Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Mada imekushinda toka mwanzo hadi mwisho! Sasa kama umeficha madini hapo katikati ambapo sikupasoma kwa kukosa uvumilivu na niliyosoma mwanzo mwa mada na mwisho wake, lawama ni yako kwa mtindo wako mbovu wa uandishi.

Niliposoma kichwa cha habari tu, nikavutiwa sana na kutaka kujuwa yaliyomo ndani ya mada yenyewe.

Mstari wa kwanza tu, nikaona mada imepinda. Sikukata tamaa nikajikaza nivute subira. Nikasoma hadi nusu ya andiko; nikaishia hapo. Sikuwa na nguvu tena za kuendelea hadi mwisho wa andiko refu lisilokuwa na mvuto kulisoma.
Lakini nikawa na wasiwasi kwamba pengine nikiruka hadi kule mwisho nitakuta mambo yanayohusiana na kichwa cha mada yenyewe, hata kama itakuwa ni katika mhitasari tu!

Looo, sikuona kitu. Nikaamua kunyanyua hayo niliyobamiza hapo juu kwa kuwa 'disappointed' na mada nzima, isipokuwa kichwa chake cha habari tu basi!

Pole yako ya kuwa na muda wa kupoteza, na pole yetu wasomaji wako kwa kupotezewa muda.

😀😀😀
Kamuonyeshe Mchumba wako ulicho-comment alafu mpe na Mada niliyoandika alafu utaona Nani anafaa kuambiwa pole.

Embu kaa, tulia, soma Mada uolewe, kisha Kama umeamua kupinga uje Kwa hoja.
Na sio uje ujivue nguo hapa alafu hujatoa hoja yoyote.

Labda ningekuuliza, Mada hii dhamira yake kuu ni ipi?
 
Kuna mambo yanashangaza Sana. TMA ishatangaza kuwa kutakuwa na uhaba wa mvua ndani ya nchi.

Wizara ya maji tangazo Hilo ingekuwa ni Alert kwao kuwa kutakuwa na upungufu wa Maji Kwa mwaka huu au miaka hii miwili mitatu. Hivyo tayari kabla tatizo la maji halijajitokeza mbele za watu wa kawaida au wachini kabisa wangetakiwa washajiandaa kukabiliana na changamoto zote za uhaba WA Maji unaotokana na uhaba wa mvua.

Yaani kuna mambo mengine ukiyatafakari unabaki kusikitika Sana.

Serikali lazima iongozwe na watu wenye AKILI.
Na Kama wenye akili sio watawala Kwa sababu ya uoga basi Wale majasiri wawe watawala alafu wawatumie wenye akili katika kuwapa mawazo na ushauri.
Pole Sana ndio maana huwa nasema Kama huna taarifa usiongee la hasha unakuwa mpumbavu..

Wizara ya Maji inajenga mabwawa makubwa 31 mwaka huu kwenye maeneo kame achilia mbali mabwawa ya wizara ya kilimo na mabwawa makubwa zaidi yanayoendelea na ujenzi Kama Farkwa na Kidunda.
 
Mbaya zaidi waliopo juu kwenye uongozi wengi ni weupe mpaka huruma. Unajiuliza kama kiongozi wao yupo hivi wananchi watakuwaje. Tz haina huo utajiri katika nyanja zote iwe ni siasa, maofisini, michezo nk

Mbaya zaidi awamu ya 5 na 6 watu wanaotumia akili hawatakiwi
Wewe ambae sio mweupe endelea kusubiria mbeleko
 
Mkuu hili tatizo la watu wenye uwezo mdogo kuwa viongozi ni la kihistoria. Wakati Nyerere anachukua nchi wasomi walikuwa ni wachache, hivyo watu wenye elimu kubwa wakawa wanajikita zaidi kwenye kazi za taaluma.

Matokeo yake wasio na elimu wakajikita kwenye siasa. Kidogo kidogo wasio na elimu wakaanza kuwa na maamuzi.

