Wabunge wa Kagera wapinga Mkoa wao kumegwa na kupelekwa Chato

Wabunge wa Kagera wapinga Mkoa wao kumegwa na kupelekwa Chato

Bado chato haifai kuwa mkoa ulikuwa ubinafsi tu wa jiwe aisee Yani wilaya imeze mkoa wa Geita selfish idea kabisa hyo
Tena wewe kama umeajiriwa serikalini unapaswa uhamishiwe wilaya mojawapo za mkoa mpya wa chato ukawatumikie wananchi
 
Chato ina miradi ya kitaifa. Isipofanywa mkoa hiyo miradi itakuwa magofu.
So hakuna namna zaidi ya kupafanya mkoa ili miradi iendelee kuwa hai.
Mkoa wa Rubondo kitawekwa kituo kikubwa cha kusafisha mafuta ya Uganda..kwa ajili ya kuuza kanda ya ziwa,burundi,Congo na Rwanda
Solution ni Makao makuu ya mkoa wa Geita yahamishiwe Chato halafu mkoa wa Geita ubadilishwe jina uitwe CHATO.

Ombi la muombolezaji aitwae Bigambo litakuwa limeshatekelezwa bila ya kuwaathiri Wana KAGERA
 
Mkoa wa kagera ni maskini in general usiwasingizie hao sijui wasubi na wengine kwa kujiona wahaya ni Bora aisee
Wilaya ya biharamulo ndo maskini zaidi mkoani kagera ...
Biharamulo ni ya pili nchini kwa umaskini huku zaidi ya 60% ya wakazi wake ni maskini kadri ya takwimu.

Ngara ipo top ten ya umaskini nchini zaidi ya 52% ni maskini na ni wilaya ya pili kwa umaskini kagera.




So Bora ziunganishwe na kutengenezewa mkoa wake ili ziangaliwe zaidi
 
Ila wahaya ni kiburi, nyie....

Nimesoma maneno machache sana hasa hapo kwenye CHIMBUKO LA MKOA MPYA WA CHATO na naomba kunukuu:-

"Chimbuko la kuomba mkoa mpya wa Chato halina mashiko kisiasa, kiuchumi wala kisheria"

Naendelea kunukuu....

"Chimbuko la mkoa wa Chato linatokana na muombolezaji mmoja aitwaye Bigambo wakati wa msiba wa hayati Magufuli."

"Muombolezaji huyo alidai kusikia kwamba Magufuli alitaka Chato uwe mkoa, jambo ambalo halina uthibitisho wowote wa kisiasa"

Mwisho wa kunukuu.

My take:
Yaani hawa jamaa (Wahaya) "wameikataa" kabisa Chato na wakafika mbali zaidi kwa kusema "zilikua ni hasira tu" za kufiwa (za msiba) za bwana Bigambo.
Lakini pia wametanabaisha kwamba alichokisikia bwana Bigambo hakina uthibitisho wowote, kwahiyo huenda Bigambo alikua "anatujaza tu".

Si walisema Mkoa wa Geita ubadilishwe uitwe Chato. Simple as that!
 
Mimi sio wa kagera ila kugawa mkoa kwa Nia ya ubinafsi wa kiongozi mmoja ni hasara how about history ya mkoa wa kagera, hao wabunge wa ngara acha wasaidiwe kama wamelala kutetea mkoa mzima wa Kagera, hafu why chato wakati Kuna mikoa mingi mikubwa kuliko Geita na hawajapeleka hyo kugawa.
Umaskini nchi hii utaisha kwa serikali kupeleka maendeleo Hadi ngazi ya chini kabisa na sio kuongeza mikoa na wilaya ambazo zitaongeza cost of administration.
Kwani kuanzisha mkoa wa chato inazuia nini kumegwa kwa mkoa wa tabora na morogoro kama navyo vimekidhi vigezo ?

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
 
Hoja kubwa wanasema hizo wilaya zinazotakiwa kumegwa, pamoja na Chato, wakazi wake wengi ni warundi, kiusalama, ina hatari.

