Ushauri: Chakula Bure mashuleni kirudishwe ili kuboresha uelewa wa wanafunzi

Ushauri: Chakula Bure mashuleni kirudishwe ili kuboresha uelewa wa wanafunzi

kilimanjaro asilimia kubwa za shule wanakula shuleni sijajua kwa miongo ya karibuni ila nimesoma msingi toka std 3 mpaka O level nikiwa nakula shuleni.
Na sec ilikuwa pia shule ya kata tena ugali maharage,wali nyama, wali maharahe, ugali nyama, makande. asubuhi uji wa sukari unatiwa mafuta na mboga za majani tulikwa na bustani za kutosha.
Shule nyingine mzazi anapeleka mahindi na maharage kwaajili ya chakula cha mtoto, nadhani wale ambao hawapeleki, watoto wao wanashinda njaa
 
Wazo zuri, sema wazazi waelimishwe kutoa michango, ila kusema serikali iwalipie kila kitu ni kulemezana,
Halafu hapo hapo serikali itapata kichaka cha kutoongeza mishahara au kuajiri
Wazazi wachangie wanapoweza,

Mikoa ya Moshi na Kilimanjaro wamefanikiwa,

Nachosema, Kwa mikoa yenye hamasa ya chini, wabunge waongeze juhudi, waombe michango Kwa banks, companies na asasi zingine, pungufu ya hapo waombe serikalini,

Pia jambo hili la chakula mashuleni liwe la kitaifa Nchi nzima.

Nchi yetu ni ya wakulima, Serikali haiwezi shindwa kuhakikisha mtoto anapata kikombe Cha uji.🙏🙏
 
Shule nyingine mzazi anapeleka mahindi na maharage kwaajili ya chakula cha mtoto, nadhani wale ambao hawapeleki, watoto wao wanashinda njaa
naona hili mikoa mingi ijifunze kwa weli maana mpaka sasa hivi shule za msingi kijijini kwetu wanakula
 
Shule nyingine mzazi anapeleka mahindi na maharage kwaajili ya chakula cha mtoto, nadhani wale ambao hawapeleki, watoto wao wanashinda njaa
Ndo hapo tutafute sababu za wazazi kutochangia,

Kama ni Umaskini ndo chanzo, Serikali iweke mkono wake.
 
naona hili mikoa mingi ijifunze kwa weli maana mpaka sasa hivi shule za msingi kijijini kwetu wanakula
Huku mijini ni mtihani ndugu yangu,

Wanashindia ubuyu Kwa kuomba wenzao wenye uwezo.

Jambo hili ni muhimu likawa flat Nchi nzima.
 
Wazazi wachangie wanapoweza,

Mikoa ya Moshi na Kilimanjaro wamefanikiwa,

Nachosema, Kwa mikoa yenye hamasa ya chini, wabunge waongeze juhudi, waombe michango Kwa banks, companies na asasi zingine, pungufu ya hapo waombe serikalini,

Pia jambo hili la chakula mashuleni liwe la kitaifa Nchi nzima.

Nchi yetu ni ya wakulima, Serikali haiwezi shindwa kuhakikisha mtoto anapata kikombe Cha uji.🙏🙏
Hakuna chochote cha kuomba mzee, tusiwe omba omba ndo mwisho tunatengeneza kizazi cha ombaomba,
Watoto ni wa wazazi, hivyo wao watoe michango yote, watoto walishwe na wazazi wao na wajue jinsi wazazi wanavyoteseka hivyo waongeze juhudi.

Kuombaomba tutalea kizazi ambacho hata kusafisha mtaro wa barabaran wanasema serikali iingilie kati 🤣
 
Poleni "wadanganyika" chakula hakirudi kamwe mpaka siku mkijitambua.

Watoto wao hawasomi huko kwenye njaa , wamewaachia nyinyi.

Ukimuangalia huyo dogo hapo na nembo ya shule aliyopo unafikiri anaelewa kitu kinachoitwa njaa?

Siku akija kuwa kiongozi kwa mfumo huu wa vimemo, kujuana , kutembelea jina la baba atajua kuna shule huko Ikwiriri wanafunzi wanashinda njaa?

Never .
images.jpeg
 
Hakuna chochote cha kuomba mzee, tusiwe omba omba ndo mwisho tunatengeneza kizazi cha ombaomba,
Watoto ni wa wazazi, hivyo wao watoe michango yote, watoto walishwe na wazazi wao na wajue jinsi wazazi wanavyoteseka hivyo waongeze juhudi,
Kuombaomba tutalea kizazi ambacho hata kusafisha mtaro wa barabaran wanasema serikali iingilie kati 🤣
Kwahiyo tusitoe ushuru masokoni Ili tuzoe taka wenyewe,

Au tugomee tozo za mazao tunazolipia Ili tupate pesa ya kuwapa watoto shuleni?
 
