Visa vya Uchawi na Ushirikina Mkoani Kigoma Mwisho wa Reli

Visa vya Uchawi na Ushirikina Mkoani Kigoma Mwisho wa Reli

2 Wafalme 17:17
"Wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, wakapiga ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa BWANA, hata kumkasirisha."

Uchawi upo, Ramli ipo.. Ninafahamu upo na ni kazi yangu kwa IMANI yangu kupambana nao kila iitwapo leo.

Isaya 47:12
"Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda."

Huko kwa waganga ndiko ulikojaa uchawi, Lakini Tumaini letu ni kwa Bwana, Kristo Yesu Mfufuka.

Binafsi, nimekwisha kutuna na visa kadhaa vya kichawi na ndio maana nikasema mbona visa vyake si vya kusisimua.. nimekishwa pambana na visa vingi vya kichawi juu yangu na juu ya watu wa Mungu, Lakini katika yote Wachawi ni watu wasio na uwezo wowote mbele ya waamino halisi.. mchawi hana nguvu mbele ya Damu na Jina Takatifu lipitalo Majina yote la YESU KRISTO WA NAZARETH.

Je, unataka kufahamishwa nini kuhusu wachawi?
Safi sana mtumishi
 
Kigoma Visa vya Uchawi na Ushirikina.

Kigoma ni moja ya Mikoa ambayo inasifika kwa Uchawi nchini Tanzania. Huu mkoa kiasili una watu wachapa kazi sana. Si wazembe ukilinganisha na mikoa mingine yenye ushirikina kama Tanga,Pwani au Zanzibar.

Kigoma maeneo ambayo yanasifika sana kwa Uchawi ni Mwandiga, Ujiji,Mwamgongo n.k

Hapo Mwamgongo ni hatari sana karibu na Mbuga ya Gombe. Kunasifika na moja ya visa vya uchawi ni kimoja ambacho kilitokea mwaka 2020 ni kifo cha Diwani mmoja ambaye inasemekana alichukua Mke wa mtu.

Huyu Diwani ambaye allhamdulilah alikuwa na vijicent ilitokea akawa anatembea na mke wa raia mmoja kijijini hapo.

Yule bwana Raia alipata taarifa. Akanyamaza. Diwani akafikia hatua akaona aoe kabisa mke wa jamaa. Na mke akadai talaka ili akaolewe na Diwani.

Jamaa alimfuata Diwani na kumwambia kwa upole tu kuwa "Mheshimiwa najua unatembea na mke wangu, tafadhali usimwoe maana mimi ntapata shida kulea watoto hawa 6 nlio nao na nina mke mwingine. Uwe na uhusiano naye lakini usimuoe"

Diwani alijibu kwa jeuri tu kuwa "mkeo ndiye anayenilazimisha mzuie yeye siyo mimi"

Jamaa akamenda mpaka kwa viongozi wengine wa kijijini pale akitaka wakamsihi Diwani asimwoe mkewe. Diwani akakaza.

Mpaka jamaa akaenda kwa Rafiki mkubwa wa Diwani kumwomba amsihi rafiki yake asimwoe mkewe yeye atapata shida na watoto. Diwani akamtolea nje jamaa.

Basi jamaa akanyamaza. Siku moja Diwani akakutana na Jamaa Mitaa flani kuna Soko. Diwani akaanza mshambulia jamaa kwa maneno kuwa "nasikia unataka niroga..

Huniwezi,mimi mpaka kufika kuwa Diwani nmetoka mbali sana..." Akaendelea mbele na kumwambia haya nakupa mate na nyayo hii chukua." Akatema mate. Jamaa alimwambia tu Diwani "huo uchawi wa kuchukua mate na nyayo ni mdogo sana,wa watu ambao ni underdog/amateur"

Akaondoka zake. Baada ya siku chache tu Diwani akaanza kuumwa sukari ikapanda mara akaanguka ndo basi tena. Akafa.

Akazikwa. Baada ya siku chache wanafamilia yake wakawa wanamwona Diwani anakuja anagonga pale kwao kuwa afunguliwe mlango anateswa sana.

Diwani alikuwa amevaa pensi chafu.anagonga dirishani akisema anachapwa sana viboko. Afunguliwe.

Mke na watoto wakawa nao wanajawa woga.

Hili tukio lilitokea Mkoani Kigoma mwisho wa Reli.

