Vita ya Uchumi haijawahi kuwa nyepesi, Hayati Magufuli aheshimiwe

Vita ya Uchumi haijawahi kuwa nyepesi, Hayati Magufuli aheshimiwe

Yep. Hili halina ubishi. Alikuwa anachukia ufisadi na uzembe kutoka rohoni lakini tatizo alikuwa hana upeo wa kushughulikia. N ambaya zaidi akawa anachagua wanafiki kwenye serikali yake na watu waliokuwa wanamwambia ukweli alikuwa anawaona kama maadui. Pengine hii ilitokana na kasoro mbili kubwa alizokuwa nazo. 1. kupenda kusifiwa 2. kupenda baadhi ya watu kutoka kanda fulani na kuchukia wengine.


Hii statement hapa inakuvua uhalisia wako.

Ina maana unashindwa kabisa kutenganisha personalities za mtu na utendaji kazi wake?

1) Kupenda kusifiwa- anaweza kumzidi aliyebariki taasisi ya “Chawa wa Mama? Na mwana mtandao mashughuli wa “Boys 2 Men?

2) Kupenda baadhi ya watu kutoka kanda fulani - kwamba hapa amewazidi wengine wote waliomtangulia kukalia hicho kiti? Kabisa?!


Ni hatari kujifanya kipofu na kuchangia mjadala huku ukivutia upande wako ilhali dhamira yako sio safi kihivyo.
 
Watanzania wengi (haswa vijana) wamegeukia kazi ya ushabiki (uchawa) kwa wanasiasa kiasi hawajali tena maslahi mapana ya kitaifa ila itikadi za kichama na kisiasa.



Na hao vibaraka ndio mwiba haswa kwenye moyo wa Tanzania. Kibaya zaidi siku hizi ukibaraka wao hawaufichi tena, mabwana zao wanawaita eti investors. Very disgusting.
Kuna watu wanajiita chawa wa mama
 
Nani aliwanyima hivyo unavyo andika hapa hivi unajua unacho ongea au unaropoka ?

Vita vya kiuchumi unavijua wewe au unaropoka tu kwa kelele za wanasiasa.

Nchi hamna mnacho zalisha cha kujitosheleza unasema tulikuwa na vita vya kiuchumi mkipigwa vita vya kiuchumi nyie na kisarafu chenu kisicho na thamani yoyote si mtaanza kula majani.
Hamna hoja. Nilidhani huwa wanakuja na silaha kupora. Kumbe ni tamaa za viongozi wetu ndiyo zinasababisha haya yote? Sasa unalia nini?
Wakuu mnafikiri kwanini tunashidwa kuzalisha vyakujitosheleza na ziada, Hapa tuzungumzie mazao ya kimkakati na industry zinazohitaji capital na mobilization kubwa achana na single individual ambao scale yao ya uzalishaji haina impact kwa taifa. eg. Sukari, ngano, mafuta ya kula, hata nishati.
Yaani kila awamu makosa ni yale yale.

Nakili ya kwamba sisi wa Africa tunachangamoto zetu lakini si kwa level hizi, pia mimi mwenyewe sipendi kuona mtu analalamika tu na kuwatupia watu lawama kwa mambo ambayo ni wajibu wake yeye kuyatekeleza, ni ujinga kama sio upumbavu.

Lakini mbali na hizo changamoto tulizonazo kama wa Afrika, wajanja wanaishi na sisi humo humo wanatumia udhaifu wetu kama fursa kupitia uishawishi wa kidiplomasia na nguvu ya kiuchumi walionayo ni rahisi sana kuhadaa viongozi wetu, na kumbuka yupo madarakani under pressure anahitaji support kuendelea kubaki.

Na ukikataa wenzako wanakula ukitafakari unagundua hakuna ulichofanya maana ulichopigania wezako wanakigawa maisha yanaendelea ila wewe unakua umejiweka kwenye angle mbaya, na wakikuamulia wanakuchafua kwa propaganda ile iwe fundisho kwa wazalendo waliobakia(discourage). Yaani unakufa maskini na skendo juu.👇👇👇
Mikataba wanaandaa wao, wanawaletea viongozi wenu wasome. Haiandaliwi na wanasheria wenu.

Kabla ya kuleta huo mkataba Kuna kua na Ile tunaita chachandu. Utasikia rais kaenda kule Leo kesho kutwa kaenda kule Tena. Hata mara kumi kabla ya huo mkataba kuandikwa. Wanampa na chake kabisa. Akikataa anakua sio mwenzao.

