Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

Nimetoka tu nje ya ofisi nikakutana na gari ya tangazo inaanza kutangaza, watu wameshika vichwa wengine wanacheka na mimi ikabidi nicheke.

Ila wametubana sana watembea kwa miguu aisee
Yaani wametubanaaje!!! Tunakoswa koswa na magari utadhani hatuna haki kutembea pembeni maana wamejaa wao. Halafu ole wako ukanyage kitu cha mtu!!!!
 
Hiyo poa saaaana. Na iwe hivyo na majiji mengine,hususani mbeya. Bajaji pia mbeya ni bomu linalosubili kulipuka. Imekuwa kero
 
Gari la tangazo linapita kutangaza ya kuwa ifikapo tarehe 18 mwezi huu hakitakiwi kibanda chochote kuonekana kando kando ya barabara katika jiji la Dar es salaam.
Hii nimeisikia hata kwenye Jiji la Dodoma. Wamewaambia wahamie kwenye masoko ya Ndugai, Sabasaba na Majengo. Tena ndani ya majengo ya masoko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…