Wakimbizi wa Burundi walifanikiwa kutoa Rais wa Tanzania!!
Kuna kitu kikubwa sana hapa umekiongelea kuhusu warund na madhara yako kisiasa na kijamii na kiusalama. sema tu weng hawajui kubold maneno. Sabab zote tunaweza kuziachia lakin walau ya ukubwa wa eneo likimegwa kubak km za mraba 16000 si la kudharau. Tujue Mkoa mpya ni kuzalisha matumiz zaid ya serkali katika mapato yale yale.
 
Walitakiwa kuwa na misimamo kama hii kipindi cha lile jendawazimu vinginevyo wanatupigia kelele tu, ila mimi nilishawahi kusema jiwe alitaka chattle iwe nchi kabisa sio mkoa ,tumsuhukru saana Mungu , yaani alitamani hata bahari na yenyewe aipeleke kule , jinga kabisa lile janaharamu
 
Nimefika Chato. Ile wilaya JPM aliijaza miradi mikubwa sana ya kitaifa.
Uwanja wa ndege.
Miradi kibao ya NHC.
MABANKA MAKUBWA.
IKO MIRADI MINGI SANAAAAAA.

HII MIRADI ISIPOTENGENEZEWA MIKAKATI YA KUITUMIA ITAKUFA NA SERIKALI ITAPATA HASARA.
KUIGEUZA MKOA NI SOLUTION ILIYOPO.

SABABU ZA WAHAYA KUUKATAA MKOA WA RUBONDO ZIMEKAA KIHUNI TU.
Wahaya wanasema bwana Bigambo (muombolezaji) "atuache kidogo"

Hapo bado waha nao hawajatoa tamko, maana na wao wilaya yao ya Kakonko "iko kwenye menyu"
 
Kumbe wabunge wa Bukoba, nilifikiri wabunge wa Ngara na Biharamulo maeneo yanayopendekezwa kumegwa...nyie wahaya acheni ubinafsi mnajidai leo ndio mnazithamini Ngara na Biharamulo pathetic!
Wanasema mkoa wao usiguswe, tena hawataki mazoea katika hili.
 
Mkoa kumegwa si tatizo kubwa bali hoja ni kuwa kuanzishwa kwa mkoa kunamnufaishaje mwananchi wa kawaida.
Ni wananchi wangapi wanaohitaji huduma za kimkoa.

Wananchi wengi tunahitaji kurahisishwa/kuboreshwa kwa huduma za vitongoji, vijiji na kata.
Nakumbuka miaka ya karibuni kuna baadhi ya vitongoji viliungwa vikaongezwa ukubwa.

Tusaidieni kupunguza ukubwa wa maeneo yaliyo jirani yetu.
Wapeni posho, vyombo vya usafiri, vifaa vya kazi nk viongozi wa chini ili wawahiudumie wananchi kwenye vitongoji, vijiji na kata zao.

Kuanzisha mkoa kuna gharama kubwa mno ikiwamo majengo, magari, mishahara na mengineyo.
Kuboresha maeneo ya chini kutaharakisha maendeleo.

Naamini hitaji la wananchi si Wilaya wala mkoa mpya.
Tuleteeni wataalam wa kilimo, afya, elimu, maendeleo na ustawi wa jamii, mifugo nk huku chini.

Mungu ibariki Tanzania.

Sent from my Infinix X624 using JamiiForums mobile app
Umeupiga mwingi sana
 
Wabunge wa Mkoa wa Kagera, Wamepinga kitendo cha kuendelea kuumega Mkoa wa Kagera. Hii imekuja baada ya Kuanzishwa Mchakato wa kufanya Wilaya ya Chato iliyopo Geita kuwa Mkoa.


1
This is strengthening the weakest by weakening the strongest. Yaani kutengeneza na kufufuagari mbovu kwa kuchomoa spea kutoka gari linalotemea
 
Back
Top Bottom