Mathayo 12
25 Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.
26 Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?
Marko 3
23 Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?
24 Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;
25 na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
26 Na kama Shetani ameondoka juu ya nafsi yake, akafitinika, hawezi kusimama, bali huwa na kikomo.