Wadau wapendekeza mambo 12 mabadiliko ya Mfumo wa Uchaguzi na Vyama vya Siasa

Wadau wapendekeza mambo 12 mabadiliko ya Mfumo wa Uchaguzi na Vyama vya Siasa

Matokeo ya Urais kupingwa mahakamani kutahitaji mabadiliko kwenye Katiba ya sasa
 
Namba 5,7,8 na 10 ni mwiba kwa CCM usitegemee wako tayari.
 
Kwa kifupi;

1. Matokeo ya urais kuruhusiwa kupingwa mahakamani.

2. Mfumo kuruhusu Mgombea binafsi.

3. Kuwepo kigezo cha 50 + 1 kwa mshindi.

4. Kuwe na uwakilishi sawa wa 50/50 kwa jinsia zote.

5. Jeshi la polisi kutoingilia shughuli za vyama vya siasa kabla, wakati na baada ya uchaguzi.

6. Tume ya uchaguzi iwe na watumishi wake.

7. Wakurugenzi wa Halmashauri wasiwe wasimamizi wa uchaguzi.

8. Mkurugenzi wa Uchaguzi, Mwenyekiti wa tume na Makamishina wapatikane kwa kuomba kazi ambazo zitatangazwa hadharani.

9. Uteuzi wa wajumbe wa tume uzingatie uwakilishi wa vyama vikubwa vya siasa, asasi za kiraia, taasisi za kidini na wanataaluma.

10. Kigezo cha kupita bila kupingwa kiondolewe.

11. Pamoja na kuzingatia jinsia jamii ya walemavu izingatiwe wakati wa uteuzi.

12. Mikutano ya vyama vya siasa ifanyike kwa usawa na nafasi ya Msajili wa vyama vya siasa itangazwe hadharani.

NB: Mimi naongeza 13. Atakayebainika kutangaza matokeo ya uongo ashitakiwe kwa makosa ya Uhujumu Uchumi, kwa sababu kalihujumu taifa zima lililotumia gharama kubwa kuandaa uchaguzi.
Hivi ni vilaka vipya kwenye nguo chakavu.

Heri kununua nguo mpya (katiba mpya) kabisa.
 
Bahati mbaya haya ni "mawazo ya mtandaoni" ila kama yangekuwa ya watanzania issue ya 50/50 ni takataka tupa jalalani.

Wamwezeshwa vya kutosha waingie wenyewe uwanjani wakapambane, mpaka lini wabwebwe?, yaani kina Makinda, Marry Nagu, yule mama wa ukerewe, nk bado wameshindwa kutoa wanawake wenye uwezo wa kupambana wenyewe?.
 
1. Matokeo ya urais kuruhusiwa kupingwa mahakamani- Itahitaji mabadiliko ya Katiba

2. Mfumo kuruhusu Mgombea binafsi- Itahitaji mabadiliko ya Katiba ya sasa

3. Kuwepo kigezo cha 50 + 1 kwa mshindi- Itahitaji mabadiliko ya Katiba ya sasa

4. Kuwe na uwakilishi sawa wa 50/50 kwa jinsia zote- Sio muhimu, watu wachaguliwe kwa uwezo wao

5. Jeshi la polisi kutoingilia shughuli za vyama vya siasa kabla, wakati n

6. Tume ya uchaguzi iwe na watumishi wake - Kwa ngazi za chini kuhesabu kura wakitumika walimu ni sawa. Hii iwe upande wa wakurugenzi na wasimamizi wakuu.

7. Wakurugenzi wa Halmashauri wasiwe wasimamizi wa uchaguzi - Ilitakiwa kuwa hivi miaka mingi sana.

8. Mkurugenzi wa Uchaguzi, Mwenyekiti wa tume na Makamishina wapatikane kwa kuomba kazi ambazo zitatangazwa hadharani - Itahitaji mabadiliko katika Katiba ya sasa

9. Uteuzi wa wajumbe wa tume uzingatie uwakilishi wa vyama vikubwa vya siasa, asasi za kiraia, taasisi za kidini na wanataaluma - Taasisi za Kidini watakuwa na kazi gani kwenye tume? Au kufanya maombi?

