Ushauri: Nimepewa RB kwa kosa la kufanya fujo kanisani

Ushauri: Nimepewa RB kwa kosa la kufanya fujo kanisani

Soma Kwa kutulia na wewe acha mihemuko mleta mada kasema hao Watoto Wana miezi minne na hutumia maziwa ya kopo pia yaliisha kabeba watoto sababu maziwa ya kopo.yameisha kaenda kumtoa mke madhabahuni aende kunyonyesha watoto mshenzi huyo mumewe watoto wanatumia maziwa ya kopo yameisha alishindwa kununua Hadi aende kusumbua Mkewe kanisani? Ina maana yeye analelelewa na mke hata Hela ya kopo la maziwa tu Hana likiisha anamfuata Mkewe hata kama Yuko madhabahuni akanunue kopo la maziwa.Hakuna mume mwanaume hapo huyo mume ni mume suruali tu na lile dudu katikati ya mapaja.Hakuna mume hapo
Wewe mi mpumbavu sana, mleta mada kasema alipiga marufuku kutumia maziwa ya kopo, incase of emergency ikabidi anunue maziwa ya kopo.
Poor you jinga sana wewe
 
Wewe mi mpumbavu sana, mleta mada kasema alipiga marufuku kutumia maziwa ya kopo,
Mwanaume anajua kulea mtoto.mchanga kuliko Mwanamke mshinda kiliniki na mtoto Kila siku ya kliniki?

Anapiga marufuku kama nani ? Anamiliki kiliniki ya watoto hapo kwake?
 
Mwanaume anajua kulea mtoto.mchanga kuliko Mwanamke mshinda kiliniki na mtoto Kila siku ya kliniki?

Anapiga marufuku kama nani ? Anamiliki kiliniki ya watoto hapo kwake?
Mimi ni daktari by professional unajua breastfeeding inajenga bond nzuri katika ya mama na mtoto?
Kama mleta mada amejua ilo kwanini atumie maziwa ya kopo???
 
Soma Kwa kutulia na wewe acha mihemuko mleta mada kasema hao Watoto Wana miezi minne na hutumia maziwa ya kopo pia yaliisha kabeba watoto sababu maziwa ya kopo.yameisha kaenda kumtoa mke madhabahuni aende kunyonyesha watoto mshenzi huyo mumewe watoto wanatumia maziwa ya kopo yameisha alishindwa kununua Hadi aende kusumbua Mkewe kanisani? Ina maana yeye analelelewa na mke hata Hela ya kopo la maziwa tu Hana likiisha anamfuata Mkewe hata kama Yuko madhabahuni akanunue kopo la maziwa.Hakuna mume mwanaume hapo huyo mume ni mume suruali tu na lile dudu katikati ya mapaja.Hakuna mume hapo
Wewe ndio soma kwa kutulia faller wewe. Jamaa kasema hapendelei watoto watumie maziwa ya kopo ila alilazimika kununua kwa sababu watoto walikuwa wanalia sana. By the way jamaa ana mke bogus. Mke wa namna hii ni stress sana.
 
Wasaalam?
Ipo hivi juzi asubuhi Jumapili niliingia nyumbani nilikuwa SA kwa mambo ya kikazi, kufika nyumbani nilimkuta binti yangu wa kwanza pamoja na dada wa kazi kumuuliza mama yako yuko wapi? Akasema ameenda kanisani, nikamuuliza mbona hajaenda na watoto(watoto ni mapacha wana miezi 4) wakashindwa kunipa jibu nikapiga kimya nikaenda kupumzika kutokana na uchovu.

Imefika saa 7 mchana nikashtushwa na kelele za watoto walikuwa wanalia mno nahisi walikuwa wanataka kunyonya kuangalia makopo ya maziwa yameisha nikatoa pesa wakaenda kununua lakini nilipiga marufuku matumizi ya maziwa ya kopo.

Nimebuy time mpaka saa 10 jioni kimya mtu hajarudi nikipiga simu inaita tu haipokelewi, nikashikwa na gadhabu sana nikachukua watoto nikawatupia kwenye gari safari mpaka kanisani kwa wife.
Nimefika kanisani nimemkuta wife yupo madhabauni anaombea watu nikachukua watoto nikawaweka pale pale madhabauni nikamwambia awanyonyeshe watoto wana njaa, akagoma akasema nimemfanyia vitendo vya aibu!!

Ghafla mchungaji mkuu akaja akauliza kuna nini? Mimi nikamwambia mchungaji hayakuhusu nataka watoto wanyonye niondoke nao nyie endeleeni na ibada zenu,mchungaji akadakia akasema ibada ya leo inahitaji utulivu ndio maana tulitangaza watoto wote wabaki majumbani.

