Ushawahi kwenda sehemu, baada ya kukuona wakakuchukulia poa, baadaye wakajua wewe ni mtu wa aina gani, wakaanza kukuonea aibu?

Ushawahi kwenda sehemu, baada ya kukuona wakakuchukulia poa, baadaye wakajua wewe ni mtu wa aina gani, wakaanza kukuonea aibu?

Mimi kazi yangu ina jina kubwa sanaa.Sasa watu wanafikiri nalipwa mamilioni masikini ya Mungu ,kumbe nakunja mia tisa na chenji kabla ya makato mpaka kurudi laki nne na kitu mfukoni.Basi watu mara waniombe niwaazime milioni kumi,mara niletewe prado linauzwa,mara mgeni rasmi wa kuongoza harambee.Kadi za harusi ndio hazina idadi.Kumbe ni masikini mwenye jina kubwaaaa.
Mheshimiwa Hakimu 😂😂😂
 
Wakuu, habari za jioni,

Katika maisha, mtu anaweza kuwa na kariba ya kawaida kabisa kiasi cha mtu mwingine kutojua au kutozoea tabia yake, hali inayoweza kusababisha kudharauliwa. Hata hivyo, baadaye watu hao huweza kugundua kwamba mtu waliyemdhani si wa kawaida kabisa na mawazo yao yanabadilika.

Iliwahi kunitokea siku moja nilipoenda ofisi fulani na kuwakuta wafanyakazi wote wakiwa wanawake. Nilipowasalimia, mmoja tu alijibu, tena kwa nyodo sana. Nilipowaambia kwamba nilihitaji bahasha zilizoachwa na bosi wao, waliniangalia kwa dharau. Wakati huo, nilikuwa nimevaa mavazi rahisi—pensi na sandle—na waliniuliza, "Wewe unazichukua kama nani?" Nikajibu kuwa nimeagizwa, lakini bado walinidharau na kuniambia, "Haya chukua, wahi daladala zimejaa sasa hivi."

Kumbe nilikuwa nimekuja na BMW nje ya ofisi. Walipokuwa wakijiandaa kuondoka, nikashuka ngazi na kwenda kwenye gari langu. Nilipofika kwenye eneo la kuegesha, walionekana kushangaa. Kwa heshima, nikawaambia, "Ingieni niwasogeze." Walikubali, lakini ndani ya gari walikuwa kimya kama wamemwagiwa maji. Walianza kucheka na kutabasamu huku wakifurahia upepo wa AC. Mmoja aliyekaa mbele aliniomba namba yangu ya simu, lakini sikufanya juhudi zozote za kuendelea mazungumzo naye, nikalipotezea tu.

Je, wewe umewahi kudharauliwa na watu, familia, au marafiki kutokana na mwonekano au hali fulani katika harakati za maisha?
Aise japo naona kama chai

Ngoja niseme tu

Mwaka 2019 kama sikosei nlikiwa nafanya kazi sehemu nchi jirani kwa boss mmoja yeye ni maarufu na anahela kweli

Aliniagiza niende makao makuu ya benk moja nchi jirani kuna jambo nifuatilie

Nilipofika nikakutana na warembo kweli , si unajua staff wa bank wanavopendeza

Mimi huwa ni simple sana japo sipendi kuwa hivo , sasa nikawaambia nahitaji huduma fulani nianzie ofisi gani?
Aise waliniangalia hovyo na kutokunkzingatia hadi nikaamua sasa niwaambie naomba nionane na fulani,maana sikutaka wafanye wajibu wao kisa fulani naenda kwake ,nilitaka wanipe maelezo ndio niingie

Baada ya kutaja naomba kumuona fulani na huyo mtu kushuka hadi floor ya chini walihaha sana , hawakuamini 😀

Sometimes tuwe humble tu , mimi sijawah mkandamiza mtu kisa ninauwezo wakufanya hicho
Mfano hata nikienda sehemu kunahuduma naweza ipata kwa haraka kisa namjua boss wa hilo eneo situmii hio advantage


