Vijana ndoa muhimu, Gerald Hando amezeeka ghafla

Jambo umelieleza lina uhalisia hili.

Kakangu alikuwa mzima, mama yetu anaumwa kaparalaiz miguu, hatembei.

Kaka akawa anapigia mahesabu mirathi ya mali na mashamba ya mgonjwa.

Kaja kuugua gonjwa la ajabu kwa muda mfupi na kuaga dunia na kumwacha mgonjwa bado yuko hai na mali zake.

Miaka ilipita ndo mama akaja kufariki.

Usije ukamuwazia mwenzako kifo na wewe kujiweka kando kama vile hakikuhusu!

Utakuja kung'ata shuka huku ukiwaacha ambao ulidhani watatangulia wakiendelea kudunda.
 
Hivi kwa nini binadamu huwa tunasahau hili?yaani mimi hata nione kakonda kabaki moja huwa simtabirii kifo haya mambo yanasiri kubwa mgonjwa kuwa hai mzima kufariki
 
Tena siku hizi vijana wanakufa sana kuliko na hao wazee, mwaka jana tulikuwa na kamgogoro ka nyumba na bamkubwa bhana, sasa dogo anaenifata akawa anaongea mbovu sana, kuwa mtu mwnyewe kazeeka hana muda mrefu ataondoka nikamwambia hata km anatunyanyasa vipi huwezi kusema hivyo kifo kinakuja bila hodi, usishangae ukamuacha we ukatangulia, akasema aaah we sis nitolee busara zako huyu atatuacha na huo wakati ukifika tutaonyeshana!!!!! Ooohhhh mwaka huu mwanzoni kapiga chini kalala aliyekuwa anamkandia alikuwepo msibani mpaka sasa yupo,, hicho ndio kifo
 
Nina mjomba wangu anatumia ARV huu mwaka wa 20+wazima waliokuwa wanamnanga tumeshawazika yeye anakula tu maisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…