Poleni "wadanganyika" chakula hakirudi kamwe mpaka siku mkijitambua.

Watoto wao hawasomi huko kwenye njaa , wamewaachia nyinyi.

Ukimuangalia huyo dogo hapo na nembo ya shule aliyopo unafikiri anaelewa kitu kinachoitwa njaa?

Siku akija kuwa kiongozi kwa mfumo huu wa vimemo, kujuana , kutembelea jina la baba atajua kuna shule huko Ikwiriri wanafunzi wanashinda njaa?

Never .
View attachment 2763968
Ni ubinafsi tu,

Madelu alikula chakula Cha Bure Cha Nyerere!!
 
Poleni "wadanganyika" chakula hakirudi kamwe mpaka siku mkijitambua.

Watoto wao hawasomi huko kwenye njaa , wamewaachia nyinyi.

Ukimuangalia huyo dogo hapo na nembo ya shule aliyopo unafikiri anaelewa kitu kinachoitwa njaa?

Siku akija kuwa kiongozi kwa mfumo huu wa vimemo, kujuana , kutembelea jina la baba atajua kuna shule huko Ikwiriri wanafunzi wanashinda njaa?

Never .
View attachment 2763968
Wananchi wa Jimbo la Iramba, tumkatae Madelu nchemba uchaguzi ujao sababu ni kiongozi wa Umma na waziri lakini anatusaliti kupeleka mwanae private school ilhali anasahau shule za kata.

Tunahitaji viongozi aina ya Mwl Nyerere na Magu ambao watoto wao walisoma shule za kata za Serikali. Na walijali elimu
 
Kiongozi wetu mkuu wa sasa ni mama na mwenye vichengerwa kadhaa, tafadhali unaweza kukumbukwa hata Kwa hili jambo dogo lenye mchango mkubwa sana mbeleni.
Mwenye shibe atamkumbuka mwenye njaa nchi hii!!!?
 
Twende haraka kwenye mada.


Mama mwenye Upendo Kwa wanae, Yuko radhi ashinde njaa, ajinyime kununua kipande Cha kanga Ili mtoto wake apate kula chakula na kupata mahitaji muhimu, Watoto mashuleni katika shule za kata ni watoto wa Serikali wawapo mashuleni.

Viongozi wengi wa juu waliopo sasa ni mashuhuda kuwa zamani wanafunzi tulikula mashuleni Bure uji, ugali wa wanga, Hadi maziwa, tulionekana Kwa nje maskini lakini tulipata huduma muhimu ya CHAKULA muhimu shuleni na Elimu ilipaa na kuthaminika sana. Nini kimetokea, mbona mmebadilika ghafula?

Wazazi wanapokabidhi watoto wao Kwa Serikali kupitia shule za kata Ili wapewe Elimu, ni JUKUMU la Serikali kuhakikisha watoto wanapatachochote kitu tumboni Ili masomo yaeleweke na kumrahisishia mwalimu kufundisha Kwa muda wawapo shuleni.


ELIMU Bora inachagizwa na Mazingira Bora ya kufundishia kama madarasa, walimu wenye Viwango Bora, Madawati, nk nk

Uwezo wa kulisha wanafunzi wetu tunao, Nia tunayo? Ari tunayo kuhakikisha watoto wanapata chakula Bure mashuleni.?

Kuna watoto shule za msingi na sekondari wanatembea zaidi ya 5km kwenda na kurudi shuleni, na hurudi jioni saa kumi Hadi 12 jioni bila kula chochote shuleni, kusoma imekuwa ADHABU?

Nikisema Serikali itoe chakula Bure mashuleni, haimaanishi Bure, wazazi wanalipa Kodi serikalini Kwa njia mbalimbali.

Pia wazazi wengi Hasa wazazi wakulima wanalima chakula na kikiuza katika maghala ya Serikali.

Hivyo pakiwepo Nia thabiti, tunaweza kuhakikisha tunaanza japo na UJI mashuleni, wanafunzi wapate japo kikombe kimoja.

Shule Zina Utaratibu wa kuwafungia watoto mashuleni Hadi jioni saa kumi bila kula chochote.

Nauliza, hivi mtoto wa MKULIMA aliyetoka nyumbani bila kula chochote nyumbani wazazi wakienda shambani kulima, anawezaje kuelewa nasomo darasani bila kula chochote ?

Narudia tena, Serikali haitapata HASARA yoyote kuhakikisha wanafunzi wanapata japo kikombe Cha uji mashuleni Nchi nzima.

