Vita ya madaraka Makanisani ilivyoanzisha Kanisa halisi kutoka Siloam!

Vita ya madaraka Makanisani ilivyoanzisha Kanisa halisi kutoka Siloam!

Girland

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2016
Posts
2,489
Reaction score
4,253
UMEWAHI kusikia kanisa liitwalo KANISA HALISI LA MUNGU BABA? Wanavaa nguo nyeupe kanisa zima, ibada zao nyingi zinarushwa STAR TV?Hawataji jina MUNGU wala YESU wao wanaita CHANZO HALISI 😁Hapa nakuletea historia fupi ya kiongozi huyo maarufu kwa jina la ELISHA ELIYA MIAKA 1000 (anaandika michuzi blog)

Rusomo ambaye baadae alijulikana kwa jina la Elisha Eliya Miaka1000 akiwa na matatizo mbalimbali ambapo aliombewa na kufunguliwa kisha akajiunga na huduma ya Siloam Bible School ambapo alifundishwa utumishi.

Wakati tayari akiwa kuhani wa kanda ya Dar es Salaam Miaka 1000 alisaliti kiapo cha utumishi, kwani baada ya kiongozi mkuu wa huduma hiyo kutwaliwa na kabla ya mchakato wa kumpata kiongozi mwingine, yeye alijivua safu ya ukuhani na akajipa cheo cha Mzeituni, Mpaka Mafuta, Mzee wa Siku, Wakili wa Mungu, mungu aliyetuma wote, baba wa uzao, baba halisi nk.

Mpaka aliacha kabisa imani aliyoikuta Siloam na aliazimia kupora thamani, uzuri na kibali cha kusanyiko la Siloam akiwa kwenye majengo ya Siloam.

Aliwapindua waumini kwa kuingiza mafundisho yaliyoacha maswali na hadithi za Kanisa Halisi la Mungu baba. E. E. Miaka1000 alitumia mbinu mbalimbali za kuvuruga safu za makuhani mikoani ambapo aliwashawishi waungane naye kusaliti maono ya mwanzilishi wa Huduma.

Ili kuhalalisha mapinduzi hayo alitunga Katiba yake akitaka kusajili The Pool of Siloam Church lakini haikupitishwa na Serikali kwa kuwa hakuwa mmoja wa viongozi wa Kikatiba. Hivyo, alizalisha mzozo ili Serikali ifute usajili halali wa Siloam Ministry InternationaI.

Hata hivyo hilo nalo halikufanikiwa.

Hivyo yeye na kundi lake la waumini aliofanikiwa kuwashaiwishi katika vituo mbalimbali waliendelea kutumia mali na majengo ya SMI kufanyia ibada na kuondoka na sadaka.


Serikali, viongozi na makuhani waaminifu walijitahidi kunusuru mgogoro huo lakini Miaka 1000 alikataa utengamano kwa madai kuwa yeye ni mungu na hawezi kujadiliwa, kuhojiwa wala kushauriwa.

WAUMINI WAKE MJE HAPA 😂😂😂TUNA KIKAO
 
UMEWAHI kusikia kanisa liitwalo KANISA HALISI LA MUNGU BABA? Wanavaa nguo nyeupe kanisa zima, ibada zao nyingi zinarushwa STAR TV?Hawataji jina MUNGU wala YESU wao wanaita CHANZO HALISI 😁Hapa nakuletea historia fupi ya kiongozi huyo maarufu kwa jina la ELISHA ELIYA MIAKA 1000 (anaandika michuzi blog)

Rusomo ambaye baadae alijulikana kwa jina la Elisha Eliya Miaka1000 akiwa na matatizo mbalimbali ambapo aliombewa na kufunguliwa kisha akajiunga na huduma ya Siloam Bible School ambapo alifundishwa utumishi.

Wakati tayari akiwa kuhani wa kanda ya Dar es Salaam Miaka 1000 alisaliti kiapo cha utumishi, kwani baada ya kiongozi mkuu wa huduma hiyo kutwaliwa na kabla ya mchakato wa kumpata kiongozi mwingine, yeye alijivua safu ya ukuhani na akajipa cheo cha Mzeituni, Mpaka Mafuta, Mzee wa Siku, Wakili wa Mungu, mungu aliyetuma wote, baba wa uzao, baba halisi nk.

Mpaka aliacha kabisa imani aliyoikuta Siloam na aliazimia kupora thamani, uzuri na kibali cha kusanyiko la Siloam akiwa kwenye majengo ya Siloam.

Aliwapindua waumini kwa kuingiza mafundisho yaliyoacha maswali na hadithi za Kanisa Halisi la Mungu baba. E. E. Miaka1000 alitumia mbinu mbalimbali za kuvuruga safu za makuhani mikoani ambapo aliwashawishi waungane naye kusaliti maono ya mwanzilishi wa Huduma.

Ili kuhalalisha mapinduzi hayo alitunga Katiba yake akitaka kusajili The Pool of Siloam Church lakini haikupitishwa na Serikali kwa kuwa hakuwa mmoja wa viongozi wa Kikatiba. Hivyo, alizalisha mzozo ili Serikali ifute usajili halali wa Siloam Ministry InternationaI.

Hata hivyo hilo nalo halikufanikiwa.

Hivyo yeye na kundi lake la waumini aliofanikiwa kuwashaiwishi katika vituo mbalimbali waliendelea kutumia mali na majengo ya SMI kufanyia ibada na kuondoka na sadaka.


Serikali, viongozi na makuhani waaminifu walijitahidi kunusuru mgogoro huo lakini Miaka 1000 alikataa utengamano kwa madai kuwa yeye ni mungu na hawezi kujadiliwa, kuhojiwa wala kushauriwa.

WAUMINI WAKE MJE HAPA 😂😂😂TUNA KIKAO
Tumefikia hapa 🤔
 

Attachments

  • 1.JPG
    1.JPG
    94.9 KB · Views: 10
Back
Top Bottom