Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

Viondoke haaaraaakaaaaa.
Wanachelewaaaaah hawa!
Jiji lilikuwa takataka kabisaaaah!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Watakao subiri ya mjini itakula kwao! Watakapozinduka Gezaulole Mpya itakuwa imejaa; kupata eneo watatakiwa kulipia gharama kubwa kama mjini. Sisi tuliopo vijijini tukisikia kuwa kuna eneo jipya limefunguliwa tutachangamkia fursa. Wa mjini wamezoea kuwa wachuuzi watasubiri kuchuuza pilipili, mboga na maboga yetu.
 
Yani kwa hili naunga mko kwa 100% kulikuwa hakuna usawa wa kibiashara,
Machinga wengi ni wafanya biashara wakubwa walioamua kujifichia humo.
 
Swala la machinga waondoke tu mjini wanaua biashara watengewe maeneo yao Magufuli alibugi sana


Kwanza hawalipi kodi na wanaponunua bidhaa hawaombi risiti kwenye maduka makubwa so serikali inapata hasara ya kodi.

Vile vile wengi mjini ni wafanya biashara wakubwa wanafanya kutoa pesa kwenye mfuko wa suluali na kuweka kwenye mfuko wa shati.


Ndio maana ukwepaji kodi unaongezeka kwa sababu watu wenye address za kulipa kodi biashara zao wanachukua machinga.

Halafu machinga wenyewe wanauza sana halafu hawana leseni za biashara za kufanyia kazi wengine unakuta ndio wale waliofunga maduka kipindi cha Magufuli unakuta machinga ameweka bidhaa za milio 10 nje hii sio haki hata kidogo.

Watafutiwe maeneo maalumu kama Tandika tegeta, Ubungo mbagala wawe na shopping mail zao na walipe kodi ili tuone kama watauza tens bidhaa ovyo na kuhatarisha hata maisha ya wanunuzi.

Unakuta mtu anauza nyanya kariakoo katikati ya barabara seriously sehemu ambayo mnasema ni soko la kimataifa.?
Halafu wanauza bei ya kutupa washenzi wale...mmfano kiatu jumla kinauzwa 3200 ye anatoka nacho nje anauza 3500. Ana hasara gani..anauza piece hamsini kwa siku halipii chochote
 
Tatizo vijana hawapendi kulima wanapenda kukaa mjini wakati mikoani ndio kuna utajiri . Nguvu kazi ya machinga ingekuwa vijijini nchi inge export Mazao mengi nje na kupata dola
 
Sasa nje ya mji wakati wao target yao ni wale watu wanaopita pita stand
Si nje sana,angalia sasa hivi mbagala mwisho pale au tandika kushakua full,lile shazi sasa hivi linahamia mbezi na tegeta nyuki huko,sasa maeneo kama hayo kama yanaandaliwa ipasavyo baada ya miaka kadhaa watu watazoea huko nje ya mji na pale town patamua kimtindo
 
Tayari wameshatafutiwa au watoke kwanza,
MAANA kilio chao toka zamani ni kuwa maranyinhi huwa wanapelekwa au kutengewa maeneo yasiyo na tija kwa biashara zao
Duh sijui itakuwaje
... "maeneo yasiyo na tija"; hapo ndipo tatizo lilipo! Kwao maeneo yenye tija ni maeneo yenye "watu wengi" na maeneo yenye watu wengi obviously ni katikati ya miji na pembezoni mwa barabara kuu kuingia mijini.

Yaani ni as if wanalazimisha, kwa mfano, kwa Dar wote warundikane Karakoo, Posta, Buguruni, Magomeni, Mwenge, Manzese, Temeke Mwisho, Gongo la Mboto Mwisho, na pia wajengewe mabanda along Nyerere, Morogoro, Ali Hassan Mwinyi, Mandela, or similar roads! Hii haiwezekani.
 
Gari la tangazo linapita kutangaza ya kuwa ifikapo tarehe 18 mwezi huu hakitakiwi kibanda chochote kuonekana kando kando ya barabara katika jiji la Dar es Salaam.

Katika mambo nitakayo muunga Mkono Mama ni hili la wafanya biashara wa vibanda mitaani, waondolewe, na kama wawepo ni kwa utaratibu maalumu na wawe na efd machine au wafuate utaratibu wa Rwanda kuwa sehemu moja .


