mshamba_hachekwi
JF-Expert Member
- Mar 3, 2023
- 20,704
- 66,337
HujaulizwaChai. Umechemsha chai hapo kukuambia wahi daladala saa hizi zimejaa. Yaani from no where mtu alopoke kukupangia usafiri wa kuondoka nao?. Haiji
Mheshimiwa Hakimu 😂😂😂Mimi kazi yangu ina jina kubwa sanaa.Sasa watu wanafikiri nalipwa mamilioni masikini ya Mungu ,kumbe nakunja mia tisa na chenji kabla ya makato mpaka kurudi laki nne na kitu mfukoni.Basi watu mara waniombe niwaazime milioni kumi,mara niletewe prado linauzwa,mara mgeni rasmi wa kuongoza harambee.Kadi za harusi ndio hazina idadi.Kumbe ni masikini mwenye jina kubwaaaa.
Aise japo naona kama chaiWakuu, habari za jioni,
Katika maisha, mtu anaweza kuwa na kariba ya kawaida kabisa kiasi cha mtu mwingine kutojua au kutozoea tabia yake, hali inayoweza kusababisha kudharauliwa. Hata hivyo, baadaye watu hao huweza kugundua kwamba mtu waliyemdhani si wa kawaida kabisa na mawazo yao yanabadilika.
Iliwahi kunitokea siku moja nilipoenda ofisi fulani na kuwakuta wafanyakazi wote wakiwa wanawake. Nilipowasalimia, mmoja tu alijibu, tena kwa nyodo sana. Nilipowaambia kwamba nilihitaji bahasha zilizoachwa na bosi wao, waliniangalia kwa dharau. Wakati huo, nilikuwa nimevaa mavazi rahisi—pensi na sandle—na waliniuliza, "Wewe unazichukua kama nani?" Nikajibu kuwa nimeagizwa, lakini bado walinidharau na kuniambia, "Haya chukua, wahi daladala zimejaa sasa hivi."
Kumbe nilikuwa nimekuja na BMW nje ya ofisi. Walipokuwa wakijiandaa kuondoka, nikashuka ngazi na kwenda kwenye gari langu. Nilipofika kwenye eneo la kuegesha, walionekana kushangaa. Kwa heshima, nikawaambia, "Ingieni niwasogeze." Walikubali, lakini ndani ya gari walikuwa kimya kama wamemwagiwa maji. Walianza kucheka na kutabasamu huku wakifurahia upepo wa AC. Mmoja aliyekaa mbele aliniomba namba yangu ya simu, lakini sikufanya juhudi zozote za kuendelea mazungumzo naye, nikalipotezea tu.
Je, wewe umewahi kudharauliwa na watu, familia, au marafiki kutokana na mwonekano au hali fulani katika harakati za maisha?
Hakuna nunda haijakukutaMimi hapa aisee
Anaota ndoto😀Huyu jamaa ni muongo kinoma😀
Kabisa first impression inaweza fukuza watu wa muhimuIla kwakweli first impression inamata sana ndio maana matapeli pale posta mpya wana suti kali unaingia mkenge mwenyewe,kwahiyo huyo mtoa mada sio kwamba muongo ni kweli kabisa,watu wanakuchukulia jinsi wanavyokuona
Nakumbuka wakati mzee amehamishiwa wilaya ya kinondoni tukaenda kuishi oysterbay,sasa pale hatupo mbali sana na coco beach,so unaweza tupia yebo yebo tu kisha unajisogeza tu beach
Nimekaa zangu beach,nikamuona mrembo anapita nikamuita,sasa wakati huo miguu yangu ilikuwa imezibwa na kigogo cha mnazi,demu kusogea si ndio akaniona nimevaa yebo yebo huwezi amini demu akasepa,,kimoyo moyo nacheka we hujui mimi ni mtoto wa kishua
Kwahiyo kwa kifupi jinsi gani unajiweka ndio watu wanakupa hadhi yako
AiseeHakuna nunda haijakukuta
Mimi kuna kipindi nilienda mlimani city bookshop pale , nilikutana na mzee mmoja very simple
Nilivomuona akawa ananiongelesha namjibu kawaida kabisa na kutozingatia mengine anayoniambia, alitaka nizoea haraka sana nikachukulia poa wakati hata namba tungebadilishana
Sasa kwa njia zangu za haraka haraka wakati wa kulipia kitabu nikakuta kachukua vitabu kama 10+ sasa alilipa akaondoka
Baadae nikaambiwa huyu ni fulani ambaye ni mtu mzito sana na muhimu kwenye network za mjini
Kumbe ningemzingatia sana ningepata connection lakini nilimchukia poa sana nikawa simzingatii
Be active , connect with people bila ku assume tu
Ushaanza kutamani BMW yake😂..ndio anamiliki hata haringihuo mshangazi una BM?