Kipindi hicho wanakua na watu wao wa kuwapa ABC. Watafatilia nani kasababisha ukatae na Kwa nini. Unajikuta upo katika risk kubwa.

Wasiowajasiri hukubali kuepusha shari Ili maisha yaendelee na familia zao zineemeke. Watu kama JPM hawakubali.

Kwenye vita ya uchumi hawapandikizwi viongozi tu, kila sector ambayo ni potential kunakua na agent wao hasa hasa hizi sector ambazo moja kwa moja zinashikilia uchumi wa nchi mfano. Nishati, wafanyabiashara wakubwa wa bidhaa muhimu ie, vyakula. Sasa hawa kuna michezo hua wanaicheza kwa kufuata maelekezo kuhakikisha nchi haiwi stable katika uzalishaji at the same time wanalinda soko la bidhaa zao kutoka nje ya nchi ambako ndio kwa wenyewe(mabeberu) Kwahiyo wao wanarisha raia wao wanapata ajira kupitia mnyororo wa thamani sisi tunatumia kwa gharama kubwa tunaishia kurumbana vijiweni.


Vita vya kiuchumi achia warusi, wachina, Iran, NK , Venezuela at least Zimbabwe akiongea Nita muelewa.
Mbinu mbalimbali hua zinatumia Kulingana na aina(nature) ya nchi na level ya maendeleo na ushawishi ilipofikia nchi husika.
Namna USA wanavyod-deal na mchina au mrusi ni tofauti watakavyo deal na sisi huku. Inaonekana sisi sio stubborn saana hivyo haina haja ya kutumia nguvu kubwa.

Nb vita ya kiuchumi kati ya USA na China hata sisi huku tunahusika kwa maana maslahi yao mapana yaliyopo kwetu huku yako rehani. Hii kasheshe sisi tukiwa bado tunapambania masrahi mapana ya nchi yetu. Kumbe wezetu wana masrahi yoa mapana juu ya nchi yetu (ukanda wetu).
 
Hakuna cha vita vya uchumi wala nini roho ni mbaya tu ndiyo ilikuwa inamsumbua na uroho wa hela maana alihakikisha anavunja mikataba waliyoingia wenzake ili apige yeye.
 
Hamna hoja. Nilidhani huwa wanakuja na silaha kupora. Kumbe ni tamaa za viongozi wetu ndiyo zinasababisha haya yote? Sasa unalia nini?
Wewe hata walichoongea hao viongozi kwenye hizo clip huelewi kitu. Uchawa umekuzidi sana. Acha upuuzi na kujitoa akili. Tumia utimamu wa akili zako.

Hivyo ulivyo ndio tofauti ya "wale" na wewe.

Hamna mtu anaelia hapo, Nyerere kaongea na vicheko kaweka. JPM kaongea sijaona kalia.

Kwenyejadala watu wanaeleza ukweli wa mambo yalivyo, wewe u akuja kulaumu viongozi kua wanatamaa.

Wewe unaweza muachaniza hata mkeo akaliwa na wadau na u kumlaumu mkeo kua anatamaa bila kuangalia deep inside Kwa nini imekua hivyo.

Tumia akili Yako acha uchawa.
 
Vita ya uchumi ni changamoto kubwa ambayo inahitaji uongozi thabiti na mikakati madhubuti. Hayati John Pombe Magufuli, Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alikuwa kiongozi aliyefahamika kwa ufanisi wake katika kutekeleza sera za maendeleo na mapambano dhidi ya rushwa. Baadhi ya sera na mikakati aliyoiweka ililenga kuimarisha uchumi wa nchi, kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima, na kukuza maendeleo ya miradi ya miundombinu.
Ni muhimu kutambua kwamba maoni kuhusu utendaji wa kiongozi fulani yanaweza kutofautiana kulingana na mtazamo wa kisiasa na maoni ya watu binafsi. Wapo wanaomsifia kwa hatua zake za kufanya mageuzi na kuchochea maendeleo, wakati wengine wanaweza kuwa na wasiwasi kuhusu madhara yoyote au athari za sera zake.
Katika kumuenzi Hayati Magufuli, ni muhimu kuchambua matokeo ya sera na mikakati aliyoiweka, pamoja na kujadili mafanikio na changamoto zilizojitokeza. Kila kiongozi ana athari zake kwa uchumi na jamii, na mjadala juu ya mchango wake unaweza kutoa mwanga zaidi kuhusu njia zinazofaa kwa maendeleo ya nchi.
Ni vizuri kuzingatia umuhimu wa mjadala wa wazi, heshima kwa maoni tofauti, na kutafuta mbinu za kuendeleza maendeleo na ustawi wa nchi. Historia ya kiongozi yeyote inahitaji kuangaliwa kwa kina na kwa uwazi ili kuweza kutoa tathmini yenye busara na haki.
Nice analysis
 
