Ushawahi Kupokea muujiza gani ukaamini kuwa Mungu yupo?

Ushawahi Kupokea muujiza gani ukaamini kuwa Mungu yupo?

Nikiwa nasoma UDSM, nilikuwa natoka likizo kurudi chuoni. Nilikuwa na mdogo wangu aliyekuwa anasoma chuo kingine.

Tukaingia kwenye basi, mdogo wangu akiwa ametangulia. Kwa kuwa basi lilikuwa tupu, mdogo wangu akakaa viti vya mbele. Mimi nilipoingia, nikamwambia aondoke alipokuwa amekaa, twende tukakae nyuma. Yule mdogo wangu alitii bila hata ya kuuliza. Na hata angeniuliza, wala sikuwa na jibu lolote, na hata mimi mwenyewe sikujua kwa nini nataka kwenda kukaa nyuma.

Tukaenda kukaa nyuma kabisa, kama mstari wa 3 tokea nyuma. Baada kama ya masaa mawili, basi lilipata ajali mbaya ya kugongana na lorry kubwa aina ya Fiat, kisha magari yote mawili yakashika moto. Madereva na watu wote kuanzia eneo la mbele mpaka karibia katikati ya basi ama walikufa au kuumia vibaya sana. Wengine waliungulia vibaya ndani ya basi.

Tulionusurika tulikimbizwa hospitali, baada kama ya masaa 8 ya uangalizi, niliruhusiwa kutoka hospitali.

Siwezi kusema kupona kwangu ulikuwa ni werevu wangu, bali Mungu alipenda niendelee kuishi.
Vip mdogo wako naye?
 
Au labda hao wanaokufa hawamtafuti kwa bidiii? Kwa sababu katika kitabu cha yeremia 29.13 ana sema



"Nanyi mtanitafuta na kuniona , mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote"
Hata hao wanaohangaika kumtafuta Mungu kila kukicha bado wanakufa na watakufa tu.

Kwa hiyo suala la kifo bado halijitoshelezi kusema kwamba ukimtafuta Mungu hutakufa.

Kila mtu atakufa na kifo kipo palepale.
 
Alafu akina Kiranga wakiwaambia mthibitishe mnaanza kujilizaliza!
Unaelewa nini maana ya muujiza ?? Kama unaweza logically kuieleza huo sio muujiza .
Nina jamaa rafiki yangu mpendwa kabisa , enzi zile sisi ndio werevu chuo ila tulikuwa maskini wa kutupwa .
Tulipigika miasha kufikia kuchimba choo.
Hatukuenda hata ft 4 tulipata kipande cha dhahabu , ikumbukwe gold haiexist in its purest form mchangani ila tuliipata size nzuri tu tena safi kabisa .
Mpaka leo kijijini mtu akifa wanasema tumemshusha kusingizia ndagu .
Hela tuliopiga nikiisema utaona nakutania na ndivo umaskini ulituondokea mpaka leo .
Mungu yupo hili naamini
 
Wakuu
kumekuwepo na mijadala mingi humu ya mivutano baina ya wanaokubali uwepo wa Mungu na wasioamini uwepo huo

Mungu mala zote ni mtenda miujiza,na amekuwa akifanya hivyo mala zote kwa waja wake, amekuwa akiponya magonjwa yaliyoshindikana,vipofu wanaona,viziwi wanasikia,viwete,bubu,wasio na kazi, watoto, mume,mke nk wote wamekuwa wakiuona mkono wa BWANA/ALLAH.

Tuambie mkuu, ulipokea muujiza gani kutoka kwa Mungu ukaamini uwepo wake?

KARIBUNI.
Kwanza tuelewe kuwa muujiza ni tendo au uwezo ambao kibinadamu hauwezi kufanyika. Kuoa, kuzaa, kupata kazi (na zipo nyingi sana kuliko ajira), kupata pesa, kujenga nyumba, kununua gari, nk.; si miujiza bali ni baraka tu na tunaweza kuzifanya au kuzipata kadri tulivyojaaliwa.

Lakini kutembea juu ya maji, kufufua mfu, tasa kuzaa, kipofu kuona, bubu kuongea, kiziwi kusikia, kupona ugonjwa usio na dawa, kuumba kitu au vitu, nk.; hiyo ni miujiza maana haiwezekani kufanyika kibinadamu. Na tukumbuke kuwa binadamu tunatengeneza vitu, hatuumbi!

Baada ya kumlilia Mungu, mimi nilipata muujiza wa kupona ugonjwa wa kisukari ambao niliambiwa na matabibu kuwa hauna dawa ya kuuponya isipokuwa kuudhibiti au kuupunguza tu makali yake.
 
