Vijana mnakwama wapi? Kuna kijana nilimuunganisha ajira hata asante hajanipa anataka nimtafutie ajira sehemu nyingine sasa

Vijana mnakwama wapi? Kuna kijana nilimuunganisha ajira hata asante hajanipa anataka nimtafutie ajira sehemu nyingine sasa

Hello!
Huyu dogo kama atakuwa humu atasoma bandiko hili maana si baya kivile.
Imepita mwaka sasa tangu nimuunganishe kwenye ajira (sekta binafsi) kama dereva wa malori. Kampuni kubwa tu hapa Bongo. Anapokea around 500k -800k kwa mwezi.
Sasa ile stori na wenzake anapata kujua fursa zaidi kwenye kampuni zingine.
Si unajua stori za wafanyakazi kupenda kuambiana sehemu B wako vizuri kimaslahi.
Lengo langu si kutazamia malipo kwake, nilimsaidia tu , kilichonishangaza bado anataka tena connection kutoka kwangu anashindwa kujisimamia afike huko anakowaza.
Sasa akisikia kuna sehemu wanalipa vizuri zaidi ananipigia simu kutaka nimuunganishe ajira huko.
Mtu alikuwa juu ya mawe umemfanyia mpango hajakumbuka hata ile brother Asante kilo ya sukari hii hapa unywe chai na watoto leo anataka umpigañie sehemu nyingine.
Ikumbukwe huyu dogo hatuna undugu , nilidanhanya ni mtoto wa dada yangu ili apate ajira maana ningesema mdogo wangu majina yangeumbua.
Sikuhitaji malipo, nilikuwa nikimpa kampani ndogo ndogo kabla hajaajiriwa. Hata alipoajiriwa kuna siku alikwama akaomba nimkopeshe pesa kidogo atalipa mwisho wa mwezi. Nikamtumia pesa zaidi ya aliyohitaji na nikamwambia siwezi kukukopesha nakupa tu free, si vyema tuishi maisha ya kukopana fedha. Leo kanitext nilijua anataka anishukuru arudishe kiutu uzima ile pesa niliyomtumia kumbe anataka nimpigabie ajira ofisi fulani ya umma.
Nadhani hii tabia ya kutojielewa sijui ni mazao ya origin ya mtu. Watu wa kusini shukrani kwetu ni kitendawili.
Ok . Badala ya kujipambania sasa unataka ubebwe tena.
Note: Mimi si dalali wa ajira na sihitaji pesa ya mtu . Nimezungumza tu kijana lazima uwe na akili timamu katika utafutaji wako wa maisha.
Mtafutie, kwani mpaka akwambie kuwa alikuombea baraka kwa mungu wake ili uendelee kuwa daraja la wengine?
 
😅😅😅
Nakufuata pm nimeona comment zinasema una maokoto
Nije tushinde wote kko
Ht sio marketing
We unamsikiliza Lamomy nae, sema njoo huwezi lala njaa...tupige makofi na kuimba ili wateja wanunue mitumba 🎶 haya haya elfu mbili elfu mbili🎶
 
Hello!

Huyu dogo kama atakuwa humu atasoma bandiko hili maana si baya kivile. Imepita mwaka sasa tangu nimuunganishe kwenye ajira (sekta binafsi) kama dereva wa malori. Kampuni kubwa tu hapa Bongo. Anapokea around 500k -800k kwa mwezi.

Sasa ile stori na wenzake anapata kujua fursa zaidi kwenye kampuni zingine. Si unajua stori za wafanyakazi kupenda kuambiana sehemu B wako vizuri kimaslahi.

Lengo langu si kutazamia malipo kwake, nilimsaidia tu, kilichonishangaza bado anataka tena connection kutoka kwangu anashindwa kujisimamia afike huko anakowaza.

Sasa akisikia kuna sehemu wanalipa vizuri zaidi ananipigia simu kutaka nimuunganishe ajira huko. Mtu alikuwa juu ya mawe umemfanyia mpango hajakumbuka hata ile brother Asante kilo ya sukari hii hapa unywe chai na watoto leo anataka umpigañie sehemu nyingine.

Ikumbukwe huyu dogo hatuna undugu , nilidanhanya ni mtoto wa dada yangu ili apate ajira maana ningesema mdogo wangu majina yangeumbua.

Sikuhitaji malipo, nilikuwa nikimpa kampani ndogo ndogo kabla hajaajiriwa. Hata alipoajiriwa kuna siku alikwama akaomba nimkopeshe pesa kidogo atalipa mwisho wa mwezi.

Nikamtumia pesa zaidi ya aliyohitaji na nikamwambia siwezi kukukopesha nakupa tu free, si vyema tuishi maisha ya kukopana fedha. Leo kanitext nilijua anataka anishukuru arudishe kiutu uzima ile pesa niliyomtumia kumbe anataka nimpigabie ajira ofisi fulani ya umma.

Nadhani hii tabia ya kutojielewa sijui ni mazao ya origin ya mtu. Watu wa kusini shukrani kwetu ni kitendawili. Ok . Badala ya kujipambania sasa unataka ubebwe tena.

Note: Mimi si dalali wa ajira na sihitaji pesa ya mtu . Nimezungumza tu kijana lazima uwe na akili timamu katika utafutaji wako wa maisha.
Huyo dogo kiazi sana. Hajui kuishi na watu na hatoenda zaidi ya hapo
 
Leo kanitext nilijua anataka anishukuru arudishe kiutu uzima ile pesa niliyomtumia kumbe anataka nimpigabie ajira ofisi fulani ya umma.
Dogo amekupa Cheo kikubwa sana wewe anakuona km godfather, sasa haya unayoyasema hapa inabidi umweke chini umweleze akipata Pesa anunue hata Sukari au kilo ya nyama akuletee akishindwa basi hata fungu za nyanya na vitunguu au viazi mviringo au Samaki wabichi akuletee
 
Asante ni neno kubwa sana.

Kuna wakati unasaidiwa pakubwa hadi unapagawa ni kwa namna gani unaweza kushukuru.

Ukipiga hesabu za manufaa uliyoyapata unashindwa utoe kiasi gani kumshukuru aliyekusaidia.

Inawezekana kijana yupo katika hali hiyo ila kumbe wewe upo mtandaoni kumlaumu.
 
Back
Top Bottom