Uwanja wa Mkapa: Yanga yashindwa kutamba uwanja wa nyumbani, yalazimishwa sare na Kagera Sugar

Utopolo wametepeta tena. Sare ya 3 mfululizo kwenye ligi. Simba akishinda viporo vyake vyote anakuwa na pointi +2. Tuendelee kuwaombea washinde Simba.
Simba wakishinda viporo vyake vyote atakua na points ngapi?
 
Wamekosa magoli ya wazi lakini utawasikia wanaililia bodi ya ligi na waamuzi
 
Tupe matokeo, mvua na jua ikawaje tena mtani?
 
Siku zote utopolo ilikuwa inashinda kwa bahati na si ujuzi zaidi. Kiujuzi utopolo ni ya kawaida sana na huwezi ukategemea bahati kuwa bingwa.
 
Yaani hawa ndio wanataka wachukue ubingwa wakacheze klabu bingwa? Hebu kuwe serious jamani..!
 
Yanga ni kama kikundii tu cha ngoma wala tusiwalaumu wachezaji wote wamecheza kwa uwezo wao wotee ila uwezo ndio umeishia pale
 
Hivi awa waamuzi kutoziona izi penalty wanazo stahili kupata Yanga ni makosa ya kibinadamu au ndio rushwa michezoni. Maana linaonekana Kama Jambo linalo endelea na mbaka sasa halionyeshi mabadiliko. Awa wachezaji wa Yanga ni binadamu Kama wengine wanavyo porwa ushindi kwa njia Kama hizi kunasiku uvumilivu utawashinda watajichukulia hatua. Bodi ya Ligi iwe makini Kuna Jambo si la kawaida linafanyika kuvuruga mpira.
 
Na bado leo tena Wachezaji wa Yanga wameendelea na Ugonjwa wa kumzonga mwamuzi! Bodi ya Ligi toeni matokeo ya Vurugu za Mbeya Haraka. KASEKE, KAZE NA LAMINE Pini ya miezi 6 tunaisubiri haraka.
 
Kwa kweli Yanga leo wamewakalia vibaya Kagera...na kuweza kulazimisha droo ya 3-3 baada ya kagera kuongoza mda wote huku Yanga wakisawazisha mda woote. Naiona Yanga iliyobora sasa tofauti na ile ya mwaka jana...Wakiendelea na juhudi hii hawakosi nafasi ya pili msimu huu
 
Mashabikia maaandraazzi wanatema povu[emoji196][emoji196][emoji196]
 
Upo uwekano sio bodi ya ligi na TFF tu, hata FIFA wachunguzwe wanaikandamiza Yanga! Anyway ' Vimba Mwanayanga Vimba' msemaji kasema
 
Aaaah unafiki wa kihaya huu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…