mshamba_mwingine
JF-Expert Member
- Jul 23, 2023
- 1,057
- 4,145
mzee shikamoo...vipi kuhusu chimbuko
wewe si umeishi kwenye ndoa muda mrefu,
inaondoa upweke kweli?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mzee shikamoo...vipi kuhusu chimbuko
MTIBELI🙂....treekengeleUPWEKE UMEWAANZA VIJANA MAPEMA, UZEENI SIJUI ITAKUWAJE. NI JANGA KUBWA.
Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Huwezi sema unafurahia maisha ukiwa pekeako. Mtu mpweke hawezi kuwa na furaha. Mpweke ni tafsiri halisi ya maiti inayoishi.
Utoto ni raha kwa sababu utoto unahusisha ushirikiano wa mtoto na watoto wenzake. Mtoto na wazazi. Mtoto na michezo. Ndio maana mtoto katika umri wa utoto Unaowajibu wa kumfanya ashirikiane na watoto wengine. Na sio uanze kumfungia ndani kama mfungwa.
Upweke ndio hufanya kijana au binti aoe. Mapenzi ni moja ya tiba ya upweke. Ukiwa na mtu mnayependana na kuelewana automatically upweke utakuwa umedhibitiwa.
Njia nyingine ya kudhibiti upweke ni kujihusisha na vikundi vya kijamii, kidini pamoja na michezo. Lakini hivi ni wakati ukiwa nje ya nyumba yako. Nyumbani ukirudi kama huna mpenzi iwe mke au mume ambaye mnapendana. Utaiona siku ni ndefu na mara nyingi utayaona maisha hayana maana.
Vijana wa sasa wapo vile uwaonavyo, ni kama hawana utulivu, wamechanganyikiwa, wengi wao ni kwa sababu ya Upweke. Upweke unaleta Sonona kama sio Depression. Upweke ni chanzo cha Kifo.
Mabinti wengi ninaowasiliana nao na ambao wanapata huduma kwangu wanakabiliwa na changamoto ya upweke. Wanaishi wenyewé. Wengi wao ni kati ya miaka 22-40. Unakuta Mwanamke amepanga chumba au nyumba anaishi mwenyewe au na watoto, hana mume.
Pia vijana nao wengi wenye umri huo wapo single. Na wanaishi vikundi vikundi kwenye Maghetto yao. Licha ya kuishi vijana kuanzia wawili lakini bado upweke unawasumbua. Hii ni kwa sababu. Wao sio familia moja.
Familia ni Mume, mke na watoto.
Kuanguka kwa taasisi ya ndoa kumeongeza Upweke ndani ya jamii. Na hii itachukuliwa kama fursa kwa wamiliki wa mitandao ya kijamii kwani Watu wengi hutumia mitandao kama sehemu ya kudhibiti upweke.
Upweke ubaya wake upo siku za Weekend kwa wale wanaofanya kazi. Lakini pia upweke huonekana Dhahiri nyakati za usiku Watu wanaporudi kupumzika majumbani kwao.
Wapo Watu ambao usiku kwao hauna faida.
Sababu nyingine kubwa ya wanaume kufa mapema zaidi ni hiihii, UPWEKE. Mtu mpweke hulazimika kufa mapema kutokana na matatizo kama ya msongo wa mawazo.
Wanawake kwa upande wao muda mwingi huweza kuutumia na watoto waliowazaa kuwalea kama kuwabembeleza, kuwaogesha, kuwalisha chakula, kupishana nao kelele, kucheza nao.
Lakini vipi kwa mwanaume?
Mwanaume zaidi ya kwenda Bar kutuliza nafsi na kuondoa upweke ambao kimsingi hauondoki hana pengine pamoja kukimbilia.
Jambo moja lazima ulielewe, Taikon kama Mastermind ninakuambia Upweke huwezi uondoa na Watu Baki. UPWEKE unaondolewa na Watu unaowapenda na unaostahili kuwapenda. Upweke unahusu Moyo. Hisia za UPENDO.
Mke au Mume ndio mtu wa kwanza kuondoa upweke wako.
Kisha Watoto wako.
Alafu Wazazi wako.
Ndipo ndugu na marafiki.
Niliwahi kufanya uchunguzi wa kuona ni namna gani mtu Baki anaweza kukuondolea upweke nikagundua kuwa ni ngumu sana. Ni kwa sababu akili italazimisha moyo u-pretend kuwa haupo pweke.
Kama utaenda Kasino ukachukua Kahaba hata wawili au watatu kwaajili ya kukuondolea upweke, utagundua ya kuwa hawawezi kufanya jambo hilo kwa sababu wao wapo kwaajili ya kujifurahisha kimwili na sio kinafsi(Moyo).
Mtu aliyempweke huweza kufanya lolote la hatari. Upweke huathiri mtu kisaikolojia na huweza msababishia mtu kukosa UTU.
Mtu akikosa anayemjali na wanaomjali moyo wa kujali wengine huanza kufa polepole. Na kama utakufa kabisa utu huondoka nafsini mwake.
Ushauri kwa vijana,
Wapende na kaa karibu na Wazazi wako. Husaidia kuondoa upweke.
