Viongozi wangu wa CCM inatosha sasa, TEC hawatatuelewa hadi tueleweke!

Viongozi wangu wa CCM inatosha sasa, TEC hawatatuelewa hadi tueleweke!

😂 😂 😂 😂
Sema yote lakini usipingane na ukweli aliouandika VUTA-NKUVUTE. Inaweza isiwe kwa uwazi unaoutaka wewe, lakini uhalisia ndo upo hivyo. Hiv unajuwa matamko mangapi yametoka kuhusu suala la bandari na DPW? La TEC ndo limeonekana kushika hatamu..!! Yaani kila mtu aliibuka toka alikuwa..!! Hiyo pekee inatosha kukuambia kuwa TEC wapo very powerful.
Inaonekana huyo kijana hamfahamu Mzee Tupa Tupa
 
Wewe ndo muakilishi wa hao TEC au unesemea hisia zako? Kuna mtu ambaye anaweza kugomea CCm hapa Tz kweli, wewe utakua hujui siasa za CCM, TEC inahitaji sana CCM kiliko CCM inavo hitaji TEC, au umesahau pesa za kifisad za Escrow zilipitia Mkombozi benk ambayo ni Benki ya kanisa na Kanisa elipokea fungu, wataka uchunguzi wa hiyo kesi ufufuliwe uone kama mkombozi bank itakuepo tena............acha kushezea state hususani ukiwa Africa.
Umazungumza utumbo

Benki ya Mkombozi inafanya kazi za kibenki kwa,mujibu wa sheria na inasimamiwa na Benki kuu . Benki hiyo haikufanya kosa lolote kupokea, pesa zilizowekwa na mteja wake na ilichukua hatua zote ikiwemo kuitaarifu TRA.

Mkombozi haiwezi kufutwa hata zje nani mradi sheria zinafuatwa. Kanisa kwanza halikupokea fungu kama unavyolopoka. Pili yule askofu alipewa pesa na muumini kama matoleo na si kazi ya anayepewa pesa kuhoji uhalali wa pesa inayotolewa sadaka . Wewe hapo unapotoa sadaka huwa unatoa maelezo ya hizo hela umepata wapi.

Tena huyo aliyetoa pesa ni zake kwa sababu aliuza hisa zake kihalali na alikuwa anatambulika Brella kuwa anamiliki hisa hizo na hakuna mahakama yeyote inayoweza ku.mtia hatiani.

Fanya analysis kidogo kabla hujakurupuka kuposti.
 
Mi naona mnaongea sana.Muhimu ni hili TEC inaundwa na watanzania,TEC ni mdau muhimu wa marndeleo ya nchi hivyo viongozi kuwa karibu na TEC sio kujikomba Bali ni kuwa karibu na mdau,TEC kuwa karibu na serikali au viongozi ndio wajibu wake kwa ndio wachunga kondoo.Huwezi mwacha kondoo wako ajichunge.Hivyo linapoinuka jambo na kutofautiana maono haimanishi kanisa linajitenga au kushawishi watu waichukie serikali ni wajibu wake kuwatia moyo viongozi na kuwakemea kwa kuwa wakati huo husema kwa niaba ya waamini na wasio waamini.
 
Lazima niseme. Nguvu kubwa inafanywa na viongozi wetu wa CCM Taifa ambao pia ni viongozi serikalini kupata 'uungwaji mkono' na Maaskofu wa Kanisa Katoliki. Ni maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Kuanzia Mwenyekiti/Rais hadi viongozi wengine waandamizi wamekuwa 'busy' na kutafuta kukubalika na wakatoliki.

Pamoja na ukweli kuwa ili ushindi upatikane na utulivu wa kiuongozi utamalaki lazima ukubalike na TEC, sasa imekuwa 'too much'. Makada wabobezi na waandamizi (hasa tulio wakatoliki) tunatumwa bila kusemwa kwa Kardinali, Maaskofu, Mapadre na wengineo ili kusaka kukubalika kwa viongozi wetu.

Amini nawaambia viongozi wangu wa kichama na kiserikali, TEC hawatashawishika kirahisi.

Hawatasahaulishwa msimamo na Tamko lao juu ya mkataba tata wa DP World. Hawatalaghaiwa kwa ahadi za kifedha; kupokelewa uwanjani au kupewa kanzu. TEC bado wanalo la bandari na wamejipanga kuusimamia msimamo wao.

Ili CCM tujisafishe mbele ya TEC, Tamko lao liheshimiwe. Kupigana vikumbo kujisogeza kwao hakutasaidia chochote. TEC imesheheni waelewa wa mambo zaidi ya wanasiasa wa zamani na wa sasa. Si wepesi kuyumbishwa kwa ahadi zisizo na kadi; michngo ya michongo na zawadi maridadi.

CCM tumeshaanza kampeni, wenzetu vipi?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
TEC haiwezi kutaka CCM ishindwe uchaguzi hata mara moja !!
 