Nikamvuta kinguvu wife nikaondoka nae nikamwambia Leo ndio mwanzo na mwisho kusali katika makanisa ya kiroho kama hauwezi kusali roman Catholic pumzika nyumbani tu.

Nimepigiwa simu sasa hivi natakiwa kituo cha polisi kwa kosa la kufanya fujo kanisani na kufanya shambulio la kimwili dhidi ya wife, niende au nisiende? Kwa sababu kesho asubuhi inabidi niende Bujumbura kikazi.

Asante

MREJESHO.
Nimeripoti police nimewekwa selo kwa dakika 30 mama mkwe amekuja ameniwekea dhamana nimetoka.
Cha ajabu muda huu nimerudi nyumbani nimemkuta dada wa kazi tu.. kuuliza naambiwa ameenda kanisani yeye na watoto wote .

Kusikia kwa kenge mpaka damu zimtoke ngoja niende kwanza Bujumbura.
Asa

Haya makanisa kuna namna huwa sielewi na hapo nachelea kusema shem ni mjinga kiasi hicho wenda hata yeye hajui nini anafanya kwa sasa. kuna bro wetu Mmoja alikuwa mkatolik mzuri kabisaa na misingi yake ya dini ilikuwa thabiti mpaka pale alipoalikwa na rafiki yake kuwa aende kuudhuria kongamano kanisani kwao. Toka hapo yeye na familia vilitengana lasmi hakutaka tena kusikia juu ya familia, Mazaa alikuwa kampambania kazi flani Serikalin na tayar ilikuwa hatua ya mwisho ilikuwa ni yeye tuu kwenda kuripot na kuanza kazi lakin alikataa kabisaa kuwa hataki kazi. Toka 2010 mpaka leo yupo yupo tuu amebaki kuugua magonjwa yasiyo elezeweka kila kukicha
Mke wako amekamatwq kwenye cult, hilo sio kanisa la kiroho ni cult.
Muondoe mke wako hapo haraka kabla hajaharibikiwa.
 
Nenda kaka,na uombe rehema ya Mungu kwa kufanya fujo madhabahuni. Kumbuka madhabahu haichezewi. Hapo alikuwa kanisani,imagine huyo mkeo angekuwa yuko kwenye kikao na mkuu wa nchi ungempelekea watoto hapo? Angekuwa daktari yuko theatere ungempelekea?
Angekuwa amekwama safarini ama amelazwa wodini ungempelekea watoto hapo?
Hiyo sio madhabahu ya Mungu. Mungu ninayemjua hayupo hivyo, hiyo ni cult.
 
Wewe ndio soma kwa kutulia faller wewe. Jamaa kasema hapendelei watoto watumie maziwa ya kopo ila alilazimika kununua kwa sababu watoto walikuwa wanalia sana. By the way jamaa ana mke bogus. Mke wa namna hii ni stress sana.
To cut the story short siwezi mwaga Kila kitu humu tukutane mahakamani huyo Mkewe atakuwa na mawakili kibao na hiyo case judgement hata hakimu au jaji akiamua itakuwa quoted kama presedence ya case zingine kama hizo mbeleini

Mwambieni huyo mume tunamsubiri Kwa hamu mahakamani
 
Wewe mi mpumbavu sana, mleta mada kasema alipiga marufuku kutumia maziwa ya kopo, incase of emergency ikabidi anunue maziwa ya kopo.
Poor you jinga sana wewe
Ndio maana sijataka kumjibu coz inaonekana huyo jamaa hata mada hajaisoma na kuielewa,amekurupuka tu na kuanza kutapika matapishi yako hovyo tu hapa.
 
To cut the story short siwezi mwaga Kila kitu humu tukutane mahakamani huyo Mkewe atakuwa na mawakili kibao na hiyo case judgement hata hakimu au jaji akiamua itakuwa quoted kama presedence ya case zingine kama hizo mbeleini

Mwambieni huyo mume tunamsubiri Kwa hamu mahakamani
Wewe ndio mke wa huyo jamaa? Mbona povu linakutoka kama mgonjwa wa kifafa?
 
Duh kweli ww jamaa ni mpole sana .mm ningemchukua kwenye gari narudisha kwao .
 
Itoshe kusema watoto ni wa baba mchungaji 😂😂😂
 
To cut the story short siwezi mwaga Kila kitu humu tukutane mahakamani huyo Mkewe atakuwa na mawakili kibao na hiyo case judgement hata hakimu au jaji akiamua itakuwa quoted kama presedence ya case zingine kama hizo mbeleini

Mwambieni huyo mume tunamsubiri Kwa hamu mahakamani
Vyovyote please tell him tukutane mahakamani
Mbona hii thread umeishikilia kidete hivi? Naweza kuamini wewe ndio mchungaji husika unataka kuharibu ndoa ya watu
 
sipendi mwanamke asiye na kiasi kwa kweli.
 
