Usifanye hii Kazi, Hata Kama Maisha yakiwa magumu sana

Usifanye hii Kazi, Hata Kama Maisha yakiwa magumu sana

1. Kuokota chupa za plastic za kupima kwa kilo.

Hii kazi inauhusiano wa moja kwa moja na ukichaa.
Katika tafiti yangu ndogo nimegundua wanaojihusisha na hii kazi lazima akili ziruke kidogo.

Kuna mmoja hapo External alikuwa mzima kabisa hadi alipoanza kuzunguka na mfuko huko barabarani kutafuta chupa/makopo ya maji/soda n.k! Mwingine ni wa Maramba mawili, hawakuchukua muda sana akili kuvuruga.

Jihadhari na hii kazi, hata maisha yawe magumu kiasi gani...

2. Bodaboda (esp. Graduates) Hapa nawazungumzia vijana walioenda shule kidogo, at least una shahada. Jiepushe sana na Bodaboda!! zinaharibu sana akili.
Vijana wengi waliohitimu vyuo vikuu na kujiingiza kwenye boda, kuchomoka huwa ni shughuli sana, japo wapo wachache sana wanaojitahidi.

3. Udalali; (hii kwa graduates pia)
Wapo vijana wengi wa sasa hasa kwa Dar wakimaliza vyuo wanaaanza kazi ya udalali wa nyumba na viwanja.
Kigamboni huko wamejazana sana, wengi wao ni walevi tu hakuna cha maana wanachoweza kufanya zaidi yakupata pesa na kuishia kwenye ulevi.
Hii kazi Usifanye. Haina matunda yoyote kwenye future yako.

4. Usidange; (hasa mabinti) umemaliza chuo huna ishu ya maana mjini rudi kwenu kakae na wazazi wako huku ukiendelea kutafuta cha kufanya.


Nawasilisha.
Kazi yoyote hile inaweza kuwa daraja la kuvuka kuifikia kazi iliokuwa bora zaidi inategemea na malengo yako

Wapo waliokota Makopo ikawa daraja la kufikia malengo yao

Wapo walioanza kubeba watu kwa baisikeli kisha bodaboda sasa wana safirilisha watu kwa mabasi yao

Wapo madalali wa viwanja vyumba wako vizuri tu

Ulisahau wabeba mizigo wapiga debe Makonda wa dala dala wavuzi wachana mbao kweli ukiwatazama maisha yao wengi wao walevi wazinzi sababu kipata ni kikubwa cha kila siku walicho kosa ni malengo tu
 
Mzee Baba Kuna Wengine Walikuwa Na Akili Timamu Kabisa, Baada Ya Kuingia Kwenye Ndoa Wakarukwa Na Akili.
 
kazi ni kazi kikubwa uwe na nidhamu,maadili na utu.
N.B: Never ever break your personal laws.
 
Back
Top Bottom