PILI
Kunamda nilikuwa naonekana mimi ni dereva tu maana sieleweki, jamani tujiweke sawa

Tunaweza pishana na wawekezaji au watu muhimu kwa kutuchukulia poa


Ngoja tunitahidi tujimwambafai na kutafuta magari ya hadhi ya juu😀

Maoni tu
 
Mimi hapa aisee
Hakuna nunda haijakukuta

Mimi kuna kipindi nilienda mlimani city bookshop pale , nilikutana na mzee mmoja very simple

Nilivomuona akawa ananiongelesha namjibu kawaida kabisa na kutozingatia mengine anayoniambia, alitaka nizoea haraka sana nikachukulia poa wakati hata namba tungebadilishana

Sasa kwa njia zangu za haraka haraka wakati wa kulipia kitabu nikakuta kachukua vitabu kama 10+ sasa alilipa akaondoka

Baadae nikaambiwa huyu ni fulani ambaye ni mtu mzito sana na muhimu kwenye network za mjini

Kumbe ningemzingatia sana ningepata connection lakini nilimchukia poa sana nikawa simzingatii

Be active , connect with people bila ku assume tu
 
Ila kwakweli first impression inamata sana ndio maana matapeli pale posta mpya wana suti kali unaingia mkenge mwenyewe,kwahiyo huyo mtoa mada sio kwamba muongo ni kweli kabisa,watu wanakuchukulia jinsi wanavyokuona

Nakumbuka wakati mzee amehamishiwa wilaya ya kinondoni tukaenda kuishi oysterbay,sasa pale hatupo mbali sana na coco beach,so unaweza tupia yebo yebo tu kisha unajisogeza tu beach

Nimekaa zangu beach,nikamuona mrembo anapita nikamuita,sasa wakati huo miguu yangu ilikuwa imezibwa na kigogo cha mnazi,demu kusogea si ndio akaniona nimevaa yebo yebo huwezi amini demu akasepa,,kimoyo moyo nacheka we hujui mimi ni mtoto wa kishua

Kwahiyo kwa kifupi jinsi gani unajiweka ndio watu wanakupa hadhi yako
Kabisa first impression inaweza fukuza watu wa muhimu
 
Hakuna nunda haijakukuta

Mimi kuna kipindi nilienda mlimani city bookshop pale , nilikutana na mzee mmoja very simple

Nilivomuona akawa ananiongelesha namjibu kawaida kabisa na kutozingatia mengine anayoniambia, alitaka nizoea haraka sana nikachukulia poa wakati hata namba tungebadilishana

Sasa kwa njia zangu za haraka haraka wakati wa kulipia kitabu nikakuta kachukua vitabu kama 10+ sasa alilipa akaondoka

Baadae nikaambiwa huyu ni fulani ambaye ni mtu mzito sana na muhimu kwenye network za mjini

Kumbe ningemzingatia sana ningepata connection lakini nilimchukia poa sana nikawa simzingatii

Be active , connect with people bila ku assume tu
Aisee
 
Wakuu, habari za jioni,

Katika maisha, mtu anaweza kuwa na kariba ya kawaida kabisa kiasi cha mtu mwingine kutojua au kutozoea tabia yake, hali inayoweza kusababisha kudharauliwa. Hata hivyo, baadaye watu hao huweza kugundua kwamba mtu waliyemdhani si wa kawaida kabisa na mawazo yao yanabadilika.

Iliwahi kunitokea siku moja nilipoenda ofisi fulani na kuwakuta wafanyakazi wote wakiwa wanawake. Nilipowasalimia, mmoja tu alijibu, tena kwa nyodo sana. Nilipowaambia kwamba nilihitaji bahasha zilizoachwa na bosi wao, waliniangalia kwa dharau. Wakati huo, nilikuwa nimevaa mavazi rahisi—pensi na sandle—na waliniuliza, "Wewe unazichukua kama nani?" Nikajibu kuwa nimeagizwa, lakini bado walinidharau na kuniambia, "Haya chukua, wahi daladala zimejaa sasa hivi."

