Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hahahhaa.... umenichekesha sana we jamaa...Hahaha... Akikujibu na mimi nitai copy hiyo sentensi niwe naitumia...
Asante mkuuMzee mwenzangu,pole sana kwa hilo tatizo,shusha pumzi,jipe nafasi kidogo upunguze hasira na jazba,halafu kaa chini wewe na binti tu,zungumza nae,kwa ukweli na uwazi,jukumu la kumlea mtoto ni lako wewe kumpa miongozo sahihi na kumrekebisha pale anapokosea,sioni kwa nini uwakaribishe watu wengine katika tatizo hili ni mtoto,kwangu mimi naona ni mapema sana.
Zungumza na mtoto kirafiki kabisa,kumbuka kwa kizazi hiki watoto wetu wanakuwa watu wazima wakiwa na miaka 10 tu huo ndio uhalisia,mueleze alivyokuumiza na mueleze jinsi ambavyo unamthamini kiasi kwamba hujamwambia mtu mwingine yoyote tatizo hili,zungumzeni kwa uwazi,urafiki na upendo,naamini binti atajenga imani na wewe,na atakueleza kwa kina kinachoendelea,kutokea hapo utaelewa ukubwa wa tatizo ulilonalo na utapata njia sahihi ya kudeal nalo,
Pole sana,ulezi kazi ngumu sana mshirikishe na MUNGU pia kwenye hii kazi.
Kingine jitahidi kubadili tabia yako kadri utakavyoweza ili kwenda sambamba na binti,mfano ukali,ulevi,kuchelewa kurudi home na kutompa nafasi ya kuongea nae.
Mke umemkatia tamaa,mtoto unamkatia tamaa,kwakweli hiyo nyumba niyahatari sana,kimaadili.[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].kiukweli mimi uwa sipendi UPEKUZI.MAANA UTAJIPA PRESHA.
Sent from my TECNO-Y4 using JamiiForums mobile app
Na kama imeshindikana wao kuishi wawili kama mke na mume, amruhusu mama kuwa karibu na watoto wake wote wawili. Lazima kuwe na maamuzi ya hekima; unless aseme huyo mwanamke hafai kuwa mke na hata mama kwa watoto wakerudisha mke mlee watoto
demi humu mie nimegundua kuna wattbwa miaka 19! amini hilo yan hum hatuna tena usalam ukihis wapo watu wanaojielewa! kuna katoto kalinifata bobo kna miaka 19 form six!vimeharibikiwa mnoo! na haya mambo ya kumnunulia mtoto simu ni kosa sana! na ukute na huyo nae wale wale yupo kwenye 20's
In the name of UKOSEFU wa adabu,several things tend to happen,kisheria askari wa kike hatakiwi kumkagua au kumkamata mtuhumiwa mwanaume,likewise kwa askari wakiume kumkamata mtuhumiwa wakike,lakini inapobidi,inafanyika,baba kasema mazingira,wewe unakomaa na adabu,unataka mtoto wa mwenzio waendelee kumuamshia dude tu kila wakati nakila waaume wanapohitaji au..?Umezidi umbea baba lazma uwe na adabu uwez kufungua mikoba ya mwanao....
Mm uyo dada angu tu au mtoto wa kike siwwz kufungua vitu vyako hata chumban kwake kuingia
Kuweni na adabu
Sent from my SHV-E275S using JamiiForums mobile app
Mkuu kabla ya kumuomba MUNGU mjitazame ninyi wenyewe mko sawa kwanza ? Kwani Mungu ndiye anayeshuka kutoa ushauri ?Kwanza kiri moyoni wazazi wawili mlikosea. Huyo dogo alipata uhuru saana haiwezekani mtoto wa miaka 14 afanye hayo.
Binafsi : ningemuita kirafiki nikamuuliza kipimo ni cha nini na anitajie ameanza lini huo mchezo. Friendly kabisa. Asiposena nitampiga hadi atakiri.
Akishakiri tunakaa tunazungumza namshauri kama mwanangu na nampa miongozo ya kuishi. Kuwa naye karibu saana.
Hahaha nimefurahi kukuona
Hapo juu ya comments amejibu,lawama kamtupia mama mtoto wake hivyo hawez waza kumshirikisha Mwenyezi Mungu zaidi ya kulaumu tu bila kuchunguza chanzo cha mkasa mzima
Huwezi kusema arudishe mke walee watoto wakati hujui ni nini kimewatenganisha. Kuishi kwenye ndoa isiyo na afya haipendezi, kuna wakati inabidi tu kutengana. Wazazi wakiweka mawazo yao kwa watoto hata kama hawaishi wote mambo yanaenda sawa.Wajanja washa teleza kwenye kifua cha mwanao.... Malezi bila mama na baba ni sawa na kulea kizazi cha wezi na kuongeza idadi ya watoto wa mitaani na kuongeza idadi ya ma single mother mitaani
Rudisha mkeo, watoto sijui wataridhi nini kutoka kwa wazazi,
Kesho asbh nitaenda shuleni kwake.Napata hofu sana alafu yeye ndo mtoto wangu wa kwanza,yaani ni mtihaniitakuwa nyinyi ni vitoto vya secondari
hivi mnajua kuwa MZAZI NI MCHUNGA NA KILA MCHUNGA ATAULIZWA KUHUSU ALOWACHUNGA
mimi ushauri wangu first nenda polisi ongea na maafande vizuri hasa wakike kwanza apewe kibano akitaja anaemfanya kamata then utajua mwenyewe mtavyomalizana pengine utakuta mtuu mzima kabisa heli awe wa rika lake kidogo unaweza sema barehe zinawachanganya kuliko ukute anaemuharibu ni mtu mzima na midevu yake then nenda school kwake ongea na ticha wa nidhamu kirafiki amuadabisge na kibano huko kinaendelea wasichana wakishaanza kubanduliwa umri huo busara hazisaidii tena zaidi ya utemi tuu mm nawaambia nina uzoefu na wadogo zangu walikuwa wanaleta ukauzu km huo baada hapo heshima na adabu hakuna siasa katika mambo km hayo ni vipigo tu wasichana wanaogopa mzazi mkali sio hayo mambo ya urafiki eti kuwalea kizungu kuongea nao kiurafiki eti usimfatilie ni ujinga mwisho utalea wajukuu mkuu
Asante mkuuHilo karatasi ni ushahidi kwamba mtoto anajihusisha kwenye ngono zembe. Tumia ndugu wa kike hasa Shangazi kama wapo wamu interrogate. Pole sana
Sent from my TECNO-L5 using JamiiForums mobile app
Ni kweli. Mzazi yoyote anayesema usimfatilie mtoto namshangaa. Halafu akiharibika unaanza kumlaumu mtoto wakati wewe mwenyewe mzazi ni tatizo. Wangu namlinda aisee..ni wa kike. Haendi sehemu bila mimi, bahati nzuri nina nafasi akiwa likizo nipo nae 24/7, ana miaka 13 sasa hivi..akifikisha 17 ndo nitamlegezea kidogo ila kwa sasa hapana aisee...