Ushauri wangu kwa vijana wa kidato cha 6 na wengine wote ambao bado hawajafikia elimu ya Chuo Kikuu

Ushauri wangu kwa vijana wa kidato cha 6 na wengine wote ambao bado hawajafikia elimu ya Chuo Kikuu

Vipimo kati ya elbow moja na nyingine hapo ni universal havibadiliki.

Hiyo ni shower hapo kuna elbow ya maji moto naya maji baridi. Kikawaida kutoka centre ya elbow moja hadi nyingine ni 15 cm kokote uendapo duniani haibadiliki
Nija nyingine mwanzo mwa elbow ya kwanza mpaka ya pili ni cm 18 au center to center kati ya elbow na elbow ni inch 6
 
Yes wale jamaa naona wanafundishwa mamichoro tu mara nyingi wanacheza na program za computer kuchora ramani za nyumba huo mda wa kushika konobao sijui koleo mwiko atautoa wapi?
Nenda kampuni za ujenzi kutoka nchi za nje injinia anajua kujenga kushika mwiko inshort ni fundi kamili lakini kwetu ni tofauti sana
 
Yes ndicho ninachokisema, lakini hayo masomo ya kukusaidia mbeleni ndio hayo yawe ya ufundi wa VETA iwe option lakini kwa wanafunzi wanaopenda.
Shida ni moja Veta wana kwenda kwa level na kule mwisho ni level 3 ina maana ina masomo ya sceince kama hesabu,egineering scince ambayo ni kama physics so kwa mtu aliye kimbia masomo ya science kwake bado itakuwa mtihani
 
Nitakuwa wa mwisho katika watu zaidi ya bilioni 7 waliopo duniani kukubaliana na hii hoja ya mleta uzi. Kusema vijana waache kwenda kusoma degree ili waende VETA kwanza ni ufinyu wa fikra na kukata tamaa. Ni sawa na wale wanaosema hela sio kila kitu huku hawajawahi zishika za kutosha. DEGREE NI MUHIMU KULIKO CHETI CHA VETA. Degree itakusaidia kufika ambako mtu wa VETA hawezi fika.

Tusipotoshane kwamba degree haina maana. Kama kwa nchi maskini kama yetu degree haitakuwa na maana basi huko Ulaya na kwingine kulikoendelea inabidi wafunge tu vyuo. Bado kwa nchi yetu tunahitaji wasomi wengi. Haya mabadiliko tunayoyataka yatapatikana haraka kukiwa na wasomi wengi. Kijana mwenye ndoto za kuwa daktari bingwa aache kwenda MUHAS ajiunge VETA? Aisee acheni kukata tamaa. Kama wewe bado maisha hayajakaa vizuri usitake kupotosha vijana. Zamu yako ikifika hata wewe utafanikiwa.

NINAWASIHI VIJANA WAUPUUZE HUU UZI NA KUCHANGAMKIA DEGREE HUKO UDSM, MUHAS, SOKOINE, SAUT na vyuo vingine vinavyotoa degree. Ila pia wasiridhike na degree peke yake. Wajiongeze na maarifa mengine.
 
Serikali haina budi kuueleza huu ukweli kwa Wananchi wake.
 
Shida ni moja Veta wana kwenda kwa level na kule mwisho ni level 3 ina maana ina masomo ya sceince kama hesabu,egineering scince ambayo ni kama physics so kwa mtu aliye kimbia masomo ya science kwake bado itakuwa mtihani
Sijakuelewa mkuu, courses zote zinazotolewa na Veta zina science content ndani yake? Fafanua please
 
Sasa hapo itategemea na maamuzi ya wizara husika ingawa sio suala baya ingawa linahitaji mchakato wa mda,
Hili nalo wakalitazame…😎😀

Kama wameshindwa kuincorporate ujuzi kwenye syllabus za hizo degree , basi watoe additional classes za ufundi …

I guess vijana wakiambiwa what to expect Huku mtaani, watachukulia positive hizo opportunities za masomo ya ufundi
 
Dunia ya Sasa inataka ujuzi na maarifa na Sio vyeti.
Mr kucha mshika vidole vya wanawake anaingiza pesa nyingi kuliko mwajiriwa mwenye masters nchini.
Housemaid Anaefanya kazi uarabuni anakunja Hela ndefu kuliko mwajiriwa mwenye elimu ya masters nchini.
Maisha Sio vyeti bali ni wewe unajua Nini kuhusu maisha.
Mkuu Mr kucha man sawa anamake hela..
housemaid uarabuni achana nao ile sio kazi labda wawe tofauti na hao niliowaskia mimi..nina evidence ni unyanyasaji tu majamaa wa uarabuni wanao.sio case moja.ila moja ni close kabisa ndugu wa damu.aliapa hatarudi tena huko.Wana ROHO MBAYA sana.
 