Wakuu hoja zenu wote ziko sahihi ila anaeunga mkono hoja ya vita ya kiuchumi yuko sahihi zaidi changamoto inakuja anakosa namna sahihi ya kuwakilisha hoja yake na anakosa mifano halisi ya kujazia hoja.

Hii yote ni kwasababu katika vita za kiuchumi mataifa mengi huwa wanatumia Taasisi za siri za usalama, na kama mnavyojua Taasisi za usalama watu wao wanakuaga ni selection of talented elites (Akili nyingi)... Yaani wanapiga tukio ambalo kiratiba liko mbele ya muda arafu limesukwa kwaustadi mkubwa kiasi kwamba raia wa kawaida akikutana na tukio hilo kwanza anakua too late, pili anahisi tukio hilo ni lakimazingara(nguvu za giza zimehusika). Yaani liko beyond na upeo wake wa fikra.

Sasa watu kama hawa wakija kwenye suala la ujasusi wa kiuchumi wanatumia mifumo mingi tu lakini moja ya mfumo wanaocheza nao kwa weledi na ustadi wa hali ya juu ni mfumo ulio katika sector ya sheria,

Wanapitia vizuri kabisa katiba na sheria ya nchi ambayo wameitarget then wanaenda specific kwenye vifungu vinavyohusu resource wanayoitaka wao, lazima watakutana na mwanya tu (weakness) hata wakikosa hiyo weakness watafanya namna tu kupata mazingira favourable kwao.

Baada ya hapo wazee wa kazi wanaingia kazini... Unasukwa mkataba konki ulioshiba(mama mkanye mwanao). My friend hiiiii!!! Kama unavyoona engine za magari zilivyosuka kwa weledi na ustadi mkubwa hadi gari inatembea basi ndio hivyo hivyo mkataba inasukwa na inakuja imepakwa asali kama chambo tu, Sasa wewe jichanganye ingia kwenye mkataba kama huo utakuja kushtuka tayari umeshachelewa na kila ukitafuta namna ya kujitoa vifungu vinakubana.

Na hawa watu hawawezi kuacha clue yoyote ambayo wewe unaweza kuitumia kama evidence mahakamani.

Hiyo kitaalamu tunaita "ulipo lala leo wenzako wameamkia jana kama sio mwaka jana" yaani unakua kama panya alienasa kwenye ule mtego ambao kuingia rahisi ila kutoka Sasa ndio changamoto, mpaka aje mwenye mtego.

Sisemi kwamba kung'amua njama kama hizi kunahitaji rocket science lakini umakini unahitajika na wala hakuna haja yakuharakisha mambo, kuna msemo unasema "ukiona unaitwa kwenye fursa basi ujue fursa ni wewe mwenyewe"
Nice view
 
Yaan hua najiuliza watu wa namna hii, hata kama ni umasikin ndio ushindwe kutambua how African nations are made under developed? Ufusadi mkubwa ni ule wa maliasili. Kusaini mkataba unaompendelea beberu, nchi inakosa wewe binafsi unapewa kidogo unazani maraisi wote wa Afrika wanapenda? Kikwete alipenda Ile namna ya uongozi wake wa Kila mtu holela?

Kuna kua na nguvu kubwa inayokusukuma ukubali hayo. Kukukataa unakua sio mmoja wao. Watakufanyia figisu Hadi uchoke.

Tambua ndani ya nchi sio Kila mtu anakua na mawazo kama ya kwako. Hata katika chama sio wote wanakukua na mawazo ya kutimiza Irani ya vyama vyao. Wengine wapo Kwa masrahi yao.

Wewe kama mwenyekiti wa chama kupambana nao ndani ya chama ni kama Magufuri na kina Nape na January na wengine. Watu waliomlengwa tofauti na wewe ni rahisi kuhongeka na kukufanyizia lollote like Ili masrahi ya mabeberu yatawale. Wewe usipochukua wenzio watachukua.Ukikataa wanaremove obstacle.

