Wadada siku hizi wanatongoza, hawana aibu tena

Wadada siku hizi wanatongoza, hawana aibu tena

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kuna siku nilitembelea chuo fulani, kwa ajili ya shughuli tu za kikazi.

Ile nikiwa kwenye foleni katika kusubiri huduma, nikakutana na jamaa zangu wawili ambao tulikuwa tunafahamiana huko mtaani; tukawa tunaongea na kubadilishana mawazo ya hapa na pale.

Mara akaja mkufunzi mmoja wa kike, akatupa hai, tukawa tunaongea huku tunacheka. Mara yule mkufunzi akaniuliza, ''huna mdogo wako aje anioe, nimechoka kuwa mwenyewe''. Nilishtuka ghafla kutokana na huo ujasiri aliokuwa nao, mpaka kunitamkia hayo maneno bila kupepesa macho.

Nikamuuliza, uko siriazi? Akanijibu, ndio; nami nikamjibu, ''kwa bahati mbaya wote walishaoa, na wakike walishaolewa''.

Ila katika kutafakari, nikahisi ujumbe ulikuwa unanilenga mimi, kwa sababu huwa nikitembea huwa sivai pete ya ndoa.

Ikabidi nimjibu kwa kifupi, nitakutafutia.

Swali langu; kwa nini nyakati hizi wadada wamekuwa wepesi kuwafungukia wanaume?
 
Jibu.
Mambo ni mengi
Mda mchache
... Ma men now wana mambo mengi
Bado ajabet.. bado awaze kutongoza

Hana budi ajiongeze..
Sema mii hiyi bahati sijawahi pata na huwa natafuta kwa hali na mali lakini wapi..... 😂😂😂🤓🤓🤓🤓🤓
 
Kuna siku nilitembelea chuo fulani, kwa ajili ya shughuli tu za kikazi.

Ile nikiwa kwenye foleni katika kusubiri huduma, nikakutana na jamaa zangu wawili ambao tulikuwa tunafahamiana huko mtaani; tukawa tunaongea na kubadilishana mawazo ya hapa na pale.

Mara akaja mkufunzi mmoja wa kike, akatupa hai, tukawa tunaongea huku tunacheka. Mara yule mkufunzi akaniuliza, ''huna mdogo wako aje anioe, nimechoka kuwa mwenyewe''. Nilishtuka ghafla kutokana na huo ujasiri aliokuwa nao, mpaka kunitamkia hayo maneno bila kupepesa macho.

Nikamuuliza, uko siriazi? Akanijibu, ndio; nami nikamjibu, ''kwa bahati mbaya wote walishaoa, na wakike walishaolewa''.

Ila katika kutafakari, nikahisi ujumbe ulikuwa unanilenga mimi, kwa sababu huwa nikitembea huwa sivai pete ya ndoa.

Ikabidi nimjibu kwa kifupi, nitakutafutia.

Swali langu; kwa nini nyakati hizi wadada wamekuwa wepesi kuwafungukia wanaume?​
Duh..!! Ngoja nimuulize mamdogo wangu Amehlo kama hili ni kweli au la..!!
 
Back
Top Bottom