Usianike life style yako mtandaoni, binadamu hana tabia ya kusahau, binadamu hasamehi

Kuna sababu gani ya kumpost mtoto wako mchanga kwenye mitandao?
Au kula kwako Bata?
Km Ni kupost tupost vitu km biashara ili kupata wateja nk.
Huo ni mtazamo wangu
Una mtizamo chanya. Hongera sana. Lakini inakuja hoja kwamba unampost mtoto wako na maelezo kwamba eti mwanangu anakojoa kitandani nifanyeje? ana tatizo la mgongo wazi nfanyeje? Sasa ukiliangalia swali hilo unaweza kujiuliza ; Je, hapa Jf ni Hospitali? au mtu anamsema mume/mke wake kwamba haachi fedha ya matumizi nyumbani, anamchepuko wake kule, ni mlevi n.k. Hapo unajiuliza kwani hapa Jf ni mahakama au ni kitengo cha ushauri nasaha? Mwulizaji anaishia kupata kejeli, anapewa ushauri wa kumdidimiza zaidi au anapata tena kazi ya kusoma, kutafakari achukue lipi kati ya majibu mengi yatakayotolewa na wadau n.k. Huo ni matazamo wangu pia.
 
Hapo ndo penye shida,
 
Upo sahihi kila mtu anafanya kile kinachompa raha na amani ya moyo, binafsi hata nilipwe kupost nadhani nitatumia nguvu kubwa sana kulitekeleza hilo.
 
Siku ukijua tu wewe unatumia ID fake utakuwa ushamwelewa mlera Uzi.
 
Acheni kufanya maisha yawe magumu hivyo bhana.!!
😁😁😁 sio maisha kuwa magumu Ila kuwa na kiasi. Lazma ujue details gani ni za kuweka mtandaoni na zingine zibaki kwenye private zone miss.

Haitakiwi mtu akikufanyia background check mtandaoni akujue nje ndani kwa sababu kuna vitu vingine unavifanya kama fun Ila watu muhimu wanakutengenezea picha mbovu. Kupost tupost Ila tuwe makini na tunapost nini
 
maisha siku zote yana pande mbili 2.
kila mtu na aishi kwenye mfumo wake ambao anataka kuishi.
 
Unaishi vingunguti ndani ndani huko watu tunajua mpaka ratiba yako ya kula miguu ya kuku magengeni afu unaanza kutuletea soga zako za my life my privacy,privace ya nyoko.hayo maisha praivesi tuwaachie kina bill gates na kina bakhresa,wengi wanaounga mkono eti tuishi maisha ya Siri Siri na upweke upweke kama wachawi wengi wao ni wale SADISM ambao wanapenda kufurahia matatizo ya wenzao ndio maana watu wakipost mambo yao mitandaoni tena ya wakaida tu huwa na wivu,husda,gele,roho mbaya na ndio maana wanapiga vita ili wenzao wawe kama wao kwa kisingizio cha kuishi maisha privacy.Kwani mtu akimpost mwanae ana birthday kuna shida gani!!??? au mtu yuko na wana wanakula bia wana show love wewe kinakuuma nini!!?? SADISM IS REAL
 
Naunga mkono hoja
 
Nchi inatakiwa ichangamke hii, unataka tukose connection za waungwana sasa.!! 😹

Madilu alikuwa hapost chochote na kiongozi muadilifu lakini kimada wake akauza connection kwa Mangeanalia anatetemeka binti alivyompagawisha, na yule baba Askofu naye genye zimemsaliti kaletwa nginjanginja analia anamsifia kondoo wake alivyonona 🀣🀣🀣
 
Tuanze na wewe kwanza, kwanini hausahau? Kwanini hausamehi? Kwanini ukoseshe amani watu wanaoonyesha furaha yao mtandaoni? Tuanze kwa kusolve tatizo kwanza sio kuliepuka kwa kubadili lifestyle!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…