Wasomi walipoamua kuingia kwenye siasa wakakuta wameshachelewa maana wasio na elimu ni mabingwa wa fitina na zengwe.

Hii ndio sababu kwenye siasa zetu hasa ndani ya ccm mizengwe ni njia namba moja ya kupambana.
Wewe mwenye uwezo mkubwa mbona huchukui uongozi unasinguzia historia?
 
Bila Akili hivyo vitu haiviwezi kuwa Rasilimali.
Ili kitu kiwe Rasilimali lazima Akili iwepo.

Jambo lolote lile linaweza kuwa Rasilimali ukiwa akili ipo.

Mfano, kabla ya Wazungu kuja mambo mengi hayakuwa Rasilimali, kama nawe ya dhahabu hayakuwa madini mpaka wenye akili walipokuja.

Gesi ya mtwara tupo nayo miaka nenda Rudi lakini hatukujua kama ipo na hata tungejua tusingejua matumizi yake Kwa sababu hatuna Akili.


Akili ndio hukipa kitu thamani, kitu chenyee Kama kitu hakina thamani mpaka akili ikipe thamani
Hizo rasilimali ndio zimeshakuwepo na thamani yake ipo, usiturudishe enzi za ujima tuanze uvumbuzi upya.

Muhimu ni usimamizi wa kueleweka ili thamani yake ilete manufaa kwa jamii husika, kuzipiga teke hizo rasilimali kisha tutafute akili pekee kama utakavyo utakuwa ni uchizi.
 
Wewe umeambiwa kutakua na ukame na nishati kama umeme unategemea maji na kila mwaka unalia kuna ukame yaani haujaona vyanzo anuwai kama upepo, makaa ya mawe, gesi ukatumia kuzalisha umeme wa kukutosha na mwingine ukauza? Yaani kila mwaka unalia tatizo lilelile bado hata kama ni kiongozi useme una akili wakati kutatua changamoto umeshindwa miaka yote
Kwa hiyo Serikali iko.kimya haifanyii kazi hivyo vyanzo anuwai au? Punguzeni uzuzu, vyanzo mbadala sio madarasa kwamba ndani ya mda mfupi vinakuwa tayari..

Pili Hakuna rasilimali fedha za kutosha kugawanya ili kila kitu kiende sawia..Mathalani leo Serikali ikipunguza Pesa za bwawa la Nyerere then mvua ikanyesha na bwawa likachelewa mtaanza Tena kulaumu ooh wanachelewesha bwawa na blaa blaa zingine za kijinga..

Ndio maana huwa nasema ili kuongoza vyema hapa Afrika lazima kuwapiga Pini wajinga wengi Kama wanavyofanya kina PK,M7,Al Sisi nk.
 
Kulaumu viongozi ni sawa ila tatizo ni sisi, kwanza viongozi ni reflection ya watu wake maana hatukodi kutoka nje badi ni sisi wenyewe, kama kiongozi umemuweka madarakani lakini akizingua kumtoa huwezi sasa hapo alaumiwe nani kama sio wewe uliemchagua..
Watetezi wa ujinga nchini hapo watakwambia, wananchi wameshindwa kumtoa kiongozi mpumbavu kama tulionao kwa sababu wanalindwa na bunduki.
 
Mada imekushinda toka mwanzo hadi mwisho! Sasa kama umeficha madini hapo katikati ambapo sikupasoma kwa kukosa uvumilivu na niliyosoma mwanzo mwa mada na mwisho wake, lawama ni yako kwa mtindo wako mbovu wa uandishi.

Niliposoma kichwa cha habari tu, nikavutiwa sana na kutaka kujuwa yaliyomo ndani ya mada yenyewe.