Umazungumza utumbo

Benki ya Mkombozi inafanya kazi za kibenki kwa,mujibu wa sheria na inasimamiwa na Benki kuu . Benki hiyo haikufanya kosa lolote kupokea, pesa zilizowekwa na mteja wake na ilichukua hatua zote ikiwemo kuitaarifu TRA.

Mkombozi haiwezi kufutwa hata zje nani mradi sheria zinafuatwa. Kanisa kwanza halikupokea fungu kama unavyolopoka. Pili yule askofu alipewa pesa na muumini kama matoleo na si kazi ya anayepewa pesa kuhoji uhalali wa pesa inayotolewa sadaka . Wewe hapo unapotoa sadaka huwa unatoa maelezo ya hizo hela umepata wapi.

Tena huyo aliyetoa pesa ni zake kwa sababu aliuza hisa zake kihalali na alikuwa anatambulika Brella kuwa anamiliki hisa hizo na hakuna mahakama yeyote inayoweza ku.mtia hatiani.

Fanya analysis kidogo kabla hujakurupuka kuposti.
Benki ilitumika kutakatisha pesa za wizi hilo hawawezi kulikuepa hamna sadaka ya 100m huo ni wizi, nyie chokozeni serikali na TEC yenu isio kua na mchango wote katika uchumi wetu, mtaliona la mtema kuni......
 
Mmmh
Wewe ndo muakilishi wa hao TEC au unesemea hisia zako? Kuna mtu ambaye anaweza kugomea CCm hapa Tz kweli, wewe utakua hujui siasa za CCM, TEC inahitaji sana CCM kiliko CCM inavo hitaji TEC, au umesahau pesa za kifisad za Escrow zilipitia Mkombozi benk ambayo ni Benki ya kanisa na Kanisa elipokea fungu, wataka uchunguzi wa hiyo kesi ufufuliwe uone kama mkombozi bank itakuepo tena............acha kushezea state hususani ukiwa Africa.
Mmmh... nadhan huna Nia njema na baadhi ya watu Mashuhuri...Mkombozi haiwezi kufungwa..na ikifungwa hiyo ndio watajua hawajui... Serikali ni watu na watu wenyewe sasa
 
🤣🤣🤣
Limebarikiwa au ndo ivoivo tu.....?

Nitajuaje ,kwani nimelitoa Mimi?
Hata yusuph walimpelekea mzee wake yakobo kanzu yake iliyokuwa na damu ,akapapasa akasema ni kanzu ya mwanangu yusuph,hapo mzee yakobo alikuwa mzee kwa upofu,akamlilia mwanae yusuph mwaka mzima ,akaomboleza🤣Kumbe mwanae yusuph alikuwa kauzwa na ndugu zake kwa wafanyabiashara wamidiani,walioenda kumwuza yusuph utumwani Misri,ambapo baadae yusuph alikuja kuwa waziri mkuu wa Misri 🙏
 
Wewe ndo muakilishi wa hao TEC au unesemea hisia zako? Kuna mtu ambaye anaweza kugomea CCm hapa Tz kweli, wewe utakua hujui siasa za CCM, TEC inahitaji sana CCM kiliko CCM inavo hitaji TEC, au umesahau pesa za kifisad za Escrow zilipitia Mkombozi benk ambayo ni Benki ya kanisa na Kanisa elipokea fungu, wataka uchunguzi wa hiyo kesi ufufuliwe uone kama mkombozi bank itakuepo tena............acha kushezea state hususani ukiwa Africa.
Kweli wewe akili yako haijui kupambanua mambo! Ngoja nikusaidie........
Kwanza ujue walio mshauri Samia kwenda Kwa Maaskofu ndio hao hao state....
Pili, Bank ya mkombozi katika Saka like ilitumika kama kakapu kinavyo tumika kubeba matunda sokoni. Fedha zile ni za mtu mwenye akaunti halali pale na akataka fedha zake zipitie kwenye akaunti Ile. Lakini pia lazima ujue Bank kuu walijulushwa kabla muamala ule haijatoka!!
 
Hata Mimi naunga mkono,kwani lazima Kila kitu hao TEC waunge mkono? Ni upuuzi kutokubalia kukubaliana na itakuwa Haina maana Sasa ya kuwa na Taifa.

Maendeleo huletwa katikati ya mgongano wa fikra,TEC na RC hawaendeshi hii Nchi ni mambo ya kipuuzi kuwaza hivyo na inajenga mbegu ya chuki kw watu wa madhehebu na dini zingine.

Inakera sana.
Mkuu mpaka ww umemind , ujue kwenye DP World kuna kitu hakiko sawa,
 
Viongozi kuwa na madhehebu Yao ni sawa ila msimamo wa madhehebu Yao haupaswi kuwa msimamo wa Nchi.

Ukiwa na madaraka kwenye Nchi hipaswi kuleta mambo ya madhehebu yenu.

