Ushauri: Nitumie mbinu gani kuongea na baba aachane na mchepuko wake?

Ushauri: Nitumie mbinu gani kuongea na baba aachane na mchepuko wake?

Wakuu salaam....

Mara kadhaa mama amekuwa akimtuhumu mzee kujihusisha kimahusiano na mama flani ambae ni shemeji yake. Mama amejaribu kufanya jitihada zakuwaachanisha kwa njia ya mazungumzo lakini wamegoma kuachana kabisa.
Una umri gani? Halafu nitaendelea
 
Mtoa mada chukua huu ushauri[emoji115]. Nina experience na jambo kama hilo. Usisahau kuvaa kimaafia kama siku unamtimbia huyo mamdogo. Mzura, jacket kubwa, buti, gloves za mikononi zile za sweater halafu sauti kama umekula ndumu na ulikuwa umepania kungawanya vipande ila umensamehe na kumpa chance ajirekebishe mwenyewe. Muwe watu wawili au watatu. Akitoka hapo amejikojolea na mnaweza kumvuta masikio kidogo. Au unaweza kunipa hiyo kazi, tunamweka mtu kati , sie machalii wa chuga huwa haturembeshi. Au ukitaka huyo mshua wako tunamweka kitako na bapa za sime kuwa sisi ni vijana(ndugu) wa huyo mamdogo au mimi nae ni mchepuo wangu na ukituruhusu tunampiga bapa moja tuu kisha tunampa chance atimue mbio
[emoji23]nimecheka utadhan mazuri.Asante mkuu
 
Haya mambo yanahitaji akili na utulivu; ukileta hisia za kumpigania bi.mkubwa unaharibu sana
Ndo maana me bi mkubwa akisema niongee na mzee inabdi ntulize akili kwanzaa lasivyo mzee lazima mkosane
 
Haya mambo wewe kama mtoto hayakuhusu na ulipaswa kumuambia mama kuwa hayo ni mambo ya mahusiano yenu kati yenu nyie hivyo wajue namna ya kuelewana wao kwao.

Hii tabia ya kuhusisha watoto kwenye masuala ya mahusiano ya kimapenzi baina ya wazazi siyo busara na halipaswi kufanyika.

Mzazi kaa na mzazi mwenzio muone namna ya kuelewana na kila mmoja aeleze kile anachokikosa kwa mwingine ili ajirekebishe na siyo kumuambia mtoto aongee na Baba kuhusu hayo mambo.


Baba yako akikuambia mama yako hamridhishi utamsaidiaje??


Utaenda kuongea na mama pia kuwa amridhishe baba yako kitandani??

Mahusiano kati ya watu wawili yana mambo mengi na mengine mazito, wewe mtoto hayakuhusu maana hata kipindi wanatongozana wewe hukuwepo na hujui mengi kuhusu wao wawili.


Mwambie mama yako hilo suala halikuhusu na waongee wao wamalizane na uendelee na majukumu yako.
 
Unaweza ukafanikiwa kumachanisha mshua na huyo mchepuko wake, halafu mshua akachukua mchepuko mwingine.
Vipi utaendelea na hiyo kazi mpaka lini?
 
Ndugu,

Licha ya upendo mkubwa uliyonao kwa mama yako, nikushauri tu hili jambo ni la kuliendea kwa akili na sio mhemko.

Moja; huna mamlaka juu ya mahusiano ya baba yako na huyo mwanamke mwingine, kama ameshindwa kuwasikia na kusitisha mahusiano baada ya kusemwa na mkewe pamoja na ndugu zake, unadhani una nafasi kubwa sana ya kumshawishi huyo mzee?

Mbili; usianzishe chuki na baba yako kwa kuwa tu ana mahusiano nje ya ndoa na kwa namna moja yanamuumiza mama yako. Wewe ni mtoto wa kiume; endelea kutafuta suluhu bila kuharibu mahusiano yao.

Tatu; kamwe usithubutu kumuuliza mzee wako juu ya hayo mahusiano; endelea kutafuta suluhu bila kumuuliza huyo mzee. Hapa ni vyema ukatumia wazee wenzake na sio wewe mtoto aliyekuzaa mwenyewe.

Nne; fanya uchunguzi binafsi juu ya hilo jambo na sio kuamini moja kwa moja maneno ya mama yako; alisema mzee Kikwete ''za kuambiwa changanya na za kwako''

Mwisho ; japo si kwa umuhimu; yaone mahusiano ya baba na mama yako kama mahusiano ya watu binafsi; mapenzi yana mengi; kuna siku watakuja kupatana huku wakipeana huba zito na wewe utabaki unashangaa usijue namna ya kuwatazama.