Na watu wa Kigoma tofauti na Mikoa ya Pwani. Pwani mchawi wako mnaweza mkawa mnacheka naye na kula naye huku anakuroga.

Kigoma ukikorofishana na mtu anakwambia kabisa bila kuuma uma maneno "nitakuroga" hata hatumii sauti ya vitisho. Anakuambia kwa upole tu akikuahidi kuwa kweli atakuroga mbele za watu wengine.na anaenda kukuroga kweli.

Hiki ni moja ya kisa cha mambo ya Uchawi Kigoma.nitaleta Visa vingine vya Uchawi na Ushirikina Kigoma.

Kisa Cha Pili.
Kuna jamaa mmoja alikuwa ana tatizo dogo tu na jirani yake shambani. Akawa anasema migomba flani ni ya kwake.yule mzee akamwambia hapana hili shina la Mgomba lipo shambani kwangu. Jamaa mbabe akasema ni lake na atakata.

Kweli ule mgomba mmoja ukazaa. Siku hiyo jamaa akaenda shambani akachonga chonga majani ili akate ndizi. Kunyanyua panga. Mkono ulipigwa ganzi haukushuka. Ukabaki juu na panga.

Akapiga kelele sana maana mkono ukawa kama unanyongwa hivi.watu wakamchukua kumpeleka kwake. Mkono ulipooza.

Mtoa mada upige na kwetu ukelewe
 
Kwa sifa hizi za Ujiji huwezi amini ndio mahali Livingston na Henry Stanley walikutana.
Kwanini hawakulogwa?
 
Uzi mzuri lakini umejaa mahubiri na ubishi ubishi.
Ufunuo wa Yohana 21:8
"Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili."

Kinyume cha wasiopenda mahubiri ni wasioamini.. maana mahubiri ni kwa waaminio.

Mahubiri ni sehemu ya ulimwengu wa Nuru, yaani kinyume cha ulimwengu wa giza (uchawi ukiwemo), hivyo Usishangae wala usipate shida ukisikia Mahubiri katikati ya mada za kichawi, Nguvu ya Bwana iko hapa KUTAFUTA WALIO WAKE, WASIPOTEE.

Unapenda uchawi kiasi cha kuchukia mahubiri/Neno La Mungu?
 
Kuna yule alikuwa Mkuu wa Mkoa toka Sumbawanga ambaye amefariki miezi michache iliyopita,alipimana ubavu kichawi na wazee wa Ujiji ngoma ikawa droo wakaanza kuheshimiana
Nadhani ni marehemu Mzindakaya! Kama sikosei huyu alishindikana Kigoma.
 
Kuna siku nilikiwa kibondo pale wilaya ya kgm sasa kuna guest nifikia (jina lina anza na miku...) sasa umefika ucku mda wa kulala nikavyua ngua zangu nikazitupa chini tu, asubu kuamka nikakuta nguo zimeloanishwa maji yani ukizikamua zinatoa maji na hakuna mvua iliyonyesha wala maji waliyoingia ndan chumba kizima likuwa kikavu na chumba kilikukuwa sio self labda kusema maji yametoka chooni kuingia ndani na chumba nilifunga na funguo kwa ndani!

Sitisahau lile tukio
Ulizokojolea
 
Wakuu uchawi upo, mimi pia nilikuwa siamini hii kitu lakini niliwahi shuhudia kwa macho ndugu yangu aliyekiwa akiuguzwa home tena kwenye chumba changu baada ya hospital kushindwa. Huyo ndugu yangu alifariki lakini akawa anakoroma kupitia mdomo. Doctor alikuja kumpima akasema kaisha kufa, lakini anapumua kwa kukoroma kupitia mdomoni.

Kuna jirani yetu alileta dawa akawa anamnywesha lakini kila alipoweka ile dawa mdomoni, hakuimeza maana alikuwa akikoroma inarudi yote. Wengine wakashauri paa la nyumba liezuliwe ili mionzi ya jua imchome eti angetulia kitu ambacho wazee waligoma kuepusha gharama. mwisho ndugu akatulia japo alichukua masaa.

Anayesema uchawi haupo ni kiazi
 
Ukishikwa chuchu husisimki hata kidogo?😳😳😳😳😳😳 Kwa nini.

Ndugu ulikusudia kuni-quote mimi?

