Wanabodi,
Ili CHADEMA kiendelee kuishi ni lazima kiukubali ukweli, kikubalini matokeo ya uchaguzi, kiandike barua NEC, kwanza kufanya due diligence ya majina hayo yamefikaje NEC, wakibaini ni kwa njia ya kughushi, then, this is criminal issue, sio tena issue ya Bunge au NEC, hii ni jinai, waanze kwa kuipeleka polisi, ili kuwaadhibu wahusika kwa kuwavua uanachama hao wahusika wakiwemo hao wasaliti 19, kisha kipeleke majina mapya 19, kiendelee kuvuta ruzuku and survives, or kiendelee kushupaza shingo, kuwa hakiyatambui matokeo ya uchaguzi, hakimtambui rais wa Jamhuri ya Muungano wa hakilitambui Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, then CHADEMA will just go straight to hell by being buried 6ft Under!.
Mbele ya macho ya jamii, hao ambao kwao ni wasaliti, kwa wengine hao ni makamanda mashujaa wapambanaji ambao ni wa kiwango cha makomandoo, ambao wameipigania Chadema kwa machozi, jasho na damu, na licha ya kufutwa uanachama wa CHADEMA, wataendelea kuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Ubunge wao sasa utakuwa ni ubunge wa Spika, Ubunge wa Taifa.