Usianzishe biashara wala kutafuta kazi kupitia waganga wa kienyeji

Usianzishe biashara wala kutafuta kazi kupitia waganga wa kienyeji

Okay.

Umesema jini ni kiumbe roho asietokana na binadamu na pepo ni kiumbe roho anaetokana na wafu na viumbe roho wengine ambao sio binadamu.

Je viumbe roho hao wengine ni wapi? Na je mapepo ina maana ndio mizimu?
We kiongozi kuna kitu unakijua na sasa unalinganisha kidogo na akijuacho mtoa mada ili uje na conclusion yako ambayo itaenda sawa na mtoa mada au itatofautiana!
 
Mshana ni sawa na mwanamke, leo atasema ameokoka kesho atasema amerudi kilingeni, hajui anashikilia nini...

Ni mjinga, na nimefikia kuhisi huenda ni double agent, watu wa namna hii hawafai kufuata.

Hata hivyo kuishi katika dunia hii ni inahitaji unafiki mtupu, watu wajifanya kumkiri Mungu mbele ya watu ila mambo wayatendayo sirini ni hovyo kabisa.

Mshana uache unafiki, maana unafiki Ni asili ya wachawi...
Dah, mdau matusi haya ya nini?!!!!! Kwa kosa lipi?!!!! Hv umeona kuwa habari zake zinasomwa na kujibiwa na wengi sana?
 
Je inawezekana hao viumbe roho wa wanyama wakaingilia ulimwengu wa viumbe roho wa kibinadamu?

Na je ikiwa mimi sipo kwenye cycle ya viumbe roho vya aina hizo. Mafano sifanyi matambiko na rituals zozote za ku invoke viumbe roho hivyo. Pia sijawahi kuroga mtu wala uchawi siujui, sijawahi kwenda kwa mganga wala mambo ya wanga na ulozi sijawahi kushiriki.

Yani katika nyanja hiyo unaweza kusema mimi sipo kabisa. Je watu na viumbe roho vya ulimwengu huo vinaweza kunidhuru?
Hapana umeme haupiti pasipopitisha umeme,means sio mtu wao,labda uwachokoze uanze vita nao
 
Natangaza maslahi yangu! Mimi sio mganga na sifanyi ushirikina tena..!

Kati ya waganga wote wa kienyeji ni asililia kumi hivi kati ya mia moja ndio wakweli na kati ya hao wakweli ni asilimia 5 tu ndio wenye masharti nafuu na wanaoweza kukusaidia moja kwa moja..! Ishu ya kuwajua feki na wakweli tutaona huko mbele

Kwanza lazima tukubaliane kuwa ushirikina ni utumwa, na ushirikina ni masharti na vigezo..Na ushirikina ni kitu chenye kuhitaji update kila wakati.. Na waganga wengi ni wapigaji..!

Pamoja na shida zako zote usijaribu kwenda huko kwenye ushirikina kutafuta 'assist' huko unaenda kufanya registration kwenye data base yao na hatimaye kuwa kwenye himaya yao..MAKINIKA!

Chochote kinachohusika na ajira ama biashara ukiachana na visomo vya kidini lazima kitahusisha damu.. Automatically itakuwa damu ya mnyama hasa mbuzi na ng'ombe ama kuku.. Kwa uchache kabisa na kwa siri kubwa damu ya mtu itahusika..

Mnyama anayechinjwa kwa shughuli za ushirikina ni wazi analazimishwa kufa kabla ya muda wake wa kufa kutimia.. Vita yake yoyote ya kiroho baada ya hapo utaibeba wewe.. Kwahiyo utakuwa na vita mbili ama zaidi ya kupigana.. Vita yako, vita ya kuku, vita ya mbuzi nknk.. Na hapa ndio siri ya side effect asiyokwambia mganga, Lakini lingjne ni hili... Yule mnyama aliyetumika kukutengenezea mambo yako ana ukomo wake wa kuwa, hivyo wakati wake wa kufa ukifika, kafara ulilotengenezewa nalo hufa rasmi..! Hapo ndio utaona mambo yako yanavyoanza kuyumba na hatimaye kuharibika kabisa

