Vita ya madaraka Makanisani ilivyoanzisha Kanisa halisi kutoka Siloam!

Vita ya madaraka Makanisani ilivyoanzisha Kanisa halisi kutoka Siloam!

Alitoka Sloam ya marehemu Munuo aliyekuwa mtumishi wa TANESCO? Si Sloam kwa sasa inaongozwa na Mrs Munuo? Wallah yule mama alivyo na roho mbaya watakaokwenda mbinguni ni wa kuokoteza!
Huyo Munuo mwanzillishi wa Sloam alijufa muda mfupi tu alipohubiri kuwa hawezi tumia jina la Yesu kuhubiri au kuombea watu sababu hakuna mtu mwenye dhambi duniani mwenye dhambi kama Yesu kuwa yeye Yesu alikiri kuwa alichukua dhambi zote za ulimwengu hivyo hawezi muheshimu wala kutumia jina lake

Wote hao Slloam na huyo miaka 1000 wote wana imani za kipepo tu hakuna mwenye nafuu
 
1724610304586.png
 
Huyo Munuo mwanzillishi wa Sloam alijufa muda mfupi tu alipohubiri kuwa hawezi tumia jina la Yesu kuhubiri au kuombea watu sababu hakuna mtu mwenye dhambi duniani mwenye dhambi kama Yesu kuwa yeye Yesu alikiri kuwa alichukua dhambi zote za ulimwengu hivyo hawezi muheshimu wala kutumia jina lake

Wote hao Slloam na huyo miaka 1000 wote wana imani za kipepo tu hakuna mwenye nafuu
Pole yake ndiye mwanzilishi wa kanisa hilo?
 
Hawa ndo wanaosababisha dini zinatukanwa na wale watu wanaojiita wachokonozi ..ukiwasikiliza kwa makini muda mwingine wanakuwa na logic kwa vile wanaongea kuhusu dini hizi na mazingaombwe yake
 
UMEWAHI kusikia kanisa liitwalo KANISA HALISI LA MUNGU BABA? Wanavaa nguo nyeupe kanisa zima, ibada zao nyingi zinarushwa STAR TV?Hawataji jina MUNGU wala YESU wao wanaita CHANZO HALISI 😁Hapa nakuletea historia fupi ya kiongozi huyo maarufu kwa jina la ELISHA ELIYA MIAKA 1000 (anaandika michuzi blog)

Rusomo ambaye baadae alijulikana kwa jina la Elisha Eliya Miaka1000 akiwa na matatizo mbalimbali ambapo aliombewa na kufunguliwa kisha akajiunga na huduma ya Siloam Bible School ambapo alifundishwa utumishi.

Wakati tayari akiwa kuhani wa kanda ya Dar es Salaam Miaka 1000 alisaliti kiapo cha utumishi, kwani baada ya kiongozi mkuu wa huduma hiyo kutwaliwa na kabla ya mchakato wa kumpata kiongozi mwingine, yeye alijivua safu ya ukuhani na akajipa cheo cha Mzeituni, Mpaka Mafuta, Mzee wa Siku, Wakili wa Mungu, mungu aliyetuma wote, baba wa uzao, baba halisi nk.

Mpaka aliacha kabisa imani aliyoikuta Siloam na aliazimia kupora thamani, uzuri na kibali cha kusanyiko la Siloam akiwa kwenye majengo ya Siloam.

Aliwapindua waumini kwa kuingiza mafundisho yaliyoacha maswali na hadithi za Kanisa Halisi la Mungu baba. E. E. Miaka1000 alitumia mbinu mbalimbali za kuvuruga safu za makuhani mikoani ambapo aliwashawishi waungane naye kusaliti maono ya mwanzilishi wa Huduma.

Ili kuhalalisha mapinduzi hayo alitunga Katiba yake akitaka kusajili The Pool of Siloam Church lakini haikupitishwa na Serikali kwa kuwa hakuwa mmoja wa viongozi wa Kikatiba. Hivyo, alizalisha mzozo ili Serikali ifute usajili halali wa Siloam Ministry InternationaI.

Hata hivyo hilo nalo halikufanikiwa.

Hivyo yeye na kundi lake la waumini aliofanikiwa kuwashaiwishi katika vituo mbalimbali waliendelea kutumia mali na majengo ya SMI kufanyia ibada na kuondoka na sadaka.


Serikali, viongozi na makuhani waaminifu walijitahidi kunusuru mgogoro huo lakini Miaka 1000 alikataa utengamano kwa madai kuwa yeye ni mungu na hawezi kujadiliwa, kuhojiwa wala kushauriwa.

WAUMINI WAKE MJE HAPA 😂😂😂TUNA KIKAO
Yani ni upuuzi wa kiwango cha lami.
 
Hawa ndo wanaosababisha dini zinatukanwa na wale watu wanaojiita wachokonozi ..ukiwasikiliza kwa makini muda mwingine wanakuwa na logic kwa vile wanaongea kuhusu dini hizi na mazingaombwe yake
Sijaelewa
 
Back
Top Bottom