Kumbe nilikuwa nimekuja na BMW nje ya ofisi. Walipokuwa wakijiandaa kuondoka, nikashuka ngazi na kwenda kwenye gari langu. Nilipofika kwenye eneo la kuegesha, walionekana kushangaa. Kwa heshima, nikawaambia, "Ingieni niwasogeze." Walikubali, lakini ndani ya gari walikuwa kimya kama wamemwagiwa maji. Walianza kucheka na kutabasamu huku wakifurahia upepo wa AC. Mmoja aliyekaa mbele aliniomba namba yangu ya simu, lakini sikufanya juhudi zozote za kuendelea mazungumzo naye, nikalipotezea tu.

Je, wewe umewahi kudharauliwa na watu, familia, au marafiki kutokana na mwonekano au hali fulani katika harakati za maisha?
Ungesubiri wakuombe lift kwanza ndo uwape..by the way hukuamua kuwaletea ukauzu
 
Mimi kazi yangu ina jina kubwa sanaa.Sasa watu wanafikiri nalipwa mamilioni masikini ya Mungu ,kumbe nakunja mia tisa na chenji kabla ya makato mpaka kurudi laki nne na kitu mfukoni.Basi watu mara waniombe niwaazime milioni kumi,mara niletewe prado linauzwa,mara mgeni rasmi wa kuongoza harambee.Kadi za harusi ndio hazina idadi.Kumbe ni masikini mwenye jina kubwaaaa.
Mzee wewe sio masikini...vichenchi unavyo
 
Wakuu, habari za jioni,

Katika maisha, mtu anaweza kuwa na kariba ya kawaida kabisa kiasi cha mtu mwingine kutojua au kutozoea tabia yake, hali inayoweza kusababisha kudharauliwa. Hata hivyo, baadaye watu hao huweza kugundua kwamba mtu waliyemdhani si wa kawaida kabisa na mawazo yao yanabadilika.

Iliwahi kunitokea siku moja nilipoenda ofisi fulani na kuwakuta wafanyakazi wote wakiwa wanawake. Nilipowasalimia, mmoja tu alijibu, tena kwa nyodo sana. Nilipowaambia kwamba nilihitaji bahasha zilizoachwa na bosi wao, waliniangalia kwa dharau. Wakati huo, nilikuwa nimevaa mavazi rahisi—pensi na sandle—na waliniuliza, "Wewe unazichukua kama nani?" Nikajibu kuwa nimeagizwa, lakini bado walinidharau na kuniambia, "Haya chukua, wahi daladala zimejaa sasa hivi."

Kumbe nilikuwa nimekuja na BMW nje ya ofisi. Walipokuwa wakijiandaa kuondoka, nikashuka ngazi na kwenda kwenye gari langu. Nilipofika kwenye eneo la kuegesha, walionekana kushangaa. Kwa heshima, nikawaambia, "Ingieni niwasogeze." Walikubali, lakini ndani ya gari walikuwa kimya kama wamemwagiwa maji. Walianza kucheka na kutabasamu huku wakifurahia upepo wa AC. Mmoja aliyekaa mbele aliniomba namba yangu ya simu, lakini sikufanya juhudi zozote za kuendelea mazungumzo naye, nikalipotezea tu.

