yaani viongozi wanachukulia majengo madogo baada ya final fix.

Hapo bado kuleta miundombinu ya simu kwenye kibanda Cha mlinzi ambapo ni mbali sana na main saver..
 
eee Mungu wetu watu watakoma lini kuiba fedh za umma?!

mara nyingi huwa njiuliza, inakuwaje mpaka Waziri Mkuu afike ndipo ubadhirifu uonekane?!! inamaana viongozi wengine k kt eneo husika huwa wamelala?!
 
Akili za Watanzania ni finyu pamoja na viongozi wetu.
Watanzania wakisikia kuna mtu kasimamishwa kazi au katumbuliwa mioyoni wanapata raha.
Hapa haijaibwa hata mia
Daah huku ni kutafuta sifa na kutrend.
Hicho kibanda ni cha serikali kingejengwa sh ngapi?

1. Posho za ma consultants
2. Site visiting za viongozi???
3. Milango 2 pamoja na finishing 700k
4. Tofali za serikali ni grade one
5. Cement ni grade one( 42.5 )
6. Bati na usafiri wake
7. Plasta
8. Rangi
9. Tiles
10. Malipo ya ufundi..khaa
Kama imepigwa ni 500,000
Takukuru itatumia kiasi gani kujilipa ufuatiliaji?. Hii ni kesi ya wizi wa kifaranga
 
Watu ambao hawajawahi kujenga ndio watashangaa mimi nikikiangalia hicho kibanda mbona pesa hiyo ni halali!.

  1. Kuchimba msingi vibarua 500,00
  2. Kujenga Msingi mawe zege 1,000,000
  3. Kuinua kuta 1,000,000
  4. Madirisha 3 ya PVC za Uturuki 3,000,000
  5. Milango miwili ya Mninga 1,000,00
  6. Bati ya South 1,000,000
  7. Tails za mable 1,000,000
  8. Scatting ya black granite 500,000
  9. Rangi ile washable 500,000
  10. Msimamizi 1,000,000
  11. 10% ya aliyetoa kazi 1,000,000 hapo kuna wizi gani?.
JIfunze kuangalia quality kabla hatujakimbilia kupigia kelele wizi na ufisadi, ujenzi wa majengo yoyote ya umma unatanguliwa na BOQ.
Kwa msio jua quality ya ujenzi, nendeni makaburi ya Kinondoni kuna kaburi pale limegharimu TZS 36.M!.

Mfano mimi natamani tomb stone yangu iwe kama ile ya ku roll, find out how much it costs, tusishabikie tuu ufisadi!.
P
Hapo hakuna tiles za Mable,hakuna scating ya Mable,hakuna pvc windows wala bati ya msouth. Hata kama unaunga juhudi sio hivi.
 
Kwa ujenzi wa kiserikali hiyo bei ni sahihi.
Kuna physibility study ya jengo kikao.
Kuna kunununa eneo kikao.
Kuna kupima udongo wa kiwanja kikao.
Kuna kumtafuta mkandarasi mshauri kikao.
Kuna kutangaza zabuni kikao.
Kuna kumchagua mzabuni kikao.

Vikao vyote vina posho.

Ikijumlisha na ujenzi imara wa hiyo ofisi hiyo gharama ni halari kabisa.
Hapo weka na kunywa bia na nyama choma baada ya kikao,pia weka mafuta ya magari ya mabosi waliopo kwenye kikao.
 
Daah huku ni kutafuta sifa na kutrend.
Hicho kibanda ni cha serikali kingejengwa sh ngapi?

1. Posho za ma consultants
2. Site visiting za viongozi???
3. Milango 2 pamoja na finishing 700k
4. Tofali za serikali ni grade one
5. Cement ni grade one( 42.5 )
6. Bati na usafiri wake
7. Plasta
8. Rangi
9. Tiles
10. Malipo ya ufundi..khaa
Kama imepigwa ni 500,000
Takukuru itatumia kiasi gani kujilipa ufuatiliaji?. Hii ni kesi ya wizi wa kifaranga
Aisee! I was sarcastic sijui wewe.
 
Back
Top Bottom