Nimekueleza haya kutokana na uzoefu mbalimbali.

Uwe na siku njema.
Nimepokea
 
Sijui ni Mimi tu yaan mi mtu kuwa na mchepuko naona is not big deal ilmradi anatunza familia tu...Cha kumkumbusha hapo ni kondomu au kupima mara Kwa mara.Maana maradhi nayo ni changamoto yakiingia ndani coz hapo tayari ni rectangle relationship
 
Sijui ni Mimi tu yaan mi mtu kuwa na mchepuko naona is not big deal ilmradi anatunza familia tu...Cha kumkumbusha hapo ni kondomu au kupima mara Kwa mara.Maana maradhi nayo ni changamoto yakiingia ndani coz hapo tayari ni rectangle relationship
Mkuu mda mwingine huwa nakuelewa sana nataman hii mindset wangekuwa nayo wanawake wote..kikubwa ni kujilinda na maradhi tu

NB:mke/mume asiekua na hofu ya Mungu ni lazima ipo cku atachepuka tu
 
Sijui ni Mimi tu yaan mi mtu kuwa na mchepuko naona is not big deal ilmradi anatunza familia tu...Cha kumkumbusha hapo ni kondomu au kupima mara Kwa mara.Maana maradhi nayo ni changamoto yakiingia ndani coz hapo tayari ni rectangle relationship
Ujue hata mimi hayo mahusiano yamzee na mchepuko wake sikuona Yana shida San cz majority ya wanaume tupo hivyo.Hata hapa kinachonichanganya sio mzee kuchepuka,noo...kinachonisumbua ni jinsi bimkubwa alivyoamua kunishirikisha.
 
Talking about my experience mzee wangu aliwahi kuwa na mchepuko na sisi kama watoto(mimi na kaka yangu) tuliamua kukaa chini na kumuandikia barua mzee kumchimba mkwara kwamba tumeshajua mambo yote na tunamuomba aachane na huyo mchepuko mara moja kabla hatujaamua kufanya maamuzi magumu

Mbinu hii ilisaidia sana kwan tangu kipindi tumeandika hiyo barua hatukuwahi kumuona akipokea tena simu zake wala yeye akimpigia
 
Nakushauri, acha na masuala ya baba na mama yako.Pambana na maisha yako hao ni watu wazima kwani mambo ya ndani ya shuka za wapenzi usijaribu kuingilia.Vinginevyo unatafuta laana ya asubuhi na mapema
 
talking about my experience mzee wangu aliwahi kuwa na mchepuko na sisi kama watoto(mimi na kaka yangu) tuliamua kukaa chini na kumuandikia barua mzee kumchimba mkwara kwamba tumeshajua mambo yote na tunamuomba aachane na huyo mchepuko mara moja kabla hatujaamua kufanya maamuzi magumu


mbinu hii ilisaidia sana kwan tangu kipindi tumeandika hiyo barua hatukuwahi kumuona akipokea tena simu zake wala yeye akimpigia
Alibadilisha mbinu na jiulize wewe hauna mchepuko pamoja na kuwa katika ndoa?
 
Poleni sana, kwenye familia yakishaingia mambo kama haya hata Ile amani inatoweka, too bad mzee wako ameahindwa kucontrol issues zake za Nje, Wadau wamekwambia umwambie kwa utaratibu na hekima ukifika Tu umeharibu fanya hivyo, kama ni mzazi mwelewa basi atajifunza kitu.
 
Ujue hata mimi hayo mahusiano yamzee na mchepuko wake sikuona Yana shida San cz majority ya wanaume tupo hivyo.Hata hapa kinachonichanganya sio mzee kuchepuka,noo...kinachonisumbua ni jinsi bimkubwa alivyoamua kunishirikisha.
Bas anakwepa dharau,msaidie Kwa kumwonya mwanamke huyo wa nje
 
mkuu mda mwingine huwa nakuelewa sana nataman hii mindset wangekuwa nayo wanawake wote..kikubwa ni kujilinda na maradhi tu

NB:mke/mume asiekua na hofu ya Mungu ni lazima ipo cku atachepuka tu
Yeah sure
 
Usijiingize kwenye mambo hayo, usimuulize baba yako ni kumkosea heshima......mama amekosea sana kukushirikisha alitakiwa awashirikishe watu wazima...ikishindikana...amlilie Mungu
 
Ongea na mzee mwambie aache nyege za kitineja acheat kwa akili, afiche michepuko yake....

Nb: usimshauri aache make michepuko inaimarisha ndoa, mwambie tu afanye kwa siri.
Jibu sahihi ni hili. Ila huwa natamani nikuine we mwanamke, UNAFAA SANA
 
Back
Top Bottom