Elewa kwamba masrahi ya mabeberu ndio chanzo Cha matatizo na ufusadi uliokithiri. Ukiwa mzalendo wanakupa jina la obstacle, then grant ya kukuremove Kwa support ya watu wako wa ndani na sio wao.

Mafisadi wa ndani ya nchi bila support ya mabeberu kumuweza rais aliekua amejidhatiti Kwa ulinzi kama JOM sio rahisi kihivyo ufikiriavyo.

R.I.P Jembe Magu...
Uchambuzi murua
 
Wakuu mnafikiri kwanini tunashidwa kuzalisha vyakujitosheleza na ziada, Hapa tuzungumzie mazao ya kimkakati na industry zinazohitaji capital na mobilization kubwa achana na single individual ambao scale yao ya uzalishaji haina impact kwa taifa. eg. Sukari, ngano, mafuta ya kula, hata nishati.
Yaani kila awamu makosa ni yale yale.

Nakili ya kwamba sisi wa Africa tunachangamoto zetu lakini si kwa level hizi, pia mimi mwenyewe sipendi kuona mtu analalamika tu na kuwatupia watu lawama kwa mambo ambayo ni wajibu wake yeye kuyatekeleza, ni ujinga kama sio upumbavu.

Lakini mbali na hizo changamoto tulizonazo kama wa Afrika, wajanja wanaishi na sisi humo humo wanatumia udhaifu wetu kama fursa kupitia uishawishi wa kidiplomasia na nguvu ya kiuchumi walionayo ni rahisi sana kuhadaa viongozi wetu, na kumbuka yupo madarakani under pressure anahitaji support kuendelea kubaki.

Na ukikataa wenzako wanakula ukitafakari unagundua hakuna ulichofanya maana ulichopigania wezako wanakigawa maisha yanaendelea ila wewe unakua umejiweka kwenye angle mbaya, na wakikuamulia wanakuchafua kwa propaganda ile iwe fundisho kwa wazalendo waliobakia(discourage). Yaani unakufa maskini na skendo juu.👇👇👇


Kwenye vita ya uchumi hawapandikizwi viongozi tu, kila sector ambayo ni potential kunakua na agent wao hasa hasa hizi sector ambazo moja kwa moja zinashikilia uchumi wa nchi mfano. Nishati, wafanyabiashara wakubwa wa bidhaa muhimu ie, vyakula. Sasa hawa kuna michezo hua wanaicheza kwa kufuata maelekezo kuhakikisha nchi haiwi stable katika uzalishaji at the same time wanalinda soko la bidhaa zao kutoka nje ya nchi ambako ndio kwa wenyewe(mabeberu) Kwahiyo wao wanarisha raia wao wanapata ajira kupitia mnyororo wa thamani sisi tunatumia kwa gharama kubwa tunaishia kurumbana vijiweni.



Mbinu mbalimbali hua zinatumia Kulingana na aina(nature) ya nchi na level ya maendeleo na ushawishi ilipofikia nchi husika.
Namna USA wanavyod-deal na mchina au mrusi ni tofauti watakavyo deal na sisi huku. Inaonekana sisi sio stubborn saana hivyo haina haja ya kutumia nguvu kubwa.

Nb vita ya kiuchumi kati ya USA na China hata sisi huku tunahusika kwa maana maslahi yao mapana yaliyopo kwetu huku yako rehani. Hii kasheshe sisi tukiwa bado tunapambania masrahi mapana ya nchi yetu. Kumbe wezetu wana masrahi yoa mapana juu ya nchi yetu (ukanda wetu).
Umeeleweka vizuri ingawa kuna wachache hawawezi kukuelewa
 
Habari JF, vita ya Uchumi kuanzia mitaani, mirathi na makazini hata iwe ndogo haijawahi kuwa nyepesi na haijawahi acha mtu salama.

Ukiwa kiongozi wa juu nchi za Africa huwa hakuna vita nyepesi ya uchumi sababu unakuwa unapigana watu wa ndani ya nchi lakini pia na mataifa ya nje.

Magufuli pamoja na mapungufu yake yote alieonyesha jitihada katika kupambana hii vita ndani ya nchi lakini pia nje ya kwa kupitia mikataba mibovu mbali mbali na kuivunja ingawa wimbi la kesi za kushindwa kimataifa limeongezeka. Kwanini hizi kesi ni kipindi hiki? Kuna watu wana nufaika na hizi kesi?

