UTEUZI: Maharage Chande aondolewa TTCL, ateuliwa kuwa Postamasta, Ulanga arudishwa TTCL

UTEUZI: Maharage Chande aondolewa TTCL, ateuliwa kuwa Postamasta, Ulanga arudishwa TTCL

🤣 Zuhura Yunusi mwambie mama asifanye ukatili huu wa kisaikolojia.

Yaani ndio tumetoka Kanisa kwenye misa ya shukrani kwa uteuzi wa TTCL, kufika nje kuwasha tu simu tunakutana na pdf la Zuhura Yunusi 🤣 tumeng'atuliwa na kuteuliwa tena kwenye taasisi nyingine.

Tutawasiliana na Baba paroko tena kesho
Kwa ajili ya Misa nyingine sio? By the time mnamaliza mkitoka nje unapewa taarifa mandondo atapangiwa kazi nyingine.
 
Liwapo kwenye maji boya huwa linaeleaelea likienda huku na kule kutegemeana na mawimbi na upepo, lakini lenyewe huwa halina mwelekeo wala maamuzi.
Ukiona linazama ujue limevutwa kuzamishwa, likiibuka uju limeachiwa, likienza kwenda ujue limapelekwa likirudi ujue limerudishwa and the story goes on just like that.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Maharage seems to be a failed man. Why then the appointee dont dump him into a TRUSH BIN??

Hii katiba yetu licha ya kwamba inampa mamlaka makubwa sana Rais, lakini at the same time inamfanya aonekane ni mtu wa KUPUYANGA.
Wamemtoa private sector akiwa na package kali tu kila mwisho wa mwezi. Nadhani alivyoletwa kwenye sector ya umma, kati ya makubaliano nae ilikuwa kumuhakikishia job security. So Maharage tuko nae sana tu ndugu yangu.
 
Ni kweli kwamba Teuzi zinafanyika , lakini za safari hii ni Kiboko !

Ulanga aliondolewa Juzi TTCL , leo karejeshwa tena , sasa hatujui shida ilikuwa wapi ? bali tunaona kwamba uteuzi wa namna hii unapaswa kuwekwa kwenye vitabu vya Kumbukumbu .

Screenshot_2023-09-25-20-38-52-1.png


Tahadhari : Mkubwa Hakosei
 
Maharage seems to be a failed man. Why then the appointee dont dump him into a TRUSH BIN??

Hii katiba yetu licha ya kwamba inampa mamlaka makubwa sana Rais, lakini at the same time inamfanya aonekane ni mtu wa KUPUYANGA.
Kwamba shida/tatizo ni huyo Maharage? Acheni hizo bwana, sote tunajua tatizo lilipo...tunalifumbia macho tu.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi kama ifuatavyo:

Amemteua Bw. John Ulanga kuwa Balozi. Bw. Ulanga ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Amevunja Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na amemteua Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Amemteua Bw. Maharage Chande kuwa Postamasta, Shirika la Posta Tanzania. Kabla ya uteuzi huu Bw. Chande aliteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL). Bw. Chande anachukua nafasi ya Bw. Macrice Daniel Mbodo ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Aidha, Mhandisi Peter Ulanga ataendelea kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL).
Yaani Maharage wamemtafutia nafasi kwa nguvu, mbona posta master alikuwa vizuri sana! Yaani wameangalia wapi pana mtu ambaye hana Godfather, ila tunaamini cha mtu huwa hakipotei. Maharage is a tota failure anapaswa awe jela
 
Watu wanasema ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni.
Maneno hayo yamedhihirishwa na Serikali ya Awamu ya sita na kudhihirisha ule usemi wa kuruka ruka kwa maharage ndo Kuiva kwake!.

Baada ya Maharage chande kuliwa kichwa cha Mkurugenzi mtendaji TANESCO na kupewa UKURUGENZI MKUU TTCL leo Mchana ameliwa Tena kichwa na kupelekewa kuwa Postamasta mkuu na kunyang'anywa Medani ya UKURUGENZI MKUU..

HONGERA ENG.PETER ULANGA...
POLEE SANA MAHARAGE NDO MAISHA YALIVYO..
Screenshot_20230925-205000.png
 
Back
Top Bottom