Vita ya kisiasa baina ya Tanganyika na Zanzibar ipo wazi sasa

Vita ya kisiasa baina ya Tanganyika na Zanzibar ipo wazi sasa

Mods kufuta post kunahusiana vipi na kutawala/kutwaa huko unaposema?
Kwamba wewe kuweka post ni kikwazo kwa wanaotaka kufanya hivyo?
Hapa ni akili kubwa aisee imetumika
Nadhani ipo above your capacity, yaani leo ndio nimeamini muungano unalindwa kwa nguvu zote
Vinginevyo hakukuwa na sababu ya kuufuta ule uzi
 
Hapo patamu Rais wa Zanzibar ni Mzanzibar,Rais wa Tanganyika ni Mzanzibar !.

Nchi mbili zote zinaongozwa na Raia kutoka nchi moja ya Zanzibar.Tanganyika hakuna watu wa kuongoza Tanganyika.

Hapa tatizo ni katiba mbovu ambayo imeizika Tanganyika.
Sio kweli, mwinyi ni mtanganyika.

Halafu pia wakati wa nyerer na Mwinyi baba akiwa Zanzibar huoni kama watanganyika wawili walitawala pamoja?
 
Hapa ni akili kubwa aisee imetumika
Nadhani ipo above your capacity, yaani leo ndio nimeamini muungano unalindwa kwa nguvu zote
Vinginevyo hakukuwa na sababu ya kuufuta ule uzi
Unajua nilichouliza kinalenga kujua mods wanahusika vipi na kutwaa Hilo eneo unalosema?
Na post yako Ina uzito gani hao unaosema kushindwa kufanya kile wamedhamiria?
 
Sio kweli, mwinyi ni mtanganyika.

Halafu pia wakati wa nyerer na Mwinyi baba akiwa Zanzibar huoni kama watanganyika wawili walitawala pamoja?
Ukifuatilia kwa kina utagundua kuwa asilimia kubwa ya waZanzibari weusi asili yao ni Tanganyika, hivyo karibu marais wote wa Zanzibar wanaasili ya Tanganyika. Kwa hoja hiyo, itachukua miongo kupata rais asiekuwa na asili ya Tanganyika.
 
Kuna mambo mtu ukisoma huku unabaki na maswali
Kwa jinsi ulivyojibu unakibaliana na alichosema kwamba Zanzibar Ina jeshi lake? Ina benki kuu yake? Na Ina passport yake?
Zanzibar ina majeshi yake ambayo kwa lugha za medani tunayaita jeshi usu sawa na jeshi la Polisi,Jeshi la uhifadhi,Jeshi la uhamiaji.........

Majeshi mengine yote ni jeshi usu.Jeshi kamili ni Jeshi la wananchi.

Hakuna mahali nimesema Zanzibar wana Benk Kuu.

Zanzibar ni nchi kama ilivyo Rwanda au Burundi yapo baadhi ya mambo ni ya muungano ikiwemo passport.
 
Zanzibar ina majeshi yake ambayo kwa lugha za medani tunayaita jeshi usu sawa na jeshi la Polisi,Jeshi la uhifadhi,Jeshi la uhamiaji.........

Majeshi mengine yote ni jeshi usu.Jeshi kamili ni Jeshi la wananchi.

Hakuna mahali nimesema Zanzibar wana Benk Kuu.

Zanzibar ni nchi kama ilivyo Rwanda au Burundi yapo baadhi ya mambo ni ya muungano ikiwemo passport.
Hapo kwenye jeshi umezunguka sana, zanzibar haina jeshi.
Unaposema nchi Ina jeshi lake, hii ni lugha rahisi tu kueleweka. Hata Tunaposema Tanzania ina jeshi basi maana yake ni JWTZ. Wala hatumaanishi uhamiaji, au Askari wa tanapa.

Kuhusu benki kuu na passport nilikuuliza sababu ya ulichojibu maana ulipaswa ushange huyo dada hapo anawezaje kusema Zanzibar Ina benki kuu na Ina passport yake. Hii kwa mtu yoyote timamu lazima angeshangaa sana
 
Hapo kwenye jeshi umezunguka sana, zanzibar haina jeshi.
Unaposema nchi Ina jeshi lake, hii ni lugha rahisi tu kueleweka. Hata Tunaposema Tanzania ina jeshi basi maana yake ni JWTZ. Wala hatumaanishi uhamiaji, au Askari wa tanapa.

Kuhusu benki kuu na passport nilikuuliza sababu ya ulichojibu maana ulipaswa ushange huyo dada hapo anawezaje kusema Zanzibar Ina benki kuu na Ina passport yake. Hii kwa mtu yoyote timamu lazima angeshangaa sana
KMKM ni wacheza mdumange ?.
 
Heshima sana wanajamvi,

Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar ambao uliasisiwa na watu wawili ambao sasa hawapo, tena bila ridhaa ya wananchi wa pande zote mbili sasa unapitia katika msuko suko mkubwa.

Ni wazi Mwl Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume waliziunganisha zao Tanganyika na Zanzibar pasipo ridhaa za wananchi wa pande zote mbili.

Muungano wao (Nyerere & Karume) kwa hakika umejaa kasoro nyingi mno, kuubadili au kuufanyia marekebisho kutahitaji kuzifumua katiba za nchi zote mbili jambo ambalo kwa sasa ni vigumu sana.