Hili nalo wakalitazame…😎😀

Kama wameshindwa kuincorporate ujuzi kwenye syllabus za hizo degree , basi watoe additional classes za ufundi …

I guess vijana wakiambiwa what to expect Huku mtaani, watachukulia positive hizo opportunities za masomo ya ufundi
Yeah ni kweli
 
Ushauri wangu kwa vijana wa form 6 na wengine wote ambao bado hawajafikia elimu ya chuo kikuu.

Tanzania ya sasa haihitaji Degree, zimeshakuwa nyingi sana mtaani mpaka copy za vyeti zinafungiwa vitumbua. Yaani degree ni luxury sio hitaji muhimu.

Tanzania ama dunia ya sasa inahitaji stadi na ujuzi, ambao mfumo wa elimu yetu haujauweka kupatikana chuo kikuu. Yaani huwezi kwenda chuo kikuu ukapata degree ya kupaka rangi kwa mfano. Na kwa kiasi kikubwa ujuzi huu unapatikana VETA. Watu wengi huwa wanadharau kwa kuchukulia kama ni njia ya waliofeli shule.

Hata hivyo kutokana na maisha yanavyoenda, elimu ya chuo kikuu ni kipimo cha daraja la elimu tu kama ilivyo darasa la saba, form 4 na form 6 na unahitajika kuwa na kitu kingine nje ya hivyo ili uweze kufanya kitu. Hasa ikiwa umetoka moja kwa moja Form 6, ndo una hali mbaya zaidi.

Lakini kama utaamua kujitengea miaka miwili au mmoja kabla ya kwenda kujiunga na hiyo elimu ya ndoto yako. Ukaenda VETA na kusomea ujuzi tofautitofauti kama udereva, umeme wa magari, umeme wa majumbani, ujenzi na ufundi wa vitu vya aluminium nk.

Basi utakuwa na uwezo mkubwa sana wa kufanikiwa kimaisha popote ulipo na hutolala njaa kwa kukosa ajira kwani utakuwa na vyeti zaidi ya vitano vya ujuzi vitakavyokuwezesha kupenya sehemu nyingi sana kuliko namna ambavyo cheti chako kimoja cha degree kinavyoweza. Na kwa ujuzi huo utaweza kujipatia pesa za kujisomesha hiyo degree muda wowote utakaotaka. Ni vigumu kulala njaa ukiwa na elimu ya VETA, ila uwe na uhakika kuwa utalala njaa ukiwa na cheti cha degree kabla hujapata ajira. Kitu ambacho ni kitendawili.

Ukweli ni kwamba, kama una uhakika wa ajira yaani kuna mahala umeandaliwa, au kuna mtu wako yuko ofisi fulani na atakuwepo mpaka muda utakapomaliza kusoma hiyo degree, basi kasome. Kama huna uhakika basi nenda kwanza VETA. Wengi wanaopata ajira huwekwa na watu wao, au kuhonga mishahara yao mmoja au miwili ya awali ili kuajiriwa.

Hata utakapomaliza maisha ya mtaani yatakulazimisha na yatakudai ujuzi au stadi fulani utakaopaswa kuwa nao nje ya hiyo degree yako ili ujiingizie kipato. Na ndicho ninachokisema hapa. Kwa bahati mbaya hutakuwa nao, na hutakuwa na uwezo wa kusoma VETA tena kwani hela ambayo ungeweza kuitumia kama mtaji wako wa kujipatia ujuzi huo utakuwa umeimaliza kwenye degree.

Elimu ya VETA ina uwezo wa kukusomesha degree, ila elimu ya degree ni vigumu mno kukusomesha kama bado hujapata ajira. Ni rahisi kujiajiri ukiwa na elimu ya VETA ila ni ngumu sana ukiwa na degree. Kwani utahitaji mtaji, na huo mtaji ndio utakuwa umeutumia kusomea degree. Kwa hivyo utakuwa mtaji huna na ujuzi huna, na itakuwia vigumu sana kujitafuta. Hapa wadada wengi waliohitimu ndio hudanga kusiko kawaida na wa kiume kupinduka na bodaboda kukimbilia abiria wapate hela nyingi ndani ya muda mfupi ili waache kazi hiyo.

Na uzuri wa kuya face maisha kwa ujuzi na stadi utakazopata VETA, ni kwamba utakuwa na uzoefu na namna ya kukabiliana na maisha ya mtaani na kikubwa zaidi utatambua wazi ni aina gani ya degree inayohitajika mtaani kwani vijana wengi huchagua degree kwa kutazama uzuri wake wa kutamkwa mdomoni. Ukitoka na cheti chako cha chuo kikuu hapa Tanzania ukaenda nchi za ughaibuni, kuna uwezekano mkubwa ukahitajika kusoma tena au kujiboresha kwa elimu watakayokupa wenyewe.

Yaani kwa kifupi, elimu yetu haiaminiki. Na ndio maana watoto wa viongozi na watu wenye pesa husoma nje ili kuepuka hili. Lakini ukitoka na Vyeti vyako vya VETA hata vikachanwachanwa, ujuzi wako utaongea. Na popote pale utapata nafasi, kisha utajisomesha hiyo degree.

