Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaan mm unijui na mm sikujui.Halafu unaniandikia utoporo.Hauoni kuwa ,ww hauna kitu kichwani.Ni popoma.Pia lazima ujue Kama hao wanaoteuliwa kwa kuwa wana urafiki na Msoga Gang ndio maana nchi ipo nyuma siku zote.Hizo CV zingekuwa za ukweli ,tusingekuwa na umasikini mkubwa Kama huu.Wanaojua na wenye akili sana ,wengi wapo nje ya system.Beside ,Nehemia alichaguliwa kwa upendeleo pale NHC.Ilihitishwa interview ambayo Ilikuwa chini ya kampuni moja ya kimataifa.Na kampuni hiyo katika kipindi hicho ililipwa pesa nyingi sana kwa ajili ya hiyo kazi.Watu wengi walijitokeza kwenye usaili.Nehemiah alipata point za chini sana.Lakin aliteuliwa kwa hila kuwa mkurugenzi.Pesa nyingi za serikali zilipotea kwa kuwa tu Katibu mkuu wa Ikulu those big days alikuwa wa Njombe pia.Kutolewa kwake pale na JPM Ilikuwa sawa tu.Hana jipya.For reference kindly review the past threads of JF in regard to appointment of Msechu to be a director of NHC in those big days.Definetely most of the threads were so discourage with his appointment.Wewe una CV gani ya kuaminiwa kupewa enterprise kama NHC? Ungekuwa na uwezo ungepewa
Weka ushahidi wa wizi wake hadharani nasi tupate kuufahamuHuyu Ahmad ni mwizi tu aliyekuwa NHC zamani
utajuaje kama ni mtanganyika au mpemba kwa kutumia jina tu? Watanganyika wameoa wapemba wengi tu pengine ni jina la babu yake, au imekuwa ni dhambi kuitwa jina hilo>Kuna makame mtanganyika ?
Uwe wazir wa barabara ushindwe kujenga Hako kajengo jmn![]()
Tetesi mitaani: jengo la Mbarawa hapo Mwenge.
Wabongo bana.kwani kuwa na jengo ni kosa?![]()
Tetesi mitaani: jengo la Mbarawa hapo Mwenge.
Bila sababu???
Huyo mzanzibari. Walinga'ng'ania kutenga mambo ya mafuta na gas. Huyu makame anatafuta nini tpdc.Kuna makame mtanganyika ?
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi kama ifuatavyo:-
1. Amemteua Bw. Nehemia Kyando Mchechu, kuwa Msajili wa Hazina. Kabla ya uteuzi huo Bw. Mchechu alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC). Bw. Mchechu anachukua nafasi ya Bw. Mgonya Benedicto ambaye atapangiwa kazi nyingine.
2. Amemteua Bw. Hamad Abdallah, kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC). Kabla ya uteuzi huo, Bw. Abdallah alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Gimcoafrica Limited na anachukua nafasi ya Bw. Mchechu ambaye ameteuliwa kuwa Msajili wa Hazina.
3. Amemteua Bw. Mussa Mohammed Makame, kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC). Kabla ya uteuzi huo, Bw. Makame alikuwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), na pia ni Mshauri Mwelekezi wa masuala ya mafuta na gesi nchini Tanzania. Bw Makame anachukua nafasi ya Dkt. James Mataragio ambaye atapangiwa kazi nyingine.
Uteuzi huu ni kuanzia tarehe 24 Februari, 2023.
View attachment 2528416
=====
MAJUKUMU YA OFISI YA MSAJILI WA HAZINAKwa mujibu wa Kifungu cha 10 cha Sheria ya Msajili wa Hazina Sura 370 kama ilivyorekebishwa, Ofisi imepewa majukumu yafuatayo: –
1. Kufanya mapitio ya kudumu ama kuhakikisha kunafanyika mapitio ya kudumu ya shughuli na mwenendo wa watu ama Taasisi ambazo Msajili wa Hazina anamiliki mali ama ana maslahi kwa mujibu wa Sheria.