Lingine ni kwamba kuna wakati katika maisha mambo huenda mrama bila sababu yoyote ile..ni asili tu inafanya kazi, wewe kwa kuhofia kuwa tayari umeshapigwa na kitu kizito tena, utakimbilia kwa mtaalam wako tena, na yeye hata kama hakuna tatizo atalitengeneza na kukutisha sana.. Juu ya yote kwakuwa tayari uko kwenye database zao kuna wakati huamua kukorofisha mambo ili tu umuendee ajione bingwa ama kuna kitu umtimizie

Mwishowe unakosa kabisa ladha ya maisha unafanya biashara lakini hutulii ni makafara kwa kwenda mbele, una kazi yako nzuri Lakini masharti ni kama yote ...unapata pesa Lakini huna furaha nazo
Mganga naye ni binadamu akiamua kula bata hutengeneza tatizo kwakuwa kila mganga ni mchawi.. Pesa ya kutengeneza tatizo ndio huwa pesa ya starehe kwakuwa haimpi masharti kama ile pesa ya kilinge inayotokana na tatizo genuine!

Mwanzoni mwa biashara, ajira na hata mahusiano na miradi mingine epuka sana kuyanajisi na ishu za giza yasije yakaja kukutesa mbeleni, kwa kuwa kuingia huko ni rahisi sana lakini kutoka ni habari nyingine..Na ni shughuli pevu
Vipi kuhusu kucha na nywele mkuu.
 
Natangaza maslahi yangu! Mimi sio mganga na sifanyi ushirikina tena..!
Waganga/ wachawi wako tofauti na hawa wanaotoa dawa za miti shamba? Unakuta una mchango tumbo linauma unaelekezwa kwa mtu akupatie dawa, unaenda unachukuwa dawa unakunywa, sometimes unapona au hauponi.

Na kila unapooenda atakubadilishua dawa, mara hii inatinu UTI, mara hii hutibu matatizo ya mgongo kuuma, na dawa nyingine anakupa majani uyapike unywe ila hayo majani unakuta unayajua etc

Je hawa watoa dawa za miti shamba nao ni genge moja na waganga?
 
Dah, mdau matusi haya ya nini?!!!!! Kwa kosa lipi?!!!! Hv umeona kuwa habari zake zinasomwa na kujibiwa na wengi sana?
Hakuna jamii ambayo imeendelea bila Mambo ya mila/waganga, Hakuna. Anzia hata huko Geita Gold Mine Mtu mweupe anapofanya kazi zake lazima mila zitumike.

Sasa huyu Mshana anachofanya ni kumdhihaki Mungu, leo anajifanya anasifia Mambo ya uganga na mara nyingi yeye husifia uchawi hata hivyo na kesho ajifanya yuko katika dini.

Hata Serikali zote duniani zimesimama katika misingi ya mila/uganga, na katika watu wanaologwa Sana ni watu wa dini, ninao uhakika, kwanini udiscourage kitu ambacho kinasaidia watu?

White people religions have failed to destroy witchcraft in Africa, why should you still continue to look for them?

Angalia Tanga kuna dini sana na ushirikina umejaa, tena walioleta dini ndo wakaleta na huo ushirikina...

Mshana abadilike aache tabia ya unafiki...
 
Uganga ama uchawi haupo, ni watu wenye akili fupi tu wanaweza kuamini kitu kinaitwa uganga, uchawi, ulozi ama ushirikina, ni watu wenye akili ndogo tu wanaamini hayo mambo.

Mwenye akili ndefu hebu jaribu kusoma historia lakini pia soma hata vitabu vya dini vimeandika kuhusu haya mambo ya ulizi, unless uwe haupo kote kote kwende dini na si muumini wa historia. Lakini pia unaweza kuuliza maswali kwa wazee wako waliokutangulia...tusikaze vichwa kuonekana wajuaji.
 
Back
Top Bottom