Tafuta familia, mke au mume, naye huondoa upweke.
Kuwa na watoto kisha fanya wajibu wako kama mzazi kwa hao watoto.
Kukosa familia ni kukosa maana halisi ya maisha.
Acha Nipumzike sasa
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Na wanao zaliwa mapachaHuman being is supposed to be a lonely creature, umekuja mwenyewe na utaondoka mwenyewe. Hao watu wengine kwa kweli ni ghasia tu
Chimbuko la nini mkuuvipi kuhusu chimbuko
MTIBELI🙂....treekengele
Umezunguka kote lengo lako ni ndoa
Siwezi kua mpweke wakati wanawake wazuri (nyumbu) wenye shape wamejaa mtaani[emoji23][emoji23] mapigo na mwendoUPWEKE UMEWAANZA VIJANA MAPEMA, UZEENI SIJUI ITAKUWAJE. NI JANGA KUBWA.
Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Huwezi sema unafurahia maisha ukiwa pekeako. Mtu mpweke hawezi kuwa na furaha. Mpweke ni tafsiri halisi ya maiti inayoishi.
Utoto ni raha kwa sababu utoto unahusisha ushirikiano wa mtoto na watoto wenzake. Mtoto na wazazi. Mtoto na michezo. Ndio maana mtoto katika umri wa utoto Unaowajibu wa kumfanya ashirikiane na watoto wengine. Na sio uanze kumfungia ndani kama mfungwa.
Upweke ndio hufanya kijana au binti aoe. Mapenzi ni moja ya tiba ya upweke. Ukiwa na mtu mnayependana na kuelewana automatically upweke utakuwa umedhibitiwa.
Njia nyingine ya kudhibiti upweke ni kujihusisha na vikundi vya kijamii, kidini pamoja na michezo. Lakini hivi ni wakati ukiwa nje ya nyumba yako. Nyumbani ukirudi kama huna mpenzi iwe mke au mume ambaye mnapendana. Utaiona siku ni ndefu na mara nyingi utayaona maisha hayana maana.
Vijana wa sasa wapo vile uwaonavyo, ni kama hawana utulivu, wamechanganyikiwa, wengi wao ni kwa sababu ya Upweke. Upweke unaleta Sonona kama sio Depression. Upweke ni chanzo cha Kifo.
Mabinti wengi ninaowasiliana nao na ambao wanapata huduma kwangu wanakabiliwa na changamoto ya upweke. Wanaishi wenyewé. Wengi wao ni kati ya miaka 22-40. Unakuta Mwanamke amepanga chumba au nyumba anaishi mwenyewe au na watoto, hana mume.
Pia vijana nao wengi wenye umri huo wapo single. Na wanaishi vikundi vikundi kwenye Maghetto yao. Licha ya kuishi vijana kuanzia wawili lakini bado upweke unawasumbua. Hii ni kwa sababu. Wao sio familia moja.
Familia ni Mume, mke na watoto.
Kuanguka kwa taasisi ya ndoa kumeongeza Upweke ndani ya jamii. Na hii itachukuliwa kama fursa kwa wamiliki wa mitandao ya kijamii kwani Watu wengi hutumia mitandao kama sehemu ya kudhibiti upweke.
Upweke ubaya wake upo siku za Weekend kwa wale wanaofanya kazi. Lakini pia upweke huonekana Dhahiri nyakati za usiku Watu wanaporudi kupumzika majumbani kwao.
Wapo Watu ambao usiku kwao hauna faida.
Sababu nyingine kubwa ya wanaume kufa mapema zaidi ni hiihii, UPWEKE. Mtu mpweke hulazimika kufa mapema kutokana na matatizo kama ya msongo wa mawazo.
Wanawake kwa upande wao muda mwingi huweza kuutumia na watoto waliowazaa kuwalea kama kuwabembeleza, kuwaogesha, kuwalisha chakula, kupishana nao kelele, kucheza nao.
Lakini vipi kwa mwanaume?
Mwanaume zaidi ya kwenda Bar kutuliza nafsi na kuondoa upweke ambao kimsingi hauondoki hana pengine pamoja kukimbilia.
Jambo moja lazima ulielewe, Taikon kama Mastermind ninakuambia Upweke huwezi uondoa na Watu Baki. UPWEKE unaondolewa na Watu unaowapenda na unaostahili kuwapenda. Upweke unahusu Moyo. Hisia za UPENDO.
Mke au Mume ndio mtu wa kwanza kuondoa upweke wako.
Kisha Watoto wako.
Alafu Wazazi wako.
Ndipo ndugu na marafiki.
Niliwahi kufanya uchunguzi wa kuona ni namna gani mtu Baki anaweza kukuondolea upweke nikagundua kuwa ni ngumu sana. Ni kwa sababu akili italazimisha moyo u-pretend kuwa haupo pweke.
Kama utaenda Kasino ukachukua Kahaba hata wawili au watatu kwaajili ya kukuondolea upweke, utagundua ya kuwa hawawezi kufanya jambo hilo kwa sababu wao wapo kwaajili ya kujifurahisha kimwili na sio kinafsi(Moyo).