Mstari wa kwanza tu, nikaona mada imepinda. Sikukata tamaa nikajikaza nivute subira. Nikasoma hadi nusu ya andiko; nikaishia hapo. Sikuwa na nguvu tena za kuendelea hadi mwisho wa andiko refu lisilokuwa na mvuto kulisoma.
Lakini nikawa na wasiwasi kwamba pengine nikiruka hadi kule mwisho nitakuta mambo yanayohusiana na kichwa cha mada yenyewe, hata kama itakuwa ni katika mhitasari tu!

Looo, sikuona kitu. Nikaamua kunyanyua hayo niliyobamiza hapo juu kwa kuwa 'disappointed' na mada nzima, isipokuwa kichwa chake cha habari tu basi!

Pole yako ya kuwa na muda wa kupoteza, na pole yetu wasomaji wako kwa kupotezewa muda.
Ipo haja ya kupitisha sheria kali ya kupiga risasi hadharani watu wote mnaoonesha dalili za kutokuwa na akili hapa nchini.

Hii kwa namna moja au nyingine itasaidia kupunguza idadi kubwa ya watu nchini ambao hawana umuhimu au mchango wowote kwenye mustakabali wa Taifa letu.

Kuna chama fulani tukipitisha hii sheria kinaweza kupoteza wanachama wake wengi sana maana ndicho kina idadi kubwa ya wajinga nchini. Ifike kipindi wananchi wenye akili wafanye movement ya kukataa kuongozwa na wananchi wengine wenye changamoto au upungufu wa akili unaowafanya washindwe ku make sound judgement kwenye masuala mbalimbali ya taifa letu.
 
Wewe, 'mkulu senkonda' si mtunzi wala mwanzilishi wa haya uliyoyaweka hapa, umeyanyanyua tu toka mahala, lakini hukutaka kuonyesha ulikoyatoa.
Unafanya kazi chafu bila ya kujuwa ni nani unayemfanyia kazi hiyo, tena bila malipo yoyote. Hii inadhihirisha wazi kabisa wewe kuwa mfano wa hao weusi wanaosemwa kwenye mada yenyewe.

Sasa kama hata huwezi kutambua kwamba Xi Jinping hawezi kusema hayo yanayosemekana kayasema, wewe akili yako itakuwa imelala kabisa.
Siwezi kufanya vile unavyotaka wewe. Ni ujumbe tu wenye maana inayojitosheleza uliotolewa na watu wanaojielewa na wala sijasema kama mm ndio namiliki hayo maudhui.
 
Mpaka hapa andiko lako limesadifu maudhui kwa kuangalia michango ya wadau karibu 90% ya waliochangia.
90% wote wameinyooshea kidole serikali na kujisahau wao.
Wamesahau kuwa mtaji wa kwanza wa serikali ni rasilimali watu.
Serikali kwa kiwango kikubwa inategemea kufanya maendeleo kwa kutegemea kodi toka kwa watu.Watu ambao ni wakulima,wafanya biashara,wavuvi,wafugaji n.k.
Serikali hayo yote haifanyi imewaachia wananchi.
Sasa je,sisi wananchi tunaopaswa kufanya shughuli hizo ili kuiletea serikali kodi stahiki,tunatumia akili zetu vizuri katika shughuli zetu?.Je,sisi raia tumetumia uwezo kiasi gani wa kufikiri ili kufikia mafanikio ya juu?.
Kwa nini sisi raia tunaridhika na mafanikio kidogo tu tunayoweza kupata?.
Kwa nini mimi mwenye kimtaji ch 10m nina kuwa rough na matumizi ya pesa yasiyo ya lazima?.
Kwa nini mimi niamini eti Mo Dewij hapo alipofika ni kwa sababu eti ya mali za urithi?.
Kwa nini mimi nisizitafute na kuzipitia njia alizopita Bhakhresa ili nami niwe juu kiuchumi?.

Katika maskani mbalimbali za vijana na watu wazi,maongeze makuu ni juu ya NGONO, POMBE NA MIPIRA.Yaani hakuna mipango na mikakati utayokuta ikijadiliwa.