Upuuzi wa hivi ukome maana unaweza kuja kuleta shida baadae
Mazeli anatafuta ungwaji mkono Kwa nguvu Sana,
 
Hata Mimi naunga mkono,kwani lazima Kila kitu hao TEC waunge mkono? Ni upuuzi kutokubalia kukubaliana na itakuwa Haina maana Sasa ya kuwa na Taifa.

Maendeleo huletwa katikati ya mgongano wa fikra,TEC na RC hawaendeshi hii Nchi ni mambo ya kipuuzi kuwaza hivyo na inajenga mbegu ya chuki kw watu wa madhehebu na dini zingine.

Inakera sana.
Umeandika chuki zako kwa Wakatoliki, unataka chuki iwe hoja, usipoukubali ukweli haiwezi kushughulikia changamoto
 
Lazima niseme. Nguvu kubwa inafanywa na viongozi wetu wa CCM Taifa ambao pia ni viongozi serikalini kupata 'uungwaji mkono' na Maaskofu wa Kanisa Katoliki. Ni maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Kuanzia Mwenyekiti/Rais hadi viongozi wengine waandamizi wamekuwa 'busy' na kutafuta kukubalika na wakatoliki.

Pamoja na ukweli kuwa ili ushindi upatikane na utulivu wa kiuongozi utamalaki lazima ukubalike na TEC, sasa imekuwa 'too much'. Makada wabobezi na waandamizi (hasa tulio wakatoliki) tunatumwa bila kusemwa kwa Kardinali, Maaskofu, Mapadre na wengineo ili kusaka kukubalika kwa viongozi wetu.

Amini nawaambia viongozi wangu wa kichama na kiserikali, TEC hawatashawishika kirahisi.

Hawatasahaulishwa msimamo na Tamko lao juu ya mkataba tata wa DP World. Hawatalaghaiwa kwa ahadi za kifedha; kupokelewa uwanjani au kupewa kanzu. TEC bado wanalo la bandari na wamejipanga kuusimamia msimamo wao.

Ili CCM tujisafishe mbele ya TEC, Tamko lao liheshimiwe. Kupigana vikumbo kujisogeza kwao hakutasaidia chochote. TEC imesheheni waelewa wa mambo zaidi ya wanasiasa wa zamani na wa sasa. Si wepesi kuyumbishwa kwa ahadi zisizo na kadi; michngo ya michongo na zawadi maridadi.

CCM tumeshaanza kampeni, wenzetu vipi?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Na isiwe na hao TEC pekee, CCM hii na viongozi wake wanatakiwa kukataliwa na kila mTanzania mwenye mapenzi mema na nchi hii.

Uongozi huu na serikali zake ni kundi linaloendeshwa na genge hatari sana. Hawa wakipewa awamu yao ya uongozi wataitumbukiza nchi nzima katika majanga yasiyoelezeka.

Mifano ipo wazi, hata wakijitahidi kuifunika na kusahaulisha watu.
Kule kushika madaraka tu toka kwa mtu waliyekuwa wasaidizi kwake, huku wakiwa wamejivika joho la kondoo waonekane wapo pamoja na kiongozi huyo, kule kushika tu madaraka, wakaanza kukana kila kitu kilichofanywa na uongozi ule ule waliokuwa sehemu yake. Sasa mara hii wanataka tena kujivisha joho la kondoo watu wasahau maovu yote yaliyokwishafanyika chini ya uongozi wao? Ufisadi umekuwa ni kama jadi kwao. Hawana wanalojua kuhusu mwelekeo wa nchi inakokwenda. Wanadhani watu wenye akili hawaoni haya maovu yote yaliyofanyika kwa muda mfupi sana chini ya utawala wao?

Hawaoni hata aibu, kwenda kwa watu hao hao TEC, waliokataa kunajisiwa kwa nchi hii; wao wanadhani hilo lililkuwa jambo dogo?
Wamejitokeza mbele na kueleza hiyo DP World na IGA yake kwa nini ilikuwa vile. Wameomba msamaha kwa makosa (?) waliyotaka kulifanyia taifa hili?

Wanataka sasa waungwe mkono na hao hao TEC waliowatapisha hujuma waliyopanga kuifanyia nchi hii ili iweje? Kwamba wakishasimikwa madarakani waendelee na mipango yao miovu?

Hawa watu washukuru tu kwamba nchi hii ni ya watu watulivu sana, vinginevyo matendo yao yangekuwa yametosha kabisa kuwatupilia mbali, na baadhi yao kuwekwa magerezani.
 
Wewe ndo muakilishi wa hao TEC au unesemea hisia zako? Kuna mtu ambaye anaweza kugomea CCm hapa Tz kweli, wewe utakua hujui siasa za CCM, TEC inahitaji sana CCM kiliko CCM inavo hitaji TEC, au umesahau pesa za kifisad za Escrow zilipitia Mkombozi benk ambayo ni Benki ya kanisa na Kanisa elipokea fungu, wataka uchunguzi wa hiyo kesi ufufuliwe uone kama mkombozi bank itakuepo tena............acha kushezea state hususani ukiwa Africa.
Tuliza povu mzee!
 
Back
Top Bottom