Moronight walker
JF-Expert Member
- Aug 3, 2021
- 3,103
- 4,704
- Thread starter
-
- #261
Madam mimi sijui hii issue umeichukuriaje.Wanadhani Ndoa ni kama hizo betting zao,
Mijinga ya mwisho.
Hata wanaume wapo wanaficha.Mwanamke / mwanaume kama ulishawahi kupata mtoto wa ujanani hakikisha unaweka wazi mambo yako pindi unapoingia kwenye mahusiano mapya. Hili suala la kuficha ficha linawaumbua wengi hususani wanawake hawapendi kuweka mambo yao wazi.
Weka wazi me/ke ajue ukweli na aamue lipi lililo bora kwake aendelee na wewe au muachane mapema.
Mwisho ukikitana na me/ke aliwahi kupata mtoto kabla ya ndoa na hakuwahi kukwambia, jua hao wazazj bado wana mahusiano kwa kigezo cha mzazi mwenza.
Epuka matapeli mwanamke aliyezalishwa na mwanaume wake yupo hai hafai.
Wapo wanaume wengi tuu wanaficha watoto.Hongera Mwanaume imara umeandika point kubwa sana, Wanawake wa Kiafrica wameshikiwa akili na the so called Mila na Desturi, mfumo dume umewaharibu kiasi cha kutoitambua hata thamani yao,
Kosa hilo hilo angefanya Mwanaume na Mwanamke akataka kuachika wangemwambia avumilie tu alee watoto ndio ishatokea,
Ujinga ujinga tu.
Nahic iyo ndo sababu alikuwa anahc ataolewa.Katika vitu vya kuzingatia kwenye mahusiano kabla ya kuingia kwenye ndoa ni ukweli na uwazi hasa hasa wa vitu ambavyo ni muhimu kama kuwa na mtoto. Ni bora kumwambia mwenza wako ukweli ili yeye aamue kukubali kuendelea au lah.
Mwenzetu alikosea sana miaka 15 kumficha mume wake sio busara kabisa kinachoumiza sio kuzaa kabla ila ni kumficha mwenzie. Ila inawezekana kuna sababu kubwa nyuma yake au alijua akisema ana mtoto hataolewa maana wanaume wanawadharau sana single mothers na inapelekea situations kama hizi.
sababu mdada....hujui maumivu ya kulishwa iliyoliwa kwa ushahidi kwa miaka 15 bila kujua.Sababu lazima anayo, hayo ni mambo yanayoongeleka na sio kuvunja ndoa, angemfumania hapo sawa ila sio hilo ni dogo sana kikubwa ni kumpa nafasi atoe sababu zake.
Glenn Unaweza kakuta anamtetea huyo dada cos na yeye amewahi kufanya huo mchezo si unajua wanawake akili zao zinafananaUmeanza mihemko isiyo na sababu.
Pili tusijadili mambo kimazoea ya kiswahili.
Mwanzo wa mahusiano una mambo mengi.
Kuna mwanamke mkianza mahusiano anakutaka uwe wazi kwake kama umewahi kuoa au kuzaa nje.
Kwa moyo mkunjufu unamweleza ukweli.
Naye anakwambia hajawahi kuolewa wala kuzaa, baada ya miska 15 ukagundua alizaa na alikuficha kwanini udimwache?
Mwanzoni ukiniambia hata una watoto wawili kwa uwazi huo mimi nitakuoa.
Napendezwa na mwanamke muwazi, makosa kila mtu hufanya.
Lakini kitendo cha kumficha binadamu aliyetoka kiunoni mwako, si unaweza kumficha mmeo jambo lingine kubwa?
Ongea uhalisia uache hasira
Na ndio kulichokiwa kinatokea...hawa wanawake hawawezi mnyima mbususu bby daddy ata siku mojaHapo utakuwa na uhakika gani kama lijamaa halikuendelea kupeleka moto usikute watoto wote ni wa hilo jamaaa.
