Vyama vya upinzani mwacheni Rais Samia 2025 apite bila kupingwa ili awanyooshe mapito yenu 2030

Vyama vya upinzani mwacheni Rais Samia 2025 apite bila kupingwa ili awanyooshe mapito yenu 2030

Wapinzani watakubali hoja YAKO LAKINI KWA serikali mseto ijayo AMBAYO Mama Anaweza asiwe sehemu ya HIYO serikali!!2025 ni Mbali Sana kwani wewe unawasiliana na Mungu!!!???
Mungu ni WA wote, anaondoa maisha na kuongeza maisha ya amtakae. Tunapanga kama vile tupo milele,
 
CCMni laana kwa taifa
Kuondoka nayo hakuhitaji mihemko, hata akina Nyerere kama wangedai Uhuru kwa mihemko wasingeupata haraka na wengepotea wengi.

Wapinzani wenye weledi wangetumia weledi kudai demokrasia nchini. Sisi ni waafrika malezi yetu tangu utotoni ni ya ubabeubabe na short cut. Ndio maana kama utamkwaza Rais wa Africa ni rahisi kuonyesha ubabe
 
Kuna watu wanaamini as long as wewe ni chadema basi tayari taifa linakuona mkombozi.

Wanaamini hata wakisimama majukwaani wakanyanyua makwapa tu watu watawapigia kura.

Nyinyi kama chama mmejipangaje? Niliwahi kuuliza hili swali hadi leo sijajibiwa:;- NAOMBA MTU ANIPANGIE SAFI YA SERIKALI YA CHADEMA ikitokea hata ndotoni wamepata nchi nani atakua Rais nani Makamu nani Pm na safu ya mawaziri.

Povu ruksa ila hakika nawaambia mchawi wa chama wala hayuko nje. Chama hakipo tayari kwa uongozi all they want is CCM out. Hata mkisema mpewe leo hivyo vyeo uozo utabaki pale pale. Selfishness mbele. Hakuna mwanadamu anaetamani maendeleo ya mtu mwengine kabla ya kwake.

Haya hawa tulionao wamekula weeee waje na Chadema nao waaanze kula kufidia muda wote waliokua wanazengea vyeo. Tanzania kuja kupata ahueni ni 2080.

Tulieni huko maendeleo hayana chama
 
Namkumbuka hayati Benjamin Mkapa kwa kauli yake kuhusu "watu kuwa wavivu wa kufikiria"

Kila Rais mpya akitokea fikra kama hizi hujitokeza. Pale JPM alipokuwa hai, pia alipambwa kwa kauli kama hizi, na hata yakajitokeza matamanio ya kubadili katiba ili tu azidi kubakia madarakani baada ya kuhudumu kwa kipindi chake cha miaka 10.

Leo mwaka mmoja baada ya kutokuwepo kwake, unaanza unafiki kama ule ule, eti haijapata kutokea Rais kiutendaji mfano wa SSH toka tupate uhuru wa Tanganyika, ama sijui pia ulikuwa una maanisha pia na ule wa Zanzibar.

Hivi unazijua changamoto mbalimbali ambazo taifa letu ilizipitia katika vipindi tofauti vya awamu za uongozi wa taifa letu? Hivi unajua vipaumbele vya kitaifa vya kijamii na kiuchumi vilivyokuwepo, miundombinu ya nchi yetu, vyanzo vikubwa vya mapato ya nchi, miradi mikubwa ya kimkakati, deni la taifa, idadi ya rasilimali watu muhimu iliyokuwepo na vitu vingine muhimu kama hivyo, kiasi kwamba ufikie kiwango cha kutoa majisifu kama hayo?
Wahenga wanasema kama hujui unakokwenda huwezi kupotea na hata kama umepotea hujui kama umepotea. Hii tabia ya kumsifu kila Rais wa kila awamu ni dalili kuwa taifa halijui linaelekea wapi na watu hawajui pia wanaelekea wapi na walipaswa kuwa wapi. Hivyo ni vigumu kujua ni kiongozi gani anahitaji kusifiwa na yupi anastahili kuzomewa. Mfano, kama taifa tungekuwa kumekubaliana kwa pamoja tangu kupata uhuru kuwa tunataka kila mkoa uwe na vyuo vikuu 3 vya serikali ifikapo 2025 na kila wamu LAZIMA ijenge angalau vyuo vikuu 5 sisi wananchi tungeweza kumbaini ni rais yupi hakujenga vyuo 5 kwenye awamu yake ili tumsifu na yupi hakujenga hata 2 ili tumzomee.

Kama taifa lazima tutengeneze dira yetu ya miaka 100 ijayo kuhusu wapi tunataka taifa letu liwe, kisha tugawanye malengo ya kufika huko kwa kila awamu. Sasa hivi kila awamu inakuja na mpango wake yenyewe.

Tunaposema mama Samia anafanya vizuri ni kwa kulinganisha tu mambo fulanifulani na awamu iliyopita kwenye jambo hilo. Mfano, vyama vya upinzani vilitiwa kolokoloni na JPM lakini Mama SSH amepatia ahueni. Sasa ni wajibu wa vyama vya upinzani kutumia ahueni hii kwa weledi ili SSH apanue zaidi dirisha la demokrasia ikibidi kwa kutumia dialogue zaidi kuliko nguvu, kejeli na sarakasi nyingi na kusahau kuwa katiba hii inampa uwezo hata SSH kuvitia roba ya mbao vyama vya upinzani kama walivyofanya wengine.
 
Back
Top Bottom