Ukimsikiliza hapa mwalimu Nyerere kuna kitu unaweza elewa.

View attachment 2900394

Lakini JPM mwenyewe mara kadhaa kaongea kwa uchungu sana.
View attachment 2900408

Kwa kifupi kabla hatujalaumu kwa yote tuliyopitia Awamu ya Tano au Tunayopitia awamu Hii cha kwanza jiulize unaweza vaa hivyo viatu na ukapigana na Mafisadi na Mabeberu?

Binafsi huwa namlaumu Magufuli kwa kitu kimoja tu, kutotuletea Katiba Mpya.

Tumuache mzee wetu apumzike kwa Amani.​
Wajinga watabaki kuwa wajinga unajua kwanini alimrudisha Rostam ? Mambo yalikuwa hayaendi. JPM alidhani nyerere alikuwa mjinga kutopendelea kabila lake bali kuteua watu kutokana na uwezo wao. Baada ya JPM mama ameiga sasa kajaza watu wa visiwani na wavaa makobazi. Na Rais atakayekuja nae ataendelea na mwendo aliouanzisha JPM. Viongozi wa kiafrika wanafikiria leo lakini hawafikirii kesho. Hakuna nchi ambayo haina amani ilipata uhuru kwa njia ya amani. Nyerere alikuwa na mapungufu lakini hakuna Rais mzuri kuliko yeye na hatokaa atokee. Alikuwa kati ya watu wachache waliokuwa exposed angeweza kutumia ujuzi wake kutunyonya kama alivyofanya Jomo Kenyata Kenya.
 
Hii statement hapa inakuvua uhalisia wako.

Ina maana unashindwa kabisa kutenganisha personalities za mtu na utendaji kazi wake?

1) Kupenda kusifiwa- anaweza kumzidi aliyebariki taasisi ya “Chawa wa Mama? Na mwana mtandao mashughuli wa “Boys 2 Men?

2) Kupenda baadhi ya watu kutoka kanda fulani - kwamba hapa amewazidi wengine wote waliomtangulia kukalia hicho kiti? Kabisa?!


Ni hatari kujifanya kipofu na kuchangia mjadala huku ukivutia upande wako ilhali dhamira yako sio safi kihivyo.
Hakuna rais aliekuwa na ukabila katika serikali yake kabla ya 2015. JPM ndio alioanzisha ukabila ndani ya serikali na Mama ndio anaendeleza. Na kama hakuna kitakachofanyika Rais atakaefuata atafanya hivyo hivyo. Tuangalie kijijini kwa Mkapa, Nyerere, Mwinyi na Kikwete. Halafu tuje tuangalie Mkoa aliotoka JPM. Baada ya hapo tuangalie Rais gani aliyetaka kugeuza wilaya aliyotoka kuwa mkoa ? Rais gani aliyetaka kuweka mbuga ya wanyama kwao ? Rais gani aliyejenga uwanja wa ndege kwao ? Rais gani aliyejenga hospitali ya rufaa kwao ? Rais gani aliyejenga Ikulu kwao ? Rais gani aliyeagiza kufungua tawi la CRDB kwao ? JPM alikuwa Rais wa wasukuma na sio wa watanzania. Hii ipo wazi kabisa na mbaya zaidi ukitumia hii system unapata wanafiki wengi kama H.K. Hata ukiwa na biashara ukimuweka ndugu yako haogopi kuiba na hata ukiambiwa anaiba hauwezi kuamini kwa sababu ni ndugu. Na kaa chini uangalie mama anaendeleza alipoishia JPM mbadala wa chato ni kizimkazi. Nchi inapasuka vibaya sana na sijui nani atairudisha Tanzania ya umoja.
 