Oa kwenye Koo ambayo babu wa babu wa mtu wako anajulikana. Kuoa sio unakutana naa mtu town akapendeza hujui vizuri Koo yake, kisa akapendeza,kavutia machoni,akasoma,anafanya kazi nzuri panono,ana biashara kubwa za uhakika,hisia zinazidi akili unaoa/unaolewa nay. Inabidi umjue mtu nje ndani Koo yake ambaye unaunda naye familia,Kuna watu Koo zao Zina makandokando.Ndani ya hizi ndoa wengi tunaowaita mashemeji mara nyingi huwa ni watoto wa wake zetu.
Unakuta katoto unatambulishwa kama mdogo wa mwisho au mtoto wa dada/kaka kumbe ni mtoto wa mkeo.
Ni nadra kwa wanaume kuficha watoto waliopatikana kabla ya mahusiano ila wanawake mara nyingi wanahusisha kuwa na mtoto kabla na kushuka kwao kwa thamani kupelekea kuficha watoto wao wa kabla ya ndoa/mahusiano.
Mkuu tufafanue kidogomimi niligundua tu ana namba ya simu ya siri ambayo anaitumia nikapiga chini, sembuse toto tena la miaka 20 kabisa.
Alikuwa anatumia na michepuko?mimi niligundua tu ana namba ya simu ya siri ambayo anaitumia nikapiga chini, sembuse toto tena la miaka 20 kabisa
Unaachwa tu maana siyo mwaminifu na msema kweli........Umeishi na mtu kwa miaka 15, mmezaa watoto 4, unakuja kumuacha kisa hakukwambia kua aliwahi kuzaa kabla!!?
Ukisikia kutafutiana sababu ndio huko sasa.
Huyo mume kuna uwezekana mkubwa alikuwa ameishamchoka huyo mke; alikuwa anatafuta sababu tu na hiyo sababu tayari imeishapatikana. Anyway, ndoa ni maua. Cha muhimu baba awatunze watoto na kama walifanikiwa kujenga nyumba na kumiliki mali nyingine, basi hizo mali zimilikishwe watoto kwa usimamizi wa mama yao. Mume aondoke hapo akatafute chaka lingine aendeshe maisha yake mapya, isiwe shida.Habari wana JF.
Kuna Ndoa imevunjika hapa ndoa ya miaka 15.
Mke alizaa kabla ya ndoa, sasa mama huyu alimficha mtoto,
Huyu mtoto alikuwa anaishi na Baba yake.
Mume alijua kwa mawasiliano ya simu Mama alipokuwa anaongea na mwanae.
Na mtoto ana umri wa miaka 20.
Mume wa ndoa kazaa naye watoto 4.
Dawati la suluhisho walijaribu kuweka sawa ili wasiachane ila ilishindika. Hata wachungaji walishauri kuwa asamehe tuu kwani hata mtoto kashakuwa mkubwa hakuna shida yoyote lkn ndo hivyo ndoa imevunjwa jana na mahakama.
Huyu mama alizaa kipindi ana umri wa miaka 21.
Sasa wanajamii hivi vitu vinatokana na nini mpk mmoja anaamua kuficha mtoto?
NI NINI CHA KUFANYA BAADA YA KUJUA HATA KWA MUME KAMA ALIFICHA KUWA ALIKUWA ANAMTOTO.
Unajua mwanamke aliyezaa na mwanaume mwingine, kumbuka yule ni mzazi mwenzake unajua kile kilichokuwa kinaendelea? Kosa lingine anaweza kusameheka ila siyo udanganyifuNingemsikiliza sababu yake lazima iwe na mashiko na kuendelea na Maisha, nisingeivunja ndoa
Inawezekana nikawa namtetea huyo dada kumbe hata mama ako mzazi aliwahi kufanya hayo.... maana hata mama ako ni mwanamke.Glenn Unaweza kakuta anamtetea huyo dada cos na yeye amewahi kufanya huo mchezo si unajua wanawake akili zao zinafanana
Wewe umemjulisha mwenzako au bado hujafanya maamuzi? π π π πWengi hawasemi ukweli.
Tatizo ikijulikana ambapo na ni lazima ijulikane tuu.
Mume anaona kama walikuwa wanaume wawili kwa mwanamke mmoja.
Better to be open karma kusuka au kunyoa ijulikane mapema