Upinzani Tanzania una matatizo? Vyama havina Succession Plan hivyo vina Usultani! CHADEMA kuna Usultani? Usultani huu Utakiinua au Utakiangamiza?

We ni mmoja Kati ya mwenye iQ kubwa hapa jamvini na umetumia akili kubwa Sana kumjibu mtu mjinga mwenye kuongozwa na ushabiki.
 
Soon baada ya uchaguzi mkuu 2015 hasa baada ya aliyekuwa waziri mkuu aliyejiuzuru kwa kashfa ya rushwa kupitia kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond ndugu Edward Ngoyayi Lowasa kujiunga Chadema kwa njia zisizojulikana zilizoleta utata, upinzani nchini uli paralyse na mpaka leo haujarudi kwenye line. Nasema hivyo kwa sababu ni kipindi ambacho chama cha mapinduzi (CCM) kilikuwa kimeoza na kupoteza imani kwa watanzania ambao walikiona Chadema kama mkombozi na mbadala wa CCM Tanzania. Kupitia katibu mkuu wa Chadema kipindi hicho Dkt Slaa aliyeichachafya vilivyo serikali ya CCM kwa kashfa kibao hasa za rushwa,huduma mbovu za jamii,uchumi uliokuwa unaporomoka kwa kasi,mfumuko wa bei,uzembe serikalini hakika CCM ilionekana dhahili inaelekea kaburini.
Sifa pekee ziwaendee wazee wa CCM waliomuona Dkt Magufuli kama mbadala hasa kutokana na kambi mbili zilizokuwa na nguvu ndani ya CCM. Ujio wa Magufuli na kuondoka kwa Dkt Slaa Chadema vilikuwa ni pigo kuu kwa upinzani nchini na hakika wasipokuwa makini tutarudi kwenye mfumo wa chama kimoja au CCM itaunda chama kingine cha kuzugia kuonyesha Tanzania tupo kwenye mfumo wa vyama vyingi.
Upinzani ulipo sasa unahitaji damu changa,mawazo mapya yenye kuja na strategies za kupambana na CCM ambayo kupitia serikali yake imejikita kupambana si tu na kero zinazowagusa watanzania hasa masikini lakini pia imeleta maendeleo makubwa katika kipindi kifupi.
Hali hii imepelekea upinzani kuwa wadandiaji wa hoja,huku wakigeuka kuihujumu nchi kupitia kampuni zilizokuwa zinaneemeka na rasilimali nchini lakini pia kupitia serikali za magharibi ambazo kimsingi hawataki kuona waafrika wakipiga hatua.
 
No need of a Succession Plan with this situations of defection from opposition parties to CCM. there is a need of keeping the die hard only who can not be easily be bought ''cheap politicians do not withstand'
 
Kubadilibadili mwisho unalikwaa pandikizi kutoka ccm halafu linaua chama kama walivyokiua chama cha CUF.
Kwani Chadema haijauawa?
Chama kufa ni viongozi kuhama hama kama ilivyo kwa Chadema.
CUF imekufa kutokana na Lipumba na wapambe wake kuwaaminisha watanzania kuwa hakuna mtu anayeweza kuongoza CUF zaidi ya Prof.Lipumba.
Analofanya Mbowe ndilo linalotokea CUF.
Mawazo Mbowe anayowajengea wanachama wake yatakigharimu Chama siku atakayotoka kwani wengi watakosa imani na Kila kiongozi na matokeo yake watakua na migogoro na kutoaminiana wakimuona Kila mtu ni msaliti wa Chama.

Mbowe amekosea sana. Hili wala tusifichane.
 
Nenda shule jifunze juu ya "Succession Plan" umeandika tu
Succession plan ipo CCM. Katoka Mwinyi kamuachia Mkapa, katoka Mkapa kamuachia Kikwete katoka Kikwete kamuachia Magufuli, akitoka Magufuli atamuachia mwingine.

Mbowe ana mwaka wa 15 kakiHkalia kiti, anaelekea mwaka wa 20, hapo ndipo haipo succession plan.