Kiongozi wetu mkuu wa sasa ni mama na mwenye vichengerwa kadhaa, tafadhali unaweza kukumbukwa hata Kwa hili jambo dogo lenye mchango mkubwa sana mbeleni.

Angalizo: Katika chaguzi zijazo msipokuja na HOJA nzito na muhimu kama Chakula mashuleni, maji safi, Nishati ya umeme shule za vijijini Kwa wanafunzi kujisomea usiku,sahauni kuchaguliwa.

Karibuni, Amen.
Hiyo hoja isubiri kwanza tumalize mambo muhimu:
  • tuwalipe kwanza mafao wenza wa wastaafu.
  • tutor kwanza elimu ya katiba
- tupeleke kwanza wasanii wakajifunze uendeshaji wa bandari Dubai.
 
Hiyo hoja isubiri kwanza tumalize mambo muhimu:
  • tuwalipe kwanza mafao wenza wa wastaafu.
  • tutor kwanza elimu ya katiba
- tupeleke kwanza wasanii wakajifunze uendeshaji wa bandari Dubai.
Tanzania nchi yangu😭
 
Enyi viongozi mnaofanya biashara serikalini, hamwoni kuwa Kwa namna moja au ingine mnahujumu uwezekano wa Nchi kurudisha chakula Bure Kwa wanafunzi mashuleni?
 
Twende haraka kwenye mada.


Mama mwenye Upendo Kwa wanae, Yuko radhi ashinde njaa, ajinyime kununua kipande Cha kanga Ili mtoto wake apate kula chakula na kupata mahitaji muhimu, Watoto mashuleni katika shule za kata ni watoto wa Serikali wawapo mashuleni.

Viongozi wengi wa juu waliopo sasa ni mashuhuda kuwa zamani wanafunzi tulikula mashuleni Bure uji, ugali wa wanga, Hadi maziwa, tulionekana Kwa nje maskini lakini tulipata huduma muhimu ya CHAKULA muhimu shuleni na Elimu ilipaa na kuthaminika sana. Nini kimetokea, mbona mmebadilika ghafula?

Wazazi wanapokabidhi watoto wao Kwa Serikali kupitia shule za kata Ili wapewe Elimu, ni JUKUMU la Serikali kuhakikisha watoto wanapatachochote kitu tumboni Ili masomo yaeleweke na kumrahisishia mwalimu kufundisha Kwa muda wawapo shuleni.


ELIMU Bora inachagizwa na Mazingira Bora ya kufundishia kama madarasa, walimu wenye Viwango Bora, Madawati, nk nk

Uwezo wa kulisha wanafunzi wetu tunao, Nia tunayo? Ari tunayo kuhakikisha watoto wanapata chakula Bure mashuleni.?

Kuna watoto shule za msingi na sekondari wanatembea zaidi ya 5km kwenda na kurudi shuleni, na hurudi jioni saa kumi Hadi 12 jioni bila kula chochote shuleni, kusoma imekuwa ADHABU?

Nikisema Serikali itoe chakula Bure mashuleni, haimaanishi Bure, wazazi wanalipa Kodi serikalini Kwa njia mbalimbali.

Pia wazazi wengi Hasa wazazi wakulima wanalima chakula na kikiuza katika maghala ya Serikali.

Hivyo pakiwepo Nia thabiti, tunaweza kuhakikisha tunaanza japo na UJI mashuleni, wanafunzi wapate japo kikombe kimoja.

Shule Zina Utaratibu wa kuwafungia watoto mashuleni Hadi jioni saa kumi bila kula chochote.

Nauliza, hivi mtoto wa MKULIMA aliyetoka nyumbani bila kula chochote nyumbani wazazi wakienda shambani kulima, anawezaje kuelewa nasomo darasani bila kula chochote ?

Narudia tena, Serikali haitapata HASARA yoyote kuhakikisha wanafunzi wanapata japo kikombe Cha uji mashuleni Nchi nzima.

Kiongozi wetu mkuu wa sasa ni mama na mwenye vichengerwa kadhaa, tafadhali unaweza kukumbukwa hata Kwa hili jambo dogo lenye mchango mkubwa sana mbeleni.

Angalizo: Katika chaguzi zijazo msipokuja na HOJA nzito na muhimu kama Chakula mashuleni, maji safi, Nishati ya umeme shule za vijijini Kwa wanafunzi kujisomea usiku,sahauni kuchaguliwa.

Karibuni, Amen.
Ni mwaka gani palikuwa na chakula mashuleni?.
 
Chakula Serikali ilichotunza katika maghala, itoe kidogo Kwa watoto Walio mashuleni wapate japo uji🙏
 
Back
Top Bottom