Ukija kimwili nakulipua kimwili ukija kiroho nakumaliza kiroho na ukija kifedhuli Mungu amenipa kibali cha kukupasua kifedhuli.

Katika yote, nakukumbusha tubu dhambi zako na Mungu ATAKUSAMEHE.
 
Kwa sifa hizi za Ujiji huwezi amini ndio mahali Livingston na Henry Stanley walikutana.
Kwanini hawakulogwa?

Ndo hapo sasa. Hawa ndio walioamini ukisema maji risasi haikupati kipindi cha majimaji war.
 
Mtu anaoaje mke wa watoto 6 huko si kuvunja familia aisee, useless diwani adhabu aliyopata alistahili

Yeyote atayenipa jina la huyo Diwani nampa 500k taslim TSH. Jina tu ili nithibitishe uhalali wa hii habari.

NB: Diwani ni ofisi ya umma na jina lake ni public record.
 
Uchawi upo na hakika Upo. Nimewahi pata ladha ya hii kitu usiombe. Ila hii Dunia ina mambo.

Usiku mmelala unasikia watu wanaongea na kucheka ndanii ukiangalia huoni watu. Watu wanatembea ndani au harufu ya ugali kupikwa ndani. Acha tu Haya mambo.

Miaka ya 90s nikiwa mdogo huko kijijini kwetu kuna bibi alikua anasifika kwa uchawi balaa na alikua anaishi peke yake tu. Siku moja nimetumwa jioni jioni nikakutana nae huko vijijini unakuta barabara nyingi pembezoni zimepandwa maminyaa alafu kuna kua na gizagiza afu barabara zina vichakavichaka basi nikakutana nae yule mzee anatembelea fimbo yuko pekee na nywele zake nyeupe peee, aseee ukimtazama tu kwa macho unakubali huyu ni jabali. Sema Ardhi imemeza vingi.

Ulitaka asitoke nyumbani kwake ungempelekea wewe mahitaji yake?

Hujui features za binadamu zinabadilika kadri umri unavyoenda? Hata mvi nazo unasema ni uchawi, basi Mzee Lowassa na mvi zake atakua kiongozi wa washirikina. Hata wewe utakua kama huyo mzee kama ukibahatika kufikia uzee.

Nyie ndo mnaoua wazee kwa kisingizio ni washirikina I pray muandamwe hivyo hivyo mkifikia umri huo. Empty set kabisa nyie midanganyika.
 
2 Wafalme 17:17
"Wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, wakapiga ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa BWANA, hata kumkasirisha."

Uchawi upo, Ramli ipo.. Ninafahamu upo na ni kazi yangu kwa IMANI yangu kupambana nao kila iitwapo leo.

Isaya 47:12
"Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda."

Huko kwa waganga ndiko ulikojaa uchawi, Lakini Tumaini letu ni kwa Bwana, Kristo Yesu Mfufuka.

Binafsi, nimekwisha kutuna na visa kadhaa vya kichawi na ndio maana nikasema mbona visa vyake si vya kusisimua.. nimekishwa pambana na visa vingi vya kichawi juu yangu na juu ya watu wa Mungu, Lakini katika yote Wachawi ni watu wasio na uwezo wowote mbele ya waamino halisi.. mchawi hana nguvu mbele ya Damu na Jina Takatifu lipitalo Majina yote la YESU KRISTO WA NAZARETH.

Je, unataka kufahamishwa nini kuhusu wachawi?
Mkuu umejibu vizuri sana si kama baadhi ya watu wachache ambao hujifanya kumjua Yesu na hapohapo wakidai hakuna uchawi
 
Mkuu I will gladly do so. Huyu muuza hii chai atoe jina tu.

Ilibidi aambatanishe jina la Mh Diwani kwenye uzi bila sisi kuulizia ila sasa anaficha tena kwa malipo kama sio chai ni nini?

Namshangaa zaidi anayeamini hii chai kuliko mtunga chai mwenyewe Chizi Maarifa
Bufa ishu ni simple CHUKUA iyo laki 5 Yako......Nenda kigoma field then uje utupe mrejesho......

Musa alitupa fimbo yake ikawa nyoka kwa uwezo wa MUNGU,
Hata farao aliwaita wachawi na washirikina na wao walipo tupa fimbo Zao zikawa nyoka..... Nyoka wa musa aka meza nyoka wengine wote....

This is one among evidences to prove uchawi
 
Back
Top Bottom