wewe...
Ukiletewa hiyo mialiko ya ugeni rasmi unafanya nin?Wapi niko sehemu nazunguka na mafaili tu kama kichaa🤣🤣
Nawaambia tu ukweli huko mnakoniitia kuna hitajika fedha na mimi sina fedha.Za Kanisani kwetu huwa natokea najipiga piga ingawa ndani kwa ndani cha moto nakiona.Ukiletewa hiyo mialiko ya ugeni rasmi unafanya nin?
Ungesubiri wakuombe lift kwanza ndo uwape..by the way hukuamua kuwaletea ukauzuWakuu, habari za jioni,
Katika maisha, mtu anaweza kuwa na kariba ya kawaida kabisa kiasi cha mtu mwingine kutojua au kutozoea tabia yake, hali inayoweza kusababisha kudharauliwa. Hata hivyo, baadaye watu hao huweza kugundua kwamba mtu waliyemdhani si wa kawaida kabisa na mawazo yao yanabadilika.
Iliwahi kunitokea siku moja nilipoenda ofisi fulani na kuwakuta wafanyakazi wote wakiwa wanawake. Nilipowasalimia, mmoja tu alijibu, tena kwa nyodo sana. Nilipowaambia kwamba nilihitaji bahasha zilizoachwa na bosi wao, waliniangalia kwa dharau. Wakati huo, nilikuwa nimevaa mavazi rahisi—pensi na sandle—na waliniuliza, "Wewe unazichukua kama nani?" Nikajibu kuwa nimeagizwa, lakini bado walinidharau na kuniambia, "Haya chukua, wahi daladala zimejaa sasa hivi."
Kumbe nilikuwa nimekuja na BMW nje ya ofisi. Walipokuwa wakijiandaa kuondoka, nikashuka ngazi na kwenda kwenye gari langu. Nilipofika kwenye eneo la kuegesha, walionekana kushangaa. Kwa heshima, nikawaambia, "Ingieni niwasogeze." Walikubali, lakini ndani ya gari walikuwa kimya kama wamemwagiwa maji. Walianza kucheka na kutabasamu huku wakifurahia upepo wa AC. Mmoja aliyekaa mbele aliniomba namba yangu ya simu, lakini sikufanya juhudi zozote za kuendelea mazungumzo naye, nikalipotezea tu.
Je, wewe umewahi kudharauliwa na watu, familia, au marafiki kutokana na mwonekano au hali fulani katika harakati za maisha?
Yupo chini ya 30?
Mzee wewe sio masikini...vichenchi unavyoMimi kazi yangu ina jina kubwa sanaa.Sasa watu wanafikiri nalipwa mamilioni masikini ya Mungu ,kumbe nakunja mia tisa na chenji kabla ya makato mpaka kurudi laki nne na kitu mfukoni.Basi watu mara waniombe niwaazime milioni kumi,mara niletewe prado linauzwa,mara mgeni rasmi wa kuongoza harambee.Kadi za harusi ndio hazina idadi.Kumbe ni masikini mwenye jina kubwaaaa.
Yes, niliunganishwa na senior wangu kazi moja hivi ambayo alialikwa akaifanye yeye, na kwa namna ilivyokuwa nilikuwa naimudu vizuri sababu nishawahi kufanya zaidi ya hiyoWakuu, habari za jioni,
Katika maisha, mtu anaweza kuwa na kariba ya kawaida kabisa kiasi cha mtu mwingine kutojua au kutozoea tabia yake, hali inayoweza kusababisha kudharauliwa. Hata hivyo, baadaye watu hao huweza kugundua kwamba mtu waliyemdhani si wa kawaida kabisa na mawazo yao yanabadilika.