Na succession plan ya CCM inashuka mpaka kwa vijana, Mwalimu Nyerere aliwalea kina Mkuchika, Chiligati na Kikwete.

Wao wanawalea kina Makonda, Hapi, Herry James na wengine watakaowaandaa wadogo zao siku zijazo.
 
Umetumia nguvu kubwa sana kujenga hoja yako, ukasahau enzi za TAA na hizi za kidigitali ni vitu viwili tofauti.
 
Hawezi kuweka mazingira sawa na vyama vinavyojenga Ukabila nchini.
Kumbuka yule naye ni mwenyekiti wa Chama.
Na yeye anatumia nguvu yake kujenga chama chake na kuwaaminisha watanzania kuwa bila yeye hakuna Maendeleo ya Chama chake cha CCM wala maendeleo ya nchi.
Mbowe alione hilo kwanza.

Kuna agenda gani nyuma ya Huo Ukabila anaoutumia Mbowe kama silaha yake ya kukijenga Chama?

Mbowe alikua na nafasi kubwa ya kumkabidhi mtu mwingine kama John Heche Chama ili kashfa ya Ukabila ihame. Hata mtu akiitisha maandamano makubwa yanakua na sura ya Kitaifa na sio sura ya kupigania maslahi binafsi ya ukoo.

Demokrasia haiji kwa kujigamba kuwa wewe ndio sio msaliti.
Demokrasia inapiganiwa ndio maana Lisu amepata kilama kwa kupigania Demokrasia na mpaka sasa anaonekana kama mkimbizi.
Sio hawa akina Mbowe wana vikesi mbuzi halafu wanalia lia tu.
 
Wenyewe wanasema ''kwa hali ilivyo sasa Mbowe tu ndiye anaweza kukiongoza Chama'' tafsiri yake ni kuwa bila Mbowe chadema haipo, yeye ndiye ''mrithi'' mwenye uchungu na chama.
 
Tatizo kubwa na utawala wa nchi ni CCM. Tatizo la uongoza mbaya ndanibya CCM ni CCM. Tatizo la uongozi ndani ya vyama vya siasa vya upinzani ni CCM.

CCM inaendesha siasa za hila, uwongo, udanganyifu, udikteta na kwa kiasi fulani siasa za kigaidi. Siasa ovu za CCM zinajenga hali ya kutoaminiana ndani ya vyama vya siasa vya upinzani kiasi kwamba wengi wafia vyama ndani ya vyama vya siasa vinaona aheri kubakia na viongozi hao hao wanaoaminika kuwa siasa mamluki na wasioweza kununulika kwa muda mrefu, hata kama hawataleta mabadiliko kuliko kumpa uongozi mtu ambaye kesho wakasikia ameunga mkono juhudi.

CCM itakapokuwa na siasa nzuri, itasababisha serikali kuwa na utawala mzuri, itasababisha vyombo vya ulinzi na usalama kusiamamia sheria na kutenda haki, mahakama kutoa haki na Bunge kufanya kazi mujibu wa katiba na kwa maslahi ya nchi. Mazingira hayo yatakapokuwepo, tutashuhudia uongozi na demokrasia kila mahali, pamoja na ndani ya vyama vya upinzani.

Kwa sasa CCM inanajisi kila mahali. Kila mahali inapakaza uchafu. Inanajisi vyombo vya ulinzi na usalama, inanajisi mfumo wa mahakama, inalinajisi Bunge mpaka taasisi za Elimu kiasi cha kuwa na wasomi wasiokuwa na akili kama hawa maprofesa wa majalalani, madokta wanaoweza kumtisha na kumwelekeza msajili wa vyama namna ya kufanya kazi, n.k.
 
