Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

Mama ameshasema yeye na Mwendazake ni kitu kimoja, kwa hiyo hatolewi Mtu.
 
1620739444202.png


Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Jumanne Shauri amewataka wafanyabiashara waliojenga vibanda katikati ya Jiji la Dar es Salaam kuviondoa kabla ya Mei 18, 2021.

Wakati Shauri akieleza hayo, gari lenye spika za matangazo linapita katikati la mitaa ya Jiji hilo likitangaza kuhusu mchakato huo kwamba vibanda havitakiwi kuonekana kando ya barabara.

Akizungumza na Mwananchi Digitial leo Jumanne Mei 11, 2021 Shauri amesema hawajazuia wafanyabiashara kuendelea na shughuli zao, wanachotakiwa kufanya ni kutojenga vibanda na kuwataka wauze bidhaa zao kwenye meza ili wakimaliza iwe rahisi kuziondoa na kuacha maeneo wazi.

Amebainisha kuwa sheria ya mipango miji hairuhusu kujenga vibanda, kuwataka wafanyabiashara hao kutii agizo hilo.

“Mwisho Mei 18 kama ambavyo gari la matangazo linavyotangaza waviondoe vibanda vyao kwa sababu vingine vinajengwa hadi kwenye njia za watembea kwa miguu na barabarani na kuleta adha kwa watumiaji. Wanatakiwa watii sheria bila shuruti waviondoe wenyewe,” amesema Shauri.

MWANANCHI
 
View attachment 1780963

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Jumanne Shauri amewataka wafanyabiashara waliojenga vibanda katikati ya Jiji la Dar es Salaam kuviondoa kabla ya Mei 18, 2021.

Wakati Shauri akieleza hayo, gari lenye spika za matangazo linapita katikati la mitaa ya Jiji hilo likitangaza kuhusu mchakato huo kwamba vibanda havitakiwi kuonekana kando ya barabara.

Akizungumza na Mwananchi Digitial leo Jumanne Mei 11, 2021 Shauri amesema hawajazuia wafanyabiashara kuendelea na shughuli zao, wanachotakiwa kufanya ni kutojenga vibanda na kuwataka wauze bidhaa zao kwenye meza ili wakimaliza iwe rahisi kuziondoa na kuacha maeneo wazi.

Amebainisha kuwa sheria ya mipango miji hairuhusu kujenga vibanda, kuwataka wafanyabiashara hao kutii agizo hilo.

“Mwisho Mei 18 kama ambavyo gari la matangazo linavyotangaza waviondoe vibanda vyao kwa sababu vingine vinajengwa hadi kwenye njia za watembea kwa miguu na barabarani na kuleta adha kwa watumiaji. Wanatakiwa watii sheria bila shuruti waviondoe wenyewe,” amesema Shauri.

MWANANCHI
Kumbe ni vibanda tu na wataendelea kuwa kero!!!!
 
The solution of Tanzanian problems was temporarily halted on 17 March of this year. But real, permanent freedom is coming tomorrow.
 
Hii habari si ilishaletwa last saturday Gari la Matangazo lilipita
 
Jiji la Dsm limerudi lini tena?
Jiji ni wilaya ya Ilala na halituhusu wengine na hatuna mkurugenzi wa Jiji la dsm.
 
Nimetoka tu nje ya ofisi nikakutana na gari ya tangazo inaanza kutangaza, watu wameshika vichwa wengine wanacheka na mimi ikabidi nicheke.

Ila wametubana sana watembea kwa miguu aisee
Kariakoo barabara ya Msimbazi nafikiri wameigawana ni sisi tu hatujui...watembea kwa miguu hatuna chetu..
 
mim nilishangaa kweny nchi za wenzetu kuna flea maarket.unaweka meza ya kukunja ikifika jion unapaacha pasaf na meza yako unaondoka nayo.ajabu nimepita hapo mbele ya mahakama ya rufaa naona ubaz huu wa bahar mabanda kabisa yamejengwa nikashangaa sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwendazake akutengeneza solution ya kudumu kuhusu machinga yaani kuwapitia maeneo sahihi bali aliwatengeneza awatumie kisiasa.
 
Jambo jema kwa sababu ilikuwa ni changamoto kubwa kwa watembea kwa miguu. Muhimu ni kufata na kutii sheria za mipango miji.
 
Gari la tangazo linapita kutangaza ya kuwa ifikapo tarehe 18 mwezi huu hakitakiwi kibanda chochote kuonekana kando kando ya barabara katika jiji la Dar es Salaam...
Dar ndio wapi? Mbezi Luis inatia kinyaa mabanda mpaka mitaroni huko wameruhusiwa kujenga mabanda mitaro ya maji?

Hebu na wasafishe jiji letu
 
yaani haya mambo yanaathiri sana, kila mtu anakuja na lake, sijui tutafika lini kuwe na sera/sheria ambazo itakuwa ni vigumu kugeuzwageuzwa. Na kwakweli imekuwa ni hatari hata vyakula vinapikwa tu barabarani sijui usalama wa afya za watu ukoje?
 
Ila wenyewe wako busy kugawana ma benz na kujengeana mijumba, maskin wanaotafuta kwa jasho lao wanawafukuza kama mbwa
 
Dar ndio wapi? Mbezi Luis inatia kinyaa mabanda mpaka mitaroni huko wameruhusiwa kujenga mabanda mitaro ya maji?

Hebu na wasafishe jiji letu
Mkuu kweli Mbezi Luis imezidi mno kwa uchafuzi wa mazingira nadhani hali hii imechangiwa na uwepo wa Magufuli Bus Stand. Ile Stand ya daladala kuanzia saa 12 jioni inageuka na kuwa soko, nawahurumia sana wahudumu wa ufasi.
 
Back
Top Bottom