Aisee!Maswali ni mengi sana dhidi yetu sisi raia tulio mtaji wa kwanza kwa serikali kuliko
Serikali yenyewe.
 
Pole Sana ndio maana huwa nasema Kama huna taarifa usiongee la hasha unakuwa mpumbavu..

Wizara ya Maji inajenga mabwawa makubwa 31 mwaka huu kwenye maeneo kame achilia mbali mabwawa ya wizara ya kilimo na mabwawa makubwa zaidi yanayoendelea na ujenzi Kama Farkwa na Kidunda.

😀😀😀

Ni hatua nzuri Kabisa.
Ila ninachozungumzia ni kuwa kama taarifa imetolewa mapema hatua hizo zingechukuliwa mapema pia.

Ni Sawa TANGAZO litolewe kuwa walio mabondeni wahame Kwa sababu mvua zitakuwa nyingi Hali itakayosababisha mafuriko.
Alafu hakuna hatua iliyofanyika mpaka mvua zimenyesha na watu wanaathirika na mafuriko ndio hatua zinachukuliwa.

Hiyo ndio hoja yangu
 
Mpaka hapa andiko lako limesadifu maudhui kwa kuangalia michango ya wadau karibu 90% ya waliochangia.
90% wote wameinyooshea kidole serikali na kujisahau wao.
Wamesahau kuwa mtaji wa kwanza wa serikali ni rasilimali watu.
Serikali kwa kiwango kikubwa inategemea kufanya maendeleo kwa kutegemea kodi toka kwa watu.Watu ambao ni wakulima,wafanya biashara,wavuvi,wafugaji n.k.
Serikali hayo yote haifanyi imewaachia wananchi.
Sasa je,sisi wananchi tunaopaswa kufanya shughuli hizo ili kuiletea serikali kodi stahiki,tunatumia akili zetu vizuri katika shughuli zetu?.Je,sisi raia tumetumia uwezo kiasi gani wa kufikiri ili kufikia mafanikio ya juu?.
Kwa nini sisi raia tunaridhika na mafanikio kidogo tu tunayoweza kupata?.
Kwa nini mimi mwenyewe kimtaji ch 10m nina kuwa rough na matumizi ya pesa yasiyo ya lazima?.
Kwa nini mimi niamini eti Mo Dewij hapo alipofika ni kwa sababu eti ya mali za urithi?.
Kwa nini mimi nisizitafute na kuzipitia njia alizopita Bhakhresa ili nami niwe juu kiuchumi?.

Katika maskani mbalimbali za vijana na watu wazi,maongeze makuu ni juu ya NGONO, POMBE NA MIPIRA.Yaani hakuna mipango na makakati utayokuta ikijadiliwa.

Aisee!Maswali ni mengi sana dhidi yetu sisi raia tulio mtaji wa kwanza kwa serikali kuliko
Serikali yenyewe.

Watanzania Kodi hatutaki kutoa alafu ndio wakwanza kulalamika.
Lakini pia ukitoa Kodi kuna wenye uroho wanazitumbua kifisadi Kwa mambo Yao binafsi na kujineemesha wenyewe. Hapo ndipo msala Ulipo.

Serikali ilikuwa inahitaji watu sampuli ya kina Nyerere ndio washike nyazifa za juu. Watu wasio na tamaa ya Mali.
Lakini watu sampuli ya kina Nyerere ni wachache Mno sio ajabu nchi nzima wasifike 10.

Watoto wanakuzwa kibinafsi hivyo wakikua nao wanakuwa wabinafsi
 
Siwezi kufanya vile unavyotaka wewe. Ni ujumbe tu wenye maana inayojitosheleza uliotolewa na watu wanaojielewa na wala sijasema kama mm ndio namiliki hayo maudhui.