Kuwa na digrii si kigezo cha kuijua siasa na wala sio kigezo cha kujifanya kila kitu unajua na wala haimaanishi wasiokuwa na digrii hawaelewi kila kitu tunajua unayasema hayo kwa ajili gani na ukikazana najua utafanikiwa kwa sababu umesoma alama za nyakati huko nyuma usingefanikiwa ww ukitaka kujua kama cdm ipo au itakufa shawishi haya uwanja sawa wa siasa ....katiba huru....tume huru....uhuru wa habari.... mbowe kuendelea....alafu upime kwenye uchaguzi
Lakini swala la uchaguzi wa chama ni la wanachama wenyewe m navyozidi kumkataa mbowe ndio mnavyozidi kuwashitua watu haiwezekani chama A kimkatae kiongozi wa cham B halafu wanachama waunge mkono hata chama chenu kinalazimisha mtu mmoja kuwa na vyeo 2 chamani na serekalini kama unafikiri ni rahisi anzia kwenu kuondoa huo usultani ni lazima chama chochote kiunde safu imara na yenye mafanikio na ndio maana lissu amepangwa bado katibu mkuu ni lazima aandaliwe kila safu inapangwa kutokana safu iliopo kwa wakati husika sasa ngonjera zenu haziwezi kuyumbisha msimamo wa wanachama
 
Sio kweli.
Wamarangu wapo na TLP.
Hata Wamachame wengi wangependa kuona mabadiliko.

Kuna watu kama John Heche na Lisu wanakubalika sana kwa watanzania.

Wachaga hawamshabikii Mbowe Bali hoja za watu kama ilivyokuwa kwa Dr. Slaa.
Mbowe amekua mjanja sana kuwatumia watu wenye hoja nzito kwenye chama.

Chadema itazorota sio kwa sababu ya kumkosa Mbowe Bali kwa sababu ya kukosa mtu sahihi wa kupigania Demokrasia.
Mbowe angekua makini angepigania bunge live na kuhakikisha kuwa Uhuru wa kisiasa unakuwepo.
Mbowe ni MTU dhaifu sana sana ndio maana busara zake ni za upande mmoja tu wa kuvumilia na kukosa majawabu ya kuzorota kwa demokrasia nchini kuanzia ndani ya chama chake.
Hata kung'atuka lilikua ni jawabu sana kwa mustakabali mpana wa vizazi vijavyo.
Kuna wakati mwingine busara ya mzazi inakua ni kumchapa mtoto anapokosea .
 
Kwani Chadema haijauawa?
Tokea nihamie Chadema nimegundua pamoja na ccm kutumia mabilioni ya fedha za walipakodi masikini ili kuhakikisha Chadema kinakufa imeshindikana.
Ndani ya Chadema kuna watu makini sana sana na wanaijua mikakati ya chama cha ccm

Uongo mbaya ccm ndio iliyojiua yenyewe ccm kwa sasa inategemea mtutu na uhuni kutawala.
 
Nonsense
 
Mbowe na mashabiki wake mnaupotosha umma.
Enzi hizo hapakua na Harakati za kidemokrsia Bali kudai Uhuru wa mtu mweusi kujitawala mwenyewe.

Hata hivyo kwenye harakati hizo za kudai Uhuru hakunawenyekiti aliyekaa muda mrefu kwenye Chama.
Nyerere alikaa muda mrefu baada ya kupata Uhuru sio labla.
Kabla ya Uhuru watu walikua wanaachiana kulingana na uwezo na Mawazo mapya ili kusongesha mbele mapambano ya kudai Uhuru.


Kwa sasa ni zama za kupigania Demokrasia . Ni lazima ionekane kwa vitendo ikijengwa kuanzia Chini vinginevyo tunaandaa vyama vibovu kuliko CCM kututawala kwa mabavu zaidi kwani katiba yetu ni ya kimabavu.
Hatuwezi kuwa na katiba ya nchi ya kimabavu na vyama vya kimabavu tutapoteza kabisa Demokrasia kwa vizazi vyetu.

Je, tujifunze wapi Demokrasia kama Chama cha Demokrasia kinaendesha mambo yake kidikteta.?
 
Succession plan ipo CCM. Katoka Mwinyi kamuachia Mkapa, katoka Mkapa kamuachia Kikwete katoka Kikwete kamuachia Magufuli, akitoka Magufuli atamuachia mwingine.
Na kuhakikishia hiyo Successful plani ya Ccm iliyo undwa na Magu akiondoka leo ni vita kuu ndani ya Ccm na nchi kwa ujumla kwani itakuwa visasi kwenda mbele Mungu tusimamie hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…