Nimeandika kwa uzoefu wangu, na degree yangu niliyonayo ikiwa ni mwaka wa tatu tangu nihitimu na sijui hata interview inafananaje. 😀. Kabla sijaenda chuo niliambiwa karibia kama hivi nilivyoandika hapa, sikutilia maanani sana, na nikasoma degree kwa cash zaidi ya milioni 11, yaani ada pamoja na gharama za kuendesha maisha ya chuo baada ya kukosa mkopo. Mzazi asingenipa pesa hizi nikajiajiri, na sikuwa na lolote kuhusu kujiajiri. Mimi nimejitahidi hapa kuyanyoosha zaidi kwa vijana wenzangu.

Jitathmini kisha utajijibu. Ukiparamia degree, utakapomaliza hata hela za vocha utagongea kwa washkaji zako walioenda VETA na hao ndio watakusave vimeo vyako vyote. Hutaamini. Sikukatishi tamaa, ndio ukweli.

Kwa kifupi, degree imekuwa sio kitu cha kuanza nacho mtaani yaani ni lazima uwe na kitu kingine kwanza kisha ndio uongezee na elimu ya degree. Wanaonufaika moja kwa moja na elimu hiyo ni wale ambao tayari wako kazini, wanaenda vyuo kuongeza elimu kisha kurudi kazini kupandishwa vyeo. Sio mtoto wa form 6 au diploma.

Lakini kama umebahatika kupata mkopo, nenda kasome ila hakikisha unajinyima sana na hela zako una save ili utakapomaliza upate ada ya kwenda VETA kujiongezea kitu cha ziada au kufungua biashara yako binafsi lakini sio ajira. Na hata kama utatafuta ajira utahitaji nauli za kunguka mjini, hata ukipata sehemu ya kujitolea bado utahitaji kujigharamia kwa karibu miezi 6.

Mzazi hatokupa gharama hizo, kwani wazazi wetu wengi mkataba wao wa kukugharamia huishia siku una graduate. Baada ya hapo huanza kukutazama wewe sasa namna utakavyoweza kurudisha fadhila. Baada ya graduation hakutakiwa na pocket money wala boom la serikali.

Semester 6 au 8 ni muda mchache sana, lakini una mambo mengi na graduation halisi ni kurudi mtaani si ile ya kuvaa joho.
Ushauri muhimu sana kwa vijana wetu
 
Dunia ya Sasa inataka ujuzi na maarifa na Sio vyeti.
Mr kucha mshika vidole vya wanawake anaingiza pesa nyingi kuliko mwajiriwa mwenye masters nchini.
Housemaid Anaefanya kazi uarabuni anakunja Hela ndefu kuliko mwajiriwa mwenye elimu ya masters nchini.
Maisha Sio vyeti bali ni wewe unajua Nini kuhusu maisha.
Ndivyo ilivyo kwa hakika
 
Sijakuelewa mkuu, courses zote zinazotolewa na Veta zina science content ndani yake? Fafanua please
Kozi za mda mrefu nyingi zina masomo ya science
Ushonaji
Magari
Bomba
Umeme
Uchomereaji
Ujenzi

Fani chache ambazo najua hazina masomo ya acience ni mifugo na upishi

Masomo ya scince ambayo yana somwa kama somo ni engineering scince hili somo ni physics kwa upande wa secondary kuna math ni ya kidato 1 kwanza mpaka 4 na mwisho Technical drawing hili lina patika chuo kikuu kwa wanao chukua engineering
 
Elimu ya Tz inahitaji mabadiliko makubwa mno sababu asilimia kubwa imebase kwenye kukariri karibia levo zote , kwenye mitaala vitu vingine vipi lakini havina umuhimu wala msingi , sehemu kunaweza kuwepo mafunzo ya kwa vitendo lakini vitendea kazi ni duni na vichache kucompare na idadi ya wanafunzi..
 
Elimu ya Tz inahitaji mabadiliko makubwa mno sababu asilimia kubwa imebase kwenye kukariri karibia levo zote , kwenye mitaala vitu vingine vipi lakini havina umuhimu wala msingi , sehemu kunaweza kuwepo mafunzo ya kwa vitendo lakini vitendea kazi ni duni na vichache kucompare na idadi ya wanafunzi..
Kila sehemu ni matobo matobo tu yamejaa
 
Niliutambua ukweli huu baada ya kumaliza chuo na kukaa mtaani kwa miaka miwili bila ajira hadi pale rafiki yangu aliponishika mkono na kuanza kupata tumaini jipya.Mungu akubariki rafiki yangu sina cha kukulipa ila nakuombea kwa Mungu akupe baraka katika maisha yako.
Kuna haja kubwa ya kuzingatia ujumbe wako mkuu japokuwa siyo dhambi kuitafuta degree.
 
Back
Top Bottom