Huyo Achana Naye, ni sampuli ya watu wapumbavu ambao wakiwa mbele za watu hasa kwenye mijadala wanajifanya wako na hoja lakini katika maelezo Yao watakayoyatoa hakuna kitu cha maana wanachozungumza.

Yaani ni ili Naye aonekane anauwezo na anakitu chakuongea kumbe hamnazo.
 
😀😀😀

Ni hatua nzuri Kabisa.
Ila ninachozungumzia ni kuwa kama taarifa imetolewa mapema hatua hizo zingechukuliwa mapema pia.

Ni Sawa TANGAZO litolewe kuwa walio mabondeni wahame Kwa sababu mvua zitakuwa nyingi Hali itakayosababisha mafuriko.
Alafu hakuna hatua iliyofanyika mpaka mvua zimenyesha na watu wanaathirika na mafuriko ndio hatua zinachukuliwa.

Hiyo ndio hoja yangu
Habari za ukame ziliwnza mwaka Jana ndio bajeti ya mwaka huu ikahusisha hiyo mipango na hata bajeti ijayo itahusisha masuala hayo ya kukabiliana na ukame ,Sasa shida iko wapi?

Changamoto za Sasa Ni kwa vile mifumo iliyopo haikuwa imetake hizo precautions huko tulikotoka but by 2025 hutosikia kelele za sijui maji Mara umeme nk..
 
Hizo rasilimali ndio zimeshakuwepo na thamani yake ipo, usiturudishe enzi za ujima tuanze uvumbuzi upya.

Muhimu ni usimamizi wa kueleweka ili thamani yake ilete manufaa kwa jamii husika, kuzipiga teke hizo rasilimali kisha tutafute akili pekee kama utakavyo utakuwa ni uchizi.

😀😀😀

Mimi siwarudishi watu nyuma, Ila Sisi wenyewe ndio tunajirudisha nyuma kimatendo kutokana na upeo mdogo wa Akili.

Mfano, ukataji wa miti bila kupanda miti, Nani asiyejua Miri ni Rasilimali muhimu katika uzalishaji WA hewa Safi na kuvuta mvua? Lakini Kwa sababu hatuna Akili utashangaa mtu kwenye Nyumba yake amekata miti karibu yote alafu ananunua Kiyoyozi au Feni😂😂 na kulalamika kuna Joto.
Ujinga ni gharama Sana.

Mfano mwingine, watu wanatupa takataka hovyo, wanaharisha na kunya hovyohovyo kama Mbuzi maji taka meusi yakizagaa katika makazi Yao. Kumbuka kabla hawajaja eneo Hilo kulikuwa Safi lakini tangu waje wao wendawazimu ndio Hali imekuwa hivyo.
Hawajui umuhimu wa Mazingira Safi?
Alafu muda huohuo wanataka Serikali na viongozi wawapangie come on!
Hicho ndicho ninachozungumzia.

Mimi siwarudishi watu Enzi za ujima au ukabaila Ila nataka watu tuwe na AKILI naam akili zenye Akili
 
Habari za ukame ziliwnza mwaka Jana ndio bajeti ya mwaka huu ikahusisha hiyo mipango na hata bajeti ijayo itahusisha masuala hayo ya kukabiliana na ukame ,Sasa shida iko wapi?

Changamoto za Sasa Ni kwa vile mifumo iliyopo haikuwa imetake hizo precautions huko tulikotoka but by 2025 hutosikia kelele za sijui maji Mara umeme nk..

Mimi sina tatizo wala shida na yafanywayo na Serikali.
Nachojaribu Kueleza ni kuwa tuwe na AKILI ili Kupunguza uzito wa matatizo na changamoto.
Sipo hapa kumlaumu yeyote.
Nipo hapa kuonyesha matatizo yetu ya ndani tuliyoayo Kama taifa ili kujua nini tunapaswa kufanya kujirekebisha.
 
Back
Top Bottom