Mtu aliyempweke huweza kufanya lolote la hatari. Upweke huathiri mtu kisaikolojia na huweza msababishia mtu kukosa UTU.
Mtu akikosa anayemjali na wanaomjali moyo wa kujali wengine huanza kufa polepole. Na kama utakufa kabisa utu huondoka nafsini mwake.
Ushauri kwa vijana,
Wapende na kaa karibu na Wazazi wako. Husaidia kuondoa upweke.
Tafuta familia, mke au mume, naye huondoa upweke.
Kuwa na watoto kisha fanya wajibu wako kama mzazi kwa hao watoto.
Kukosa familia ni kukosa maana halisi ya maisha.
Acha Nipumzike sasa
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Siwezi kua mpweke wakati wanawake wazuri (nyumbu) wenye shape wamejaa mtaani mapigo na mwendo View attachment 2925136
Mkuu,tamthilia zinakuharibu
Ibu yule pale, yuko hoi kitandani mke chap kambambikizia kesi, kaondoa na savings zake zote
Davis Mosha, yule pale, mke linamuibia kimya kimya, kuja kusanuka, too late
bado linataka nusu ya mali, pumbav kabisa
jidanganye tu, endeleeni kufuga majambazi
ni swala la mda kabla vilio kusikika
Nadhani watu wengi wanao angukia katika kundi hili ni matokeo ya past trauma alizoziona akikua, au ni issue za family background, au ni mambo aliyoyapitia yeye mwenyewe.Ujinga tu mnajazwa mitandaoni.
Tupe historia ya maisha ya NDOA ya wazazi wako kabla hujasoma NDOA haifai,
Ukute chanzo ni familia uliyokulia.
ndiyo maana kuna hospitali mzeeUkipata changamoto za ugonjwa
Wewe umelichukulia kwa upande wa ugonjwa. Hiyo ni sehemu kidogo sana ya maana nzima ya yaliyo andikwa. Hospital zipo na zinatibu wagonjwa, sijui kama umewahi kuwa na mgonjwa anayehitaji huduma ya karibu na ukamuhudumia akiwa hospitali au hali hiyo kukupata wewe?.ndiyo maana kuna hospitali mzee
kwa ivyo mnaoa ili msaidiwe mkiwa wagonjwa ?
Afrika bana
mwenzako huyu hapa kaliwa nusu ya mali zake kwa upumbavu wa ndoa
Hukumu ya kesi ya ndoa inakaribia kusomwa, anataka tugawane mali wakati alinikuta nimesimama. Sitaki hilo litokee, nachanganyikiwa
Nahisi kuchanganya sana, hukumu tar 8 mwezi huu, shida yangu sio kuachana naye au kwamba siwezi maisha bila yeye bali naumia sana swala kugawana mali kichwa inawaka moto na katika ukweli amenikuta tayari nina maisha yangu, nyumba viwanja na mengine ila leo hii anataka mgawanyo. Naamini kabisa...www.jamiiforums.com
Ndoa zilikuwa zamaniWewe umelichukulia kwa upande wa ugonjwa. Hiyo ni sehemu kidogo sana ya maana nzima ya yaliyo andikwa. Hospital zipo na zinatibu wagonjwa, sijui kama umewahi kuwa na mgonjwa anayehitaji huduma ya karibu na ukamuhudumia akiwa hospitali au hali hiyo kukupata wewe?.
Nimeuliza, je mama na ndugu zako nao unawaweka kwenye kundi hilo hilo?, kwa maana ni kweli mzazi wako wa kike alikuwa na tabia unazotuambia kuwa wanawake wote wanazo?, je ni kweli ndugu zako wote wa kike wana tabia kama za wanawake unawazungumzia?.
Je unajua umuhimu wa makuzi ya baba ndani ya nyumba/jamii (father figure). Amini nakwambja, kuna wakati tunachangia kutengeneza jamii dhaifu ya vizazi vijavyo kwa ajili tu ya mitazamo yetu hasi kuhusu hizi jamii.
Labda uniambie kwa mtizamo wako, huna sababu ya kuoa na wala huna sababu ya kuwa na watoto. Kama una sababu ya kuwa na watoto, embu wape nafasi ya kulelewa katika nafasi ya kuwa na mwanaume kiongozi katika maisha yao.
Hii inaenda hata kwa wale anaosema nitazaa tu, nitalea mwenyewe kwakuwa ninajiweza. Tunatengeneza jamii ambayo baadaye itapata changamoto nyingi sana huko mbeleni.
Hili unaweza kuliona lina mantiki kama hatuta lizungumza kwa ushabiki.
Wengi wamepigwa na kitu kizito kichwani.
Japo pia,walio na ndoa ama familia pia wapo wanaohangaika mpaka wanatamani siku zingerudi nyuma waanze upya kwenye kuchagua wenza.
Unakuta familia Ina Kila kitu,ila Mwanaume kurudi home usiku,kutoka alfajili na mapema.
Anakaa masaa kama 5.
Hivyo msongo kama upo Kwa mgawanyo mkuu.
Kikubwa amini kile kinachokufaa.
Maisha ni mahesabu.