Je, wewe umewahi kudharauliwa na watu, familia, au marafiki kutokana na mwonekano au hali fulani katika harakati za maisha?
Yes, niliunganishwa na senior wangu kazi moja hivi ambayo alialikwa akaifanye yeye, na kwa namna ilivyokuwa nilikuwa naimudu vizuri sababu nishawahi kufanya zaidi ya hiyo

Sasa baada ya kufika yule jamaa kugundua mwamba kanituma mimi akaanza kuongea maneno ambayo hayakuwa mazuri kwamba ameletewa mtu ambae hajui kazi hivyo nitaharibu

niliifanya ile kazi kwa huzuni kidogo sababu mwamba hakunichangamkia hata kidogo na hata ule ushirikiano wa kawaida sikupewa kivile

nilimaliza kile kimeo kikawa fresh na wateja wake (yeye alikuwa kama cordinator) wakatumiwa ile kazi na wakaifurahia, sijui kama yeye aliiona au la

Fast forward miaka kadhaa mbeleni nikaapply Mchongo kwenye kampuni yao na nikapata kwenye kada tofauti na yake ila Mungu si athumani kumbe kile kitengo mkiwa na project mnakuwa wasimamizi halafu wale wengine wanakuwa watekelezaji

Siku ya kwanza tunapishana korido nilimsalimia akauchubua (sa sijui alijua dogo kaja kutafuta ajira au hata intern maana taasisi ilikuwa kubwa sio poa)

Mara ya pili hivyo hivyo

Siku alipagawa tunakutana kwenye fingerprint anabonyeza nami nabonyeza
Hajakaa vizuri tunakutana kwenye ofisi ambayo wanaingia wafanyakazi peke yao halafu na mimi nimo

Sijui aliuliza huko akaambiwa ajira mpya huyo tupo nae hapa, maana ilikuwa full aibu alinikazia for no reason na bado akaleta mikunjo

Mpaka kesho jamaa hajawahi kuwa na amani tunapokuwa pamoja hata tukipiga stori za kiofisi na staff wengine maana anajua siku niki-raise tu ile stori wana watamwona mchawi sana
 
Aisee, ni majuzi tu nimenunua kijumba flani hvi Chenye vyumba vinne vya wapangaji Kodi elfu 40. Sasa bwana ikatokea mpangaji mmoja akawa ametoroka siku ambayo kaahidi kunilipa kodi bila mimi kujua.

Sasa siku hiyo asubuhi nipo kijiweni na wana sina hili wala lile simu inaingia kupokea ni sauti ya kike, demu anabembeleza anataka chumba ameshaoneshwa kakipenda sasa mimi namuuliza chumba gani hiko tukawa hatuelewani, akanipigia tena nikamuelewa basi nikawa nimengamua jamaa wa kile chumba kahama na dalali wamempeleka huyu binti akaone hko chumba.

Yule dada akawa anabembeleza kwa adabu kubwa anaomba aanze na kodi ya miezi miwili kutokana na hali yake si nzuri nikawa nimemkubalia tukapanga jioni tuonane anilipe hiyo hela baada ya kazi.

Jioni ikafika akanielekeza mahali alipo na mimi muda huo nilikuwa nakunywa pombe na wanangu basi chaapu nikachukua pikipiki yangu chafuchafu hadi eneo alipo huyo dada, nikafika pale na kwa namna alivokuwa amesimama ile waiting mood nikawa nimejua ni yeye nikawa nimempita kidogo nikapaki fupa langu nikaanza kazi ya kumuita sasa, kila nikimuita yeye ndo kwanza hanisikii yupo bize na simu yake huku anatingisha nywele, kila nikimuita ananiangalia tu sometimes ananiangalia chini hadi juu, mwisho wa siku akanambia wewe kaka hebu sema shida yako ukiwa hapo nakusikia. Basi ikanibidi nijishushe sana ndiyo akasogea. Nikaanza kumlaumu si vizuri kumdharau mtu namna hiyo, akaanza maneno ya Shombo na dharau.
Kwa utaratibu na unyenyekevu mkuu nikamwambia mimi ndo yule mwenye nyumba umenambia tukutane hapa!!! Yule demu aliona aibu sana akaanza kunishangaashangaa....nikachukua afu 80 nikasepa zangu.....
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Back
Top Bottom