Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 33,679
- 49,841
Kuna siku nilitembelea chuo fulani, kwa ajili ya shughuli tu za kikazi.
Ile nikiwa kwenye foleni katika kusubiri huduma, nikakutana na jamaa zangu wawili ambao tulikuwa tunafahamiana huko mtaani; tukawa tunaongea na kubadilishana mawazo ya hapa na pale.
Mara akaja mkufunzi mmoja wa kike, akatupa hai, tukawa tunaongea huku tunacheka. Mara yule mkufunzi akaniuliza, ''huna mdogo wako aje anioe, nimechoka kuwa mwenyewe''. Nilishtuka ghafla kutokana na huo ujasiri aliokuwa nao, mpaka kunitamkia hayo maneno bila kupepesa macho.
Nikamuuliza, uko siriazi? Akanijibu, ndio; nami nikamjibu, ''kwa bahati mbaya wote walishaoa, na wakike walishaolewa''.
Ila katika kutafakari, nikahisi ujumbe ulikuwa unanilenga mimi, kwa sababu huwa nikitembea huwa sivai pete ya ndoa.
Ikabidi nimjibu kwa kifupi, nitakutafutia.
Swali langu; kwa nini nyakati hizi wadada wamekuwa wepesi kuwafungukia wanaume?
Ile nikiwa kwenye foleni katika kusubiri huduma, nikakutana na jamaa zangu wawili ambao tulikuwa tunafahamiana huko mtaani; tukawa tunaongea na kubadilishana mawazo ya hapa na pale.
Mara akaja mkufunzi mmoja wa kike, akatupa hai, tukawa tunaongea huku tunacheka. Mara yule mkufunzi akaniuliza, ''huna mdogo wako aje anioe, nimechoka kuwa mwenyewe''. Nilishtuka ghafla kutokana na huo ujasiri aliokuwa nao, mpaka kunitamkia hayo maneno bila kupepesa macho.
Nikamuuliza, uko siriazi? Akanijibu, ndio; nami nikamjibu, ''kwa bahati mbaya wote walishaoa, na wakike walishaolewa''.
Ila katika kutafakari, nikahisi ujumbe ulikuwa unanilenga mimi, kwa sababu huwa nikitembea huwa sivai pete ya ndoa.
Ikabidi nimjibu kwa kifupi, nitakutafutia.
Swali langu; kwa nini nyakati hizi wadada wamekuwa wepesi kuwafungukia wanaume?