Zanzibar wana serekali yao, wana bunge lao, wana wimbo wao wa taifa lao, wana bendera yao, wana uraia wao (Uzanzibari), wana mkuu wao wa nchi, wana ardhi yao (nchi) wana kila kitu chao.

Tanganyika hawana wimbo wa taifa, hawana mkuu wao wa nchi, hawana ardhi yao, hawana bendera yao, kifupi Tanganyika hawana chochote.

Kuna Taifa la Tanzania (JMT) ambalo limepora kila kitu cha nchi ya Tanganyika. Bendera? Wimbo wa taifa, Bunge.

Tanganyika haina mtetezi wa rasilimali zake eg misitu, ardhi, bandari.

Raia wa nchi ya Zanzibar anaiongoza Tanganyika kupitia mgongo wa Muungano anauza kila rasilimali ya Tanganyika bila huruma kwakuwa hazina mtetezi.

Watanganyika wameamka sasa lugha ya Mch. Mtikila na sasa Mheshimiwa Lissu imeanza kueleweka hadi ndani ya CCM. Ugomvi mkubwa wa Kinana, Makamba na wanaCCM wengi ni Tanganyika kutawaliwa na Rais kutokea nchi ya Zanzibar ambaye amekuwa dalali mkubwa wa kuuza rasilimali za Tanganyika.

Wanaoitaka Tanganyika sasa ni Watanganyika wote bila kujali mipaka ya vyama.

Ngongo kwasasa Mjini Magharibi.

Pia soma
- Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Naam
Umenena vyema
 
Katiba ni ya nchi moja sasa unaposema za nchi mbili unatukosea
 
Unajua nilichouliza kinalenga kujua mods wanahusika vipi na kutwaa Hilo eneo unalosema?
Na post yako Ina uzito gani hao unaosema kushindwa kufanya kile wamedhamiria?
Hili jukwaa si la kitoto bwashee, limeanzia mbali na linafika mbali, kwahiyo hata wao wanaulinda kwa nguvu zote
 
Sasa wewe unaongea kama nani maana hiyo Serikali 3 hakuna ccm anaetaka.

Kinachoitwa vita ya Kisiasa na ccm hawataki Rais kutoka Zanzibar Sasa Kuna haja ya kuwa na huo Muungano? Si watu wagawane fito tuu.

Mimi ni WA Bara ila kusema hutaki Rais wa kutoka Zanzibar nadhani ni upumbavu usio na msingi vinginevyo Wazanzibar wajitawale.
Hoja ni kwamba nani anasimamia masilahi na rasilimali za Tanganyika?
 
Hili jukwaa si la kitoto bwashee, limeanzia mbali na linafika mbali, kwahiyo hata wao wanaulinda kwa nguvu zote
Inawezekana ikawa hivyo lakini usili-overrate kwa kiwango hiko kikubwa maana wapo watu influential wanatumia social media zingine kufikisha yale waliyopanga

Mm swali langu kwako ilikua ni hisia uliyonayo, mods wanafuta mada zote wanazoona zimelenga kitu flani ambacho kimetajwa direct na hakuna ushahidi, Wala hawajafuta sababu wanahusika na ulichosema

Hata sasa hivi jaribu tu kuweka post ikisema mfano: waziri bashungwa anahusika na utekaji, hapo itafutwa fasta tu kwa sababu habari kama hiyo haina ushahidi na sio kwa sababu mods wanahusika na bashungwa
 
Hata sasa hivi jaribu tu kuweka post ikisema mfano: waziri bashungwa anahusika na utekaji, hapo itafutwa fasta tu kwa sababu habari kama hiyo haina ushahidi na sio kwa sababu mods wanahusika na bashungwa
Hapa umepuyanga bwashee, makonda, magu(late), IGP, Waziri mambo ya ndani nk nk kila siku wanatajwa na kuandikwa hata humu jf kwamba ni watekaji, wauaji, wasiojulikana na hata kusemwa wazi eti wamempiga flani risasi lakini hakufa na wala hakuna ushahidi wowote na wala hatuoni nyuzi zikifutwa, na hata leo bado zipo tena nyingi tu
Nb
Muungano unalindwa kwa hali yeyote ile na upande mmoja wenye manufaa
 
Hapa umepuyanga bwashee, makonda, magu(late), IGP, Waziri mambo ya ndani nk nk kila siku wanatajwa na kuandikwa hata humu jf kwamba ni watekaji, wauaji, wasiojulikana na hata kusemwa wazi eti wamempiga flani risasi lakini hakufa na wala hakuna ushahidi wowote na wala hatuoni nyuzi zikifutwa, na hata leo bado zipo tena nyingi tu
Nb
Muungano unalindwa kwa hali yeyote ile na upande mmoja wenye manufaa
Weka hiyo post inayosema hivyo uone kama itabaki
Labda hayo yawekwe na wachangiaji kwenye comments
 
Kama upo uwezekano wa Mtanganyika kugombea ubunge Zanzibar au kuongoza nchi ya watu wa Zanzibar bila vizingiti vya kusheria muungano ungeeleweka.

Kama Mtanganyika angeweza kununua ardhi kama raia wa Tanzania huu muungano tusingeupigia kelele.
A
Kabisa tena nyie wazanzibar ndiyo hatuwataki kabisa
kWel alafu sisi watanganyika hatuna chakupoteza kwa zanzibar hata leo hii muungano huu uchwala ukivunjika wao labda wao
 
Back
Top Bottom