Mfanyakazi mwenzangu naishi nae kwenye nyumba ya shirika, mkewe amevuka mipaka hadi ya kupeleka kodi ya meza kanisani.

Huyu mwanamke kwao ni waislamu typically, ila kaanza kwenda kwa wahubiri na kaiva hasa na sanaa zao.
Jamaa yangu anasali RC. Kila siku mwanamke anakuja na wito kuwa anaitwa na Mchungaji kuwa ameona kuna watu wanachezea ndoa yao (wanarogwa). Yaani mwamba anapigwa hela hadi basi.
Mwanzoni nilijaribu kumpa ushauri, na kila nilichomwambia alikipeleka kwa mkewe. Nikaamua kukausha na sasa kila akitaka ushauri namkwepa.

Mbaya zaidi watoto wakiumwa ni mwendo wa kuwapaka na kuwaogesha maji yenye mafuta ya kanisani, hospital ni mpaka mtoto afikie hatua mbaya.

Kuna wakati jamaa alifiwa na mama yake na tulienda Moshi kwa ajili ya mazishi. Ilikaribia 40 ya kumaliza msiba, jamaa hakuwa vizuri mfukoni na aliona auze asset yake moja kwa 3,000,000/= ili akamalize msiba.

Akamshirikisha mwanamke na mwanamke akaenda kumshirikisha Mchungaji. Na baadaye majibu ya mwanamke yalikuwa kwamba wagawane 50% ya mauzo na mwanaume akatumie ile ya kwake kwenda kumalizia msiba ila ya mwanamke itabidi akatoe fungu la kumi kanisani. Imepita miezi minne sasa hawajaenda kumalizia msiba wa Mama wa mwanaume.

Kuna siku nilishangaa zaidi mwanamke alipomletea bahasha yenye fomu inayohitaji kujazwa taarifa za kazi ya mwanaume, ikiwamo mshahara. Nilimwambia mwamba huo ni mtego, ila baada ya siku mbili akaniambia kabanwa sana na mkewe na ikabidi ajaze ile fomu na kuirudisha kanisani.

USHAURI:
Wanaume tuwe makini sana na haya makanisa ya kiroho, mengi yamejaa wasanii.
Wanachofanya ni kuangalia weakness ya mwanamke ili waweze kucheza na akili yake na hatimaye kukuteka mwanaume na uchumi wa familia nzima.
Duuh
 
Haya makanisa kuna namna huwa sielewi na hapo nachelea kusema shem ni mjinga kiasi hicho wenda hata yeye hajui nini anafanya kwa sasa. kuna bro wetu Mmoja alikuwa mkatolik mzuri kabisaa na misingi yake ya dini ilikuwa thabiti mpaka pale alipoalikwa na rafiki yake kuwa aende kuudhuria kongamano kanisani kwao. Toka hapo yeye na familia vilitengana lasmi hakutaka tena kusikia juu ya familia, Mazaa alikuwa kampambania kazi flani Serikalin na tayar ilikuwa hatua ya mwisho ilikuwa ni yeye tuu kwenda kuripot na kuanza kazi lakin alikataa kabisaa kuwa hataki kazi. Toka 2010 mpaka leo yupo yupo tuu amebaki kuugua magonjwa yasiyo elezeweka kila kukicha
Aiseeee
Ila unajua siku hizi wachungaji ni wapiga ramli wazuri kuliko hata sangoma
Kuna jamaa hii ilimtokea pia alienda kanisani alipokuwa anasali mkewe,mchungaji akaona jamaa Ana maokoto..anajua alichokifanya mwisho wa siku jamaa akalowea huko kanisani na kazi akaachishwa...kila mali anapeleka kanisani hadi viwanja anatoa sadaka...alikuja kustuka too late ameshapoteza kila kituuu
Kwahiyo jamaa inabidi awe makini sana na mkewe kabla hajalowea huko
 
Subiri sasa utwangwe talaka ili ukaendeshe vizuri hayo maombi yenu fake,

Huwezi kushindana na Mwanaume.
Talaka haitolewi kienyeji sababu.mwanaume kaamua ni mahakamani sio barabarani

Uzuri mahakama huamua kisheria sio ohh mfumo dume mume anasema sikutaki Hakuna Cha mfumo dume mahakamani na hakuna Cha ohhh mimi kama mwanaume nasema!!! Una mawazo ya porini vijijini huko wewe
 
Back
Top Bottom