10. Kigezo cha kupita bila kupingwa kiondolewa- Hakuna Kigezo Kikatiba

11. Pamoja na kuzingatia jinsia jamii ya walemavu izingatiwe wakati wa uteuzi - Watu wachaguliwe na kuteuliwa kwa uwezo wao
 
Simple. CCM hayawezi kukubali.
1648030826285.png
 
Nakumbuka zamani vyama vyenye wagombea urais vilikuwa vinapewa ruzuku kwa ajili ya kampeni sikumbuki kiasi, pamoja na posho za mawakala wao.
Haijawahi kuwa hivyo, kumbuka yaliyomtokea mzee Mwinyi huko Kigoma wakati wa uchaguzi baada ya kushuka kwenye ndege, rubani mmoja alipiga picha mapokezi hayo.

Tulipoingia kwenye uchaguzi wa vyama vingi tulianza vizuri kwa haki kupatikana vyama vyote, lakini Mrema alipoonekana tishio kwenye urais CCM ikaanza kutumia mabavu ili iendelee kutawala badala ya kuiongoza nchi.
 
1. Matokeo ya urais kuruhusiwa kupingwa mahakamani- Itahitaji mabadiliko ya Katiba

2. Mfumo kuruhusu Mgombea binafsi- Itahitaji mabadiliko ya Katiba ya sasa

3. Kuwepo kigezo cha 50 + 1 kwa mshindi- Itahitaji mabadiliko ya Katiba ya sasa

4. Kuwe na uwakilishi sawa wa 50/50 kwa jinsia zote- Sio muhimu, watu wachaguliwe kwa uwezo wao

5. Jeshi la polisi kutoingilia shughuli za vyama vya siasa kabla, wakati n

6. Tume ya uchaguzi iwe na watumishi wake - Kwa ngazi za chini kuhesabu kura wakitumika walimu ni sawa. Hii iwe upande wa wakurugenzi na wasimamizi wakuu.

7. Wakurugenzi wa Halmashauri wasiwe wasimamizi wa uchaguzi - Ilitakiwa kuwa hivi miaka mingi sana.

8. Mkurugenzi wa Uchaguzi, Mwenyekiti wa tume na Makamishina wapatikane kwa kuomba kazi ambazo zitatangazwa hadharani - Itahitaji mabadiliko katika Katiba ya sasa

9. Uteuzi wa wajumbe wa tume uzingatie uwakilishi wa vyama vikubwa vya siasa, asasi za kiraia, taasisi za kidini na wanataaluma - Taasisi za Kidini watakuwa na kazi gani kwenye tume? Au kufanya maombi?

10. Kigezo cha kupita bila kupingwa kiondolewa- Hakuna Kigezo Kikatiba

11. Pamoja na kuzingatia jinsia jamii ya walemavu izingatiwe wakati wa uteuzi - Watu wachaguliwe na kuteuliwa kwa uwezo wao

Ni wazi kuwa katiba mpya ndiyo ulio ufumbuzi kamili.

Kwa vile hawataki katiba mpya, haya hawawezi kuyakubali.
 
50/50 ndio nini? Hivi kuna nchi yoyote duniani ina 50/50, mmeona wapi? Iko wazi, wanawake wengi uwezo wao bado mdogo sana kuongoza, sasa nchi inataka maendeleo, 50/50 sioni maana yake, sio nawachukia wanawake, la harsha, ukweli uko hivyo, naturally most women uongozi hawawezi, sasa maendeleo yatatoka wapi. Jamani, sielewi kama naeleweka, wanawake type ya Mama Samia ni 1 in 100 mil nasema kweli kabisa, na Mama Samia kajifunza mengi kwa JPM ndio maana amekuwa na uwezo mzuri.

Mm sioni hoja kabisa ya 50/50, na hakuna duniani mfano huo.
Ana uwezo gani mzuri!!!?

Kuweni wakweli tu....Ana uwezo mdogo mno acheni Unafiki...

Pitia mahojiano yake na vyombo vya habari, hususani BBC utaona uwezo wake..

Wabaki kuwa mama zetu tu...ni Heshima kwao
 
Kati ya yote hapo ,hilo la mgombea binafsi halina tija ,litahitaji mabadiliko makubwa zaidi ya Katiba na sheria.
Hata matokeo ya uraisi kuhojiwa mahakamani inahitaji mabadiliko ya katiba maana katiba ndo inazuia hilo jambo
 
Polisi hawaingilii uchaguzi isipokuwa wanalinda amani na wakipata habari za kiintelijensia ,hustopisha kufanyika mkutano,
tatizo habari hizo mbaya huwa nazo vyama vya upinzani tu.
 
Back
Top Bottom