Na uzuri Mama anataarifa nyingi toka Dunia nzima na wasaaidizi wataalamu wa vitu vingi
 
Wale wapumbavu walikuwa wanaita watu wanyonge na wao kujiita wanyonge utadhani unyonge ni sifa nawambia hiviii tafuteni rais wenu wa wanyonge.
Huyu tuliyenae ni rais wa kufata utaratibu sio kufata unyonge wenu umbwa nyinyi wazee wa mapambio
 
Hata hao machinga wakitafutiwa sehemu, tatizo huwa hawataki kwenda...wao wanataka kujichagulia sehemu yoyote watakayo...watu wajifunze kufuata sheria bila shuruti..... ili miji iwe safi na salama. Mambo ya kubembeleza na au kuonekana aibu ili kupata support ya kisiasa, ndo yametufikisha hapa....tafadhali safisheni miji yote,wasioweza warudi wakalime vijijini tupate chakula ili tukuze uchumi! Kazi iendelee.
Watafutiwe sehemu salama kwa ajili ya biashara zao.
 
Nadhani kama taifa lazima kuwa na utaratibu maalum, haiwezekani watu wanaamua kufanya kila sehemu ni ya kuuza matango, parachichi, chupi, blauzi Yani vurugu tupu.

Serikali imetenga maeneo ya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo masoko, viwanja vya magulio ya wiki, minada, viwanja vya mpira, na kila aina ya shughuli mbalimbali Zina maeneo yake.

Kitendo cha machinga kufanya biashara maeneo yasiyo rasmi inakosesha Halmashauri mapato ya ushuru pamoja na Kodi za pango. Pia tunakuwa tunawaumiza wale walioweka biashara zao maeneo rasmi na hii ni double standard haifai kama taifa.

So walizoea kuwekwa maeneo yasiyo rasmi na ilikuwa kuna kero zake na raha yake pia Ila hata mie naona waondoke tu waende sehemu rasmi.

Hapo zamani tulishazoea mtumba ni Karume tu baada ya manzese kutimuliwa Ila sasa najiuliza wale walioenda Karume so hawapati biashara? Hii sio sawa. Warudi kule.
Karume biashara ipo sababu sehemu imepakana na highway na kituo cha dala dala! Mbali na hivyo pako level moja yani tambarare kiasi kwamba mtu anaweza maneuver eneo lote bila hussle!

Vile ndio ambavyo site za wamachinga zinatakiwa ziwe sio kuwajengea ghorofa kama hospitali eneo ambalo hamna hata movement. Halafu watu wa almashauri wanashikilia ground floor na kuwapangishia raia kwa bei ghali wakijua kabisa sio haki. Wateja nao hivi nani yupo tayari kupanda floor ya kumi kununua soksi ambazo zipo ground floor kwa bei ile ile ya buku! Hatujafikia ustarabu huo kama wateja mtawalaumu tu hawa jamaa bure!
 
Yani kwa hili ni kutaka tu kuumiza maisha ya watu na hali ilivyokuwa mbaya yani ndo balaa..
 
😆 serikali ndo ilikuwa inapoteza.
Sasa nani anataka kuifanyia kazi serikali mzee! Mi nilipe kodi ili wapuuzi wachache wanaolipwa posho za laki 3/3 kilasiku wakajadili kurasimisha gongo na kutuchangisha shilingi 50 kila siku kwenye simu?

Nihenyeke ili hao mbwa wawekewe mafuta ya ma VX na mishahara ya kukata na shoka for non sense?
 
Style ya jiji kuvunja vibanda saiv ni usiku wa manane...yaan wanavunja na kuzoa uchafu wote, mkiamka asubuhi mnakuta peupe ndio kilichotokea ubungo mataa. Ewe mmachinga usiache mzigo bandani au kibanda tarehe wanayokutajia utakuja kulia.
 
safi vinachafua tu mandhari ya Jiji, huwezi kuweka vibanda vya biashara bila utaratibu.

ila wapangwe sehemu maalum yenye biashara sio kama walivyo sasa ni vurugu tupu!
 
Hivi hoja za ajabu kama hizi mnazitoa wapi? Nchi ifike mahali raia wafuate sheria , Sheria ni msumeno hukata mbele na nyuma, iweje sasa raia wengine Sheria iwe butu kwao kisa machinga? Raia kama hana shughuli ya Msingi ya Uzalishaji mjini kati anafanya nini? Warudi kwenye kilimo nchi ipate uchumi kukua, hii ya kufanya uchuuzi Nchi haifaidiki chochote kwa hawa raia wachuuuzi.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Kabisa, mfano serikali inajenga barabara kurahisisha usafiri, sasa mfano ukienda mbagala, tegeta, bunju B kunakua na foleni kisa vibanda vinasababisha parking kua finyu na daladala kupaki barabarani.
Hii haikubaliki asilani. Vivunjwe vyote sheria ifatwe.
Mbona kimara mbezi magorofa yalivunjwa na mwendazake(ingawa ni visasi vya ukanda) hamshoboki midomo kutetea
 
Back
Top Bottom