Mazingaombwe yapo, uchawi upo,
Kitendo Cha wewe kuwa hai NI muujiza tosha
Kitendo Cha mtu kuomba na MUNGU kujibu NI muujiza tosha
Mungu yupo afanye asifanye muujiza
Yesu alikufa na kufufuka
 
Nikiwa nasoma UDSM, nilikuwa natoka likizo kurudi chuoni. Nilikuwa na mdogo wangu aliyekuwa anasoma chuo kingine.

Tukaingia kwenye basi, mdogo wangu akiwa ametangulia. Kwa kuwa basi lilikuwa tupu, mdogo wangu akakaa viti vya mbele. Mimi nilipoingia, nikamwambia aondoke alipokuwa amekaa, twende tukakae nyuma. Yule mdogo wangu alitii bila hata ya kuuliza. Na hata angeniuliza, wala sikuwa na jibu lolote, na hata mimi mwenyewe sikujua kwa nini nataka kwenda kukaa nyuma.

Tukaenda kukaa nyuma kabisa, kama mstari wa 3 tokea nyuma. Baada kama ya masaa mawili, basi lilipata ajali mbaya ya kugongana na lorry kubwa aina ya Fiat, kisha magari yote mawili yakashika moto. Madereva na watu wote kuanzia eneo la mbele mpaka karibia katikati ya basi ama walikufa au kuumia vibaya sana. Wengine waliungulia vibaya ndani ya basi.

Tulionusurika tulikimbizwa hospitali, baada kama ya masaa 8 ya uangalizi, niliruhusiwa kutoka hospitali.

Siwezi kusema kupona kwangu ulikuwa ni werevu wangu, bali Mungu alipenda niendelee kuishi.
Amina 🙏
 
Tarehe 31 March 1993 nilipata ajali ya kukatwa na kitu chenye ncha Kali kwenye maeneo ya Mshipa wa jugula lakini Kwa uwezo wa Mungu ijapokuwa nilivuja Damu kiasi cha shati nililovaa kuwa mithili ya dekio lililowekwa kwenye ndoo ya maji lakini sikufariki, Kwa hakika siku ile niliamini Mungu Yupo kupitia damu ya Yesu Kristo.
mwaka 1993 nina miaka miwili😅😅😅
hapo cocastic hajazaliwa wala kuwazwa kuzaliwa
 
Wakuu
kumekuwepo na mijadala mingi humu ya mivutano baina ya wanaokubali uwepo wa Mungu na wasioamini uwepo huo

Mungu mala zote ni mtenda miujiza,na amekuwa akifanya hivyo mala zote kwa waja wake, amekuwa akiponya magonjwa yaliyoshindikana,vipofu wanaona,viziwi wanasikia,viwete,bubu,wasio na kazi, watoto, mume,mke nk wote wamekuwa wakiuona mkono wa BWANA/ALLAH.

Tuambie mkuu, ulipokea muujiza gani kutoka kwa Mungu ukaamini uwepo wake?

KARIBUNI.
Nilimuomba mwenyezi Mungu before 20 years nimiliki angalau 1M and about namshukuru Mungu Sasa I'm a successful man
 
Mwaka 2021 baada ya kukaa mtaani jobless Kwa Miaka Zaidi ya minne na nimechapika vibaya mno niliingia Kwenye maombi Kwa kushirikiana na Mama yangu kuomba MUNGU anipe KAZI. Usiku mmoja nikaota ndoto natembea barabara moja ambayo hata sijawahi pita na kwenye mazingira Yale nikafanikiwa kuingia Kwenye taasisi moja na kufanyiwa usaili tulikuwa watu watatu then nikawa selected pekeangu baada ya wiki Moja ile ndoto ikawa halisi vile vile Kuanzia Nguo nilizovaa Hadi mtaa nilioona Kwenye ndoto na barabara niliyopita Hadi geti la taasisi husika huku sijawahi enda eneo hilo Zaidi ya kutuma maombi Kwa njia ya email 📧 nilimshangaa sana MUNGU... In general Mimi Maisha yangu YOTE ni muujiza tu.... MUNGU UNAISHI...MKONO WAKO NI MKUU SANA
 
Miaka ya nyuma kidogo nlishawahi kufukuzwa om na sikuwa nahela wala mahala pakwenda nilikaa sehemu nikalia na kulalamika sanaa. Baadae nikapita mitaa ile ya om nikaskia mzee amehamishwa kwa dharula nilifurahi sana nakujua mungu yupo.
 
Muujiza hautoshi kuthibitisha uwepo wa M-ngu,even devils can do miracles.

Kinacho thibitisha uwepo wa M-ngu ni personal divine encounter,yaani M-ngu mwenyewe anajifunua kwako kibinafsi,hakuna dini wala sayansi inatosha kuthibitisha uwepo wa M-ngu,it must be your personal divine experience,binafsi nimeshakutana na malaika 2 times na nime encounter na Mwana wa M-ngu 1 time,sihitaji mtu wa kunithibitishia,Mimi mwenyewe nimethibitisha.
 
Back
Top Bottom