2. Bila kuathiri Kifungu kidogo cha (1) kwa ujumla wake, Msajili wa Hazina anatakiwa:
- Kutoa ushauri kwa Serikali kuhusu uanzishaji wa Mashirika ya Umma na kusimamia biashara au mali zilizowekezwa kwenye Mashirika hayo;
- Kupitia utendaji wa kifedha wa Mashirika kwa lengo la kushauri hatua za kuchukua katika kuunganisha, kuboresha muundo, kufuta au kuboresha utendaji wa Mashirika na Taasisi za Umma;
- Kuweka malengo ya kifedha na vigezo vingine vya utendaji vitakavyotumiwa na Mashirika na Taasisi za Umma;
- Kufanya tathmini mara kwa mara ili kupima utendaji wa Bodi au Menejimenti za Mashirika na kutoa mapendekezo kwa Serikali ya hatua za haraka au zilizopo za kuboresha usimamizi wa rasilimali;
- Kuidhinisha uwekezaji wa hisa unaofanywa na Mashirika ya Umma kwenye Mashirika au Kampuni nyingine;
- Kuwekeza au kuuza mali za Mashirika ya Umma;
- Kuhakikisha kuwa kila Shirika la Umma linaingia Mkataba wa Utendaji na Msajili wa Hazina mara moja baada ya kuteuliwa kwa Bodi ya Wakurugenzi;
- Kufuatilia na kutathmini programu za mafunzo katika Mashirika na Taasisi za Umma;
- Kuelekeza au kuidhinisha matumizi au marekebisho ya kanuni za fedha ili kuhakikisha usahihi wa taarifa za mapato na matumizi ya Mashirika ya Umma;
- Kuchambua na kuidhinisha Miundo na Mifumo ya Mishahara, Kanuni za Utumishi na Mpango wa Motisha kwa Mashirika na Taasisi za Umma;
- Kufuatilia misaada, ruzuku, fedha za mtaji, akiba au malimbikizo ya faida katika Mashirika ya Umma na kwenye uwekezaji mwingine wa Umma;
- Kupendekeza au kuidhinisha Mipango ya Mwaka ya Mashirika na Taasisi za Umma;
- Kufuatilia na kutathmini utendaji wa Mashirika na Taasisi za Umma; na
- Kufanya ufuatiliaji na kuhakikisha gawio, michango na mikopo kutoka katika Mashirika na Taasisi za Umma inalipwa kwa wakati.
Naamini Mchechu aliulizwa tumuweke ani badala yako,ila kuendelea kuwa na mirija NHC akamkumbuka jamaa yake . Ni mwendo wa si kulamba asali tu bali kufakamia asali,tena asali ile ya nyuki wadogo wasiong'ata.Kabla ya GIMCO alikuwa NHC pamoja na Mchechu kabla Magufuli hajawatimua bila sababu kwa WIVU wake.
Ngoja tusubiri baraza la maulamaa linasemajeWaislamu wa bara wanapiga madufu tu, zero kabisa
Uzuri halitaenda Pemba, ataliacha hapo hapo Mwenge![]()
Tetesi mitaani: jengo la Mbarawa hapo Mwenge.
Mulilazimisha rasilimali za mafuta ziwe za Muungano, au vipi?Je TPDC ni mambo ya Muungano?
Huyo Makame amefikaje hapo?
Jaji Lewis Makame na Makame Rashid yule aliyekuwa mkuu wa JKT (kwao Mtwara)Mtanganyika gani anaitwa Makame?
KATIKA KERO 11 alizotatua Hangaya juzi juzi ni kwamba Maliasili zote za Tanganyika ni halali kwa Zanzibar ila Maliasili zote za zAnzibar sio mali ya Tanganyika.Hiyo "mali ya Tanzania ni mali ya Zanzibar ila mali ya Zanzibar siyo mali ya Tanzania"yaani inakera basi tu,sijui kwenye kero za muungano haipo.
Kampuni ya kihuni haina uwezo wa kufanya just real estate managementNimeshangaa sana...
Hiyo inabidi ikatiwe rufaa kama uwezekano upo.KATIKA KERO 11 alizotatua Hangaya juzi juzi ni kwamba Maliasili zote za Tanganyika ni halali kwa Zanzibar ila Maliasili zote za zAnzibar sio mali ya Tanganyika.
Safar hii kazi mnayo