Uteuzi: Rais Samia amteua Humphrey Polepole kuwa Balozi Malawi, Mchechu arudishwa NHC

Uteuzi: Rais Samia amteua Humphrey Polepole kuwa Balozi Malawi, Mchechu arudishwa NHC

uteuzi wa kimkakati sana huu [emoji16][emoji16]
 

Maprofesa wa chuo kikuu cha Dar es salaam ninaomba mnieleweshe hili jambo:-​

Kuna watu waliteuliwa na JK akiwa Rais, alipoingia JPM watu hao walifukuzwa wote, sasa ameangia Samia anawarudisha wote waliofukuzwa na JPM ila walikuwa wameteuliwa na JK kabla.​

Swali la msingi ni nani anamshauri Samia kuteua tena waliokuwa wameteuliwa na JK ila walifukuzwa na JPM?​

 
Sawa Nahodha hapo atapewa Wizara, hongera kwa Mchechu kurudishwa NHC kwani alilihudumia vyema shirika, Polepole Malawi akatatue mgogoro wa ziwa Nyasa [emoji3][emoji3][emoji3]
 
Huwezi jua ya Mungu mengi na hujafa hujaumbika...
Huo Ni mtego ili aone Kama atakubali kuchutama, akizingua hakai hata mwaka.

Anakua kama mwenzie nchimbi kule brazil[emoji4]
 
Rais Samia Suluhu amemteua Humphrey Polepole kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi.

Sambamba na hilo Rais Samia Suluhu amemteua Shamsi Vuai Nahodha kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pia Rais Samia Suluhu amemteua Waziri Kindamba kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe.

Kindamba alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa TTCL na anachukua nafasi ya Mhandisi Marwa Rubirya ambaye amestaafu kwa umri.

Polepole na Kindamba wanatarajiwa kuapishwa kesho Jumanne tarehe 15 Machi 2022 Ikulu ya Chamwino Dodoma saa 04:00 Asubuhi.

Katika hatua nyingine Rais Samia Suluhu amemteua Nehemia Mchechu kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Mchechu ambaye amewahi kuhudumu kwenye wadhifa huo, anachukua nafasi ya Dkt. Maulid Banyani ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Pia amemteua Balozi na Mkuu wa Jeshi la Polisi (Mstaafu) Ernest Jumbe Mangu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Bandari (Tanzania Port Authority).

Na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Peter Ulanga kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL).

Ulanga ni Mkurugenzi Mstaafu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF).

Na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Meja Jenerali John Julius Mbungo, Mkurugenzi Mstaafu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuwa Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika la Meli Tanzania (MSCL).

View attachment 2150380
Duuu
Wameamua kumficha mfichua wahuni ili asiendelee kuwafichua wahuni
 
Teuzi Kama hizi huwa Ni maalum ili kukuondolea umaarufu na kukufilisi kijanja.

Ukishakua nje ya nchi attention yako inakua Ni ndogo mno, pia Kama una vimiradi vyako ulianzisha lazima viyumbe.
Ukija kurudi bongo, unakua Kama ndo unaanza upya.

Mfano mzur muone Dr. Slaa na mabalozi wengine walio wastaafu walio nje ya mfumo, yaan utadhan ndo wanaanza maisha[emoji4]
kabisa mkuu. ubalozi wanafaidi watoto tu ila balozi mwenyewe kama ni siasa anakua amepotezwa kwenye ramani kabisa
 
Acha Kukariri

Performance za Nehemia pale NHC ni sawa na ya Dau pale NSSF au ya Dr Kimei pale CRDB …hazijawahi kufikiwa kabla na baada yao wamepigiwa kelele weeeeee za kila aina lakin baada ya kuondoka hakuna lolote la maana

Awamu ya nne Ndege ya Mzee kila ikiruka kwenda ng'ambo kwny mambo ya Uchumi, fedha na uwekezaji basi mmoja kati ya hao mapacha watatu lazima awepo
Huyu mchechu amewekwa pale ili akapige vizuri
 
Back
Top Bottom