Hakuna rais aliekuwa na ukabila katika serikali yake kabla ya 2015. JPM ndio alioanzisha ukabila ndani ya serikali na Mama ndio anaendeleza. Na kama hakuna kitakachofanyika Rais atakaefuata atafanya hivyo hivyo. Tuangalie kijijini kwa Mkapa, Nyerere, Mwinyi na Kikwete. Halafu tuje tuangalie Mkoa aliotoka JPM. Baada ya hapo tuangalie Rais gani aliyetaka kugeuza wilaya aliyotoka kuwa mkoa ? Rais gani aliyetaka kuweka mbuga ya wanyama kwao ? Rais gani aliyejenga uwanja wa ndege kwao ? Rais gani aliyejenga hospitali ya rufaa kwao ? Rais gani aliyejenga Ikulu kwao ? Rais gani aliyeagiza kufungua tawi la CRDB kwao ? JPM alikuwa Rais wa wasukuma na sio wa watanzania. Hii ipo wazi kabisa na mbaya zaidi ukitumia hii system unapata wanafiki wengi kama H.K. Hata ukiwa na biashara ukimuweka ndugu yako haogopi kuiba na hata ukiambiwa anaiba hauwezi kuamini kwa sababu ni ndugu. Na kaa chini uangalie mama anaendeleza alipoishia JPM mbadala wa chato ni kizimkazi. Nchi inapasuka vibaya sana na sijui nani atairudisha Tanzania ya umoja.
Chato wanakaa Watanzania au warundi?
 
Hakuna rais aliekuwa na ukabila katika serikali yake kabla ya 2015. JPM ndio alioanzisha ukabila ndani ya serikali na Mama ndio anaendeleza. Na kama hakuna kitakachofanyika Rais atakaefuata atafanya hivyo hivyo. Tuangalie kijijini kwa Mkapa, Nyerere, Mwinyi na Kikwete. Halafu tuje tuangalie Mkoa aliotoka JPM. Baada ya hapo tuangalie Rais gani aliyetaka kugeuza wilaya aliyotoka kuwa mkoa ? Rais gani aliyetaka kuweka mbuga ya wanyama kwao ? Rais gani aliyejenga uwanja wa ndege kwao ? Rais gani aliyejenga hospitali ya rufaa kwao ? Rais gani aliyejenga Ikulu kwao ? Rais gani aliyeagiza kufungua tawi la CRDB kwao ? JPM alikuwa Rais wa wasukuma na sio wa watanzania. Hii ipo wazi kabisa na mbaya zaidi ukitumia hii system unapata wanafiki wengi kama H.K. Hata ukiwa na biashara ukimuweka ndugu yako haogopi kuiba na hata ukiambiwa anaiba hauwezi kuamini kwa sababu ni ndugu. Na kaa chini uangalie mama anaendeleza alipoishia JPM mbadala wa chato ni kizimkazi. Nchi inapasuka vibaya sana na sijui nani atairudisha Tanzania ya umoja.


Too biased.

Kwamba hujui angalau kila mkoa aliotokea Rais wa nchi hii na mikoa mikuu ya nchi kuna Ikulu ndogo za Rais?

Kwamba Magufuli kwa kauli yake aliagiza CRDB kufungua tawi Chato?! Una akili timamu kweli?

Kwamba kabla ya 2015 kwenye utumishi wa ummah hakukua na upendeleo wa kikabila/kikanda? Una hakika?

Wakati wa Nyerere wale wanajeshi zaidi ya asilimia 50 kutoka ukanda wake ilikua ni bahati mbaya ama kwamba wao ndio majasiri sana wa kukaa jeshini?

Kwa Mwinyi hata usiseme sana nenda Loliondo bado alama yake na leo yupo bado bara na visiwani. Huna macho?!

Mkapa? Hapa ukitaka kuifahamu vizuri definition ya Selfishness, msome vizuri.

Kikwete wala sihitaji kukumbusha style yake na wenzake ya wanamtando aka Boys 2 Men. Hapa ndio kulizaliwa Chama jipya Chukua Chako Mapema.

Magufuli kuwakumbuka watu wa kanda ya ziwa na kuwapa vipaumbele sio dhambi maana kwa kiasi kikubwa walisahaulika kwa kisingizio eti Nyerere aliwahi kuonya kutowapa uongozi watu wa kanda hiyo (waliokuwepo enzi hizo wanasema alikua anawasema watu wa Kaskazini)

Rais Samia anafuata nyayo za watangulizi wake na mfumo ndivyo ulivyo tangu enzi.

Wakati wa ukoloni wakoloni waliwapendelea zaidi watoto wa wafalme (machifu) na ndugu zao kwa kuwapa elimu na majukumu na hata baada ya kupata Uhuru wa kwenye makaratasi Nyerere hakufanya tofauti sana haswa pale alipokoswakoswa kupinduliwa akakimbilia Kigamboni, aliwakumbuka ndugu zake na kuwajaza!
 
Back
Top Bottom