Iliwahi kunitokea siku moja nilipoenda ofisi fulani na kuwakuta wafanyakazi wote wakiwa wanawake. Nilipowasalimia, mmoja tu alijibu, tena kwa nyodo sana. Nilipowaambia kwamba nilihitaji bahasha zilizoachwa na bosi wao, waliniangalia kwa dharau. Wakati huo, nilikuwa nimevaa mavazi rahisi—pensi na sandle—na waliniuliza, "Wewe unazichukua kama nani?" Nikajibu kuwa nimeagizwa, lakini bado walinidharau na kuniambia, "Haya chukua, wahi daladala zimejaa sasa hivi."
Kumbe nilikuwa nimekuja na BMW nje ya ofisi. Walipokuwa wakijiandaa kuondoka, nikashuka ngazi na kwenda kwenye gari langu. Nilipofika kwenye eneo la kuegesha, walionekana kushangaa. Kwa heshima, nikawaambia, "Ingieni niwasogeze." Walikubali, lakini ndani ya gari walikuwa kimya kama wamemwagiwa maji. Walianza kucheka na kutabasamu huku wakifurahia upepo wa AC. Mmoja aliyekaa mbele aliniomba namba yangu ya simu, lakini sikufanya juhudi zozote za kuendelea mazungumzo naye, nikalipotezea tu.
Je, wewe umewahi kudharauliwa na watu, familia, au marafiki kutokana na mwonekano au hali fulani katika harakati za maisha?
Kutoka moyoni kabisa kwa ukweli wa Mungu hela sina ila kazi inanibeba sanaa ina jina kubwaaa sana ila mshahara wake sisimizi.Mzee wewe sio masikini...vichenchi unavyo
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Aisee, ni majuzi tu nimenunua kijumba flani hvi Chenye vyumba vinne vya wapangaji Kodi elfu 40. Sasa bwana ikatokea mpangaji mmoja akawa ametoroka siku ambayo kaahidi kunilipa kodi bila mimi kujua.
Sasa siku hiyo asubuhi nipo kijiweni na wana sina hili wala lile simu inaingia kupokea ni sauti ya kike, demu anabembeleza anataka chumba ameshaoneshwa kakipenda sasa mimi namuuliza chumba gani hiko tukawa hatuelewani, akanipigia tena nikamuelewa basi nikawa nimengamua jamaa wa kile chumba kahama na dalali wamempeleka huyu binti akaone hko chumba.
Yule dada akawa anabembeleza kwa adabu kubwa anaomba aanze na kodi ya miezi miwili kutokana na hali yake si nzuri nikawa nimemkubalia tukapanga jioni tuonane anilipe hiyo hela baada ya kazi.
Jioni ikafika akanielekeza mahali alipo na mimi muda huo nilikuwa nakunywa pombe na wanangu basi chaapu nikachukua pikipiki yangu chafuchafu hadi eneo alipo huyo dada, nikafika pale na kwa namna alivokuwa amesimama ile waiting mood nikawa nimejua ni yeye nikawa nimempita kidogo nikapaki fupa langu nikaanza kazi ya kumuita sasa, kila nikimuita yeye ndo kwanza hanisikii yupo bize na simu yake huku anatingisha nywele, kila nikimuita ananiangalia tu sometimes ananiangalia chini hadi juu, mwisho wa siku akanambia wewe kaka hebu sema shida yako ukiwa hapo nakusikia. Basi ikanibidi nijishushe sana ndiyo akasogea. Nikaanza kumlaumu si vizuri kumdharau mtu namna hiyo, akaanza maneno ya Shombo na dharau.
Kwa utaratibu na unyenyekevu mkuu nikamwambia mimi ndo yule mwenye nyumba umenambia tukutane hapa!!! Yule demu aliona aibu sana akaanza kunishangaashangaa....nikachukua afu 80 nikasepa zangu.....